Jina la Kitabu:Maadili ya Taifa na Hatima ya Tanzania Mtunzi: Ibrahim Mohamed Kaduma Mchapishaji:Vuga Press Mpitiaji: Beda Msimbe UNAWEZA ku...

Jina la Kitabu:Maadili ya Taifa na Hatima ya Tanzania
Mtunzi: Ibrahim Mohamed Kaduma
Mchapishaji:Vuga Press
Mpitiaji: Beda Msimbe
UNAWEZA kuchoshwa na kichwa hicho cha kitabu ambacho kimeandikwa na Ibrahim Mohamed Kaduma, lakini huwezi kamwe kuchoshwa na maandiko yake mara tu unapoaanza kukisoma hasa kama wewe ni mmoja wa wanazuoni ambao huamini katika'ishu' mjadili na utatuzi wake.
Kitabu hiki ambacho thamani yake katika usomi ni kubwa hasa kwa kuzingatia mazingira na makandokando yanayotukabili kwa sasa kama taifa,kimechapwa mwaka 2004 kikitoa onyo na mwelekeo wa taifa ambalo tayari lilishachomoka katika reli.
Kaduma,mtanzania ambaye alihudumia serikali kuanzia kipindi cha ukoloni hadi mwaka 2003 katika nyadhifa mbalimbali ikiwemo ya uwaziri ameandika kitabu hiki kama mwendelezo wa juhudi za watanzania wachache wanazuoni ambaiow anaangalia wapi tumekwenda kombo hadi tukafikia hapa tuliopo.
Kimsingi Kaduma katika kitabu chake anajadili kwa undani dhambi kubwa iliyofanywa na uongozi wa nchi hii ya kuacha maadili ya kitaifa ambayo yalipiganiwa na Mwalimu Julius Nyerere tangu kuacha kufundisha pale Pugu sekondari na hata ndani ya baraza la kutunga sheria kabla ya kuwa waziri Mkuu na Rais wa Tanganyika huru na baadaye Tanzania.
Maadili ya kitaifa haya ambayo baadaye yaliandikwa katika ahadi za kumi za MwanaTanu zililenga kumlea mtu katika msingi wa Umungu, hali ambayo ilistawisha uongozi, Utanganyika, Upendo na Thamani ya ubinadamu, haja ya elimu na utii.
Kitabu hiki chenye ukurasa 118 na ambacho kimewekewa dibaji na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es salaam, mwadhamana Polycarp kardinali Pengo ni tafsiri sahihi ya kukwama kwa Watanzania baada ya kuachana na msimamo wa kitaifa uliokuwa na lengo la kuzalisha viongozi wenye maadili na watanzania wanaoweza kujituma katika nafasi zao.
Katika kuonyesha ukomavu wa hoja na haja ya watanzania kujisahihisha na kurejea katika msimamo wa awali ambao ulituongezea sifa katika maisha yetu ndani na nje ya Afrika, Kaduma, kwa kutumia mifano hai amediriki mpaka kuuliza kama Watanzania walifanya maamuzi sahihi katika uchaguzi wa mwaka 2005.
Ni wazi kuwa Kaduma aliandika kitabu hiki muda mfupi sana kabla ya uchaguzi wa mwaka huo lakini huenda watu hawakupata nafasi kubwa ya kujadili kitabu hiki ambacho mimi naamini kimeamsha dira mpya ya kujiuliza: Watanzania tumepigwa na kitu gani mpaka hatuwezi kujisaidia sisi wenyewe katika kujirekebisha na kurejea katika reli ili tufikie muono uliolengwa tangu awali wa kuwa na taifa linalojali watu wake na si viongozi wanaojijali wao wenyewe.
Usalama wa nchi hii unategemea sana mshikamano wa Watanzania, lakini katika hali iliyopo sasa ya kilio cha ufisadi ambacho ni alama ya mwanzo ya ubinafsi, mshikamano unakuwa kama vile umepigwa rehani.
Kaduma anafikia hata kukumbusha mwongozo wa Tanu wa mwaka 1971 ambao ulitamka wazi kwamba ulinzi na usalama wa Tanzania ni wa kila Mtanzania, kila Mzalendo na kila mjamaa na katika wingu hili la ufisadi (anaita ubinafsi) Watanzania wanatakiw akuhakikisha kwamba wanauondoa mzizi huu ili kuleta usalama wa Taifa.
Mzizi huu ni matokeo ya kuachana na ahqadi kumi za mwanatanu na azimio la Arusha na ili kufanikiwa ni vyema kurejea katika reli.
Kaduma katika masuala ya utaifa hazungumzii chama cha CCM bali ni wazi hata wapinzani anasema, wasingelipendelea kuharibika kwa utaifa, utaifa ni kitu muhimu na kuna msingi ambayo iliwekwa tangu awali ambayo kama ingelifuatwa shauri lingekuwa nani atasimamia msingi huu wa muono w abaadaye wa kuwa na taifa ambalo linajali maslahi ya watu wake.
Kaduma katika kitabu chake ana mifano mingi ya kuonyesha uvunjivu huu wa maadili ya taifa jinsi unavyotafuna hazina ya taifa na kuwaweka wananchi wa Tanzania katika mtazamo hasi kuhusu nchi yao na mustakabali wao.
Na hili ndilo katika ukurasa wanne analizungumzia Kaduma kwa kuangalia hotuba ya mwalimu Nyerere, baba wa taifa, Siku ya Tanganyika kupata Jamhuri mwaka 1962, kinga ya haki na mambo wanayothamini Watanzania yanayofanya kuwa maadili.
Ukurasa huu amekariri mambo muhimu juu ya wananchi ambapo kwa kufahamu haki zao wanaweza hata kumwambuia rais kwamba mambo haya si Utanzania, hatukubali kutendewa haya awe na rais wetu au rais Mraba unaweza kupata kifungu hiki kamili katika kitabu au ukasoma kitabu cha JK Nyerere cha Uhuru na Umoja Uk 174.
tutaendelea mkukiangalia kitabu hiki kw akadri inavyowezekana nashauri ukipate ili tuwe sambamba katika majadiliano.
UNAWEZA kuchoshwa na kichwa hicho cha kitabu ambacho kimeandikwa na Ibrahim Mohamed Kaduma, lakini huwezi kamwe kuchoshwa na maandiko yake mara tu unapoaanza kukisoma hasa kama wewe ni mmoja wa wanazuoni ambao huamini katika'ishu' mjadili na utatuzi wake.
Kitabu hiki ambacho thamani yake katika usomi ni kubwa hasa kwa kuzingatia mazingira na makandokando yanayotukabili kwa sasa kama taifa,kimechapwa mwaka 2004 kikitoa onyo na mwelekeo wa taifa ambalo tayari lilishachomoka katika reli.
Kaduma,mtanzania ambaye alihudumia serikali kuanzia kipindi cha ukoloni hadi mwaka 2003 katika nyadhifa mbalimbali ikiwemo ya uwaziri ameandika kitabu hiki kama mwendelezo wa juhudi za watanzania wachache wanazuoni ambaiow anaangalia wapi tumekwenda kombo hadi tukafikia hapa tuliopo.
Kimsingi Kaduma katika kitabu chake anajadili kwa undani dhambi kubwa iliyofanywa na uongozi wa nchi hii ya kuacha maadili ya kitaifa ambayo yalipiganiwa na Mwalimu Julius Nyerere tangu kuacha kufundisha pale Pugu sekondari na hata ndani ya baraza la kutunga sheria kabla ya kuwa waziri Mkuu na Rais wa Tanganyika huru na baadaye Tanzania.
Maadili ya kitaifa haya ambayo baadaye yaliandikwa katika ahadi za kumi za MwanaTanu zililenga kumlea mtu katika msingi wa Umungu, hali ambayo ilistawisha uongozi, Utanganyika, Upendo na Thamani ya ubinadamu, haja ya elimu na utii.
Kitabu hiki chenye ukurasa 118 na ambacho kimewekewa dibaji na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Dar es salaam, mwadhamana Polycarp kardinali Pengo ni tafsiri sahihi ya kukwama kwa Watanzania baada ya kuachana na msimamo wa kitaifa uliokuwa na lengo la kuzalisha viongozi wenye maadili na watanzania wanaoweza kujituma katika nafasi zao.
Katika kuonyesha ukomavu wa hoja na haja ya watanzania kujisahihisha na kurejea katika msimamo wa awali ambao ulituongezea sifa katika maisha yetu ndani na nje ya Afrika, Kaduma, kwa kutumia mifano hai amediriki mpaka kuuliza kama Watanzania walifanya maamuzi sahihi katika uchaguzi wa mwaka 2005.
Ni wazi kuwa Kaduma aliandika kitabu hiki muda mfupi sana kabla ya uchaguzi wa mwaka huo lakini huenda watu hawakupata nafasi kubwa ya kujadili kitabu hiki ambacho mimi naamini kimeamsha dira mpya ya kujiuliza: Watanzania tumepigwa na kitu gani mpaka hatuwezi kujisaidia sisi wenyewe katika kujirekebisha na kurejea katika reli ili tufikie muono uliolengwa tangu awali wa kuwa na taifa linalojali watu wake na si viongozi wanaojijali wao wenyewe.
Usalama wa nchi hii unategemea sana mshikamano wa Watanzania, lakini katika hali iliyopo sasa ya kilio cha ufisadi ambacho ni alama ya mwanzo ya ubinafsi, mshikamano unakuwa kama vile umepigwa rehani.
Kaduma anafikia hata kukumbusha mwongozo wa Tanu wa mwaka 1971 ambao ulitamka wazi kwamba ulinzi na usalama wa Tanzania ni wa kila Mtanzania, kila Mzalendo na kila mjamaa na katika wingu hili la ufisadi (anaita ubinafsi) Watanzania wanatakiw akuhakikisha kwamba wanauondoa mzizi huu ili kuleta usalama wa Taifa.
Mzizi huu ni matokeo ya kuachana na ahqadi kumi za mwanatanu na azimio la Arusha na ili kufanikiwa ni vyema kurejea katika reli.
Kaduma katika masuala ya utaifa hazungumzii chama cha CCM bali ni wazi hata wapinzani anasema, wasingelipendelea kuharibika kwa utaifa, utaifa ni kitu muhimu na kuna msingi ambayo iliwekwa tangu awali ambayo kama ingelifuatwa shauri lingekuwa nani atasimamia msingi huu wa muono w abaadaye wa kuwa na taifa ambalo linajali maslahi ya watu wake.
Kaduma katika kitabu chake ana mifano mingi ya kuonyesha uvunjivu huu wa maadili ya taifa jinsi unavyotafuna hazina ya taifa na kuwaweka wananchi wa Tanzania katika mtazamo hasi kuhusu nchi yao na mustakabali wao.
Na hili ndilo katika ukurasa wanne analizungumzia Kaduma kwa kuangalia hotuba ya mwalimu Nyerere, baba wa taifa, Siku ya Tanganyika kupata Jamhuri mwaka 1962, kinga ya haki na mambo wanayothamini Watanzania yanayofanya kuwa maadili.
Ukurasa huu amekariri mambo muhimu juu ya wananchi ambapo kwa kufahamu haki zao wanaweza hata kumwambuia rais kwamba mambo haya si Utanzania, hatukubali kutendewa haya awe na rais wetu au rais Mraba unaweza kupata kifungu hiki kamili katika kitabu au ukasoma kitabu cha JK Nyerere cha Uhuru na Umoja Uk 174.
tutaendelea mkukiangalia kitabu hiki kw akadri inavyowezekana nashauri ukipate ili tuwe sambamba katika majadiliano.
COMMENTS