BARAZA la Maaskofu Tanzania(TEC) limewaomba wasomi wa vyuo vikuu nchini kuhakikisha kuwa wanaitumikia nchi yao kwa uzalendo na ukweli. Rai h...
BARAZA la Maaskofu Tanzania(TEC) limewaomba wasomi wa vyuo vikuu nchini kuhakikisha kuwa wanaitumikia nchi yao kwa uzalendo na ukweli.
Rai hiyo ilitolewa leo Jijini hapa na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Askofu Norbet Mtega wakati wa Ibada maalum ya kuwaombea wanachuo wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Weill Bugando kwenye sherehe ya maadhimisho ya Siku ya Bugando(Bugando day) na miaka
kumi ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino (Saut) yaliyofanyika kwenye hospitalini hapo.
"Ni matarajio yetu,Sisi baraza la Maaskofu Tanzania kuwaona wasomi wetu na madaktari wetu mnakuwa na moyo wa huruma katika kuwahudumia wagonjwa mkitanguliza uzalendo wa nchi yenu,"alisema Askofu Mtega.
Akizungumzia ufisadi aliwatahadharisha wasomi wote nchini kumrudia Mungu kwa maelezo
kuwa hiyo ndiyo silaha pekee ya kujikinga dhidi ya ufisadi.
Naye Jacob Kambili, anandika kutoka mwanza kuwa Utawala wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) cha mjini Mwanza umesema kamwe taasisi hiyo ya elimu ya juu haiungi mkono migomo ya wanachuo wa vyuo vya serikali inayoendelea nchini kote, wakipinga sera ya sasa ya uchangiaji elimu.
Makamu Mkuu wa SAUT, Padre Dk. Charles Kitima alisisitiza msimamo huo hapa Alhamisi wiki hii wakati wa maadhimisho ya miaka kumi tangu kiasisiwe, ambayo mgeni wake rasmi alikuwa Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo.
"Kweli wanachuo wengi, hususani wale wanaotoka kwenye familia maskini, wanahitaji sana fedha ili waweze kukidhi mahitaji yao ya msingi ya elimu. Lakini bado sisi tunaamini kwamba tatizo hilo nyeti linaweza kupatiwa ufumbuzi kwa amani kwa njia ya mazungumzo ya kujenga pekee". alisitiza Dk Kitima.
Makamu Mkuu wa SAUT alitumia fursa hiyo ya sherehe za maadhimisho ili kuwasilisha taarifa fupi ya maendeleo ya Chuo hicho, kilchoanzishwa mwaka 1998 kutoka iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Taasisi ya Mafunzo ya Jamii Nyegezi (NSTI).
Akizungumzia mipango mkakati ya chuo chake hicho, Dk Kitima alisema baadhi ya malengo waliojiwekea yamefikiwa ikiwa ni pamoja na ongezeko la wanachuo kutoka 294 katika mwaka wa masomo wa 1998/1999 hadi kufikia wanachuo8,790 hivi sasa.
Kati ya wanachuo hao, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa Chuo, wanachuo 6,206 wanasomea sehemu ya Malimbe (main campus), 781 ni wanachuo wa chuo kishiriki cha Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Bugando (BUCHS), 1,202 walioko katika Chuo Kikuu kishiriki cha Ruaha, mkoani Iringa ili hali wanachuo 600 wanasoma katika chuo kikuu kishiriki cha Mwenge, mjini Moshi.
Kuhusu mipango ya baadaye, alisema SAUT ambayo sasa inajivunia kwa kuwa na jumla ya wahadhiri 140, inakadiria kuwapoea wanachuo 15,000 katika kipindi cha miaka sita kijacho, ikizingatiwa kwamba tayari Chuo kimewapeleka nje wahadhiri 50 kwa ajili ya masomo ya ngazi ya PhD.
"Endapo mambo yote yatakwenda kama yalivyopangwa, tunadhamiria kuanzisha vyuo vikuu vinne zaidi vishiriki katika mikoa ya Dar es Salaam, Tabora, Mtwara na Ruvuma" alidokeza.
Mapema, akiuhubiria umati huo ambao ulikusanyika hapo kama waumini wa kanisa Katoliki waliojukuika ili kutoa shukrani zao kwa Mungu kwa kuijalia SAUT kutimiza miaka kumi ya uhai wake, Mwadhama Kadinali Pengo alikemea vikali kila dalili za mmomonyoko wa maadili zilizoanza kujidhihirisha katika jamii.
