ANGALIZO: Katika gazeti la leo la Habarileo ambalo ndilo ninalofanyia kazi niliandika wazo langu. Limesomwa na watu si haba. Kuna vitu watu ...
ANGALIZO:
Katika gazeti la leo la Habarileo ambalo ndilo ninalofanyia kazi niliandika wazo langu. Limesomwa na watu si haba. Kuna vitu watu hukasirika wakisoma mawazo mengine. Lakini pia kuna watu wanaokasirika wakiulizwa maswali. Kuna hoja nyingi ambazo zingine zilitumwa katika simu yangu binafsi.Si mbaya nikasema haya yafuatayo baada ya wewe kuisoma habari yenyewe.
Lukwangule
Katiba Mpya polepole jamani
UKIFUNGUA Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 katika utangulizi wake unaona misingi ya Katiba na katika misingi hiyo unakutana na sababu kwanini tuna Katiba.
Pamoja na sababu hiyo pia inaelezwa kuwa Katiba iliandikwa na watu ikapitishwa katika Bunge na kisha kuanza kutumika kwa manufaa ya watu wa taifa hili na nchi kwa ujumla wake.
Nchi bila Katiba itakuwa nchi yenye ufisadi wa aina yake na hii inaweza kuleta mushkeri mkubwa kwa binadamu.
Kwa sasa kuna maneno, kelele na mazungumzo yanayoendelea miongoni mwa watu waliobahatika kujua maana ya Katiba na hatima ya mazungumzo yao mara zote wanataka
Katiba mpya na wanatushawishi wengine kwamba bila Katiba mpya hakutakuwa na uchaguzi huru na wa haki.
Naam, kwa Katiba hii hii tumepata uongozi wa kisiasa, kwa Katiba hii hii tuna mhimili wa Bunge na Mahakama na uongozi na kwa Katiba hii hii inayochanwa na kusimangwa
tunakuwa na demokrasia mpya.
Unapofungua Katiba na kukutana na maneno yafuatayo (nanukuu): KWAKUWASISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani: Tuendelee.
Katika mijadala inayoendelea hakuna hata mtu mmoja anayesema katika maelfu ya maneno
yaliyomo katika Katiba wapi pana tatizo na panahitaji kubadilishwa, mazungumzo na kelele ni kwamba Katiba hiyo imepigwa viraka 14 inastahili kufumuliwa na kuundwa upya.
Pia inazungumzia ujamaa ambao hatuufuati. Hili lahitaji majadiliano zaidi. Sina sababu ya kusoma alama za nyakati, kwani huona hizi alama zinapoteza watu mawazo ya kusonga
mbele na ukweli huo unazingatia mabishano ya sasa kwamba mwisho wa kuinjilisha ni mwaka
wa kesho na mwaka wa kesho kutwa Mei 21 Mungu anamaliza hesabu zake.
Mimi ni Mkatoliki nakumbuka ipo sehemu alipoulizwa Yesu mwisho wa dunia alisema ni baba
pekee anayejua siri hiyo lakini makubwa yatapita duniani kabla ya neno hilo kutimia.
Na kutokana na hilo wazo la kusoma alama za nyakati kuhusiana na Katiba huwa naliona kama ni jepesi sana.
Watu wanaozungumza suala la Katiba iliyoundwa na wachache wanaojua namna ya kuendesha nchi wakaipitisha katika Bunge, nalo ni wachache wenye dhamana ya kutunga sheria na kisha kufanyiwa kazi, lakini sasa wanataka Katiba mpya ya kuuliza kila mtu.
Naam, inawezekana kabisa. Lakini swali langu la msingi ambalo nataka kila mtu alifikirie ni hii
Katiba inayotoa nafasi ya kubadilishana mawazo kuhusu haja ya kuwa na Katiba mpya inajulikana kweli kwa watu?
Nauliza hivi kwa sababu itakapokuja hiyo drafti mpya tunaweza kujua tatizo lilikuwa wapi hasa katika kazi iliyopita? Mimi naona watu ni wa binafsi mno na wanataka kuendesha nchi katika
umri wa binadamu , hili haliwezekani, twendeni polepole ni mustakabali wa taifa na lazima kila mtu ajue nini kipo katika Katiba ya zamani, kasoro zake na kwanini ni lazima kuwa na Katiba mpya.
Kwa sababu nchi ni zaidi ya miaka 70 na ishirini ya kuazimwa na Mungu aliyonayo binadamu, inahitaji kwenda kwa mtindo kama wa jeshi kubwa katika kuwania kipito kidogo.
Katiba inaweka michoro muhimu ya maisha na kanuni na huwezi kudharau hilo kwani linaweza likatafsiriwa vibaya. Kama hali ni hiyo kama tunajadili juu juu tu ni sawa na kuona
kaburi zuri nje ndani kuna uvundo.
Pengine huo ni msimamo mbaya lakini kiukweli niseme kinachobaki katika Katiba ni muonekano unaoweza ama kukozwa au kuchushwa kwa kuzingatia mawazo ya kundi linalotaka mamlaka au linalotawala kwa wakati huo, na bila shaka tunaotaka Katiba mpya tu wapi na tuna sababu gani nje ya hii niliyoigusia.
Manake sehemu kubwa ya Katiba haifundishwi na wala vipengele vyake havijulikani vyema nini kanuni si ya msingi na itifaki za kimataifa tulizoridhia.
Kutokana na hoja yangu hapo juu napenda kuwauliza watu wanaotaka katiba , hivi ni kweli wanataka kuandikwa upya kwa Katiba au wana lao jambo? Nasema hivi kwa sababu nyingine kubwa kama hatujaaminiana.
Narejea tena hivi ni kweli tunataka katiba, nani anajua katiba ya zamani atatoa na mfano na kusema kutokana na ubaya wa Katiba hii hapa na pale na huko ni lazima kudai Katiba mpya, sivyo mimi naona kama Watanzania tunahemea juu juu kama mpira baharini, tumepigwa pampu.
Naam kwenye Biblia Waisrael walitaka kuwa kama wengine, wakataka watawala, Mungu akawapa kilichofuata nadhani walijuta, lakini wamekuwa kama wengine.
Huo ndio ukweli wa dunia ulio mchachu. Pamoja na ukweli kuwa tunahitaji katiba bado nadhani si sahihi kutuvurumisha Watanzania katika wimbo tusiouelewa; tueleweshane kwanza,
manake hiki ni kitu kikubwa na hakika tusipoeleweshana tunaweza kwenda msobemsobe halafu ikawa kiama hapa, bila taarifa ya haraka.
mwisho
HOJA ZA WATU
mwenye namba+255683019370 aliandika hivi...: Niseme moja kwa moja. kwanini uandike jambo ambalo hulifahamu na kutusumbua wapenzi wa habarileo?Soma mwenyewe wazo hableo ya tarehe 21/12 kuhusu katiba... unataka tufahamu au unaelewesha jamii kitu gani? nakuomba uiandike upya.Habarileo nalipenda... mwisho wa kunukuu.
mwingine aliandika hivi:
Katiba mpya?... Polepole jamani!
Name: DATUS MAHENDEKA
Email: datusmahendeka@yahoo.com
Date sent: 21st December 2010 @ 07:20
Comment: Una mawazo mazuri lakini Katiba Mpya inahitajika ndio maana viongozi waliopita na Mh. Pinda ameliona hilo.
na huyu naye
Katiba mpya?... Polepole jamani!
Name: joseph mwita
Email: terrell_bibbs@yahoo.com
Date sent: 21st December 2010 @ 04:05
Comment: Katiba mpya ni lazima,mwandishi sio kwa sababu unaandikia gazeti la siri kali ndio unataka kujikomba kwake. Wananchi tunataka katiba ambayo itapunguza mamlaka ya raisi,tume ya uchaguzi huru na mwananchi wa kawaida awe na uwezo wakuwachagua kwa kura viongozi wengi kuanzia watu kama wakuu wa mikoa. Wananchi wakitaka kitu hakuna kitu cha kuwazuia na wakati ni huu.
