Katiba ya Marekani yenye miaka 200 imefanyiwa marekebisho mara 27 na mara ya mwisho ilifanyiwa marekebisho Mei 7,1992 kwa Rekebisho lililope...
Katiba ya Marekani yenye miaka 200 imefanyiwa marekebisho mara 27 na mara ya mwisho ilifanyiwa marekebisho Mei 7,1992 kwa Rekebisho lililopendekezwa Septemba 25,1789.
Rekebisho la kwanza mpaka la 10 lilihusu haki za binadamu pamoja na haja ya kupasha na kupashwa habari na marekebisho yaliyobaki ambayo yalifanyika zamani pia yalihusu uawakilishi , dhamana yake na sheria.
Kimsingi pamoja na ukweli kuwa katiba ni msingi wa sheria mama kubadili katiba kiholela ni tatizo na mara nyingi watu wenye kuelewa mambo hutumia viraka kujazia maeneo ambayo yana upungufu.
Nimeamua kuchukau mfano wa Marekani kutokana na mazungumzo yanayofanyika nchini, majadiliano ambayo wakati wmingine yanaona yanaenda kasi na wengine wanaingia tu katika mkumbo bila kuelewa dhana nzima ya katiba,uwekaji viraka na pia maana nzima ya katiba mpya.
Wamarekani waliunda katiba yao ya kwanza polepole kwa makubaliano ya viongozi wa mataifa yaliyofanya Marekani lakini rasimu yao ilichukua muda kuandikwa na wala hawakuanza kuiandika mpaka wote waliohusika walikuwapo.
Ukiangalia simulizi unaposoma katiba ya Marekani utaona kwamba mkutano wa katiba uliofanyika katika Jumba la serikali(Independence Hall) mjini Philadelphia hapo Mei 14, 1787, kupitia vifungu vya katiba ulibidi kutoanza kutokana na ukweli kuwa wajumbe wa majimbo mawili tu walikuwa wamefika kwa ajili ya mkutano.
Mkutano uliahirishwa mpaka wajumbe wa majimbo saba walipofika Mei 25 mwaka huo.
Na katika majadiliano katikati ya Juni ilionekana dhahiri kwamba ile katiba ya mwanzo iliyokuwa inajadiliwa haifai na lazima itengenezwe mpya na kutoa muonekano mpya kabisa wa serikali.
Kipindi chote cha majira ya kiangazi kilitumika kuandika na kufuta na kuandika tena huku majadiliano yakiwa makali.
Mambo makubwa ambayo yalijadiliwa kwa muda mwingi ni serikali kuu iwe na mamlaka kiasi gani, watu wangapi wanatakiwa katika bunge (congress)na uwakilishi wa kila jimbo wakati suala la namna ya kuchaguliwa likitiliwa maanani.
Suala ilikuwa je wawakilishi hawa wachaguliwe na wananchi moja kwa moja au watokane na mabunge ya majimbo yao.
Walifikia mwisho na katiba ikatengenezwa lakini Wamarekani wenyewe wanasema katiba yao inatokana na ushirikiano,kukubaliana kutokukubaliana lakini ni katiba ambayo inaonesha mshikamano mkubwa wa uongozi na haja za wananchi.
Katiba kwa kuwa kimsingi ni kanuni au utaratibu wa uendeshaji wa taifa huru ambapo wananchi hutumia kwa ajili ya kuidhibiti serikali, bunge na Mahakama na kuhakikisha vyombo mvyote hivyo vinafanyakazi yake inayostahili ni kitu ambacho hakihitaji kukurupukiwa.
Ndani ya katiba kunazungumzwa mfumo wa maisha ambapo yenyewe inakuwa ndio sheria mama ya nchi.
Inapaswa ieleweke kuwa lengo kuu la katiba ni kutengeneza njia au mfumo ambao unastahili kuendeshwa na serikali kwa watu wake, kuelekeza ukomo wa mamlaka na utendaji wa mihimili ya dola.
Utengenezaji wa katiba unaweza kuwa ni kwa kuzingatia historia au bunge kutengeneza au kundi la watu kutengeneza na kupigiwa kura au watu kuzungumza lakini lazima iwepo rasimu.
Chochote kinachoweza kutokea katiba nzuri ni ile ambayo ni ndogo iliyozingatia mahitaji ya msingi ya jamii inayoeleza wazi mipaka ya kila kitu katika uendeshaji wa nchi na mamlaka zinazotolewa kwa nchi.
Katiba ya Marekani katika uhai wake imefanyiwa marekebisho ya msingi 27 na ikumbukwe kwamba hawa walitengeneza katiba yao baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Katiba ya Tanzania ambayo tayari imerekebishwa mara 14 haiwezi kuwa mbaya kuliko ya Marekani ambayo kwanza ilikuwa na historia tofauti.
India ambao walipata uhuru wao mwaka 1947 wameifanyia katiba yao marekebisho mara 50 na hawa hawana katiba nzuri zaidi ya Tanzania au mbaya zaidi ya Tanzania.
Kimtazamo ni rahisi lakini ni wazi kunatakiwa subira katika kutengeneza katiba mpya lakini kunahitaji mawazo na usahihi wa falsafa ya nchi hii kutengeneza viraka sahihi ili tuwe na mengine ya kufanya kuliko kujadili kitu ambacho wengi wetu hatuelewi.
Bado Marekani walitengeneza kundi la watu na mabadiliko yakafanyika kwa kupitia Bunge kwa kuridhia na yote unaona yanayoingizwa ni kukabiliana na mabadiliko yanayohitajika.
