NIMEPATA kuona filamu moja ambayo Mr Big alikuwa amefanya vyema kabisa. Mimi napenda kuamini kwamba bado Mr Big hajapatiwa nafasi yake kama ...
NIMEPATA kuona filamu moja ambayo Mr Big alikuwa amefanya vyema kabisa. Mimi napenda kuamini kwamba bado Mr Big hajapatiwa nafasi yake kama kinara wa filamu awe adui bora au awe mtu bora.
Napenda kuamini kwa kuwa ukiangalia filamu kadhaa za sapoti Mr Big amefanya vyema sana kuliko hii ndani ya Pain, amekuwa mtu asiyestahili kuvaa kivao kile cha mapenzi na muuaji.
Wakati mwingine hufikiria sana tatizo hili, tatizo la mtu kuona kwamba lazima aigize kokote kule na watumiaji wakijaribu kuwapata watu ambao hawafai kwa nafasi zile wanazotaka wacheze lakini maarufu na hivyo kuwatumia vibaya.
Kitendo cha kumtumia Big kama muuaji wa mpenzi wake kumenipa taabu kidogo juu ya nafasi wanazopewa waigizaji ambao wengi wao wamekuwa wakipewa nafasi ambazo si zao na kusababisha filamu kudorora na kutochukua kasi inayotakiwa ya utamu.
The Pain pamoja na kwamba imetengenezwa na mtu ambaye nilimpa big up katika Masaa 24 kwa kuweza kuweka 'tension' kwa muda wote na kuwatumia vyema waigizaji kwa namna yao, imekosa ule msisimko ambao ungeliweza kuupata kama dairekta angeliwapanga watu vyema na hadithi yake kuachana na 'flashback'.
Kuna kupwaya kwa nafasi ya uigizaji ambayo imefanya hadithi nzima hii ya mikasa ya maisha kuwa kama kituko na mchezo wa kuigiza badala ya kushika nafasi yake.
Maingiliano ya hadithi na udhaifu wa sauti inafanya kitu ambacho kinatakiwa kuwa bora kukosa mwelekeo wa utamu stahiki wa uangalizi wa sinema.
John Lister ni mtu mzuri lakini anafaa kukumbuka kwamba asikimbilie kutoa tu sinema na kutumia waigizaji wake vibaya, bali wametengeneza sinema mtu kama Mr Big, sinema ambayo ina mwenendo wake wa saa 24 kwa kuwa anafaa kwa hisia za mwili na aina fulani ya uigizaji wenye mwelekeo wa kufurahisha na kutoa burudani zaidi.
Ninapozungumza The Pain sitaki hata kumzungumzia mwanadada ambaye alionekana kupelekwa tu lakini akiwa anakosa ule umakini wa kuwa mzuri na mpenzi wa dhati tukiachiwa tu maneno ambayo hatuyasikii vyema.
Huenda kopi niliyonayo si sahihi, lakini ukiachia mbali kuendelea kutuonyesha mlevi ambaye hafanani na ulevi bado hatumtendei haki mfu wetu ambaye alionekana na kutoweka bila kutoa hisia za mwelekeo.
Naam, tunaona hasira na kejeli katika utambulisho lakini hii si dhamana pia ya mtoto ambaye anaonekana ati hajui kusema na anapata mshtuko, hivi ni kweli?Yaani spidi ya kkumkuza mtoto yule inaenda kinyume kabisa na taratibu za kitaalamu.
Tunapozungumzia uigizaji wa filamu wakati fulani inafaa tufikiri pia uwekaji vizuri wa watu wetu kwa lengo la kunogesha simulizi ambalo ama hakika linastahili kufanana nasi si kwa kutulazimisha bali natural flow.
Kila mtu anaweza kusema vyake lakini kwa leo naona heri nimjadili Mr Big tu.Muigizaji ambaye namuona yu mzuri lakini naona kapewa nafasi mbaya ndani ya Pain halkafuj tunakosa utamu wake , hali ambayo inamfanya apwaye na hii si kawaida yake.
Tazama tukio zima la mauaji na kukamatwa linavyoonekana kuwa mzaha mtupu.Lakini kwa kuona inafaa kuonwa kwani kila mtu akichangia kuona kasoro tunaisukuma mbele fani hii ambayo bado inahitajika sana kutuburudisha na kutuelimisha. Na tunapozungumza filamu za kibongo tunautaka ule ubongo wetu.
Ifuatayo ni misimamo mbalimbali ya filamu kwa wiki ilioyopita.Msimamo wa filamu katika maktaba ya Salamander( kasi ya kuazima) na pia majuu katika ten za USA.
Filamu za Kiswahili
1--- COPY
2--- MISS BONGO
3--- POINT OF NO RETURN
4--- SHE IS MY SISTER
5--- DAR TO LAGOS
6--- THE GREENA
7--- AGANO LA URITHI
8--- I CANT FORGET
9--- DIVERSION OF LOVE
10-- MAHABUBA
Filamu za Kiingereza
1--- THE RANDIOTION
2--- BATTLE TO HADITHIA
3--- THE TAKE
4--- 10.000 BC
5--- WHY DID I GET MARRIED
6--- SHOOT THEM UP
7--- FORBIDEN KINGDOM
8--- RAMBO IV
9--- WE OWN THE NIGHT
10-- NO COUNTRY FOR OLD MAN
Filamu za Hollywood (Top Office Box)
1.Kung Fu Panda
2.You Don't Mess With the Zohan
3.Indiana Jones and the Kingdom of the Crystal Skull
4.Sex and the City
5.The Strangers
6.Iron Man
7.The Chronicles of Narnia: Prince Caspian
8.What Happens in Vegas
9.Baby Mama
10.Made of Honor
Napenda kuamini kwa kuwa ukiangalia filamu kadhaa za sapoti Mr Big amefanya vyema sana kuliko hii ndani ya Pain, amekuwa mtu asiyestahili kuvaa kivao kile cha mapenzi na muuaji.
Wakati mwingine hufikiria sana tatizo hili, tatizo la mtu kuona kwamba lazima aigize kokote kule na watumiaji wakijaribu kuwapata watu ambao hawafai kwa nafasi zile wanazotaka wacheze lakini maarufu na hivyo kuwatumia vibaya.
Kitendo cha kumtumia Big kama muuaji wa mpenzi wake kumenipa taabu kidogo juu ya nafasi wanazopewa waigizaji ambao wengi wao wamekuwa wakipewa nafasi ambazo si zao na kusababisha filamu kudorora na kutochukua kasi inayotakiwa ya utamu.
The Pain pamoja na kwamba imetengenezwa na mtu ambaye nilimpa big up katika Masaa 24 kwa kuweza kuweka 'tension' kwa muda wote na kuwatumia vyema waigizaji kwa namna yao, imekosa ule msisimko ambao ungeliweza kuupata kama dairekta angeliwapanga watu vyema na hadithi yake kuachana na 'flashback'.
Kuna kupwaya kwa nafasi ya uigizaji ambayo imefanya hadithi nzima hii ya mikasa ya maisha kuwa kama kituko na mchezo wa kuigiza badala ya kushika nafasi yake.
Maingiliano ya hadithi na udhaifu wa sauti inafanya kitu ambacho kinatakiwa kuwa bora kukosa mwelekeo wa utamu stahiki wa uangalizi wa sinema.
John Lister ni mtu mzuri lakini anafaa kukumbuka kwamba asikimbilie kutoa tu sinema na kutumia waigizaji wake vibaya, bali wametengeneza sinema mtu kama Mr Big, sinema ambayo ina mwenendo wake wa saa 24 kwa kuwa anafaa kwa hisia za mwili na aina fulani ya uigizaji wenye mwelekeo wa kufurahisha na kutoa burudani zaidi.
Ninapozungumza The Pain sitaki hata kumzungumzia mwanadada ambaye alionekana kupelekwa tu lakini akiwa anakosa ule umakini wa kuwa mzuri na mpenzi wa dhati tukiachiwa tu maneno ambayo hatuyasikii vyema.
Huenda kopi niliyonayo si sahihi, lakini ukiachia mbali kuendelea kutuonyesha mlevi ambaye hafanani na ulevi bado hatumtendei haki mfu wetu ambaye alionekana na kutoweka bila kutoa hisia za mwelekeo.
Naam, tunaona hasira na kejeli katika utambulisho lakini hii si dhamana pia ya mtoto ambaye anaonekana ati hajui kusema na anapata mshtuko, hivi ni kweli?Yaani spidi ya kkumkuza mtoto yule inaenda kinyume kabisa na taratibu za kitaalamu.
Tunapozungumzia uigizaji wa filamu wakati fulani inafaa tufikiri pia uwekaji vizuri wa watu wetu kwa lengo la kunogesha simulizi ambalo ama hakika linastahili kufanana nasi si kwa kutulazimisha bali natural flow.
Kila mtu anaweza kusema vyake lakini kwa leo naona heri nimjadili Mr Big tu.Muigizaji ambaye namuona yu mzuri lakini naona kapewa nafasi mbaya ndani ya Pain halkafuj tunakosa utamu wake , hali ambayo inamfanya apwaye na hii si kawaida yake.
Tazama tukio zima la mauaji na kukamatwa linavyoonekana kuwa mzaha mtupu.Lakini kwa kuona inafaa kuonwa kwani kila mtu akichangia kuona kasoro tunaisukuma mbele fani hii ambayo bado inahitajika sana kutuburudisha na kutuelimisha. Na tunapozungumza filamu za kibongo tunautaka ule ubongo wetu.
Ifuatayo ni misimamo mbalimbali ya filamu kwa wiki ilioyopita.Msimamo wa filamu katika maktaba ya Salamander( kasi ya kuazima) na pia majuu katika ten za USA.
Filamu za Kiswahili
1--- COPY
2--- MISS BONGO
3--- POINT OF NO RETURN
4--- SHE IS MY SISTER
5--- DAR TO LAGOS
6--- THE GREENA
7--- AGANO LA URITHI
8--- I CANT FORGET
9--- DIVERSION OF LOVE
10-- MAHABUBA
Filamu za Kiingereza
1--- THE RANDIOTION
2--- BATTLE TO HADITHIA
3--- THE TAKE
4--- 10.000 BC
5--- WHY DID I GET MARRIED
6--- SHOOT THEM UP
7--- FORBIDEN KINGDOM
8--- RAMBO IV
9--- WE OWN THE NIGHT
10-- NO COUNTRY FOR OLD MAN
Filamu za Hollywood (Top Office Box)
1.Kung Fu Panda
2.You Don't Mess With the Zohan
3.Indiana Jones and the Kingdom of the Crystal Skull
4.Sex and the City
5.The Strangers
6.Iron Man
7.The Chronicles of Narnia: Prince Caspian
8.What Happens in Vegas
9.Baby Mama
10.Made of Honor
NB Makala kama haya yametoka katika gazeti la habariLeo Jumapili ambako nina nafasi ya kuzungumza na watengeneza sinema wetu.
COMMENTS