Hoja yangu:
Sikuandika ili kuma mtu yoyote pozi. nawakumbusha haja ya wananchi kuelewa ili kuwa na mchango mkubwa katika katiba na suala si haraka kwa sababu wewe unalifahamu. Asilimia 80 ya watu wa nchi hii wanategemea kilimo kujilisha na kusomesha watoto wao, ukilifahamu hilo, kifalsafa tu manake tuna watu wengi wasiojua mambo fulani yanayohusu maisha yao ndani ya jamii.wako katika jembe la mkono na dhiki yao kubwa ni chakula na wapi pa kupata vijisenti wanavyoporwa na wajanja kwa kuwapoa kima ksiichohalali kwa nguvu zao.
sasa ukiwa na watu wa aina hiyo ambayo hata maana na msingi wa katiba hawajui ni vyema kwanza ukafanya kazi ya kuwaelimisha. Zipo NGO nyingi zinazosema kwamba kazi yao ni kuelimisha jamii kuhusu mustakabali wao, lakini hawafanyi.
Mimi nataka mtu anieleze kwa kuanzia kwake mwenyewe, kama si baba yake, mkewe au mume wake kama si mjomba na shangazi yake mtoto wake wa kiume au wa kike kama kweli wanafahamu katiba tuanzie na hiyo iliyopigwa misele ya mwaka 1977.
Tuangalie katiba ya mwaka 1965 na tuangalie katiba ya mwanzo kabisa tuseme ya tanganyika ambayo ilikomba mpaka sheria ya kutozwa sh 100 kama unakutwa karibu na nyumba ya kulala wageni, sheria ambayo mpaka leo haijaondolewa wala kufanyiwa marekebisho.
Mimi si kwa sababu nafanyakazi serikalini ninajikomba, au mtu anadhani kwamba sifikiri, unatembea nchi hii unawauliza watuj maswali ya msingi kabisa kuhusu maisha yao hawajui cha kujibu, wanadhani kwamba serikali ndio mama na ndio baba yao na chama wanachokiamini hakifanyi makosa na viongozi wanawaamini hawafanyi makosa ndio wakombozi wao.
Kazi kubwa ya waandishi ni kuelimisha na kuwakumbusha watu, nimefanyakazi yangu si ya kupinga katiba bali binadamu lazima watengeneze subira katika kila hatua kubwa katika maisha ya nchi yao, itafika wakati suala linarejea kwa wananchi kwa usahihi, watasema nini kuhusu ukweli wa katiba kama wao wenyewe hawajui?
Madaraka ya Rais lazima yapunguzwe sawa tukiyapunguza tunayapeleka wapi na kiasi gani tumbakishie. Tunataka kuchagua viongozi wetu wa mikoa sisi wenyewe, kanuni zipi na aina gani ya demokrasia tunaifanya.
Tunataka haki za binadamu kwa kiwango gani na wapi mipaka . kama mimi nataka kutembea uchi kwanini unikataze , si unakataza haki yangu ya msingi.
Kuna mambo mengi yanayotakiwa kuangaliwa katika katiba si suala la kukurupuka na ili watu wawe na upeo mpana wa kuchangia ni lazima kwanza wajue nini maana ya katiba, kuangalia wenzao wamefanya nini, kuna marekebisho gani yanatakiwa na wapi ni mipaka na kwanini mashoga wasiwe sehemu ya katiba na kila mtu akafanya lake. Nini utamaduni wetu katika hili kwa sababu sisi si kisiwa lakini pia si wapuuzi.
Hilo ndilo hasa nililotaka kuwakumbusha watu. Ukiwa na hasira huwezi kuliona hili na kama hujawahi kukaa na kuongoza watu katika misukosuko hakika huwezi kuwa na busara kwa sababu wewe unataka leo kumbe unatakiwa kuangalia kasi ya mabadiliko ya mambo duniani, kuhami yale mazuri na kuhakikisha kwamba watu hawapotoki kwa kuwa na tafsiri finyu ya uhuru wao ndani ya katiba.
Labda hili linaweza kueleweka.
Tumeenda shule kwa sababu hizi hizi kuangalia wka kina masuala mazito yanayohusu jamii kwa kuishirikisha vyema lakini si kuwaburuza.
naitwa Beda Msimbe kutoka juu ya milima ya Uluguru, upande wa Magharibi wa Lukwangule.
