Kanisa Katoliki lawatenga wanachama 400 wa CCM

KATIKA kile kinachoonekana kuithibitishia jamii kuwa nyumba za ibada si mahala pa siasa, Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga limewafukuza na...

KATIKA kile kinachoonekana kuithibitishia jamii kuwa nyumba za ibada si mahala pa siasa, Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga limewafukuza na kuwazuia kushiriki shughuli za kanisa zaidi ya waumini wake 400 wanaotuhumiwa kuisaliti imani ya kanisa hilo kwa kukishabikia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu uliofanyika hivi karibuni.

Miongoni mwa waumini wanaotajwa kuwa wamesimamishwa na kanisa hilo ni pamoja na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa, Hipolitus Matete na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Sumbawanga, Charles Kabanga.

Habari za uhakika ambazo HABARILEO Jumapili imezipata zinasema kwamba, uamuzi huo wa kanisa umelenga kujisafisha na 'kashfa’ ya kuegemea upande fulani wakati wa kampeni na baadaye uchaguzi mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu.

Chanzo chetu cha habari kimepasha kwamba, wanaCCM hao wanaotuhumiwa na kanisa hilo wanahusika kufanya mikutano ya ndani, kuvaa sare za chama hicho na kumshabikia waziwazi aliyekuwa mgombea wa Ubunge kupitia CCM katika Jimbo la Sumbawanga Mjini,
Aeshi Hilaly.

Kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu huo mgombea ubunge wa CCM, Aeshi aliibuka kidedea kwa kutangazwa mshindi dhidi ya mgombea wa Chadema, Norbet Yamsebo ambaye kwa sasa amekata rufaa Mahakama Kuu mjini hapa kupinga matokeo hayo.

Inaelezwa kwamba, mgogoro wa kiimani baina ya Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga Mjini na waumini wake ambao ni wanaCCM, umetokana na waumini hao kupuuzia agizo la kanisa la kutomshabikia Aeshi kwa madai kwamba, alikufuru imani ya kanisa hilo kwa kujifananisha na Mwana wa Mungu, Yesu Kristu.

Baadhi ya viongozi wa kanisa jimboni humo wamekuwa wakimtuhumu mgombea huyo wa CCM pale alipodai katika moja ya mikutano yake ya kampeni kwa kufananisha mafiga matatu na Utatu Mtakatifu ambao mgombea huyo anadai kuwa alikufuru imani hiyo kwa kumfananisha mgombea Urais wa CCM, Rais Jakaya Kikwete kama Mungu Baba, mgombea ubunge kama Yesu Kristu mwana wa Mungu na wagombea Udiwani sawa na
Roho Mtakatifu.

Katibu wa CCM Mkoa wa Rukwa, Kapteni Fratern Kiwango amethibitisha kutengwa kwa wanachama wa chama hicho ambao ni waumini wa Kanisa Katoliki Jimbo la Sumbawanga.

“Ni kweli hadi sasa kanisa hilo limewafukuza na kuwazuia wanaCCM zaidi ya 400 kupokea sakramenti zozote kwenye Kanisa Katoliki la hapa,” alisema Kapteni Kiwango aliyewataja baadhi ya waliofukuzwa na kusimamishwa kuhudhuria ibada za misa takatifu kuwa ni pamoja na Matete, Kabanga, dereva wa Katibu wa CCM mkoa wa Rukwa aitwaye Vitalis Kalwangwa na mkewe na Katibu Mwenezi wa CCM Tawi la Majengo, Christina Tinde.

Inadaiwa kuwa waumini hao ni kutoka kanisa la Familia Takatifu lililopo Chanji mengine ni Kristu Mfalme , Katandala na Kanisa la Kiaskofu lililopo Mazwi mjini hapa ambapo kanisa lililopo kijiji cha Mlanda limefungwa na waumini wake wote wamezuiwa kupata
huduma yoyote ya kiroho kwenye kanisa hilo.

Inadaiwa kuwa pamoja na kuzuiwa kuingia makanisani na kuhudhuria ibada ya misa takatifu waumini hao wamezuiwa pia kupokea sakramenti zozote katika Kanisa Katoliki.

