MTANDAO WA JINSIA TANZANIA (TGNP) TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI NI BAJETI YA MFUMUKO!! Bajeti kitendawili Hapana shaka Watanzania wengi wali...
MTANDAO WA JINSIA TANZANIA (TGNP)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
NI BAJETI YA MFUMUKO!!
Bajeti kitendawili
Hapana shaka Watanzania wengi walitarajia kwamba Bajeti ya mwaka huu ingekuja na mikakati thabiti ya kukabili changamoto mbalimbali zinazoikabili serikali yetu na watanzania wote kwa ujumla., changamoto hizi ni pamoja na kuzidi kutanuka kwa tabaka la walalahoi na wenye vijisenti miongoni mwa jamii yetu, hasa eneo la kupatiwa huduma muhimu za jamii, na maisha bora, uporaji wa rasilimali adhimu unaofanywa na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kwa mgongo wa viongozi wa ngazi za juu serikalini, kukithiri kwa ubadhirifu wa fedha na mali ya umma, uchumi tegemezi wenye shinikizo na masharti toka kwa wafadhili, pamoja na kukithiri kwa ufisadi na ukiritimba katika ngazi zote za serikali.
swali ni je, ni kwa vipi Bajeti hii ya 2008/09 itatatua changamoto hizi na kukidhi matarajio ya Watanzania?Jibu ni hapana kama tunavyochanganua katika taarifa yetu ifuatayo:
Mapato na Utegemezi wa misaada ya nje.
Tunaipongeza serikali kwa kupunguza utegemezi wa misaada ya nje toka asilimia 42 mwaka jana hadi 34% katika bajeti ya mwaka huu, hata hivyo kiwango hiki bado ni zaidi ya theluthi moja ya Bajeti yote na kujiuliza punguzo hili la utegemezi lina mantiki gani Ikiwa 62% ya bajeti ya maendeleo hutegemea michango ya wafadhili na wahisani mbalimbali pamoja na changamoto na vipaumbele vinavyo ikabili?
Bajeti hii imeainisha kwamba 62% ya mapato yote yatatokana na na kodi, kiasi kikubwa ikiwa ni kodi itakayolipwa na wake kwa waume wanaofanya kazi katika sekta ya umma, wengi wao wakiwa ni wale wanatozwa kodi zaidi ya isivyostahiki. tunatoa mwito wa kupunguzwa kwa kiasi kikubwa cha kiwango cha kodi katika ngazi zote, mapendekezo yetu yakiwa ni kuanzia 10% kwa mapato ya kati ya shilingi 100,001 hadi 360,000: 20% kwa kati ya 720,000 hadi 3,000,000 : na mstari mpya wa 30-40% kwa wenye kipao cha zaidi ya shilingi 3,000,000
Tunaona kwamba rasilimali mbadala zingeweza kupatikana kama serikali ingeongeza lengo la toka 3% kutoka kwenye mapato yasiyo ya kodi hadi angalau 6% kukidhi madai ya wabunge pamoja na wanachi kwa ujumla.
hata hivyo tunaiona athari kubwa ya utegemezi wa misaada ya nje bado inaendelea kuwa ni shinikizo la wafadhili katika utungaji wa sera pamoja na ushirki wao katika mchakato mzima wa bajeti na jinsi wanavyoshinikiza sera ya uchumi mkubwa wa masoko huria kwa serikali yetu.
Upande wa matumizi.
Mapendekezo ya kutumia shilingi 7.1 trilioni ni kiasi kikubwa sana kwa maoni yetu, Serikali inatakiwa kwa dhati na makini kabisa kupunguza idadi ya wizara na mawaziri na kuhakikisha kwamba kila mtumishi wa umma anafanya kazi kwa ufanisi kuleta tija na kuthaminiwa kazi yake badala ya kuwa ni mzigo kwa mlipa kodi mlalahoi na Taifa kwa ujumla, tunazidi kusisitiza kwamba serikali iongeze rasilimali zaidi mbali ya watumishi walio katika sekta nyeti za huduma, wakiwemo waalimu, wauguzi,wataalamu wa maabara na maafisa kilimo hususan mabwana shamba.
kwamba asilimia 14 ya bajeti yetu imelenga kulipa madeni-huu ni upande mwingine wa utegemezi wa wafadhili na wahisani.
