Mafisadi wa EPA

Hii ni habari ambayo imeandikwa na Habarileo Mafisadi wazidi kulizwa .Watatu zaidi wafikishwa kortini .walioshitakiwa walichota Sh bilioni ...

Hii ni habari ambayo imeandikwa na Habarileo

Mafisadi wazidi kulizwa
.Watatu zaidi wafikishwa kortini
.walioshitakiwa walichota Sh bilioni 44
.Jeetu na wenzake waendelea kusota rumande
.Masharti ya dhamana yawa mwiba
Na Shadrack Sagati na Mariam Mogella
WAMILIKI wengine wa kampuni tano ambazo zilihusika kuchota mabilioni ya fedha Benki Kuu (BoT) jana walifikishwa mahakamani kujibu tuhuma za kughushi nyaraka na kuiba.
Washitakiwa hao ni Falijala Hussein, Rajab Maranda ambao ni wamiliki wa kampuni za Mbale Farm, Lashashi Tanzania Ltd, Money Planners Consultant na Kaloloma & Brothers. Mwingine ni mkazi wa Arusha, Japhet Lema anayemiliki kampuni ya Njake Enterprises ya Arusha ambayo nayo ilijichotea mabilioni kutoka katika akaunti hiyo ya EPA.
Kufikishwa kwa washitakiwa kunafanya idadi ya washitakiwa ambao tayari wamefikishwa mahakamani kuwa 13 baada ya washitakiwa wengine 10 kufikishwa mahakamani juzi.
Idadi ya kampuni wanazowakilisha ni 11 ambazo idadi ya fedha walichota ni Sh bilioni 42 kati ya Sh bilioni 133 zilizochotwa na kampuni 22 kutoka katika akaunti ya EPA iliyoko BoT mwaka 2005.
Kesi ya kwanza inayowakabili Falijala Hussein na Rajab Maranda wanadaiwa kughushi na kuiba Sh bilioni 3.9 mali za BoT kwa kutumia kampuni ya Mbale Farm wakisingizia kupewa deni na kampuni ya Lakshimi Textile Mills Ltd ya Japan.
Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Mkazi Warialwande Lema. Upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na watasomewa maelezo ya awali Novemba 14 mwezi huu.
Katika kesi hiyo washitakiwa wanatetewa na Wakili Mabere Marando. Dhamana yao iko wazi lakini wanatakiwa waweke nusu ya fedha wanazodaiwa kuiba, wawe na wadhamini wawili, kuwasilisha hati za kusafiria ofisi ya mwendesha mashitaka na kutotoka nje ya Dar es Salaam. Katika kesi nyingine Maranda alipandishwa kizimbani peke yake mbele ya hakimu Hezron Mwakenja akidaiwa kuiba Sh milioni 207.3 kutoka BoT. Ilidaiwa alifanya wizi huo baada ya kughushi nyaraka akionyesha kuwa kampuni yake ya Lashashi Tanzania Ltd ilikabidhiwa deni na kampuni ya General Marketing ya India.
Hakimu Mkazi Hezron Mwakenja ndiye anayesikiliza kesi hiyo ambayo pia upelelezi wake umekamilika. Alishindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo moja ya sharti anatakiwa aweke Sh milioni 103.6 ili aweze kupata dhamana.
Wakili wake Hashimu Rungwe alichelewa kutetea mteja wake awasilishe hati ya mali inayolingana na thamani ya fedha hizo, hali iliyomfanya hakimu asisitize kuwa mahakama hairudi nyuma katika kutoa masharti kwani tayari alishaandika masharti hayo.
Baadaye Maranda alipandishwa tena kizimbani pamoja na Falijala wote wakituhumiwa kughushi nyaraka katika ofisi ya msajili wa makampuni (Brela) na kisha kuiba Sh bilioni 2.3 kwa kutumia kampuni ya Money Planners Consultant.
Katika kesi hiyo washitakiwa hao walipandishwa mbele ya hakimu Mkazi Anyimilile Mwaseba na wote wakituhumiwa kudanganya kuwa wamepewa deni hilo na kampuni ya B Glancel Ltd ya Ujerumani.
