MAMIA ya wananchi wa Tarafa ya Mkuyuni, na Matombo wamejitokeza kwa wingi katika mazishi ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Rashid Ngo...
MAMIA ya wananchi wa Tarafa ya Mkuyuni, na Matombo wamejitokeza kwa wingi katika mazishi ya aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Rashid Ngozoma Matunda yaliyofanyika juzi ( Nov 19) kijijini kwao Lungala Tarafa ya Mkuyuni Wilayani Morogoro.
Mazishi ya kiuongozi huyo mwandamizi wa Yanga yaliyofanyika kijijini hapoNovemba 19, mwaka huu majira ya saa 12 :30 jioni na yalihudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Morogoro (MRFA) wakiongozwa na Mwenyekiti wake Athuman Kambi.
Kwa upande wa msafara wa Yanga uliongozwa Mwenyekiti wake , Iman Madega, Katibu Mkuu Lucas Kisasa na viongozi wengine waandamizi wa timu hiyo.
Akizungumza na Habari leo mjini hapa jana ( Nov 20) baada ya mazishi ya kiongozi huyo, Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Morogoro, ( MRFA) Aristos Niktas, alisema mamia ya wananchi kutoka vijiji vya Tarafa Mkuyuni na baadhi ya Matombo walishiriki kikamilifu katika mazishi ya marehemu Matunda.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo wa MRFA, uongozi wa Chama hicho na wapenzi wa soka wa Mkoa wa Morogoro kuwa wamempoteza kiongozi aliyekuwa mtetezi wa haki katika kuendeleza michezo nchini.
Alisema kwa kutambua mchango wa kiongozi huyo, MRFA imetoa ubani wa kiasi cha sh: 50,000 ikiwa ni ishara ya kuungana na familia ya marehemu na viongozi wa timu ya Yanga wakati wa kipindi cha majozi ya kumpoteza kiongozi shupavu wa michezo hapa nchini.
Hata hivyo Katibu Mkuu huyo wa MRFA alisema familia ya marehemu imeushukuru uongozi wa soka wa Mkoa wa Morogoro kwa kujitokeza kushiriki mazishi hayo kwa kuonyesha kwamba Marehemu alikuwa ni kipenzi cha wanamichezo.
Kwa upande wa uongozi wa Yanga ulioongozwa na Mwenyekiti wake Madega ulimwelezea Marehemu alikuwa ni kiongozi mwenye kuopenda mshikamano na viongozi wezake na busara zake zilitumika katika kuleta maendeleo ndani ya Yanga.
“ viongozi wa Yanya katika mazishi hayo walimzungumzia marehemu kuwa akiluwa ni kiungo kikubwa kati ya wanachama na viongozi katika kudumisha umoja na mshikamano “ alinukuu maneno ya viongozi wa Yanga
Naye Katibu Mwenezi wa Tawi la Yanga la Mji Mpya Manispaa ya Morogoro, Leonard Masawe, alityeongozana na viongozi wa Matawi ya Yanga ya Morogoro, amewataka wanachamana viongozi wenzake kumwezi Marehemu kwa kusimamia mshikamano na utulivu ndani ya Yanga.
“ binafsi yangu nina fikiri ni wakati mzuri kumwezi mzee matunda kwa kusimamia mshikamano na amani katika timu zetu iwe Yanga ama watani zetu Simba “ alisema Masawe na kuongeza.
“ Matunda alikuwa ni miongoni mwa viongozi wachache wasiopenda malumbano na siku zote hadi kifo chake amekuwa ni mtetezi wa misingi ya haki ya kila mwanachama…na ameiwezesha Yanga kuwa moja na tulivu hivyo ni wakati wa kuyaendeleza hayo” alisema Masawe
Akimzungumzia Marehemu, alisema alikuwa mhimili katika soka ndani ya Yanga na kwa timu nyingine katika kupenda maendeleo ya timu na wachezaji wake na jambo hilo ndilo lililomletea heshima kubwa katika jamii.
Katibu Mwenezi huyo alisema pamoja na kuwa muhimili katika soka, Marehemu Matunda katika kijiji alichozaliwa alikuwa ni mmoja wa wazee wanaoheshimika na wananchi wenzake wakiwemo wazee , vijana na akina mama.
Alisema wao kama viongozi wa matawi walimua kwenda katika kijiji hicho kuungana na viongozi wengine wa Yanga na MRFA na kuungana na wananchi wengine kuupokea mwili wa Marehemu majira ya saa 11 na dakika 45 ulipotokea jijini Dar es Salam na kushiriki kikamilifu mazishi hayo. Hata hivyo alisema wapenzi wa Yanga na Simba wa Tarafa hizo walijitokeza kwa wingi kuweza kumzika Mzee Matunda ambapo utani wa jadi wa timu hizo wa hapa na pale wakufurahisha zilijitokeza wakati wa shughuli za mazishi zikiwazinafanyika.
“ sijawahi kuona mazishi makubwa kama haya ya Mzee Matunda ..watu wengi walijitokeza kumzika na utani wa Simba na Yanga pia ulijitokeza wa kufurahuisha kati ya wanachama wa Simba na viongizi wa Yanga waliohuhdhuria mazishi hayo” alisema Masawe
Rashid Ngozoma Matunda alifariki dunia hivi karibuni katika Hospitali ya Mwananyamala , Dar es Salaam baada ya kuugua ghafla na mwili wake kusafirishwa juzi hadi kijijini kwake Lungala, Tarafa ya Mkuyuni Wilayani Morogoro na kuzikwa jioni ya siku hiyo.
habari hii imeletwa na mdau John nditi
Mazishi ya kiuongozi huyo mwandamizi wa Yanga yaliyofanyika kijijini hapoNovemba 19, mwaka huu majira ya saa 12 :30 jioni na yalihudhuriwa na viongozi wa ngazi mbalimbali wa chama cha Mpira wa Miguu cha Mkoa wa Morogoro (MRFA) wakiongozwa na Mwenyekiti wake Athuman Kambi.
