SERIKALI imesema uchumi wa nchi uko katika hali ngumu hali inayolazimu kuchukua hatua za dhati za kuongeza kasi ya ukuaji kwa kuzingatia kuw...
SERIKALI imesema uchumi wa nchi uko katika hali ngumu hali inayolazimu kuchukua hatua za dhati za kuongeza kasi ya ukuaji kwa kuzingatia kuwa pia idadi ya watu inazidi kuongezeka kwa asilimia 2.9 kila mwaka.
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo aliliambia Bunge Juni 12,2008 kuwa kutokana na kupanda kwa kasi kwa bei ya mafuta ya petroli, mbolea na malighafi za viwandani, inalazimika kuchukua hatua za kuzalisha chakula cha kutosha ili kujihami na changamoto hiyo.
Katika taarifa ya hali ya uchumi wa taifa mwaka 2007 na maendeleo ya muda wa kati (2008-2010/11) aliyoisoma bungeni Dodoma, Mkulo alisema kwamba idadi ya watu inaongezeka kwa asilimia 2.9 kwa mwaka hali inayoilazimu serikali kuongeza kasi ya ukuaji uchumi ili pato la kila mwananchi liongezeke.
Hata hivyo, Mkulo alisema malengo ya jumla ya uchumi katika mwaka 2008/09 hadi 2010/10 ni kwamba, pato halisi la taifa litakua kwa asilimia 7.8 mwaka huu, asilimia 8.1 mwaka kesho na asilimia 8.8 mwaka 2010 na kuongezeka hadi asilimia 9.2 mwaka 2011.
“Idadi ya watu Tanzania inakua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka, kiwango ambacho ni kikubwa na ni changamoto muhimu ya maendeleo,” alisema Mkulo na kuongeza kuwa inakadiriwa kwamba ifikapo mwaka 2025, kutakuwa na watu milioni 63 ikilinganishwa na sasa ambako kuna watu milioni 38.
Akielezea changamoto ambazo serikali inabidi izikabili kuhakikisha kuwa ukuaji wa uchumi unamnufaisha mwananchi wa kawaida kuondokana na umasikini, alisema ingawa hatua za kuwezesha wajasiriamali zimeanza kuzaa matunda, lakini uwezo wa serikali kuendelea na mpango huo kwa kiwango kikubwa ni mdogo.
Hivyo alisema ipo haja ya kupanua uwezo kwa kuviimarisha na kuhamasisha zaidi vyombo vya fedha ili kuchukua dhima hiyo hasa ikizingatiwa kuwa matokeo ya awamu ya kwanza na ya pili yanatia moyo kutokana na marejesho mazuri ya mikopo iliyotolewa.
Kuhusu mahitaji ya fedha za kigeni katika uchumi, alisema bado ni makubwa kuliko uwezo wa nchi wa kuuza bidhaa na huduma nje. Alisisitiza kuwa ni muhimu kuweka msukumo zaidi katika kukuza mauzo nje ya bidhaa na huduma kama mbinu muhimu ya kujenga uwezo wa kujitegemea.
Alisema pia taratibu za kuanzisha na kuendesha uwekezaji na biashara bado una gharama kubwa na hivyo kudhoofisha juhudi za kufanikisha azma. “Ni muhimu tujizatiti katika kuboresha mazingira ya biashara,” alisema.
Akizungumzia mpango wa kuharakisha maendeleo Tanzania maarufu kama Tanzania Mini-Tiger Plan 2020, Mkulo alisema unaendelea kwa kasi ndogo hali ambayo inabidi serikali kuirekebisha ili kupiga hatua zaidi. Miongoni mwa miradi inayotekelezwa chini ya mpango huo, ni pamoja na ujenzi wa Kanda Maalumu ya uwekezaji ya Benjamin Mkapa iliyoko Mabibo, Dar es Salaam.
Akihusisha kukua kwa uchumi wa Tanzania na ule wa dunia, Mkulo alisema ukuaji wa uchumi wa dunia mwaka 2008/09 siyo wa kuridhisha hali ambayo inahofiwa kuathiri uwekezaji katika nchi zilizoendelea (FDI) hivyo nchi hizo kushindwa kukua kwa kasi inayohitajika kupunguza umasikini.
Mkulo alisema pia uko uwezekano wa nchi zinazoendelea kushindwa kukabiliana na mfumuko wa bei kutokana na kuendelea kupanda kwa bei za mafuta, vyakula, pembejeo za kilimo na malighafi za viwandani.
Kwa mujibu wa Mkulo, kasi ya uchumi wa dunia, haitegemewi kuzidiwa wastani wa asilimia 3.7 mwaka 2008. Kutoridhisha kwake, kunatokana na kuendelea kuvurugika kwa masoko ya fedha ya kimataifa kutokana na vurugu za soko la nyumba Marekani na Ulaya Magharibi, pamoja na kupanda kwa upatikanaji wa mikopo mipya ya nyumba.
Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo aliliambia Bunge Juni 12,2008 kuwa kutokana na kupanda kwa kasi kwa bei ya mafuta ya petroli, mbolea na malighafi za viwandani, inalazimika kuchukua hatua za kuzalisha chakula cha kutosha ili kujihami na changamoto hiyo.
Katika taarifa ya hali ya uchumi wa taifa mwaka 2007 na maendeleo ya muda wa kati (2008-2010/11) aliyoisoma bungeni Dodoma, Mkulo alisema kwamba idadi ya watu inaongezeka kwa asilimia 2.9 kwa mwaka hali inayoilazimu serikali kuongeza kasi ya ukuaji uchumi ili pato la kila mwananchi liongezeke.
Hata hivyo, Mkulo alisema malengo ya jumla ya uchumi katika mwaka 2008/09 hadi 2010/10 ni kwamba, pato halisi la taifa litakua kwa asilimia 7.8 mwaka huu, asilimia 8.1 mwaka kesho na asilimia 8.8 mwaka 2010 na kuongezeka hadi asilimia 9.2 mwaka 2011.
“Idadi ya watu Tanzania inakua kwa asilimia 2.9 kwa mwaka, kiwango ambacho ni kikubwa na ni changamoto muhimu ya maendeleo,” alisema Mkulo na kuongeza kuwa inakadiriwa kwamba ifikapo mwaka 2025, kutakuwa na watu milioni 63 ikilinganishwa na sasa ambako kuna watu milioni 38.
Akielezea changamoto ambazo serikali inabidi izikabili kuhakikisha kuwa ukuaji wa uchumi unamnufaisha mwananchi wa kawaida kuondokana na umasikini, alisema ingawa hatua za kuwezesha wajasiriamali zimeanza kuzaa matunda, lakini uwezo wa serikali kuendelea na mpango huo kwa kiwango kikubwa ni mdogo.
Hivyo alisema ipo haja ya kupanua uwezo kwa kuviimarisha na kuhamasisha zaidi vyombo vya fedha ili kuchukua dhima hiyo hasa ikizingatiwa kuwa matokeo ya awamu ya kwanza na ya pili yanatia moyo kutokana na marejesho mazuri ya mikopo iliyotolewa.
Kuhusu mahitaji ya fedha za kigeni katika uchumi, alisema bado ni makubwa kuliko uwezo wa nchi wa kuuza bidhaa na huduma nje. Alisisitiza kuwa ni muhimu kuweka msukumo zaidi katika kukuza mauzo nje ya bidhaa na huduma kama mbinu muhimu ya kujenga uwezo wa kujitegemea.
Alisema pia taratibu za kuanzisha na kuendesha uwekezaji na biashara bado una gharama kubwa na hivyo kudhoofisha juhudi za kufanikisha azma. “Ni muhimu tujizatiti katika kuboresha mazingira ya biashara,” alisema.
Akizungumzia mpango wa kuharakisha maendeleo Tanzania maarufu kama Tanzania Mini-Tiger Plan 2020, Mkulo alisema unaendelea kwa kasi ndogo hali ambayo inabidi serikali kuirekebisha ili kupiga hatua zaidi. Miongoni mwa miradi inayotekelezwa chini ya mpango huo, ni pamoja na ujenzi wa Kanda Maalumu ya uwekezaji ya Benjamin Mkapa iliyoko Mabibo, Dar es Salaam.
Akihusisha kukua kwa uchumi wa Tanzania na ule wa dunia, Mkulo alisema ukuaji wa uchumi wa dunia mwaka 2008/09 siyo wa kuridhisha hali ambayo inahofiwa kuathiri uwekezaji katika nchi zilizoendelea (FDI) hivyo nchi hizo kushindwa kukua kwa kasi inayohitajika kupunguza umasikini.
Mkulo alisema pia uko uwezekano wa nchi zinazoendelea kushindwa kukabiliana na mfumuko wa bei kutokana na kuendelea kupanda kwa bei za mafuta, vyakula, pembejeo za kilimo na malighafi za viwandani.
Kwa mujibu wa Mkulo, kasi ya uchumi wa dunia, haitegemewi kuzidiwa wastani wa asilimia 3.7 mwaka 2008. Kutoridhisha kwake, kunatokana na kuendelea kuvurugika kwa masoko ya fedha ya kimataifa kutokana na vurugu za soko la nyumba Marekani na Ulaya Magharibi, pamoja na kupanda kwa upatikanaji wa mikopo mipya ya nyumba.
COMMENTS