Hakimu Mwaseba katika masharti ya dhamana pia aliwataka washitakiwa walipe nusu ya fedha zinazodaiwa kuiba au wawasilishe nyaraka ambazo zimeshafanyiwa uhakiki na mamlaka husika kuthibitisha kama zina thamani hiyo. Sharti hilo lilikuwa gumu kutimizwa kwa siku ya jana na walirudi rumande hadi Jumatatu kesi hiyo itakapoenda kwa ajili ya kufanya mchakato wa upatikanaji wa dhamana.
Maranda na Falijala baadaye tena walifikishwa mbele ya hakimu mkazi Hadija Msongo wakichota Sh bilioni 1.8 kutoka BoT. Ilidaiwa walifanikisha wizi huo kwa kutumia kampuni ya Kiloloma & Brothers baada ya kuwasilisha hati za kughushi kutoka Brela wakidai kuwa wamepewa walipwe fedha hizo na kampuni ya D.C Export Ltd ya Mumbai, India.
Mawakili wa washitakiwa hao Joseph Tadayo na Mbaya kamala licha ya kujitahidi wapatiwe dhamana, lakini bado mambo yaliendelea kuwa magumu kutokana na masharti yake kufanana na yale kwenye kesi zingine.
Hakimu Hadija alisisitiza kuwa washitakiwa wanatakiwa wawasilishe hati ambazo zimehakikiwa na mamlaka husika kuonyesha kuwa zina thamani ya nusu ya fedha zinazodaiwa kuibwa.
Mtuhumiwa mwingine aliyepandishwa jana ni Japhet Lema ambaye yeye alijichotea Sh bilioni 2.6 kwa kutumia kampuni yake ya Njake Enterprises ya mjini Arusha. Alijipatia kiasi hicho baada ya kudanganya kwa nyaraka za kughushi kuwa kampuni yake imepewa deni hilo na kampuni ya C. Itoh ya Japan.
Naye alipelekwa rumande hadi Novemba 17 pale kesi yake itakapoenda kwa ajili ya kusomewa masharti ya awali na kuendelea na mchakato wa kupatiwa dhamana ambayo ina masharti kama washitakiwa wengine katika kesi hiyo.
Katika kesi zingine ambazo zilifikishwa mahakamani hapo jana, masharti ya dhamana yameendelea kuwa machungu kwa washitakiwa akiwamo kinara Jeetu Patel na wenzake ambaye anaendelea kusota rumande.
Mahakimu kadhaa ambako kesi ya Jeetu na wenzake zinasikilizwa wameonyesha kuwa wakali kwa kusisitiza hati wanazowasilisha mahakamani hapo ziwe zimefanyiwa tathmini na mkaguzi wa serikali.
Lengo la mahakimu hao Eva Nkya na Neema Chusi ni kutaka kujiridhisha katika kuthibitisha kuwa thamani ya mali hizo inalingana na nusu ya fedha wanazotakiwa waweke mahakamani ili wapate dhamana.
Katika kesi iliyoko mbele ya hakimu Nkya, Jeetu anashitakiwa Devendra Vinodbhai Patel na Amit Nandy ambako wanadaiwa kuiba Sh bilioni 3.3 kwa kutumia kampuni Navy Cut Tobacco Ltd. Kesi hiyo itaenda tena leo kutolewa maamuzi ya dhamana.
Mbele ya kesi iliyoko mbel eya Hakimu Chusi Jeetu anashitakiwa kwa pamoja na Devendra, Nandy na Ketan Chohan na wote wanadaiwa kuiba Sh bilioni 3.9 kwa kutumia kampuni yao ya Bina Resorts Ltd.
Kinara huyo pia anadaiwa kutumia kampuni ya Bencon kwa kuchota Sh 2.6 na pia alitumia kampuni ya Malta Mining na akaiba Sh bilioni 4.9.
Washitakiwa waliotumia kampuni ya Changanyikeni ambao ni Bahati Mahenge, Davis Kamungu, Godfrey Mosha, Manase Mwakale na Edina Mwakale ambao wanatuhumiwa kuiba Sh bilioni 2 nao hawakutimiza masharti ya dhamana. Mshitakiwa mwingine ambaye alifikishwa juzi ni Johnson Lukaza ambaye alichota Sh bilioni 6.3 kwa kutumia kampuni yake ya Kernel.

COMMENTS

BLOGGER: 2
Loading...
Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7051,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Mafisadi wa EPA
Mafisadi wa EPA
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2008/11/mafisadi-wa-epa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2008/11/mafisadi-wa-epa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy