ALIYEKUWA mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond Dk Harrison Mwakyembe ame...
ALIYEKUWA mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya kuchunguza mkataba wa kampuni ya kuzalisha umeme wa dharura ya Richmond Dk Harrison Mwakyembe amevunja mzizi wa fitna na kuwapasha baadhi ya Wabunge wanaowasafisha viongozi waliojizulu kutokana na kashfa ya Richmond kuwa wanapoteza muda kwani Watanzania sio mabwege.
Dk Mwakyembe alilimbia Bunge Leo kuwa kuna kundi la Wabunge ambao wameandaliwa kuwasafisha viongozi waliotuhumiwa kuhusuka kwenye ufisadi wa Richmond na kusababisha wajiuzulu ili kamati aliyokuwa anaiongoza yeye ionekena kama iliwaonea kwenye ripoti yake.
Mbunge huyo ambaye alizungumza suala hilo kwa hisia kali alitamka bayana kuwa jaribio hilo la kuwasafisha viongozi wanaotuhumiwa katika ufisadi wa Richmond ni kujidhalilisha.
Akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu, Dk Mwakyembe alisema kama kuna Wabunge ambao wanaamini kuwa kamati iliwaonea mawaziri na wabunge waliotajwa kwenye ripoti hiyo kuhusika na mkataba mbovu wa Richmond ni vyema waombe Spika avunje kanuni za Bunge ili suala hilo liweze kujadiliwa tena bungeni.
Alisema analazimika kusema maneno hayo kwani suala hilo licha ya kujadiliwa kwa kina bungeni na kasha kutolewa maamuzi kadhaa na chombo hicho; lakini bado kuna baadhi ya Wabunge ambao wameandaliwa kujaribu kuwasafisha viongozi waliotajwa kwenye ripoti hiyo jambo alilodai yeye kama mwenyekiti wa kamati ile hawezi kulivumilia.
Viongozi ambao walijiuzulu nyadhifa zao baada ya kutajwa kuhusika kwenye mkataba mbovu wa Richmond ni aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa, aliyekuwa waziri wa nishati na madini Naziri Karamagi, aliyekuwa waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk Ibrahim Msabaha.
Ripoti hiyo pia ilimtaja Mbunge wa Igunga Rostam Aziz kuhusika na umiliki wa Richmond kampuni inayodaiwa kuwa haipo na haikuwahikusajiliwa huko Marekani kama ilivyoonyeshwa kwenye anuani yake.
Dk Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela alisema juhudi za kuwasafisha vigogo hao ni kujidhalilisha kwani Watanzania kwa saa sio tena mabwege wa kuendelea kudanganywa na kuwashawishi waamini kwamba viongozi waliotajwa kwenye ripoti wamesingiziwa na kuonewa.
Alisema Wabunge wanaomini hivyo wawasilishe maombi kwa Spika ili kanuni namba 53 na 54 za Bunge zivunjwe na kamati yake iko tayari suala hilo lijadiliwe tena bungeni na iwapo wanakamati watabainika kuwa waliwasingizia viongozi waliotajwa kuhusika na mkataba huo mbovu wa Richmond wako tayari kujiuzulu Ubunge.
Lakini akaonya kuwa kama suala hilo litajadiliwa tena na ikabainika kuwa viongozi waliotajwa na kujiuzulu walihusika kuingiza nchi kwenye mkataba wenye utata nao wawe tayari kujiuzulu na kuachia ngazi nyadhifa zote za utumishi wa umma walizonazo.
Aliongeza kuwa kamati yake iko tayari kutaja hata yale mambo ambayo waliyaficha kuyatoa hadharani kwenye ripoti hiyo ili kulinda heshima ya serikali ya CCM. Alisema hatua hiyo peke yake ndio itasaidia kuliepusha Bunge ili lisiwe sehemu ya malumbano.
"Hapa tuko busy tu kukashfiana, kwa kweli jambo hili linanikera," alisema na kusisitiza kwa mwenyekiti aliyekuwa anashikilia kiti cha Spika Jenesta Mhagama kuwa aruhusu kanuni ya 53 na 54 ivunjwe ili ibainike yupi mkweli.
