Karume ataka Wazanzibari wadumishe amani

RAIS Amani Abeid Karume amewataka waislamu kushikilia msingi wa amani uliokuwapo katika kipindi chote cha mfungo wa Ramadhan kwa kujali zaidi utulivu, amani na usalama wa nchi badala ya shari na vurugu.
Akihutubia Baraza la Idd katika sherehe za Idd el Fitr visiwani hapa leo Rais Karume alisema Waislamu wana wajibu mkubwa wa kuendeleza mema yanayozingatia amani na maadili yaliyopatikana katika mfungo mwezi Mtukufu wa Ramadhan .
Aidha Rais alionya dhidi ya tabia ya waumini wachache kutumia sherehe za Idd kama nafasi ya kurudia maovu na kusisitiza kuwa matendo hayo ni kuudhalilisha Uislamu na pia Mtume Muhamad pamoja na taifa lote.
“Tuendeleze kustahamiliana na kuvumiliana, kukuza upendo kati yetu katika jamii moja, kuheshimu tabia na taratibu za sheria za dini na nchi; na zaidi ya yote kuendelea kusaidiana katika shughuli zetu za maisha,” alisema.
Akihutubia Baraza la Idd katika sherehe za Idd el Fitr visiwani hapa leo Rais Karume alisema Waislamu wana wajibu mkubwa wa kuendeleza mema yanayozingatia amani na maadili yaliyopatikana katika mfungo mwezi Mtukufu wa Ramadhan .
Aidha Rais alionya dhidi ya tabia ya waumini wachache kutumia sherehe za Idd kama nafasi ya kurudia maovu na kusisitiza kuwa matendo hayo ni kuudhalilisha Uislamu na pia Mtume Muhamad pamoja na taifa lote.
“Tuendeleze kustahamiliana na kuvumiliana, kukuza upendo kati yetu katika jamii moja, kuheshimu tabia na taratibu za sheria za dini na nchi; na zaidi ya yote kuendelea kusaidiana katika shughuli zetu za maisha,” alisema.
Pichani ni Waziri kiongozi mstaafu wa Zanzibar Maalim Seif Shariff Hamadi (katikati) akibadilishana mawazo na Wastaafu wenzake DK Moh'd Gharib Bilali (kushoto) na Ramadhani Haji Faki Kwenye Baraza la Idd lililofanyika kwenye Hoteli ya Bwawani Mjini Zanzibar leo.Picha hii ni Martin kabemba.


1 Comments:
Good good good......
Post a Comment
Subscribe to Post Comments [Atom]
Links to this post:
Create a Link
<< Home