Rai hiyo ilitolewa leo Jijini hapa na Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu Tanzania Askofu Norbet Mtega wakati wa Ibada maalum ya kuwaombea wanachuo wa Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Weill Bugando kwenye sherehe ya maadhimisho ya Siku ya Bugando(Bugando day) na miaka
kumi ya Chuo Kikuu cha Mtakatifu Agostino (Saut) yaliyofanyika kwenye hospitalini hapo.
"Ni matarajio yetu,Sisi baraza la Maaskofu Tanzania kuwaona wasomi wetu na madaktari wetu mnakuwa na moyo wa huruma katika kuwahudumia wagonjwa mkitanguliza uzalendo wa nchi yenu,"alisema Askofu Mtega.
Akizungumzia ufisadi aliwatahadharisha wasomi wote nchini kumrudia Mungu kwa maelezo
kuwa hiyo ndiyo silaha pekee ya kujikinga dhidi ya ufisadi.
Naye Jacob Kambili, anandika kutoka mwanza kuwa Utawala wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino (SAUT) cha mjini Mwanza umesema kamwe taasisi hiyo ya elimu ya juu haiungi mkono migomo ya wanachuo wa vyuo vya serikali inayoendelea nchini kote, wakipinga sera ya sasa ya uchangiaji elimu.
Makamu Mkuu wa SAUT, Padre Dk. Charles Kitima alisisitiza msimamo huo hapa Alhamisi wiki hii wakati wa maadhimisho ya miaka kumi tangu kiasisiwe, ambayo mgeni wake rasmi alikuwa Mwadhama Kardinali Polycarp Pengo.
"Kweli wanachuo wengi, hususani wale wanaotoka kwenye familia maskini, wanahitaji sana fedha ili waweze kukidhi mahitaji yao ya msingi ya elimu. Lakini bado sisi tunaamini kwamba tatizo hilo nyeti linaweza kupatiwa ufumbuzi kwa amani kwa njia ya mazungumzo ya kujenga pekee". alisitiza Dk Kitima.
Makamu Mkuu wa SAUT alitumia fursa hiyo ya sherehe za maadhimisho ili kuwasilisha taarifa fupi ya maendeleo ya Chuo hicho, kilchoanzishwa mwaka 1998 kutoka iliyokuwa ikijulikana kwa jina la Taasisi ya Mafunzo ya Jamii Nyegezi (NSTI).
Akizungumzia mipango mkakati ya chuo chake hicho, Dk Kitima alisema baadhi ya malengo waliojiwekea yamefikiwa ikiwa ni pamoja na ongezeko la wanachuo kutoka 294 katika mwaka wa masomo wa 1998/1999 hadi kufikia wanachuo8,790 hivi sasa.
Kati ya wanachuo hao, kwa mujibu wa Makamu Mkuu wa Chuo, wanachuo 6,206 wanasomea sehemu ya Malimbe (main campus), 781 ni wanachuo wa chuo kishiriki cha Chuo Kikuu cha Sayansi ya Tiba cha Bugando (BUCHS), 1,202 walioko katika Chuo Kikuu kishiriki cha Ruaha, mkoani Iringa ili hali wanachuo 600 wanasoma katika chuo kikuu kishiriki cha Mwenge, mjini Moshi.
Kuhusu mipango ya baadaye, alisema SAUT ambayo sasa inajivunia kwa kuwa na jumla ya wahadhiri 140, inakadiria kuwapoea wanachuo 15,000 katika kipindi cha miaka sita kijacho, ikizingatiwa kwamba tayari Chuo kimewapeleka nje wahadhiri 50 kwa ajili ya masomo ya ngazi ya PhD.
"Endapo mambo yote yatakwenda kama yalivyopangwa, tunadhamiria kuanzisha vyuo vikuu vinne zaidi vishiriki katika mikoa ya Dar es Salaam, Tabora, Mtwara na Ruvuma" alidokeza.
Mapema, akiuhubiria umati huo ambao ulikusanyika hapo kama waumini wa kanisa Katoliki waliojukuika ili kutoa shukrani zao kwa Mungu kwa kuijalia SAUT kutimiza miaka kumi ya uhai wake, Mwadhama Kadinali Pengo alikemea vikali kila dalili za mmomonyoko wa maadili zilizoanza kujidhihirisha katika jamii.
COMMENTS