Kwa upande wa msafara wa Yanga uliongozwa Mwenyekiti wake , Iman Madega, Katibu Mkuu Lucas Kisasa na viongozi wengine waandamizi wa timu hiyo.
Akizungumza na Habari leo mjini hapa jana ( Nov 20) baada ya mazishi ya kiongozi huyo, Katibu Mkuu wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Morogoro, ( MRFA) Aristos Niktas, alisema mamia ya wananchi kutoka vijiji vya Tarafa Mkuyuni na baadhi ya Matombo walishiriki kikamilifu katika mazishi ya marehemu Matunda.
Kwa mujibu wa Katibu Mkuu huyo wa MRFA, uongozi wa Chama hicho na wapenzi wa soka wa Mkoa wa Morogoro kuwa wamempoteza kiongozi aliyekuwa mtetezi wa haki katika kuendeleza michezo nchini.
Alisema kwa kutambua mchango wa kiongozi huyo, MRFA imetoa ubani wa kiasi cha sh: 50,000 ikiwa ni ishara ya kuungana na familia ya marehemu na viongozi wa timu ya Yanga wakati wa kipindi cha majozi ya kumpoteza kiongozi shupavu wa michezo hapa nchini.
Hata hivyo Katibu Mkuu huyo wa MRFA alisema familia ya marehemu imeushukuru uongozi wa soka wa Mkoa wa Morogoro kwa kujitokeza kushiriki mazishi hayo kwa kuonyesha kwamba Marehemu alikuwa ni kipenzi cha wanamichezo.
Kwa upande wa uongozi wa Yanga ulioongozwa na Mwenyekiti wake Madega ulimwelezea Marehemu alikuwa ni kiongozi mwenye kuopenda mshikamano na viongozi wezake na busara zake zilitumika katika kuleta maendeleo ndani ya Yanga.
“ viongozi wa Yanya katika mazishi hayo walimzungumzia marehemu kuwa akiluwa ni kiungo kikubwa kati ya wanachama na viongozi katika kudumisha umoja na mshikamano “ alinukuu maneno ya viongozi wa Yanga
Naye Katibu Mwenezi wa Tawi la Yanga la Mji Mpya Manispaa ya Morogoro, Leonard Masawe, alityeongozana na viongozi wa Matawi ya Yanga ya Morogoro, amewataka wanachamana viongozi wenzake kumwezi Marehemu kwa kusimamia mshikamano na utulivu ndani ya Yanga.
“ binafsi yangu nina fikiri ni wakati mzuri kumwezi mzee matunda kwa kusimamia mshikamano na amani katika timu zetu iwe Yanga ama watani zetu Simba “ alisema Masawe na kuongeza.
“ Matunda alikuwa ni miongoni mwa viongozi wachache wasiopenda malumbano na siku zote hadi kifo chake amekuwa ni mtetezi wa misingi ya haki ya kila mwanachama…na ameiwezesha Yanga kuwa moja na tulivu hivyo ni wakati wa kuyaendeleza hayo” alisema Masawe
Akimzungumzia Marehemu, alisema alikuwa mhimili katika soka ndani ya Yanga na kwa timu nyingine katika kupenda maendeleo ya timu na wachezaji wake na jambo hilo ndilo lililomletea heshima kubwa katika jamii.
Katibu Mwenezi huyo alisema pamoja na kuwa muhimili katika soka, Marehemu Matunda katika kijiji alichozaliwa alikuwa ni mmoja wa wazee wanaoheshimika na wananchi wenzake wakiwemo wazee , vijana na akina mama.
Alisema wao kama viongozi wa matawi walimua kwenda katika kijiji hicho kuungana na viongozi wengine wa Yanga na MRFA na kuungana na wananchi wengine kuupokea mwili wa Marehemu majira ya saa 11 na dakika 45 ulipotokea jijini Dar es Salam na kushiriki kikamilifu mazishi hayo. Hata hivyo alisema wapenzi wa Yanga na Simba wa Tarafa hizo walijitokeza kwa wingi kuweza kumzika Mzee Matunda ambapo utani wa jadi wa timu hizo wa hapa na pale wakufurahisha zilijitokeza wakati wa shughuli za mazishi zikiwazinafanyika.
“ sijawahi kuona mazishi makubwa kama haya ya Mzee Matunda ..watu wengi walijitokeza kumzika na utani wa Simba na Yanga pia ulijitokeza wa kufurahuisha kati ya wanachama wa Simba na viongizi wa Yanga waliohuhdhuria mazishi hayo” alisema Masawe
Rashid Ngozoma Matunda alifariki dunia hivi karibuni katika Hospitali ya Mwananyamala , Dar es Salaam baada ya kuugua ghafla na mwili wake kusafirishwa juzi hadi kijijini kwake Lungala, Tarafa ya Mkuyuni Wilayani Morogoro na kuzikwa jioni ya siku hiyo.
habari hii imeletwa na mdau John nditi
COMMENTS