Pia wamezuiwa kupata huduma za kiroho kanisani zikiwemo kufunga ndoa, kubatizwa au kupata kipaimara na pia kufanyiwa ibada wakati wa maziko hadi hapo suala lao litakapopatiwa ufumbuzi ambapo itategemewa zaidi jitihada zao binafsi na huruma ya Mungu.

Mwandishi wa habari hizi alisoma baadhi ya nakala za barua za kuwasimamisha kupokea sakramenti kwenye kanisa hilo zilizosainiwa na Paroko wa Kanisa la Kristu Mfalme, Padri Pambo Mlongwa.

Sehemu ya barua hiyo inasema; "Kufuatia mwenendo mbovu wakati wa uchaguzi mkuu, huku ukiendekeza vitendo vya rushwa na usaliti wa imani Katoliki.

“Kwa heshima ya Mungu wetu na utatu mtakatifu wa kanisa, Mama kanisa Mtakatifu kwa nguvu ya Sheria ya kanisa CIC 13669, CIC1389,CIC 13712 na CIC 1391 naagiza usipokee sakramenti zozote katika Kanisa Katoliki… tekeleza amri hii mara umalizapo kuisoma barua hii.”

Padri Pambo alipohojiwa kwa njia ya simu ili kupata ufafanuzi zaidi wa suala hilo alisema kwamba, yuko mbali sana ambako hataki mtu yeyoye ajue aliko.

"Sawa mimi ni kiongozi wa kiroho kwa sasa sitaki kabisa mtu yeyote hata wewe ujue wapi nilipo, niko mbali sana kwa sasa nakushauri nenda ofisini ni suala la kiofisi hilo kwa sasa sina majibu yake,” alisema kiongozi huyo wa kiroho.

Lakini kabla ya mawasiliano ya siku hiyo, kwa nyakati tofauti Padri Pambo alipokuwa
akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu alikiri kuwa mgombea wa CCM, Aeshi alikuwa amekufuru imani na Kanisa Katoliki kwa kujifananisha na Yesu Kristu Mungu Mwana ambapo Kanisa liliwasilisha malalamiko yake kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipokuja mjini hapa kumnadi mgombea huyo, lakini hawakuweza kufikia mwafaka.

Pia zimekuwa taarifa mjini hapa kwa Padri Pambo amekimbia kanisa lake la Kristu Mfalme kwa kile kinachodaiwa kuwa amekwenda kujificha kusikojulikana ili kukwepa hasira za waumini wa kanisa hilo wanaopinga kufukuzwa kwa wenzao kwa sababu ya itikadi zao za kisiasa.

Naye Paroko wa Kanisa la Kiaskofu mjini Sumbawanga, Padri Deo Simemba hivi karibuni alipohojiwa na gazeti hili alikiri kuwa kanisa limeanza kuwasimamisha baadhi ya waumini wake kwa kile alichodai kuisaliti imani ya Kanisa Katoliki.

Kutokana na tukio hilo, Katibu wa CCM wa Mkoa amelitahadharisha kanisa hilo kwa kujiingiza kwenye malumbano ya kisiasa.

Baadaye, gazeti hili liliwasiliana na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Anthony Makunde ili aweze kulizungumzia suala hilo na alipopatikana kwa njia ya simu alisema:

“Kwa nafasi yangu, naweza kusema sijui lolote kwa sababu sijapata taarifa rasmi na inawezekana kwa kuwa katika siku za hivi karibuni nilikuwa na vikao vingi pamoja na kuhudhuria mafahali pale Chuo Kikuu cha Madaktari Bugando (Mwanza).”
SOURCE BOFYA HAPA

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Kanisa Katoliki lawatenga wanachama 400 wa CCM
Kanisa Katoliki lawatenga wanachama 400 wa CCM
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2010/12/kanisa-katoliki-lawatenga-wanachama-400.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2010/12/kanisa-katoliki-lawatenga-wanachama-400.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy