Katiba mpya?polepole Jamani

ANGALIZO: Katika gazeti la leo la Habarileo ambalo ndilo ninalofanyia kazi niliandika wazo langu. Limesomwa na watu si haba. Kuna vitu watu ...

ANGALIZO:

Katika gazeti la leo la Habarileo ambalo ndilo ninalofanyia kazi niliandika wazo langu. Limesomwa na watu si haba. Kuna vitu watu hukasirika wakisoma mawazo mengine. Lakini pia kuna watu wanaokasirika wakiulizwa maswali. Kuna hoja nyingi ambazo zingine zilitumwa katika simu yangu binafsi.Si mbaya nikasema haya yafuatayo baada ya wewe kuisoma habari yenyewe.
Lukwangule



Katiba Mpya polepole jamani

UKIFUNGUA Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 katika utangulizi wake unaona misingi ya Katiba na katika misingi hiyo unakutana na sababu kwanini tuna Katiba.

Pamoja na sababu hiyo pia inaelezwa kuwa Katiba iliandikwa na watu ikapitishwa katika Bunge na kisha kuanza kutumika kwa manufaa ya watu wa taifa hili na nchi kwa ujumla wake.

Nchi bila Katiba itakuwa nchi yenye ufisadi wa aina yake na hii inaweza kuleta mushkeri mkubwa kwa binadamu.

Kwa sasa kuna maneno, kelele na mazungumzo yanayoendelea miongoni mwa watu waliobahatika kujua maana ya Katiba na hatima ya mazungumzo yao mara zote wanataka
Katiba mpya na wanatushawishi wengine kwamba bila Katiba mpya hakutakuwa na uchaguzi huru na wa haki.

Naam, kwa Katiba hii hii tumepata uongozi wa kisiasa, kwa Katiba hii hii tuna mhimili wa Bunge na Mahakama na uongozi na kwa Katiba hii hii inayochanwa na kusimangwa
tunakuwa na demokrasia mpya.

Unapofungua Katiba na kukutana na maneno yafuatayo (nanukuu): KWAKUWASISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani: Tuendelee.

Katika mijadala inayoendelea hakuna hata mtu mmoja anayesema katika maelfu ya maneno
yaliyomo katika Katiba wapi pana tatizo na panahitaji kubadilishwa, mazungumzo na kelele ni kwamba Katiba hiyo imepigwa viraka 14 inastahili kufumuliwa na kuundwa upya.

Pia inazungumzia ujamaa ambao hatuufuati. Hili lahitaji majadiliano zaidi. Sina sababu ya kusoma alama za nyakati, kwani huona hizi alama zinapoteza watu mawazo ya kusonga
mbele na ukweli huo unazingatia mabishano ya sasa kwamba mwisho wa kuinjilisha ni mwaka
wa kesho na mwaka wa kesho kutwa Mei 21 Mungu anamaliza hesabu zake.

Mimi ni Mkatoliki nakumbuka ipo sehemu alipoulizwa Yesu mwisho wa dunia alisema ni baba
pekee anayejua siri hiyo lakini makubwa yatapita duniani kabla ya neno hilo kutimia.

Na kutokana na hilo wazo la kusoma alama za nyakati kuhusiana na Katiba huwa naliona kama ni jepesi sana.

Watu wanaozungumza suala la Katiba iliyoundwa na wachache wanaojua namna ya kuendesha nchi wakaipitisha katika Bunge, nalo ni wachache wenye dhamana ya kutunga sheria na kisha kufanyiwa kazi, lakini sasa wanataka Katiba mpya ya kuuliza kila mtu.

Naam, inawezekana kabisa. Lakini swali langu la msingi ambalo nataka kila mtu alifikirie ni hii
Katiba inayotoa nafasi ya kubadilishana mawazo kuhusu haja ya kuwa na Katiba mpya inajulikana kweli kwa watu?

Nauliza hivi kwa sababu itakapokuja hiyo drafti mpya tunaweza kujua tatizo lilikuwa wapi hasa katika kazi iliyopita? Mimi naona watu ni wa binafsi mno na wanataka kuendesha nchi katika
umri wa binadamu , hili haliwezekani, twendeni polepole ni mustakabali wa taifa na lazima kila mtu ajue nini kipo katika Katiba ya zamani, kasoro zake na kwanini ni lazima kuwa na Katiba mpya.

Kwa sababu nchi ni zaidi ya miaka 70 na ishirini ya kuazimwa na Mungu aliyonayo binadamu, inahitaji kwenda kwa mtindo kama wa jeshi kubwa katika kuwania kipito kidogo.

Katiba inaweka michoro muhimu ya maisha na kanuni na huwezi kudharau hilo kwani linaweza likatafsiriwa vibaya. Kama hali ni hiyo kama tunajadili juu juu tu ni sawa na kuona
kaburi zuri nje ndani kuna uvundo.

Pengine huo ni msimamo mbaya lakini kiukweli niseme kinachobaki katika Katiba ni muonekano unaoweza ama kukozwa au kuchushwa kwa kuzingatia mawazo ya kundi linalotaka mamlaka au linalotawala kwa wakati huo, na bila shaka tunaotaka Katiba mpya tu wapi na tuna sababu gani nje ya hii niliyoigusia.

Manake sehemu kubwa ya Katiba haifundishwi na wala vipengele vyake havijulikani vyema nini kanuni si ya msingi na itifaki za kimataifa tulizoridhia.

Kutokana na hoja yangu hapo juu napenda kuwauliza watu wanaotaka katiba , hivi ni kweli wanataka kuandikwa upya kwa Katiba au wana lao jambo? Nasema hivi kwa sababu nyingine kubwa kama hatujaaminiana.

Narejea tena hivi ni kweli tunataka katiba, nani anajua katiba ya zamani atatoa na mfano na kusema kutokana na ubaya wa Katiba hii hapa na pale na huko ni lazima kudai Katiba mpya, sivyo mimi naona kama Watanzania tunahemea juu juu kama mpira baharini, tumepigwa pampu.

Naam kwenye Biblia Waisrael walitaka kuwa kama wengine, wakataka watawala, Mungu akawapa kilichofuata nadhani walijuta, lakini wamekuwa kama wengine.

Huo ndio ukweli wa dunia ulio mchachu. Pamoja na ukweli kuwa tunahitaji katiba bado nadhani si sahihi kutuvurumisha Watanzania katika wimbo tusiouelewa; tueleweshane kwanza,
manake hiki ni kitu kikubwa na hakika tusipoeleweshana tunaweza kwenda msobemsobe halafu ikawa kiama hapa, bila taarifa ya haraka.
mwisho

HOJA ZA WATU

mwenye namba+255683019370 aliandika hivi...: Niseme moja kwa moja. kwanini uandike jambo ambalo hulifahamu na kutusumbua wapenzi wa habarileo?Soma mwenyewe wazo hableo ya tarehe 21/12 kuhusu katiba... unataka tufahamu au unaelewesha jamii kitu gani? nakuomba uiandike upya.Habarileo nalipenda... mwisho wa kunukuu.

mwingine aliandika hivi:

Katiba mpya?... Polepole jamani!
Name: DATUS MAHENDEKA
Email: datusmahendeka@yahoo.com
Date sent: 21st December 2010 @ 07:20
Comment: Una mawazo mazuri lakini Katiba Mpya inahitajika ndio maana viongozi waliopita na Mh. Pinda ameliona hilo.



na huyu naye

Katiba mpya?... Polepole jamani!
Name: joseph mwita
Email: terrell_bibbs@yahoo.com
Date sent: 21st December 2010 @ 04:05
Comment: Katiba mpya ni lazima,mwandishi sio kwa sababu unaandikia gazeti la siri kali ndio unataka kujikomba kwake. Wananchi tunataka katiba ambayo itapunguza mamlaka ya raisi,tume ya uchaguzi huru na mwananchi wa kawaida awe na uwezo wakuwachagua kwa kura viongozi wengi kuanzia watu kama wakuu wa mikoa. Wananchi wakitaka kitu hakuna kitu cha kuwazuia na wakati ni huu.

Hoja yangu:

Sikuandika ili kuma mtu yoyote pozi. nawakumbusha haja ya wananchi kuelewa ili kuwa na mchango mkubwa katika katiba na suala si haraka kwa sababu wewe unalifahamu. Asilimia 80 ya watu wa nchi hii wanategemea kilimo kujilisha na kusomesha watoto wao, ukilifahamu hilo, kifalsafa tu manake tuna watu wengi wasiojua mambo fulani yanayohusu maisha yao ndani ya jamii.wako katika jembe la mkono na dhiki yao kubwa ni chakula na wapi pa kupata vijisenti wanavyoporwa na wajanja kwa kuwapoa kima ksiichohalali kwa nguvu zao.
sasa ukiwa na watu wa aina hiyo ambayo hata maana na msingi wa katiba hawajui ni vyema kwanza ukafanya kazi ya kuwaelimisha. Zipo NGO nyingi zinazosema kwamba kazi yao ni kuelimisha jamii kuhusu mustakabali wao, lakini hawafanyi.
Mimi nataka mtu anieleze kwa kuanzia kwake mwenyewe, kama si baba yake, mkewe au mume wake kama si mjomba na shangazi yake mtoto wake wa kiume au wa kike kama kweli wanafahamu katiba tuanzie na hiyo iliyopigwa misele ya mwaka 1977.
Tuangalie katiba ya mwaka 1965 na tuangalie katiba ya mwanzo kabisa tuseme ya tanganyika ambayo ilikomba mpaka sheria ya kutozwa sh 100 kama unakutwa karibu na nyumba ya kulala wageni, sheria ambayo mpaka leo haijaondolewa wala kufanyiwa marekebisho.
Mimi si kwa sababu nafanyakazi serikalini ninajikomba, au mtu anadhani kwamba sifikiri, unatembea nchi hii unawauliza watuj maswali ya msingi kabisa kuhusu maisha yao hawajui cha kujibu, wanadhani kwamba serikali ndio mama na ndio baba yao na chama wanachokiamini hakifanyi makosa na viongozi wanawaamini hawafanyi makosa ndio wakombozi wao.
Kazi kubwa ya waandishi ni kuelimisha na kuwakumbusha watu, nimefanyakazi yangu si ya kupinga katiba bali binadamu lazima watengeneze subira katika kila hatua kubwa katika maisha ya nchi yao, itafika wakati suala linarejea kwa wananchi kwa usahihi, watasema nini kuhusu ukweli wa katiba kama wao wenyewe hawajui?
Madaraka ya Rais lazima yapunguzwe sawa tukiyapunguza tunayapeleka wapi na kiasi gani tumbakishie. Tunataka kuchagua viongozi wetu wa mikoa sisi wenyewe, kanuni zipi na aina gani ya demokrasia tunaifanya.
Tunataka haki za binadamu kwa kiwango gani na wapi mipaka . kama mimi nataka kutembea uchi kwanini unikataze , si unakataza haki yangu ya msingi.
Kuna mambo mengi yanayotakiwa kuangaliwa katika katiba si suala la kukurupuka na ili watu wawe na upeo mpana wa kuchangia ni lazima kwanza wajue nini maana ya katiba, kuangalia wenzao wamefanya nini, kuna marekebisho gani yanatakiwa na wapi ni mipaka na kwanini mashoga wasiwe sehemu ya katiba na kila mtu akafanya lake. Nini utamaduni wetu katika hili kwa sababu sisi si kisiwa lakini pia si wapuuzi.
Hilo ndilo hasa nililotaka kuwakumbusha watu. Ukiwa na hasira huwezi kuliona hili na kama hujawahi kukaa na kuongoza watu katika misukosuko hakika huwezi kuwa na busara kwa sababu wewe unataka leo kumbe unatakiwa kuangalia kasi ya mabadiliko ya mambo duniani, kuhami yale mazuri na kuhakikisha kwamba watu hawapotoki kwa kuwa na tafsiri finyu ya uhuru wao ndani ya katiba.
Labda hili linaweza kueleweka.
Tumeenda shule kwa sababu hizi hizi kuangalia wka kina masuala mazito yanayohusu jamii kwa kuishirikisha vyema lakini si kuwaburuza.
naitwa Beda Msimbe kutoka juu ya milima ya Uluguru, upande wa Magharibi wa Lukwangule.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Katiba mpya?polepole Jamani
Katiba mpya?polepole Jamani
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2010/12/katiba-mpyapolepole-jamani.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2010/12/katiba-mpyapolepole-jamani.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy