Haya ni makala ya mahojiano kuhusu suala la bima ya afya kama yalivyofanywa na TBC 1 na watu wa bima ya afya nchini. Makala hii nimeitafuta...
Haya ni makala ya mahojiano kuhusu suala la bima ya afya kama yalivyofanywa na TBC 1 na watu wa bima ya afya nchini. Makala hii nimeitafuta na kuiweka ili kuiwekea rekodi ya kimaandishi juu ya juhudi za kuhifadhi afya ya Watanzania kwa kuangalia mwenendo wa wenzetu.Chati ya maelekezo ya nini Obama alikuwa anafikiria katika afya na McCain sikuweza kuiweka hapa kwani inanisumbua kiutendaji.Bwana mdogo mmoja akizuka mitaa yangu atanisaidia kuiweka chati hiyo.Nawasilisha.
Swali
Moja katika ya mambo ambayo yamejitokeza na kuvuta zaidi hisia za watu wengi katika kampeni za uchaguzi za Marekani, ni suala la Bima ya Afya. Kwanini sasa au kwa nini suala hili limejitokeza kwa nguvu zaidi katika kampeni za mwaka huu pengine kuliko ilivyokuwa miaka mingine ya nyuma;
Majibu
Suala la Afya linagusa maisha ya watu moja kwa moja. Watu wanapokuwa na Bima ya Afya wanakuwa makini zaidi kufuatilia, hasa kwa nchi kama Marekani ambako ni Taifa. Hapa nchini watu sasa wana Bima ya Afya hivyo wanakuwa makini zaidi kujua kinachofanyika katika nchi nyingine hasa Marekani ambayo ni Taifa kubwa; Kwa Wamarekani wenyewe suala hili limekuwa Ni agenda kubwa kwa sababu zifuatazo hasa katika kipindi hiki:-
· Zaidi ya Wamarekani milioni 45 hawana Bima ya Afya isipowa wachache wenye Bima za Binafsi (2007)
· Kuna kinamama takribani milioni 17 (wenye umri kati ya miaka 18-64) ambao hawana Bima ya afya yoyote;
· Wengi wa wasio na vipato wanalazimika kununua huduma wakati wanaihitaji (out-of-pocket) ambazo ni ghali;
· Mfumo wa matibabu uliopo kwa kiasi kikubwa ni wa Bima za Afya za Binafsi ambao ni ghali zaidi kwa hiyo ni watu wachache sana ndio wanaohudumiwa;
· Hofu ya gharama za matibabu (health shocks) zinawafanya watu wasio na ajira za kudumu inawaathiri wengi kisaikolojia na wanapougua wengi wanalazimika kuuza vitu vya ndani. Sasa hivi watu wameanza kuelewa kuwa jambo linalotokea sehemu moja ya dunia linakuwa na madhara au faida kwa sehemu nyingine au sehemu zote za dunia. Na linapokuja suala la Taifa kubwa kama Marekani kila mmoja anakuwa makini.
Swali
Ukiwa kama Mwenyekiti wa kamati ya kamisheni ya dunia kuhusu Mifuko ya Bima ya Afya katika Taasisi ya kimataifa ya Hifadhi ya Jamii Duniani. unaonaje Maendeleo yaliyofikiwa kwa sasa katika sekta hii ya Afya.
Majibu
Maendeleo yaliyofikiwa sisi katika kamisheni yetu tunaona tumepiga hatua kubwa tangu kabla sijaingia, mpaka nilipokuwa makamu wa mwenyekiti miaka mitatu iliyopita na sasa kama mwenyekiti. Mafanikio:
· Nchi nyingi zaidi ya 150 sasa ni wanachama wa Taasisi ya kimataifa ya hifadhi ya Jamii ambayo masuala haya yanajadiliwa na kubadilishana uzoefu kwa kina;
· Nchi nyingi hasa za Afrika ambazo kwa kipindi kirefu zilikuwa hazina mipango ya Bima ya Afya sasa zimeanza japo chache na nyingine ingawa hazijaanza suala hili wanalijadili na wamo kwenye mchakato mfano Uganda,Zambia na Malaysia;
· Sasa hivi kumekuwa na juhudi za pamoja hata katika ngazi ya kimataifa. Mashirika na Taasisi kubwa kama ILO, GTZ, WB, WHO sasa hivi wanafanya mikutano ya pamoja kujadili suala la Bima ya Afya. Mwanzoni kila taasisi ilikuwa inafanya peke yake;
· Bima za Afya zimesaidia sio tuu kupunguza mzigo kwa serikali katika bajeti za Afya lakini pia zimekuwa kichocheo cha maendeleo. Wanajenga Hospitali (Korea Kusini), wanafungua maduka ya dawa (Rwanda), wanachangia bajeti ya afya mpaka asilimia 80 (costa Rica) hii ni kwa manufaa ya wanachama wa Mifuko na wananchi wengine.
· Bima za Afya ndio limekuwa kimbilio la watu wa hali ya chini na kipato cha wastani kwa sababu ya kupanda kwa gharama za matibabu siku hadi siku. Na hii ni kwa dunia nzima. · Serikali na hasa viongozi wa Kitaifa wao ndio wamekuwa wasimamizi na waelimishaji wakubwa wa huduma hii. Hii inaonyesha umuhimu wa suala lenyewe. Mfano hapa nchi kwetu tangu awamu ya tatu hadi sasa Mheshimiwa Rais huwa anaongelea suala la Vitambulisho. Uganda wameweka Bima ya Afya katika ilani yao ya Uchaguzi na nchi kama Marekani kama tutakavyoona.
Changamoto
· Bado mifumo hii inahudumia watu wachache hasa tabaka la wafanyakazi na hii ni kutokana na mifumo ya kisheria wakati inaanzishwa. Haya hivyo nchi nyingi zimegundua upungufu huu na sasa wanarekebisha na ILO katika Mkutano wake wa mwaka 2001 (ILO General Assembly) walipitisha mpango maalum wa kuhakikisha na makundi mengine yapate huduma hii kwa kuunganishwa na mipango ya kitaifa;
· Ugeni wa dhana yenyewe hasa kwa nchi za Kiafrika.tulizoea Serikali kufanya kila kitu. Na vile vile hofu kwa sababu
Swali
Kwa nini Bima ya Afya imekuwa ni ajenda kubwa ya dunia kwa sasa ikilinganishwa na taratibu nyingine za upatikanaji wa matibabu?
Majibu
Huu ni mfumo nafuu na rahisi unaojiendesha wenyewe bila kutegemea mapato au bajeti ya Serikali
Utaratibu wa Serikali kuhudumia watu kupitia bajeti au kodi hasa kwa nchi zinazoendelea ni mgumu na ulishindikana miaka ya mwanzo tu baada ya Uhuru
Bima za Afya za Binafsi ni mfumo ghali na unaonufaisha watu wachache wenye vipatoWaajiri wanaotoa huduma za matibabu kwa wafanyakazi wao, wengi sasa hivi wanashindwa kutokana na gharama kuwa kubwa
Mifumo ya kiasili ya ki-ujima ya kusaidiana mingi imekufa au ni dhaifu kwa sababu ya watu wengi kuhamia mijini na kila mtu sasa ni yeye na familia yake.
Swali
Unafikiri upi unaweza kuwa mchango wa Mifuko ya Bima za Binafsi katika maendeleo ya nchi.
Majibu
Bima ya Afya ya Binafsi inao mchango katika utoaji wa huduma hasa kwa watu wanaohotaji huduma maalumu zaidi ya zile zinazotolewa na mifumo ya Kiserikali; Hapa nchini kwetu zipo Bima za Binafsi kama ilivyo kwa Marekani lakini inahudumia watu wachache hivyo zinao mchango lakini sio sawa na zile za Serikali ambazo zinahudumia watu wengi kwa makundi yote. Mchango wa Bima ya Afya ya Binafsi ni huduma za nyongeza ndio maana katika nchi nyingi mifumo hii inatoa huduma za ziada mfano Kanada Baadhi ya nchi kama Ajentina wiki iliyopita wametangaza nia ya kuondoa majukumu ya mifuko ya binafsi kwenye mambo ya Pensheni na kuyarudisha Serikalini.
Swali:
Sisi kama Taifa tunajifunza nini kuhusu Mifuko ya Bima ya Afya ?
Majibu:
Ni kitu muhimu ambacho tumefanikiwa kuwa nacho kwa hiyo tukitunza kwa hali na mali;Utaratibu huu wa Bima ya Afya hapa nchini ndio jawabu kwa wananchi wengi wenye vipato vya kawaida.
Mifuko hii ikitumiwa vizuri inaweza kuleta manufaa yafuayayo:-
· Kuongeza uwigo kwa kuihusisha na mifuko ya Afya ya Jamii kama walivyofanya Korea ya Kusini;
· Mifuko hii inaweza kuboresha miundo mbinu katika sekta ya Afya;
· Mifuko hii inaweza kupunguza mzigo wa bajeti kwa serikali na kuwa chanzo imara kwa watoa huduma;
· Mifuko hii inaweza kuwapa uhakika na matumaini wale wote wenye hofu za gharama za matibabu hasa ukizingatia ongezeko la magonjwa mapya, magonjwa sugu na ya kuduma pamoja na milipuko.
Swali
Moja katika ya mambo ambayo yamejitokeza na kuvuta zaidi hisia za watu wengi katika kampeni za uchaguzi za Marekani, ni suala la Bima ya Afya. Kwanini sasa au kwa nini suala hili limejitokeza kwa nguvu zaidi katika kampeni za mwaka huu pengine kuliko ilivyokuwa miaka mingine ya nyuma;
Majibu
Suala la Afya linagusa maisha ya watu moja kwa moja. Watu wanapokuwa na Bima ya Afya wanakuwa makini zaidi kufuatilia, hasa kwa nchi kama Marekani ambako ni Taifa. Hapa nchini watu sasa wana Bima ya Afya hivyo wanakuwa makini zaidi kujua kinachofanyika katika nchi nyingine hasa Marekani ambayo ni Taifa kubwa; Kwa Wamarekani wenyewe suala hili limekuwa Ni agenda kubwa kwa sababu zifuatazo hasa katika kipindi hiki:-
· Zaidi ya Wamarekani milioni 45 hawana Bima ya Afya isipowa wachache wenye Bima za Binafsi (2007)
· Kuna kinamama takribani milioni 17 (wenye umri kati ya miaka 18-64) ambao hawana Bima ya afya yoyote;
· Wengi wa wasio na vipato wanalazimika kununua huduma wakati wanaihitaji (out-of-pocket) ambazo ni ghali;
· Mfumo wa matibabu uliopo kwa kiasi kikubwa ni wa Bima za Afya za Binafsi ambao ni ghali zaidi kwa hiyo ni watu wachache sana ndio wanaohudumiwa;
· Hofu ya gharama za matibabu (health shocks) zinawafanya watu wasio na ajira za kudumu inawaathiri wengi kisaikolojia na wanapougua wengi wanalazimika kuuza vitu vya ndani. Sasa hivi watu wameanza kuelewa kuwa jambo linalotokea sehemu moja ya dunia linakuwa na madhara au faida kwa sehemu nyingine au sehemu zote za dunia. Na linapokuja suala la Taifa kubwa kama Marekani kila mmoja anakuwa makini.
Swali
Ukiwa kama Mwenyekiti wa kamati ya kamisheni ya dunia kuhusu Mifuko ya Bima ya Afya katika Taasisi ya kimataifa ya Hifadhi ya Jamii Duniani. unaonaje Maendeleo yaliyofikiwa kwa sasa katika sekta hii ya Afya.
Majibu
Maendeleo yaliyofikiwa sisi katika kamisheni yetu tunaona tumepiga hatua kubwa tangu kabla sijaingia, mpaka nilipokuwa makamu wa mwenyekiti miaka mitatu iliyopita na sasa kama mwenyekiti. Mafanikio:
· Nchi nyingi zaidi ya 150 sasa ni wanachama wa Taasisi ya kimataifa ya hifadhi ya Jamii ambayo masuala haya yanajadiliwa na kubadilishana uzoefu kwa kina;
· Nchi nyingi hasa za Afrika ambazo kwa kipindi kirefu zilikuwa hazina mipango ya Bima ya Afya sasa zimeanza japo chache na nyingine ingawa hazijaanza suala hili wanalijadili na wamo kwenye mchakato mfano Uganda,Zambia na Malaysia;
· Sasa hivi kumekuwa na juhudi za pamoja hata katika ngazi ya kimataifa. Mashirika na Taasisi kubwa kama ILO, GTZ, WB, WHO sasa hivi wanafanya mikutano ya pamoja kujadili suala la Bima ya Afya. Mwanzoni kila taasisi ilikuwa inafanya peke yake;
· Bima za Afya zimesaidia sio tuu kupunguza mzigo kwa serikali katika bajeti za Afya lakini pia zimekuwa kichocheo cha maendeleo. Wanajenga Hospitali (Korea Kusini), wanafungua maduka ya dawa (Rwanda), wanachangia bajeti ya afya mpaka asilimia 80 (costa Rica) hii ni kwa manufaa ya wanachama wa Mifuko na wananchi wengine.
· Bima za Afya ndio limekuwa kimbilio la watu wa hali ya chini na kipato cha wastani kwa sababu ya kupanda kwa gharama za matibabu siku hadi siku. Na hii ni kwa dunia nzima. · Serikali na hasa viongozi wa Kitaifa wao ndio wamekuwa wasimamizi na waelimishaji wakubwa wa huduma hii. Hii inaonyesha umuhimu wa suala lenyewe. Mfano hapa nchi kwetu tangu awamu ya tatu hadi sasa Mheshimiwa Rais huwa anaongelea suala la Vitambulisho. Uganda wameweka Bima ya Afya katika ilani yao ya Uchaguzi na nchi kama Marekani kama tutakavyoona.
Changamoto
· Bado mifumo hii inahudumia watu wachache hasa tabaka la wafanyakazi na hii ni kutokana na mifumo ya kisheria wakati inaanzishwa. Haya hivyo nchi nyingi zimegundua upungufu huu na sasa wanarekebisha na ILO katika Mkutano wake wa mwaka 2001 (ILO General Assembly) walipitisha mpango maalum wa kuhakikisha na makundi mengine yapate huduma hii kwa kuunganishwa na mipango ya kitaifa;
· Ugeni wa dhana yenyewe hasa kwa nchi za Kiafrika.tulizoea Serikali kufanya kila kitu. Na vile vile hofu kwa sababu
Swali
Kwa nini Bima ya Afya imekuwa ni ajenda kubwa ya dunia kwa sasa ikilinganishwa na taratibu nyingine za upatikanaji wa matibabu?
Majibu
Huu ni mfumo nafuu na rahisi unaojiendesha wenyewe bila kutegemea mapato au bajeti ya Serikali
Utaratibu wa Serikali kuhudumia watu kupitia bajeti au kodi hasa kwa nchi zinazoendelea ni mgumu na ulishindikana miaka ya mwanzo tu baada ya Uhuru
Bima za Afya za Binafsi ni mfumo ghali na unaonufaisha watu wachache wenye vipatoWaajiri wanaotoa huduma za matibabu kwa wafanyakazi wao, wengi sasa hivi wanashindwa kutokana na gharama kuwa kubwa
Mifumo ya kiasili ya ki-ujima ya kusaidiana mingi imekufa au ni dhaifu kwa sababu ya watu wengi kuhamia mijini na kila mtu sasa ni yeye na familia yake.
Swali
Unafikiri upi unaweza kuwa mchango wa Mifuko ya Bima za Binafsi katika maendeleo ya nchi.
Majibu
Bima ya Afya ya Binafsi inao mchango katika utoaji wa huduma hasa kwa watu wanaohotaji huduma maalumu zaidi ya zile zinazotolewa na mifumo ya Kiserikali; Hapa nchini kwetu zipo Bima za Binafsi kama ilivyo kwa Marekani lakini inahudumia watu wachache hivyo zinao mchango lakini sio sawa na zile za Serikali ambazo zinahudumia watu wengi kwa makundi yote. Mchango wa Bima ya Afya ya Binafsi ni huduma za nyongeza ndio maana katika nchi nyingi mifumo hii inatoa huduma za ziada mfano Kanada Baadhi ya nchi kama Ajentina wiki iliyopita wametangaza nia ya kuondoa majukumu ya mifuko ya binafsi kwenye mambo ya Pensheni na kuyarudisha Serikalini.
Swali:
Sisi kama Taifa tunajifunza nini kuhusu Mifuko ya Bima ya Afya ?
Majibu:
Ni kitu muhimu ambacho tumefanikiwa kuwa nacho kwa hiyo tukitunza kwa hali na mali;Utaratibu huu wa Bima ya Afya hapa nchini ndio jawabu kwa wananchi wengi wenye vipato vya kawaida.
Mifuko hii ikitumiwa vizuri inaweza kuleta manufaa yafuayayo:-
· Kuongeza uwigo kwa kuihusisha na mifuko ya Afya ya Jamii kama walivyofanya Korea ya Kusini;
· Mifuko hii inaweza kuboresha miundo mbinu katika sekta ya Afya;
· Mifuko hii inaweza kupunguza mzigo wa bajeti kwa serikali na kuwa chanzo imara kwa watoa huduma;
· Mifuko hii inaweza kuwapa uhakika na matumaini wale wote wenye hofu za gharama za matibabu hasa ukizingatia ongezeko la magonjwa mapya, magonjwa sugu na ya kuduma pamoja na milipuko.
COMMENTS