Hii ni barua pepe ambayo imefikia blogu hii.haikuhaririwa wala kitu chochote imetolewa kama ilivyoandikwa. Je ni nani hasa anahusika? Nini h...
Hii ni barua pepe ambayo imefikia blogu hii.haikuhaririwa wala kitu chochote imetolewa kama ilivyoandikwa. Je ni nani hasa anahusika? Nini hasa kinastahili kufanywa. Je hii ndiyo adhabu rekebishi?Angalau mtu mmoja anatakiwa kuangalia haya!
Soma haya kama yalivyoletwa.
YAH: KUOMBA KURUDISHWA KWA KIDATO CHA SITA
SHULENI MWAKALELI SEKONDARI.
WILAYA YA RUNGWE MKOANI MBEYA.
Sisi wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Mwakaleli ambao ni wahusika wa tatizo la uharibifu uliofanyika shuleni tarehe 30/may 2008 siku ya Ijumaa tumeamua kufikisha madai yetu kwako ili tusaidiwe kulingana na adhabu iliyotolewa na bodi ya shule kuwa uharibifu uliofanyika ulifikia thamani ya shillingi za kitanzania milioni Arobaini (Tsh 40miliom ) wakati kitu ambacho hatujakubaliana nacho na adhabu iliyotolewa ni kuwafukuza wanafunzi themanini na watatu na Viongozi wote wa serikali ya wanafunzi. Pia wanafunzi waliorudishwa ni sabini na watatu na watalipa fidia ya shilingi za kitanzania laki nne na elfu Hamsini ( 450,000/=) Adhabu iliyotolewa na bodi ya shule haijazingatia kurekebisha matatizo yaliyosababisha uharibifu uliofanyika na vurugu zote za siku hiyo. Pia sisi kama walengwa wa shutuma (tatizo) hilo hatujapewa nafasi ya kujieleza na kusikilizwa, Hivyo tumeamuwa kuitaarifu ofisi yako ili ishughulikie shauri letu.
Sisi kama wahusika wa tatizo hilo tunakubali kuwa uharibifu ulitokea ila kuna sababu zilizo sababisha yote hayo kufikiwa. Sababu za matatizo yote hayo zimegawanyika zimegawanyika katika sehemu mbili ni kama hizi zifuatazo.
Sababu za muda mrefu na sababu za muda mfupi (wakati wa tatizo) kati ya sababu za muda mrefu ni hizi zifuatazo
(walimu wa masomo ya uchumi na geography)
Walimu kutokuingia madarasani katika vipindi kwa madai kuwa wanamajukumu mengine tofauti ya kiofisi tofauti na ufundishaji. Hivyo tulihitaji kuongea na mkuu wa shule ili suala hilo litatuliwe haraka iwezekanavyo kwani sisi ni watahiniwa. Kwani tayari tulishindwa kuelewana na walimu husika kwani walitujibu kwa kauli ambazo si nzuri mfano mwalimu Elicko sanga alitupa kauli hii” uwezo wa kuacha kufundisha ninao, nikawepo mazingira ya shule nikaotea jua na mwisho wa mwezi mshahara wangu ukawa palepale.”mwalimu huyu alikuwa akifundisha masomo ya historia na geographia ambayo ni viungo kwa wanafunzi wa Lugha na Wauchumi. Hivyo ni dhahiri kuwa shule haikuwa tayari kutusikiliza madai yetu sisi kama wanafunzi.
Pia sisi kama wanafunzi tuliodhaminiwa na Serikali kuishi maisha ya Bweni tulihitaji kuhoji uhalali wa wanafunzi wa O’level wanaoishi mabwenini shuleni hapo. Nafasi hiyo ya kujieleza na kuuhoji uongozi wa shule tulinyimwa (hatukupewa). Hiyo ikawa ni sababu nyingine iliyotuweka sisi wanafunzi katika wakati mgumu. Na tukiamini mkuu wa shule ndiye kimbilio letu lakini hakuwa tayari kutusikiliza.
Uhaba wa chakula shuleni ni tatizo jingine ambalo liliikabiri shule yetu kwa wakati huu. Ili kukabiliana na tatizo hilo pia tulihitaji kuwasiliana na Mkuu wa Shule ili tujue mstakabali wa chakula kulingana na tatizo hilo. Kunyimwa nafasi ya kuongea na mkuu wa shule ni sababu ya muda mrefu iliyotukabili shuleni kwetu.
Hizo ni sababu matatizo yaliyokuwepo shuleni kwetu kwa muda mrefu. Licha ya matatizo hayo ya muda mrefu pia kuna sababu ambazo ndizo zilizochangia kwa kiasi kikubwa matatizo mengine ya uharibifu wa siku hiyo ya tarehe 30 may 2008. sababu hizo nihizi zifuatazo
- kauli chafu kwa wanafunzi wa kidato cha sita zilizotolewa na mwalimu charles Ntimi tarehe 29/may/2008 siku moja kabla ya matatizo hayo kutokea. Mwalimu huyo ambaye ndiye aliyepigwa alikuwa katika mtafaruku na wanafunzi hivyo tulihitaji kuongea na mkuu wa shule kumueleza suala hilo ili amrekebishe lakini ikaonekana bado hayuko tayari kutusikiliza hivyo kusababisha hasira kwa wanakidato cha sita.
- Mwalimu huyo kikazi alikua bado ni mgeni na alipanga kuwagawanya wanafunzi wa kidato cha sita kwa kutumia system ya devide and rule. Kitu ambacho kiliwakera wanakidato cha sita; kwa kuwaonyesha dhamira zake kikazi. Kwa maamuzi ya utendaji huo wa mwalimu huyo na viongozi wa serikali ya wanafunzi tuliwekwa katika wakati mgumu kimaamuzi) wakiwa katika nafasi ya kutengwa mbali na wanaowaongoza.
- Iliyokuwa serikali ya wanafunzi shuleni hapo haikupewa nafasi ya kusikilizwa na kuombwa ushauri katika maamuzi ya utawala viongozi hao katika wakati mgumu kiusalama na kuamua kujiudhuru ili kujisalimisha.
Kulingana na matatizo hayo pia tuliomba mkuu wa shule tuongee nae ili kumueleza matatizo yetu lakini alikataa hatua ya kutokukubali kuongea nasi na kutoa kauli ambayo ndiyo ilileta hasira kwetu na kuona hatuna mtetezi mwingine maeneo yale. Alisema “form six hadi sasa nimewatema, sio headmaster wao tena , bebeni vitu vyenu nendeni popote mnapo hisi mtasikilizwa” baada ya hapo ndipo wanafunzi wa kidato cha sita walipokasirka na kufanya uharibifu wakati mwalimu Charles Ntimi anatafutwa aliyekuwa amejificha katika jengo la utawala. Hivyo ilikuwa katika kumtafuta mwalimu huyo ambapo ndipo vioo vya jengo la utawala vilivunjwa, milango na mila ya umeme, Computer moja, Typing machine na kuvunja vitu vya stoo ya chakula. Hivyo ndivyo vitu ambavyo kwa mtazamo wetu tunatambua viriharibiwa na tunadhani vilihesabiwa katika uharibifu huo.
- kulingana na maamuzi ya bodi ya shule imetangaza kuwa hasara ya uharibifu huo ni wa thamani ya zaidi ya Tsh milioni arobaini, gharama ambayo hatujakubaliana nalo.
- Pia imedaiwa kuwa aliibiwa zaidi ya shilingi laki saba ambazo zilikuwa katika moja ya ofisi ya shule. Kwa sheria tunaamini kuwa hakuna sheria inayohusu pesa ya serikali kukaa ofisini zaidi ya kila moja. Hivyo tunapinga mashtaka ya bodi kwa kwa suala hilo.
- Bodi hiyo imetoa adhabu ya kuwafuta shule wanafunzi themanini na watatu (83), na kuwarudisha wanafunzi sabini na nne (78) ambao watalipa fidia ya shilingi laki nne na nusu (Tsh 450,000/=) pia hatujakubaliana na maamuzi hayo kwa upande wa bodi kwani hatujajua wametumia mbinu ipi kuwapata hao sabini na nne kuwa si waharifu katika tukio hilo, ilihali hawajatuhoji sisi kama wahusika. Hivyo tunaomba ofisi yako tukufu ifuatilie mashauri yaliyofanywa na bodi ya shule, kwani haijafuata haki. Pia adhabu iliyotolewa ni ngumu kwa wazazi wetu wa hali ya kati kiuchumi.
- Pia tunapingana na kauli iliyotolewa na vyombo vya habari kuwa tulichapa walimu wetu viboko kama ilivyotangazwa. Mwalimu aliyepigwa ni mmoja tu Mwalimu Charles Ntimi na si walimu wote kama invyotangazwa. Hata mwalimu huyo alipigwa kulingana na hali tuliyojengewa na mkuu wa shule kwa kutotusikiliza.
- Pia tumedharirishwa na vyombo vya habari kuwa tulivuta bangi kwa takribani masaa manne. Shutuma hizo tunazipanga na tuko tayari kupimwa afya zetu ili kubaini kauli hiyo. Huo ni udhalilishwaji wa hari ya juu kwa wasomi kama sisi.
Ombi letu kwa Ofisi yako ni kwamba Tunaomba tume au ofisi teule iondoe ili ichunguze kwa undani sababu za matatizo hayo na wanafunzi waliofukuzwa shule warudishwe na uchunguzi ufanywe katika gharama za uharibifu, zitajwe upya baada ya kamati ya uchunguzi kumaliza kazi yake.
Wako Watiifu
Wana wa kidato cha sita shule ya sekondari Mwakaleli
Soma haya kama yalivyoletwa.
YAH: KUOMBA KURUDISHWA KWA KIDATO CHA SITA
SHULENI MWAKALELI SEKONDARI.
WILAYA YA RUNGWE MKOANI MBEYA.
Sisi wanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari Mwakaleli ambao ni wahusika wa tatizo la uharibifu uliofanyika shuleni tarehe 30/may 2008 siku ya Ijumaa tumeamua kufikisha madai yetu kwako ili tusaidiwe kulingana na adhabu iliyotolewa na bodi ya shule kuwa uharibifu uliofanyika ulifikia thamani ya shillingi za kitanzania milioni Arobaini (Tsh 40miliom ) wakati kitu ambacho hatujakubaliana nacho na adhabu iliyotolewa ni kuwafukuza wanafunzi themanini na watatu na Viongozi wote wa serikali ya wanafunzi. Pia wanafunzi waliorudishwa ni sabini na watatu na watalipa fidia ya shilingi za kitanzania laki nne na elfu Hamsini ( 450,000/=) Adhabu iliyotolewa na bodi ya shule haijazingatia kurekebisha matatizo yaliyosababisha uharibifu uliofanyika na vurugu zote za siku hiyo. Pia sisi kama walengwa wa shutuma (tatizo) hilo hatujapewa nafasi ya kujieleza na kusikilizwa, Hivyo tumeamuwa kuitaarifu ofisi yako ili ishughulikie shauri letu.
Sisi kama wahusika wa tatizo hilo tunakubali kuwa uharibifu ulitokea ila kuna sababu zilizo sababisha yote hayo kufikiwa. Sababu za matatizo yote hayo zimegawanyika zimegawanyika katika sehemu mbili ni kama hizi zifuatazo.
Sababu za muda mrefu na sababu za muda mfupi (wakati wa tatizo) kati ya sababu za muda mrefu ni hizi zifuatazo
(walimu wa masomo ya uchumi na geography)
Walimu kutokuingia madarasani katika vipindi kwa madai kuwa wanamajukumu mengine tofauti ya kiofisi tofauti na ufundishaji. Hivyo tulihitaji kuongea na mkuu wa shule ili suala hilo litatuliwe haraka iwezekanavyo kwani sisi ni watahiniwa. Kwani tayari tulishindwa kuelewana na walimu husika kwani walitujibu kwa kauli ambazo si nzuri mfano mwalimu Elicko sanga alitupa kauli hii” uwezo wa kuacha kufundisha ninao, nikawepo mazingira ya shule nikaotea jua na mwisho wa mwezi mshahara wangu ukawa palepale.”mwalimu huyu alikuwa akifundisha masomo ya historia na geographia ambayo ni viungo kwa wanafunzi wa Lugha na Wauchumi. Hivyo ni dhahiri kuwa shule haikuwa tayari kutusikiliza madai yetu sisi kama wanafunzi.
Pia sisi kama wanafunzi tuliodhaminiwa na Serikali kuishi maisha ya Bweni tulihitaji kuhoji uhalali wa wanafunzi wa O’level wanaoishi mabwenini shuleni hapo. Nafasi hiyo ya kujieleza na kuuhoji uongozi wa shule tulinyimwa (hatukupewa). Hiyo ikawa ni sababu nyingine iliyotuweka sisi wanafunzi katika wakati mgumu. Na tukiamini mkuu wa shule ndiye kimbilio letu lakini hakuwa tayari kutusikiliza.
Uhaba wa chakula shuleni ni tatizo jingine ambalo liliikabiri shule yetu kwa wakati huu. Ili kukabiliana na tatizo hilo pia tulihitaji kuwasiliana na Mkuu wa Shule ili tujue mstakabali wa chakula kulingana na tatizo hilo. Kunyimwa nafasi ya kuongea na mkuu wa shule ni sababu ya muda mrefu iliyotukabili shuleni kwetu.
Hizo ni sababu matatizo yaliyokuwepo shuleni kwetu kwa muda mrefu. Licha ya matatizo hayo ya muda mrefu pia kuna sababu ambazo ndizo zilizochangia kwa kiasi kikubwa matatizo mengine ya uharibifu wa siku hiyo ya tarehe 30 may 2008. sababu hizo nihizi zifuatazo
- kauli chafu kwa wanafunzi wa kidato cha sita zilizotolewa na mwalimu charles Ntimi tarehe 29/may/2008 siku moja kabla ya matatizo hayo kutokea. Mwalimu huyo ambaye ndiye aliyepigwa alikuwa katika mtafaruku na wanafunzi hivyo tulihitaji kuongea na mkuu wa shule kumueleza suala hilo ili amrekebishe lakini ikaonekana bado hayuko tayari kutusikiliza hivyo kusababisha hasira kwa wanakidato cha sita.
- Mwalimu huyo kikazi alikua bado ni mgeni na alipanga kuwagawanya wanafunzi wa kidato cha sita kwa kutumia system ya devide and rule. Kitu ambacho kiliwakera wanakidato cha sita; kwa kuwaonyesha dhamira zake kikazi. Kwa maamuzi ya utendaji huo wa mwalimu huyo na viongozi wa serikali ya wanafunzi tuliwekwa katika wakati mgumu kimaamuzi) wakiwa katika nafasi ya kutengwa mbali na wanaowaongoza.
- Iliyokuwa serikali ya wanafunzi shuleni hapo haikupewa nafasi ya kusikilizwa na kuombwa ushauri katika maamuzi ya utawala viongozi hao katika wakati mgumu kiusalama na kuamua kujiudhuru ili kujisalimisha.
Kulingana na matatizo hayo pia tuliomba mkuu wa shule tuongee nae ili kumueleza matatizo yetu lakini alikataa hatua ya kutokukubali kuongea nasi na kutoa kauli ambayo ndiyo ilileta hasira kwetu na kuona hatuna mtetezi mwingine maeneo yale. Alisema “form six hadi sasa nimewatema, sio headmaster wao tena , bebeni vitu vyenu nendeni popote mnapo hisi mtasikilizwa” baada ya hapo ndipo wanafunzi wa kidato cha sita walipokasirka na kufanya uharibifu wakati mwalimu Charles Ntimi anatafutwa aliyekuwa amejificha katika jengo la utawala. Hivyo ilikuwa katika kumtafuta mwalimu huyo ambapo ndipo vioo vya jengo la utawala vilivunjwa, milango na mila ya umeme, Computer moja, Typing machine na kuvunja vitu vya stoo ya chakula. Hivyo ndivyo vitu ambavyo kwa mtazamo wetu tunatambua viriharibiwa na tunadhani vilihesabiwa katika uharibifu huo.
- kulingana na maamuzi ya bodi ya shule imetangaza kuwa hasara ya uharibifu huo ni wa thamani ya zaidi ya Tsh milioni arobaini, gharama ambayo hatujakubaliana nalo.
- Pia imedaiwa kuwa aliibiwa zaidi ya shilingi laki saba ambazo zilikuwa katika moja ya ofisi ya shule. Kwa sheria tunaamini kuwa hakuna sheria inayohusu pesa ya serikali kukaa ofisini zaidi ya kila moja. Hivyo tunapinga mashtaka ya bodi kwa kwa suala hilo.
- Bodi hiyo imetoa adhabu ya kuwafuta shule wanafunzi themanini na watatu (83), na kuwarudisha wanafunzi sabini na nne (78) ambao watalipa fidia ya shilingi laki nne na nusu (Tsh 450,000/=) pia hatujakubaliana na maamuzi hayo kwa upande wa bodi kwani hatujajua wametumia mbinu ipi kuwapata hao sabini na nne kuwa si waharifu katika tukio hilo, ilihali hawajatuhoji sisi kama wahusika. Hivyo tunaomba ofisi yako tukufu ifuatilie mashauri yaliyofanywa na bodi ya shule, kwani haijafuata haki. Pia adhabu iliyotolewa ni ngumu kwa wazazi wetu wa hali ya kati kiuchumi.
- Pia tunapingana na kauli iliyotolewa na vyombo vya habari kuwa tulichapa walimu wetu viboko kama ilivyotangazwa. Mwalimu aliyepigwa ni mmoja tu Mwalimu Charles Ntimi na si walimu wote kama invyotangazwa. Hata mwalimu huyo alipigwa kulingana na hali tuliyojengewa na mkuu wa shule kwa kutotusikiliza.
- Pia tumedharirishwa na vyombo vya habari kuwa tulivuta bangi kwa takribani masaa manne. Shutuma hizo tunazipanga na tuko tayari kupimwa afya zetu ili kubaini kauli hiyo. Huo ni udhalilishwaji wa hari ya juu kwa wasomi kama sisi.
Ombi letu kwa Ofisi yako ni kwamba Tunaomba tume au ofisi teule iondoe ili ichunguze kwa undani sababu za matatizo hayo na wanafunzi waliofukuzwa shule warudishwe na uchunguzi ufanywe katika gharama za uharibifu, zitajwe upya baada ya kamati ya uchunguzi kumaliza kazi yake.
Wako Watiifu
Wana wa kidato cha sita shule ya sekondari Mwakaleli
COMMENTS