Pengine ni vyema wananchi wakatambua haja ya kutambua kilichopo katika katiba ya sasa na kuona ni namna gani wanaweza kushiriki katika mjadala huu na wala si wa siku moja, bali wa muda wa kutosha kuwawezesha kuchora ramani sawia ya uongozi wa nchi.
Rekebisho la kwanza mpaka la 10 lilihusu haki za binadamu pamoja na haja ya kupasha na kupashwa habari na marekebisho yaliyobaki ambayo yalifanyika zamani pia yalihusu uawakilishi , dhamana yake na sheria.
Kimsingi pamoja na ukweli kuwa katiba ni msingi wa sheria mama kubadili katiba kiholela ni tatizo na mara nyingi watu wenye kuelewa mambo hutumia viraka kujazia maeneo ambayo yana upungufu.
Nimeamua kuchukau mfano wa Marekani kutokana na mazungumzo yanayofanyika nchini, majadiliano ambayo wakati wmingine yanaona yanaenda kasi na wengine wanaingia tu katika mkumbo bila kuelewa dhana nzima ya katiba,uwekaji viraka na pia maana nzima ya katiba mpya.
Wamarekani waliunda katiba yao ya kwanza polepole kwa makubaliano ya viongozi wa mataifa yaliyofanya Marekani lakini rasimu yao ilichukua muda kuandikwa na wala hawakuanza kuiandika mpaka wote waliohusika walikuwapo.
Ukiangalia simulizi unaposoma katiba ya Marekani utaona kwamba mkutano wa katiba uliofanyika katika Jumba la serikali(Independence Hall) mjini Philadelphia hapo Mei 14, 1787, kupitia vifungu vya katiba ulibidi kutoanza kutokana na ukweli kuwa wajumbe wa majimbo mawili tu walikuwa wamefika kwa ajili ya mkutano.
Mkutano uliahirishwa mpaka wajumbe wa majimbo saba walipofika Mei 25 mwaka huo.
Na katika majadiliano katikati ya Juni ilionekana dhahiri kwamba ile katiba ya mwanzo iliyokuwa inajadiliwa haifai na lazima itengenezwe mpya na kutoa muonekano mpya kabisa wa serikali.
Kipindi chote cha majira ya kiangazi kilitumika kuandika na kufuta na kuandika tena huku majadiliano yakiwa makali.
Mambo makubwa ambayo yalijadiliwa kwa muda mwingi ni serikali kuu iwe na mamlaka kiasi gani, watu wangapi wanatakiwa katika bunge (congress)na uwakilishi wa kila jimbo wakati suala la namna ya kuchaguliwa likitiliwa maanani.
Suala ilikuwa je wawakilishi hawa wachaguliwe na wananchi moja kwa moja au watokane na mabunge ya majimbo yao.
Walifikia mwisho na katiba ikatengenezwa lakini Wamarekani wenyewe wanasema katiba yao inatokana na ushirikiano,kukubaliana kutokukubaliana lakini ni katiba ambayo inaonesha mshikamano mkubwa wa uongozi na haja za wananchi.
Katiba kwa kuwa kimsingi ni kanuni au utaratibu wa uendeshaji wa taifa huru ambapo wananchi hutumia kwa ajili ya kuidhibiti serikali, bunge na Mahakama na kuhakikisha vyombo mvyote hivyo vinafanyakazi yake inayostahili ni kitu ambacho hakihitaji kukurupukiwa.
Ndani ya katiba kunazungumzwa mfumo wa maisha ambapo yenyewe inakuwa ndio sheria mama ya nchi.
Inapaswa ieleweke kuwa lengo kuu la katiba ni kutengeneza njia au mfumo ambao unastahili kuendeshwa na serikali kwa watu wake, kuelekeza ukomo wa mamlaka na utendaji wa mihimili ya dola.
Utengenezaji wa katiba unaweza kuwa ni kwa kuzingatia historia au bunge kutengeneza au kundi la watu kutengeneza na kupigiwa kura au watu kuzungumza lakini lazima iwepo rasimu.
Chochote kinachoweza kutokea katiba nzuri ni ile ambayo ni ndogo iliyozingatia mahitaji ya msingi ya jamii inayoeleza wazi mipaka ya kila kitu katika uendeshaji wa nchi na mamlaka zinazotolewa kwa nchi.
Katiba ya Marekani katika uhai wake imefanyiwa marekebisho ya msingi 27 na ikumbukwe kwamba hawa walitengeneza katiba yao baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.
Katiba ya Tanzania ambayo tayari imerekebishwa mara 14 haiwezi kuwa mbaya kuliko ya Marekani ambayo kwanza ilikuwa na historia tofauti.
India ambao walipata uhuru wao mwaka 1947 wameifanyia katiba yao marekebisho mara 50 na hawa hawana katiba nzuri zaidi ya Tanzania au mbaya zaidi ya Tanzania.
Kimtazamo ni rahisi lakini ni wazi kunatakiwa subira katika kutengeneza katiba mpya lakini kunahitaji mawazo na usahihi wa falsafa ya nchi hii kutengeneza viraka sahihi ili tuwe na mengine ya kufanya kuliko kujadili kitu ambacho wengi wetu hatuelewi.
Bado Marekani walitengeneza kundi la watu na mabadiliko yakafanyika kwa kupitia Bunge kwa kuridhia na yote unaona yanayoingizwa ni kukabiliana na mabadiliko yanayohitajika.
Pengine ni vyema wananchi wakatambua haja ya kutambua kilichopo katika katiba ya sasa na kuona ni namna gani wanaweza kushiriki katika mjadala huu na wala si wa siku moja, bali wa muda wa kutosha kuwawezesha kuchora ramani sawia ya uongozi wa nchi.
COMMENTS