OFISA Mtendaji wa Kata ya Kibungo Juu, Tarafa ya Matombo, Wilaya ya Morogoro , Silvester Mpangwa na Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Chisundik...
OFISA Mtendaji wa Kata ya Kibungo Juu, Tarafa ya Matombo, Wilaya ya Morogoro , Silvester Mpangwa na Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Chisundike , Kata ya Tawa, Jumanne Zuberi , wametiwa mbaroni na Polisi na baadaye kufikishwa Mahakamani kwa kutuhumiwa wizi wa vitabu vitatu vya Vocha za Pembejeo za Ruzuku , imefahamika.
Kutiwa mbaroni kwa Watendaji hao kulitokana na agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo, Said Mwambungu , ni baada ya kufichuliwa na wenzao wanne waliokuwemo kwenye safari moja ndani ya gari la Serikali lilolobeba makasha wenye vocha hizo eneo la Kata ya Tawa , katika Tarafa hiyo .
Maofisa Watendaji hao bila aibu waliamua kuvichomoa kwa njia ya siri vitabu hivyo vilivyohifadhiwa kwenye kasha na kuvificha katika mikoba yao, huku wakifikiri kitendo chao hicho hakijabainiwa na wenzao waliokuwemo ndani ya gari hilo.
Akizungumza kutiwa mbarobni kwa watendaji hao na kufikishwa Mahakamani , mbele ya Naibu Waziri wa Tamisemi, Aggrey Mwanri, juzi , katika mkutano na wadau wa maendeleo wa Wilaya hiyo, Mkuu wa Wilaya , Said Mwambungu, alisema kuwa ndani ya gari hilo walikuwemo watendaji sita ambapo wawili ndiyo wakiochomoa vitabu na kuonwa na wezao wanne waliokuwemo katika safari hiyo.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya , kuwa wakati akipotelemka katika eneo la Tawa , watendaji wanne waliamua kuwabonyeza viongozi waliokuwAmo katika msafara huo kuhusu njama hizo za kuiba vitabu hivyo na walipobanwa na viongozi hao walikiri kuvichomoa vitabu hivyo .
Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa , katika jaribio hilo lililoshindwa, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kibungo Juu alichomoa vitabu viwili vya vocha na kuviFicha , wakati Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Chisundike alichomoa kitabu kimoja hivyo kufanya vitabu hivyo kuwa vitatu.
Sakata za kuhujumiwa kwa mpango wa ugawaji wa vocha za ruzuku ulijitokeza kwa mara ya kwanza Wilaya ya Mvomero katika Kijiji cha Maharaka , Kata ya Doma, ambapo wakulima 219 kati ya 225 waliosaonishwa vocha hizo walipewa ‘mapoozeo’ya sh: 10,000 na kusamehe kuchukua mbegu na mbolea hizo.
Katika sakata hilo , Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Fatma Mwassa, Desemba 31, mwaka jana aliamuru kukamatwa kwa Wakala wa vocha za ruzuku wa Kata hiyo, Mtendaji wa Serikali ya Kijiji hicho , na viongozi wa kamati ya vocha ya Kijiji na watu wengine na kufikia idadi ya watu 14 kutiwa mbaroni na kufikishwa mahakamani.
Hata hivyo kutokana na juhuma hizo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya , Januari 3, 2011 , aliamuakusitisha kwa muda zoezi la ugawaji wa vocha za ruzuku na kuagiza kuhakikiwa upya katika Wilaya zote na kuanza zoezi hilo upya , ambapo mawakala watakaobainika waliingia kupitian njia haramu wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria na wale waliowasaidia kupata tenda hizo.
Mkoa wa Morogoro katika mwaka huu wa fedha wa 2010/2011 umepata mgao wa vocha 422,118 , ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero imepata vocha 87,531, na Halmashauri nyingine vocha zake katika mabano ni pamoja na Kilosa (63,333), Morogoro vijijini ( 61,497, Mvomero ( 103,152), Ulanga ( 74,592) na Manispaa ya Morogoro ni 32,013.
Mwisho.
Kutiwa mbaroni kwa Watendaji hao kulitokana na agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo, Said Mwambungu , ni baada ya kufichuliwa na wenzao wanne waliokuwemo kwenye safari moja ndani ya gari la Serikali lilolobeba makasha wenye vocha hizo eneo la Kata ya Tawa , katika Tarafa hiyo .
Maofisa Watendaji hao bila aibu waliamua kuvichomoa kwa njia ya siri vitabu hivyo vilivyohifadhiwa kwenye kasha na kuvificha katika mikoba yao, huku wakifikiri kitendo chao hicho hakijabainiwa na wenzao waliokuwemo ndani ya gari hilo.
Akizungumza kutiwa mbarobni kwa watendaji hao na kufikishwa Mahakamani , mbele ya Naibu Waziri wa Tamisemi, Aggrey Mwanri, juzi , katika mkutano na wadau wa maendeleo wa Wilaya hiyo, Mkuu wa Wilaya , Said Mwambungu, alisema kuwa ndani ya gari hilo walikuwemo watendaji sita ambapo wawili ndiyo wakiochomoa vitabu na kuonwa na wezao wanne waliokuwemo katika safari hiyo.
Kwa mujibu wa Mkuu huyo wa Wilaya , kuwa wakati akipotelemka katika eneo la Tawa , watendaji wanne waliamua kuwabonyeza viongozi waliokuwAmo katika msafara huo kuhusu njama hizo za kuiba vitabu hivyo na walipobanwa na viongozi hao walikiri kuvichomoa vitabu hivyo .
Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa , katika jaribio hilo lililoshindwa, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kibungo Juu alichomoa vitabu viwili vya vocha na kuviFicha , wakati Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Chisundike alichomoa kitabu kimoja hivyo kufanya vitabu hivyo kuwa vitatu.
Sakata za kuhujumiwa kwa mpango wa ugawaji wa vocha za ruzuku ulijitokeza kwa mara ya kwanza Wilaya ya Mvomero katika Kijiji cha Maharaka , Kata ya Doma, ambapo wakulima 219 kati ya 225 waliosaonishwa vocha hizo walipewa ‘mapoozeo’ya sh: 10,000 na kusamehe kuchukua mbegu na mbolea hizo.
Katika sakata hilo , Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Fatma Mwassa, Desemba 31, mwaka jana aliamuru kukamatwa kwa Wakala wa vocha za ruzuku wa Kata hiyo, Mtendaji wa Serikali ya Kijiji hicho , na viongozi wa kamati ya vocha ya Kijiji na watu wengine na kufikia idadi ya watu 14 kutiwa mbaroni na kufikishwa mahakamani.
Hata hivyo kutokana na juhuma hizo, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Issa Machibya , Januari 3, 2011 , aliamuakusitisha kwa muda zoezi la ugawaji wa vocha za ruzuku na kuagiza kuhakikiwa upya katika Wilaya zote na kuanza zoezi hilo upya , ambapo mawakala watakaobainika waliingia kupitian njia haramu wanafikishwa kwenye vyombo vya sheria na wale waliowasaidia kupata tenda hizo.
Mkoa wa Morogoro katika mwaka huu wa fedha wa 2010/2011 umepata mgao wa vocha 422,118 , ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Kilombero imepata vocha 87,531, na Halmashauri nyingine vocha zake katika mabano ni pamoja na Kilosa (63,333), Morogoro vijijini ( 61,497, Mvomero ( 103,152), Ulanga ( 74,592) na Manispaa ya Morogoro ni 32,013.
Mwisho.
COMMENTS