Kanuni hizo za Bunge zinamkataza mbunge yeyote kuibua jambo ambalo lilishatolewa uamuzi na Bunge. Kutokana na kitendo cha baadhi ya wabunge kuliibua katika hoja mbalimbali wanazozitoa wakati wa kuchangia hotuba za bajeti na ile hotuba ya makadirio ya ofisi ya waziri mkuu, Dk Mwakyembe alisema kitendo hicho ni kuvunja kanuni hiyo.
Aliongeza kuwa baadhi ya wabunge hao wanadhani kuwa uamuzi huo ulikuwa wanakamati wakati suala hilo baada ya kuwasilishwa bungeni lilijadiliwa kwa kina na kuamriwa katika vipengele zaidi ya 50 ambavyo vinahitaji kutekelezwa na Serikali.
"Kuna wabunge hapa wanadhani uamuzi ule ulikuwa wa Mwakyembe (Harrison), Manyanya (Stella), Mnyaa (Mohamed), Selelii (Lucas), Mtangi (Herbet), hapana ule ni uamuzi wa Bunge," alisema Dk Mwakyembe ambaye mara tu baada ya kikao cha Bunge kuanza aliripotiwa kuugua ghafla.
Alisema ni vyema kifungu hicho kitenguliwe ili wenye mashaka na maamuzi yale watoe dukuduku zao na wao watasema yale yote wanayoyajua kwa namna viongozi waliotajwa kwenye ripoti hiyo walivyohusika kuiingiza nchi kwenye mkataba mbovu na kampuni hewa.
Dk Mwakyembe alisema Bunge haliwezi kugeuka la malumbano "Waje hapa waseme nasi tuko tayari kusema na mengine ambayo hatukuyataja...hatuwezi kuja hapa kila siku tukakumbushia mambo yaliyokwisha amriwa."
Alisema kitendo hicho kinachofanywa na baadhi ya Wabunge ni cha kujidhalilisha mbele ya uso wa Watanzania. Aliongeza kuwa Wabunge walishaanza kupata heshima mbele ya wananchi; lakini kwa vitendo vinavyofanywa na baadhi yao kujaribu kuwasafisha watuhumiwa wa ufisadi wa Richmond ni kujidhalilisha na heshima hiyo inapotea.
Mara tu baada ya Dk Mwakyembekumalizia kuchangia, Lowassa ambaye kwa muda wote alikuwa anamwangalia alitoka nje ya ukumbi wa Bunge na hakurudi tena hadi Jenesta alipositisha shughuli za Bunge hadi jioni.
Dk Mwakyembe alilimbia Bunge Leo kuwa kuna kundi la Wabunge ambao wameandaliwa kuwasafisha viongozi waliotuhumiwa kuhusuka kwenye ufisadi wa Richmond na kusababisha wajiuzulu ili kamati aliyokuwa anaiongoza yeye ionekena kama iliwaonea kwenye ripoti yake.
Mbunge huyo ambaye alizungumza suala hilo kwa hisia kali alitamka bayana kuwa jaribio hilo la kuwasafisha viongozi wanaotuhumiwa katika ufisadi wa Richmond ni kujidhalilisha.
Akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya ofisi ya waziri mkuu, Dk Mwakyembe alisema kama kuna Wabunge ambao wanaamini kuwa kamati iliwaonea mawaziri na wabunge waliotajwa kwenye ripoti hiyo kuhusika na mkataba mbovu wa Richmond ni vyema waombe Spika avunje kanuni za Bunge ili suala hilo liweze kujadiliwa tena bungeni.
Alisema analazimika kusema maneno hayo kwani suala hilo licha ya kujadiliwa kwa kina bungeni na kasha kutolewa maamuzi kadhaa na chombo hicho; lakini bado kuna baadhi ya Wabunge ambao wameandaliwa kujaribu kuwasafisha viongozi waliotajwa kwenye ripoti hiyo jambo alilodai yeye kama mwenyekiti wa kamati ile hawezi kulivumilia.
Viongozi ambao walijiuzulu nyadhifa zao baada ya kutajwa kuhusika kwenye mkataba mbovu wa Richmond ni aliyekuwa waziri mkuu Edward Lowassa, aliyekuwa waziri wa nishati na madini Naziri Karamagi, aliyekuwa waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dk Ibrahim Msabaha.
Ripoti hiyo pia ilimtaja Mbunge wa Igunga Rostam Aziz kuhusika na umiliki wa Richmond kampuni inayodaiwa kuwa haipo na haikuwahikusajiliwa huko Marekani kama ilivyoonyeshwa kwenye anuani yake.