Kuongezeka kwa rasilimali kulikotaarifiwa kutahamishiwa kutoka kwenye sekta kuu ya wizara za serikali (52% katika bajeti) kwenda kwa mikoa (2%) na wilaya (19%) mamlaka za serikali-kimsingi kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii ni hatua nzuri lakini bado hatujaisahau Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa serikali iliyofichua ubadhirifu na ufujaji mkubwa wa fedha za serikali katika Halmashauri zetu, tunaona kwamba ufumbuzi ni kuwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kusimamia Matumizi ya Serikali kama ilivyo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) lengo ikiwa ni kutokomeza ufisadi
swali moja la mwisho: 8% ya Bajeti kutengwa kwa "matumizi maalum"-tunajiuliza ni yapi? na kwa nini? Tunakemea vikali na hatutaki tena ufisadi!!
Tunapongeza uamuzi wa serikali kutenga karibu theluthi mbili ya bajeti yote (64%) kwa ajili ya sekta zenye kipaumbele ambazo ni elimu, miuondombinu, maji, afya kilimo na nishati.Hata hivyo tungependa kujua ni kwa jinsi gani mgawanyo wa rasilimali hizi adimu utakavyokwenda kwa kila sekta?, kwamba ni nani atakayefaidika?, ni nani hatahusishwa/husishwa na la muhimu zaidi hatua gani zitachukuliwa kuhakikisha kila sekta inarekebisha kutanuka kwa wigo wa tabaka na upendeleo katika utoaji wa huduma kwa bora kwa jamii?
katika hili mkazo wetu utakuwa ni kwenye sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na ufugaji, sekta inayoonyesha kuwa na mchango mkubwa kwenye changamoto ya ajira/kuwezesha wananchi kujikimu kimaisha na hivyo kuchangia katika ukuaji wa uchumi na pato la Taifa (soma makala yetu katika gazeti la The Citizen la Juni 11, 2008) Tunapigania sana ushirikishwaji wa wananchi unaozingatia na kulenga katika kuwakomboa kiuchumi hasa wakulima wadogowadogo (peasant farmers) ambapo wengi wao wakiwa ni wake kwa waume wamejiajiri/kuajiriwa, badala ya kusisitiza mkakati wa kuwekeza katika sekta kubwa ya kilimo. kama ilivyo sasa. Wakisha kujiundia ushirika wao, rasilimali kubwa itahitajika kuwekezwa katika kufanya tafiti, kutoa mikopo, kupanua wigo wa wataalamu, kutafuta na au kuimarisha masoko kutoa ruzuku na kuweka mfumo wa bei.
Hatua madhubuti zinahitajika ili kuthamini na kurasimisha kazi zisizo na malipo wanazofanya wanawake (free female labour) ambazo kimtazamo hazina malipo (unpaid work) na ambapo wanawake (kwa kiasi kikubwa) hubebeshwa mzigo huo na jamii, kazi hizo ni kama vile kupika, kuchota maji, kutafuta kuni na nishati nyingine za majumbani, kulea watoto, na kutunza wagonjwa na wazee majumbani. Tunaamini utatuzi wa suala hili utawezekana kwa kuwa na teknolojia mbadala na kuwa na mipango na mikakati ya utoaji wa huduma za jamii katika maeneo ya makazi ya watu.
Rasilimali zaidi zinaweza kuelekezwa katika kuboresha usafiri maeneo ya vijijini ili kupunguza ubebaji wa mizigo kichwani na pia kuunganisha na masoko ya mazao ilihali mkakati wa kuwa na viwanda vya Taifa vya kusindika mazao ya kilimo na upatikanaji wa nyenzo kuzalisha pembejeo za kilimo kwa upande mmoja, lakini piakupata malighafi na chakula kwa upande mwingine.
Sekta ya kilimo
Kumekuwepo na shinikizo toka kwa wafadhili na mashirika yaliyo katika sekta binafsi kwa mkakati wa kuwekeza mitaji kwenye mashamba makubwa na kuonekana kuungwa mkono na bajeti hii, (hitaji la mashamba makubwa ya umwagilaji) maoni yetu ni kwamba kwa kufanya hivi ni sawa na kukaribisha dhahama kwani wakulima binafsi wadogowadogo waliojiajiri wana hatari ya kukosa kukaribia ardhi kwa kuwa vibarua kwenye mashamba hayo, mfano tumeuona katika mashamba ya miwa ya Turiani Morogoro, ambapo watoto wao wengi huajiriwa katika miji ya jirani kama watumishi wa baa, wafanyabiashara ya ngono, watumishi wa ndani, wamachinga au mama lishe, hadi wanapotekwa kwenda mijini zaidi, je uu ndio mpango wa serikali kwa mustakabali wa wanachi wa vijijini? Je wataendelea kukubaliana na hali hii wataiga ya wajoli wao yanayojiri Kenya na Afrika Kusini?
Maji safi na maji taka!
nia ya serikali ya kupunguza bajei katika sekta ya maji kwa 40% kutoka 5% mwaka jana hadi 3% mwaka huu imetushtua sana! tunatoa mwito kwa kilio cha watu wote kudai zaidi na si rasiliumali pungufu katika sekta ya maji,. Tunapozungumza, wananchi wengi waishio vijijini wamesahaulika katika kupata huduma ya maji safi na salama na kuimarisha huduma ya maji machafu ukilinganisha na wqakazi wa mijini, kwa mujibu wa rioti ya umaskini na maendeleo ya Binadamu (PHDR 2007) ni moja ya tano tu ya kaya za vijijini zinazoweza kupata huduma ya maji ya bomba na hifadhi ya maji na nyingine 12% wakiwa na huduma ya hifadhi ya maji.
Zaidi ya yote chini ya nusu ya kaya za Watanzania wote (47%) wana hudima ilyoimarika ya maji taka, miaka 47 baada ya Uhuru. (PHDR 2007 UK. 46)! Maji ni miongoni mwa vipaumbele vikuu kwa wasichana/wanawake, si kwa sababu tu kwamba wao ndio wachotaji wakuu wa maji katika kaya, wakiwa wanalazimika kutembea umbali mrefu huku wakibeba maji vichwani mwao bali kwaa sababu ya majukumu yao kedekede katika kaya kama vile kupika, kuuguza, usafi pamoja na kazi nyingine za nyumbani kama matoke ya mgawanyo wa kazi kijinsia.
Masuala Mtambuka
kwa nini Bajeti imekua kimya juu ya masuala ya UKIMWI, wanawake, vijana, walemavu, mazingira na masuala mengine mtambuka ya kipaumbele? masuala haya yaanatakiwa kuchukuliwa kwa uzito wa pekee ili yasije kuzamishwaa kwenye "muongo mpya wa fedha" wa misaada na mikopo ya bajeti (General Budget Support)
Mgawanyo wa kipato
Tunatoa mwito wa mkakati dhabit wa kuhakikisha mgawanyo sawa wa kipato mijini na vijijini. Ripoti ya hivi karibuni ya (PHDR 2007) imeonyesha kwamba 25% ya Watanzania wote walikuwa wanaishi katika hali ya umasikini mwaka 2007, kama ilivyotafitiwa kwenye matumizi ya kila kaya kwa kila mkazi (per capital household consumption)
Ajira na maisha Bora
bajeti hii haina mkakati wa jinsi ya kuwezesha ajira na uhakika wa maisha bora, kwa mujibu wa PHDR uk. 11 hali ya watu wasio na ajira ni mbaya sana maeneo ya mijini kwa kila mmoja lakini hasa kwa wanawake na vijana. 40% ya wanawake katika Jiji la Dar es salaam na 19% katika maeneo mengine ya mijini hawana ajira ukilinganisha na wanaume 23% kwa Dar es salaam na 14% kwa mikoani.