Katika gazeti la leo la Habarileo ambalo ndilo ninalofanyia kazi niliandika wazo langu. Limesomwa na watu si haba. Kuna vitu watu hukasirika wakisoma mawazo mengine. Lakini pia kuna watu wanaokasirika wakiulizwa maswali. Kuna hoja nyingi ambazo zingine zilitumwa katika simu yangu binafsi.Si mbaya nikasema haya yafuatayo baada ya wewe kuisoma habari yenyewe.
Lukwangule
Katiba Mpya polepole jamani
UKIFUNGUA Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 katika utangulizi wake unaona misingi ya Katiba na katika misingi hiyo unakutana na sababu kwanini tuna Katiba.
Pamoja na sababu hiyo pia inaelezwa kuwa Katiba iliandikwa na watu ikapitishwa katika Bunge na kisha kuanza kutumika kwa manufaa ya watu wa taifa hili na nchi kwa ujumla wake.
Nchi bila Katiba itakuwa nchi yenye ufisadi wa aina yake na hii inaweza kuleta mushkeri mkubwa kwa binadamu.
Kwa sasa kuna maneno, kelele na mazungumzo yanayoendelea miongoni mwa watu waliobahatika kujua maana ya Katiba na hatima ya mazungumzo yao mara zote wanataka
Katiba mpya na wanatushawishi wengine kwamba bila Katiba mpya hakutakuwa na uchaguzi huru na wa haki.
Naam, kwa Katiba hii hii tumepata uongozi wa kisiasa, kwa Katiba hii hii tuna mhimili wa Bunge na Mahakama na uongozi na kwa Katiba hii hii inayochanwa na kusimangwa
tunakuwa na demokrasia mpya.
Unapofungua Katiba na kukutana na maneno yafuatayo (nanukuu): KWAKUWASISI Wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tumeamua rasmi na kwa dhati kujenga katika nchi yetu jamii inayozingatia misingi ya uhuru, haki, udugu na amani: Tuendelee.
Katika mijadala inayoendelea hakuna hata mtu mmoja anayesema katika maelfu ya maneno
yaliyomo katika Katiba wapi pana tatizo na panahitaji kubadilishwa, mazungumzo na kelele ni kwamba Katiba hiyo imepigwa viraka 14 inastahili kufumuliwa na kuundwa upya.
Pia inazungumzia ujamaa ambao hatuufuati. Hili lahitaji majadiliano zaidi. Sina sababu ya kusoma alama za nyakati, kwani huona hizi alama zinapoteza watu mawazo ya kusonga
mbele na ukweli huo unazingatia mabishano ya sasa kwamba mwisho wa kuinjilisha ni mwaka
wa kesho na mwaka wa kesho kutwa Mei 21 Mungu anamaliza hesabu zake.
Mimi ni Mkatoliki nakumbuka ipo sehemu alipoulizwa Yesu mwisho wa dunia alisema ni baba
pekee anayejua siri hiyo lakini makubwa yatapita duniani kabla ya neno hilo kutimia.
Na kutokana na hilo wazo la kusoma alama za nyakati kuhusiana na Katiba huwa naliona kama ni jepesi sana.
Watu wanaozungumza suala la Katiba iliyoundwa na wachache wanaojua namna ya kuendesha nchi wakaipitisha katika Bunge, nalo ni wachache wenye dhamana ya kutunga sheria na kisha kufanyiwa kazi, lakini sasa wanataka Katiba mpya ya kuuliza kila mtu.
Naam, inawezekana kabisa. Lakini swali langu la msingi ambalo nataka kila mtu alifikirie ni hii
Katiba inayotoa nafasi ya kubadilishana mawazo kuhusu haja ya kuwa na Katiba mpya inajulikana kweli kwa watu?
Nauliza hivi kwa sababu itakapokuja hiyo drafti mpya tunaweza kujua tatizo lilikuwa wapi hasa katika kazi iliyopita? Mimi naona watu ni wa binafsi mno na wanataka kuendesha nchi katika
umri wa binadamu , hili haliwezekani, twendeni polepole ni mustakabali wa taifa na lazima kila mtu ajue nini kipo katika Katiba ya zamani, kasoro zake na kwanini ni lazima kuwa na Katiba mpya.
Kwa sababu nchi ni zaidi ya miaka 70 na ishirini ya kuazimwa na Mungu aliyonayo binadamu, inahitaji kwenda kwa mtindo kama wa jeshi kubwa katika kuwania kipito kidogo.
Katiba inaweka michoro muhimu ya maisha na kanuni na huwezi kudharau hilo kwani linaweza likatafsiriwa vibaya. Kama hali ni hiyo kama tunajadili juu juu tu ni sawa na kuona
kaburi zuri nje ndani kuna uvundo.
Pengine huo ni msimamo mbaya lakini kiukweli niseme kinachobaki katika Katiba ni muonekano unaoweza ama kukozwa au kuchushwa kwa kuzingatia mawazo ya kundi linalotaka mamlaka au linalotawala kwa wakati huo, na bila shaka tunaotaka Katiba mpya tu wapi na tuna sababu gani nje ya hii niliyoigusia.
Manake sehemu kubwa ya Katiba haifundishwi na wala vipengele vyake havijulikani vyema nini kanuni si ya msingi na itifaki za kimataifa tulizoridhia.
Kutokana na hoja yangu hapo juu napenda kuwauliza watu wanaotaka katiba , hivi ni kweli wanataka kuandikwa upya kwa Katiba au wana lao jambo? Nasema hivi kwa sababu nyingine kubwa kama hatujaaminiana.
Narejea tena hivi ni kweli tunataka katiba, nani anajua katiba ya zamani atatoa na mfano na kusema kutokana na ubaya wa Katiba hii hapa na pale na huko ni lazima kudai Katiba mpya, sivyo mimi naona kama Watanzania tunahemea juu juu kama mpira baharini, tumepigwa pampu.
Naam kwenye Biblia Waisrael walitaka kuwa kama wengine, wakataka watawala, Mungu akawapa kilichofuata nadhani walijuta, lakini wamekuwa kama wengine.
Huo ndio ukweli wa dunia ulio mchachu. Pamoja na ukweli kuwa tunahitaji katiba bado nadhani si sahihi kutuvurumisha Watanzania katika wimbo tusiouelewa; tueleweshane kwanza,
manake hiki ni kitu kikubwa na hakika tusipoeleweshana tunaweza kwenda msobemsobe halafu ikawa kiama hapa, bila taarifa ya haraka.
mwisho
HOJA ZA WATU
mwenye namba+255683019370 aliandika hivi...: Niseme moja kwa moja. kwanini uandike jambo ambalo hulifahamu na kutusumbua wapenzi wa habarileo?Soma mwenyewe wazo hableo ya tarehe 21/12 kuhusu katiba... unataka tufahamu au unaelewesha jamii kitu gani? nakuomba uiandike upya.Habarileo nalipenda... mwisho wa kunukuu.
mwingine aliandika hivi:
Katiba mpya?... Polepole jamani!
Name: DATUS MAHENDEKA
Email: datusmahendeka@yahoo.com
Date sent: 21st December 2010 @ 07:20
Comment: Una mawazo mazuri lakini Katiba Mpya inahitajika ndio maana viongozi waliopita na Mh. Pinda ameliona hilo.
na huyu naye
Katiba mpya?... Polepole jamani!
Name: joseph mwita
Email: terrell_bibbs@yahoo.com
Date sent: 21st December 2010 @ 04:05
Comment: Katiba mpya ni lazima,mwandishi sio kwa sababu unaandikia gazeti la siri kali ndio unataka kujikomba kwake. Wananchi tunataka katiba ambayo itapunguza mamlaka ya raisi,tume ya uchaguzi huru na mwananchi wa kawaida awe na uwezo wakuwachagua kwa kura viongozi wengi kuanzia watu kama wakuu wa mikoa. Wananchi wakitaka kitu hakuna kitu cha kuwazuia na wakati ni huu.
Hoja yangu:
Sikuandika ili kuma mtu yoyote pozi. nawakumbusha haja ya wananchi kuelewa ili kuwa na mchango mkubwa katika katiba na suala si haraka kwa sababu wewe unalifahamu. Asilimia 80 ya watu wa nchi hii wanategemea kilimo kujilisha na kusomesha watoto wao, ukilifahamu hilo, kifalsafa tu manake tuna watu wengi wasiojua mambo fulani yanayohusu maisha yao ndani ya jamii.wako katika jembe la mkono na dhiki yao kubwa ni chakula na wapi pa kupata vijisenti wanavyoporwa na wajanja kwa kuwapoa kima ksiichohalali kwa nguvu zao.
sasa ukiwa na watu wa aina hiyo ambayo hata maana na msingi wa katiba hawajui ni vyema kwanza ukafanya kazi ya kuwaelimisha. Zipo NGO nyingi zinazosema kwamba kazi yao ni kuelimisha jamii kuhusu mustakabali wao, lakini hawafanyi.
Mimi nataka mtu anieleze kwa kuanzia kwake mwenyewe, kama si baba yake, mkewe au mume wake kama si mjomba na shangazi yake mtoto wake wa kiume au wa kike kama kweli wanafahamu katiba tuanzie na hiyo iliyopigwa misele ya mwaka 1977.
Tuangalie katiba ya mwaka 1965 na tuangalie katiba ya mwanzo kabisa tuseme ya tanganyika ambayo ilikomba mpaka sheria ya kutozwa sh 100 kama unakutwa karibu na nyumba ya kulala wageni, sheria ambayo mpaka leo haijaondolewa wala kufanyiwa marekebisho.
Mimi si kwa sababu nafanyakazi serikalini ninajikomba, au mtu anadhani kwamba sifikiri, unatembea nchi hii unawauliza watuj maswali ya msingi kabisa kuhusu maisha yao hawajui cha kujibu, wanadhani kwamba serikali ndio mama na ndio baba yao na chama wanachokiamini hakifanyi makosa na viongozi wanawaamini hawafanyi makosa ndio wakombozi wao.
Kazi kubwa ya waandishi ni kuelimisha na kuwakumbusha watu, nimefanyakazi yangu si ya kupinga katiba bali binadamu lazima watengeneze subira katika kila hatua kubwa katika maisha ya nchi yao, itafika wakati suala linarejea kwa wananchi kwa usahihi, watasema nini kuhusu ukweli wa katiba kama wao wenyewe hawajui?
Madaraka ya Rais lazima yapunguzwe sawa tukiyapunguza tunayapeleka wapi na kiasi gani tumbakishie. Tunataka kuchagua viongozi wetu wa mikoa sisi wenyewe, kanuni zipi na aina gani ya demokrasia tunaifanya.
Tunataka haki za binadamu kwa kiwango gani na wapi mipaka . kama mimi nataka kutembea uchi kwanini unikataze , si unakataza haki yangu ya msingi.
Kuna mambo mengi yanayotakiwa kuangaliwa katika katiba si suala la kukurupuka na ili watu wawe na upeo mpana wa kuchangia ni lazima kwanza wajue nini maana ya katiba, kuangalia wenzao wamefanya nini, kuna marekebisho gani yanatakiwa na wapi ni mipaka na kwanini mashoga wasiwe sehemu ya katiba na kila mtu akafanya lake. Nini utamaduni wetu katika hili kwa sababu sisi si kisiwa lakini pia si wapuuzi.
Hilo ndilo hasa nililotaka kuwakumbusha watu. Ukiwa na hasira huwezi kuliona hili na kama hujawahi kukaa na kuongoza watu katika misukosuko hakika huwezi kuwa na busara kwa sababu wewe unataka leo kumbe unatakiwa kuangalia kasi ya mabadiliko ya mambo duniani, kuhami yale mazuri na kuhakikisha kwamba watu hawapotoki kwa kuwa na tafsiri finyu ya uhuru wao ndani ya katiba.
Labda hili linaweza kueleweka.
Tumeenda shule kwa sababu hizi hizi kuangalia wka kina masuala mazito yanayohusu jamii kwa kuishirikisha vyema lakini si kuwaburuza.
naitwa Beda Msimbe kutoka juu ya milima ya Uluguru, upande wa Magharibi wa Lukwangule.
COMMENTS