Dk Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela alisema juhudi za kuwasafisha vigogo hao ni kujidhalilisha kwani Watanzania kwa saa sio tena mabwege wa kuendelea kudanganywa na kuwashawishi waamini kwamba viongozi waliotajwa kwenye ripoti wamesingiziwa na kuonewa.
Alisema Wabunge wanaomini hivyo wawasilishe maombi kwa Spika ili kanuni namba 53 na 54 za Bunge zivunjwe na kamati yake iko tayari suala hilo lijadiliwe tena bungeni na iwapo wanakamati watabainika kuwa waliwasingizia viongozi waliotajwa kuhusika na mkataba huo mbovu wa Richmond wako tayari kujiuzulu Ubunge.
Lakini akaonya kuwa kama suala hilo litajadiliwa tena na ikabainika kuwa viongozi waliotajwa na kujiuzulu walihusika kuingiza nchi kwenye mkataba wenye utata nao wawe tayari kujiuzulu na kuachia ngazi nyadhifa zote za utumishi wa umma walizonazo.
Aliongeza kuwa kamati yake iko tayari kutaja hata yale mambo ambayo waliyaficha kuyatoa hadharani kwenye ripoti hiyo ili kulinda heshima ya serikali ya CCM. Alisema hatua hiyo peke yake ndio itasaidia kuliepusha Bunge ili lisiwe sehemu ya malumbano.
"Hapa tuko busy tu kukashfiana, kwa kweli jambo hili linanikera," alisema na kusisitiza kwa mwenyekiti aliyekuwa anashikilia kiti cha Spika Jenesta Mhagama kuwa aruhusu kanuni ya 53 na 54 ivunjwe ili ibainike yupi mkweli.
Kanuni hizo za Bunge zinamkataza mbunge yeyote kuibua jambo ambalo lilishatolewa uamuzi na Bunge. Kutokana na kitendo cha baadhi ya wabunge kuliibua katika hoja mbalimbali wanazozitoa wakati wa kuchangia hotuba za bajeti na ile hotuba ya makadirio ya ofisi ya waziri mkuu, Dk Mwakyembe alisema kitendo hicho ni kuvunja kanuni hiyo.
Aliongeza kuwa baadhi ya wabunge hao wanadhani kuwa uamuzi huo ulikuwa wanakamati wakati suala hilo baada ya kuwasilishwa bungeni lilijadiliwa kwa kina na kuamriwa katika vipengele zaidi ya 50 ambavyo vinahitaji kutekelezwa na Serikali.
"Kuna wabunge hapa wanadhani uamuzi ule ulikuwa wa Mwakyembe (Harrison), Manyanya (Stella), Mnyaa (Mohamed), Selelii (Lucas), Mtangi (Herbet), hapana ule ni uamuzi wa Bunge," alisema Dk Mwakyembe ambaye mara tu baada ya kikao cha Bunge kuanza aliripotiwa kuugua ghafla.
Alisema ni vyema kifungu hicho kitenguliwe ili wenye mashaka na maamuzi yale watoe dukuduku zao na wao watasema yale yote wanayoyajua kwa namna viongozi waliotajwa kwenye ripoti hiyo walivyohusika kuiingiza nchi kwenye mkataba mbovu na kampuni hewa.
Dk Mwakyembe alisema Bunge haliwezi kugeuka la malumbano "Waje hapa waseme nasi tuko tayari kusema na mengine ambayo hatukuyataja...hatuwezi kuja hapa kila siku tukakumbushia mambo yaliyokwisha amriwa."
Alisema kitendo hicho kinachofanywa na baadhi ya Wabunge ni cha kujidhalilisha mbele ya uso wa Watanzania. Aliongeza kuwa Wabunge walishaanza kupata heshima mbele ya wananchi; lakini kwa vitendo vinavyofanywa na baadhi yao kujaribu kuwasafisha watuhumiwa wa ufisadi wa Richmond ni kujidhalilisha na heshima hiyo inapotea.
Mara tu baada ya Dk Mwakyembekumalizia kuchangia, Lowassa ambaye kwa muda wote alikuwa anamwangalia alitoka nje ya ukumbi wa Bunge na hakurudi tena hadi Jenesta alipositisha shughuli za Bunge hadi jioni.
COMMENTS