Nyanja nyingine ya ajira ni kiasi kikubwa cha wanawake wanaofanya kazi zisizo na malipo(unpaid work) zaidi kuliko wanaume majumbani, kama ilivyoainishwa katika utafiti wa hivi karibuni wa tathmini ya muda unaotumika kwa kazi hizo (time use study), kazi hizi zinahitaji kuthaminiwa hesabu za fedha na kujumuishwa katika pato la Taifa, ilihali sera/mikakati mahususi ikiundwa na kuendelezwa ili kutoa rasilimali zaidi kupunguza kiasi cha kazi zisizo na malipo kwenye huduma za msingi za matunzo kama vile malezi ya mtoto, kupika, kuchota maji na kukata kuni, kuuza wagonjwa/kutunza wazee na nyinginezo.
mfumo wa maamuzi
hotuba ya bajeti katika sehemu mbalimbali imgusia umuhimu wa sekta binafsi katika kufanikisha kufikia malengo ya bajeti, lakini kwa kiasi kidogo au kama vile hakuna mahali ambapo imeeleza mchango wa asasi za kiraia zikiwemo zile ndogondogo na zile zenye kampeni za kitaifa za ushawishi na utetezi, ukiachilia mbali mchango wa taasisi za kidini katika utoaji wa huduma. Hatua nzuri imechukuliwa katika kuzishirikisha asasi za kiraia kwenye mchakato mzima wa bajeti-matarajio yetu ni kuona muendelezo wa ushiriki katika mchakato wa kuandaa bajeti na ufuatiliaji wa mapato na matumizi ya bajeti katika ngazi zote, ukihusisha Wananchi-nyenzo pia ya kuhakikisha kwamba hii kweli ni Bajeti ya Wananchi!!!!!
Imesainiwa na
..............................
Usu Mallya
Mkurugenzi Mtendaji
Mtandao wa Jinsia Tanzania
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
NI BAJETI YA MFUMUKO!!
Bajeti kitendawili
Hapana shaka Watanzania wengi walitarajia kwamba Bajeti ya mwaka huu ingekuja na mikakati thabiti ya kukabili changamoto mbalimbali zinazoikabili serikali yetu na watanzania wote kwa ujumla., changamoto hizi ni pamoja na kuzidi kutanuka kwa tabaka la walalahoi na wenye vijisenti miongoni mwa jamii yetu, hasa eneo la kupatiwa huduma muhimu za jamii, na maisha bora, uporaji wa rasilimali adhimu unaofanywa na wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kwa mgongo wa viongozi wa ngazi za juu serikalini, kukithiri kwa ubadhirifu wa fedha na mali ya umma, uchumi tegemezi wenye shinikizo na masharti toka kwa wafadhili, pamoja na kukithiri kwa ufisadi na ukiritimba katika ngazi zote za serikali.
swali ni je, ni kwa vipi Bajeti hii ya 2008/09 itatatua changamoto hizi na kukidhi matarajio ya Watanzania?Jibu ni hapana kama tunavyochanganua katika taarifa yetu ifuatayo:
Mapato na Utegemezi wa misaada ya nje.
Tunaipongeza serikali kwa kupunguza utegemezi wa misaada ya nje toka asilimia 42 mwaka jana hadi 34% katika bajeti ya mwaka huu, hata hivyo kiwango hiki bado ni zaidi ya theluthi moja ya Bajeti yote na kujiuliza punguzo hili la utegemezi lina mantiki gani Ikiwa 62% ya bajeti ya maendeleo hutegemea michango ya wafadhili na wahisani mbalimbali pamoja na changamoto na vipaumbele vinavyo ikabili?
Bajeti hii imeainisha kwamba 62% ya mapato yote yatatokana na na kodi, kiasi kikubwa ikiwa ni kodi itakayolipwa na wake kwa waume wanaofanya kazi katika sekta ya umma, wengi wao wakiwa ni wale wanatozwa kodi zaidi ya isivyostahiki. tunatoa mwito wa kupunguzwa kwa kiasi kikubwa cha kiwango cha kodi katika ngazi zote, mapendekezo yetu yakiwa ni kuanzia 10% kwa mapato ya kati ya shilingi 100,001 hadi 360,000: 20% kwa kati ya 720,000 hadi 3,000,000 : na mstari mpya wa 30-40% kwa wenye kipao cha zaidi ya shilingi 3,000,000
Tunaona kwamba rasilimali mbadala zingeweza kupatikana kama serikali ingeongeza lengo la toka 3% kutoka kwenye mapato yasiyo ya kodi hadi angalau 6% kukidhi madai ya wabunge pamoja na wanachi kwa ujumla.
hata hivyo tunaiona athari kubwa ya utegemezi wa misaada ya nje bado inaendelea kuwa ni shinikizo la wafadhili katika utungaji wa sera pamoja na ushirki wao katika mchakato mzima wa bajeti na jinsi wanavyoshinikiza sera ya uchumi mkubwa wa masoko huria kwa serikali yetu.
Upande wa matumizi.
Mapendekezo ya kutumia shilingi 7.1 trilioni ni kiasi kikubwa sana kwa maoni yetu, Serikali inatakiwa kwa dhati na makini kabisa kupunguza idadi ya wizara na mawaziri na kuhakikisha kwamba kila mtumishi wa umma anafanya kazi kwa ufanisi kuleta tija na kuthaminiwa kazi yake badala ya kuwa ni mzigo kwa mlipa kodi mlalahoi na Taifa kwa ujumla, tunazidi kusisitiza kwamba serikali iongeze rasilimali zaidi mbali ya watumishi walio katika sekta nyeti za huduma, wakiwemo waalimu, wauguzi,wataalamu wa maabara na maafisa kilimo hususan mabwana shamba.
kwamba asilimia 14 ya bajeti yetu imelenga kulipa madeni-huu ni upande mwingine wa utegemezi wa wafadhili na wahisani.
Kuongezeka kwa rasilimali kulikotaarifiwa kutahamishiwa kutoka kwenye sekta kuu ya wizara za serikali (52% katika bajeti) kwenda kwa mikoa (2%) na wilaya (19%) mamlaka za serikali-kimsingi kuboresha utoaji wa huduma kwa jamii ni hatua nzuri lakini bado hatujaisahau Ripoti ya Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa serikali iliyofichua ubadhirifu na ufujaji mkubwa wa fedha za serikali katika Halmashauri zetu, tunaona kwamba ufumbuzi ni kuwa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kusimamia Matumizi ya Serikali kama ilivyo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) lengo ikiwa ni kutokomeza ufisadi
swali moja la mwisho: 8% ya Bajeti kutengwa kwa "matumizi maalum"-tunajiuliza ni yapi? na kwa nini? Tunakemea vikali na hatutaki tena ufisadi!!
Tunapongeza uamuzi wa serikali kutenga karibu theluthi mbili ya bajeti yote (64%) kwa ajili ya sekta zenye kipaumbele ambazo ni elimu, miuondombinu, maji, afya kilimo na nishati.Hata hivyo tungependa kujua ni kwa jinsi gani mgawanyo wa rasilimali hizi adimu utakavyokwenda kwa kila sekta?, kwamba ni nani atakayefaidika?, ni nani hatahusishwa/husishwa na la muhimu zaidi hatua gani zitachukuliwa kuhakikisha kila sekta inarekebisha kutanuka kwa wigo wa tabaka na upendeleo katika utoaji wa huduma kwa bora kwa jamii?
katika hili mkazo wetu utakuwa ni kwenye sekta ya kilimo ikiwa ni pamoja na ufugaji, sekta inayoonyesha kuwa na mchango mkubwa kwenye changamoto ya ajira/kuwezesha wananchi kujikimu kimaisha na hivyo kuchangia katika ukuaji wa uchumi na pato la Taifa (soma makala yetu katika gazeti la The Citizen la Juni 11, 2008) Tunapigania sana ushirikishwaji wa wananchi unaozingatia na kulenga katika kuwakomboa kiuchumi hasa wakulima wadogowadogo (peasant farmers) ambapo wengi wao wakiwa ni wake kwa waume wamejiajiri/kuajiriwa, badala ya kusisitiza mkakati wa kuwekeza katika sekta kubwa ya kilimo. kama ilivyo sasa. Wakisha kujiundia ushirika wao, rasilimali kubwa itahitajika kuwekezwa katika kufanya tafiti, kutoa mikopo, kupanua wigo wa wataalamu, kutafuta na au kuimarisha masoko kutoa ruzuku na kuweka mfumo wa bei.
Hatua madhubuti zinahitajika ili kuthamini na kurasimisha kazi zisizo na malipo wanazofanya wanawake (free female labour) ambazo kimtazamo hazina malipo (unpaid work) na ambapo wanawake (kwa kiasi kikubwa) hubebeshwa mzigo huo na jamii, kazi hizo ni kama vile kupika, kuchota maji, kutafuta kuni na nishati nyingine za majumbani, kulea watoto, na kutunza wagonjwa na wazee majumbani. Tunaamini utatuzi wa suala hili utawezekana kwa kuwa na teknolojia mbadala na kuwa na mipango na mikakati ya utoaji wa huduma za jamii katika maeneo ya makazi ya watu.
Rasilimali zaidi zinaweza kuelekezwa katika kuboresha usafiri maeneo ya vijijini ili kupunguza ubebaji wa mizigo kichwani na pia kuunganisha na masoko ya mazao ilihali mkakati wa kuwa na viwanda vya Taifa vya kusindika mazao ya kilimo na upatikanaji wa nyenzo kuzalisha pembejeo za kilimo kwa upande mmoja, lakini piakupata malighafi na chakula kwa upande mwingine.
Sekta ya kilimo
Kumekuwepo na shinikizo toka kwa wafadhili na mashirika yaliyo katika sekta binafsi kwa mkakati wa kuwekeza mitaji kwenye mashamba makubwa na kuonekana kuungwa mkono na bajeti hii, (hitaji la mashamba makubwa ya umwagilaji) maoni yetu ni kwamba kwa kufanya hivi ni sawa na kukaribisha dhahama kwani wakulima binafsi wadogowadogo waliojiajiri wana hatari ya kukosa kukaribia ardhi kwa kuwa vibarua kwenye mashamba hayo, mfano tumeuona katika mashamba ya miwa ya Turiani Morogoro, ambapo watoto wao wengi huajiriwa katika miji ya jirani kama watumishi wa baa, wafanyabiashara ya ngono, watumishi wa ndani, wamachinga au mama lishe, hadi wanapotekwa kwenda mijini zaidi, je uu ndio mpango wa serikali kwa mustakabali wa wanachi wa vijijini? Je wataendelea kukubaliana na hali hii wataiga ya wajoli wao yanayojiri Kenya na Afrika Kusini?
Maji safi na maji taka!
nia ya serikali ya kupunguza bajei katika sekta ya maji kwa 40% kutoka 5% mwaka jana hadi 3% mwaka huu imetushtua sana! tunatoa mwito kwa kilio cha watu wote kudai zaidi na si rasiliumali pungufu katika sekta ya maji,. Tunapozungumza, wananchi wengi waishio vijijini wamesahaulika katika kupata huduma ya maji safi na salama na kuimarisha huduma ya maji machafu ukilinganisha na wqakazi wa mijini, kwa mujibu wa rioti ya umaskini na maendeleo ya Binadamu (PHDR 2007) ni moja ya tano tu ya kaya za vijijini zinazoweza kupata huduma ya maji ya bomba na hifadhi ya maji na nyingine 12% wakiwa na huduma ya hifadhi ya maji.
Zaidi ya yote chini ya nusu ya kaya za Watanzania wote (47%) wana hudima ilyoimarika ya maji taka, miaka 47 baada ya Uhuru. (PHDR 2007 UK. 46)! Maji ni miongoni mwa vipaumbele vikuu kwa wasichana/wanawake, si kwa sababu tu kwamba wao ndio wachotaji wakuu wa maji katika kaya, wakiwa wanalazimika kutembea umbali mrefu huku wakibeba maji vichwani mwao bali kwaa sababu ya majukumu yao kedekede katika kaya kama vile kupika, kuuguza, usafi pamoja na kazi nyingine za nyumbani kama matoke ya mgawanyo wa kazi kijinsia.
Masuala Mtambuka
kwa nini Bajeti imekua kimya juu ya masuala ya UKIMWI, wanawake, vijana, walemavu, mazingira na masuala mengine mtambuka ya kipaumbele? masuala haya yaanatakiwa kuchukuliwa kwa uzito wa pekee ili yasije kuzamishwaa kwenye "muongo mpya wa fedha" wa misaada na mikopo ya bajeti (General Budget Support)
Mgawanyo wa kipato
Tunatoa mwito wa mkakati dhabit wa kuhakikisha mgawanyo sawa wa kipato mijini na vijijini. Ripoti ya hivi karibuni ya (PHDR 2007) imeonyesha kwamba 25% ya Watanzania wote walikuwa wanaishi katika hali ya umasikini mwaka 2007, kama ilivyotafitiwa kwenye matumizi ya kila kaya kwa kila mkazi (per capital household consumption)
Ajira na maisha Bora
bajeti hii haina mkakati wa jinsi ya kuwezesha ajira na uhakika wa maisha bora, kwa mujibu wa PHDR uk. 11 hali ya watu wasio na ajira ni mbaya sana maeneo ya mijini kwa kila mmoja lakini hasa kwa wanawake na vijana. 40% ya wanawake katika Jiji la Dar es salaam na 19% katika maeneo mengine ya mijini hawana ajira ukilinganisha na wanaume 23% kwa Dar es salaam na 14% kwa mikoani.
Nyanja nyingine ya ajira ni kiasi kikubwa cha wanawake wanaofanya kazi zisizo na malipo(unpaid work) zaidi kuliko wanaume majumbani, kama ilivyoainishwa katika utafiti wa hivi karibuni wa tathmini ya muda unaotumika kwa kazi hizo (time use study), kazi hizi zinahitaji kuthaminiwa hesabu za fedha na kujumuishwa katika pato la Taifa, ilihali sera/mikakati mahususi ikiundwa na kuendelezwa ili kutoa rasilimali zaidi kupunguza kiasi cha kazi zisizo na malipo kwenye huduma za msingi za matunzo kama vile malezi ya mtoto, kupika, kuchota maji na kukata kuni, kuuza wagonjwa/kutunza wazee na nyinginezo.
mfumo wa maamuzi
hotuba ya bajeti katika sehemu mbalimbali imgusia umuhimu wa sekta binafsi katika kufanikisha kufikia malengo ya bajeti, lakini kwa kiasi kidogo au kama vile hakuna mahali ambapo imeeleza mchango wa asasi za kiraia zikiwemo zile ndogondogo na zile zenye kampeni za kitaifa za ushawishi na utetezi, ukiachilia mbali mchango wa taasisi za kidini katika utoaji wa huduma. Hatua nzuri imechukuliwa katika kuzishirikisha asasi za kiraia kwenye mchakato mzima wa bajeti-matarajio yetu ni kuona muendelezo wa ushiriki katika mchakato wa kuandaa bajeti na ufuatiliaji wa mapato na matumizi ya bajeti katika ngazi zote, ukihusisha Wananchi-nyenzo pia ya kuhakikisha kwamba hii kweli ni Bajeti ya Wananchi!!!!!
Imesainiwa na
..............................
Usu Mallya
Mkurugenzi Mtendaji
Mtandao wa Jinsia Tanzania
COMMENTS