CHADEMA YAZUNGUMZIA ZIARA YA DK SLAA MIKOANI

Katibu Mkuu Chadema *TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI* KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod ...

Katibu Mkuu Chadema

*TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI*

KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dkt. Willibrod
Slaa amehitimisha ziara ya siku 10 ya kujenga chama na kukagua uhai wa
chama katika mikoa mitano, Tabora, Shinyanga, Simiyu, Geita na Mwanza,
ambako katika maeneo mbalimbali alikopita amesimamia vikao vya kiutendaji
ambavyo vimelazimika kuchukua maamuzi mazito na muhimu dhidi ya watu
waliobainika kuhujumu maendeleo ya wananchi, kukihujumu chama, kuvunja
katiba, kanuni na taratibu za CHADEMA.

Moja ya maamuzi hayo mazito ni kuvuliwa kwa uanachama kwa aliyekuwa Diwani
wa Kata ya Katoro, Gervas Daudi, kufutwa uongozi wa BAVICHA Geita, kuvuliwa
uanachama baadhi ya viongozi na wanachama ambao baada ya kuhojiwa na vikao
walibainika pasi na shaka kuwa wamekuwa wakihujumu chama hivyo kukwaza
matumaini ya wananchi kwa CHADEMA, kuwa chama mbadala nchini. Watu hao
waliovuliwa uanachama watalazimika kusubiri maamuzi zaidi ya Kamati Kuu
inayotarajiwa kuketi hivi karibuni, ili kujua hatma yao ndani ya CHADEMA.

Akiwa katika vikao hivyo vilivyofanya maamuzi hayo mazito, Katibu Mkuu Dkt.
Slaa alilazimika kutoa kauli kali akisema kuwa chama hakitakubali kulea
viongozi wasiowajibika kwa watu, akisisitiza kuwa kama kuna kiongozi yeyote
hawezi kuendana na kasi ya mahitaji ya chama hicho katika kuwatumikia watu,
anapaswa kupisha mara moja badala ya kukwaza juhudi hizo.

*“Viongozi wangu naomba mtambue, chama hiki si mali ya mtu, wala si chama
cha viongozi, ni chama cha wananchi, ni chama cha watu, ni chama cha
Watanzania. Hiki si chama cha kukaa siku nzima kutatua migogoro, ni chama
cha kutafakari suluhisho la matatizo mbalimbali yanayowakabili Watanzania.
Chadema ni tumaini pekee la Watanzania kwa sasa.*

*“Hatutavumilia ufisadi, hatutavumilia uzembe, hatutakubali viongozi
wanaojali maslahi yao badala ya wananchi, katika hili CHADEMA tutakuwa
wakali kwa yeyote hata kama angekuwa ni katibu mkuu, hatuwezi kujifungia
kuzungumzia migogoro inayosababishwa na ubinafsi wa watu badala ya kutumia
muda huu kuzungumzia kero na maendeleo ya watu,” amesisitiza Dkt. Slaa
katika ziara hiyo.*

Katika ziara hiyo iliyoanzia Nzega, mkoani Tabora, Aprili 13 na kumalizikia
Jijini Mwanza Aprili 22, 2012, Katibu Mkuu Dkt. Slaa kupitia vikao hivyo
vya kimaamuzi amelazimika pia kutoa kauli kali dhidi ya viongozi na
wanachama wanaoonekana kukwaza jitihada za CHADEMA katika kuwatumikia watu,
akisema kuwa chama hiki ndiyo tumaini pekee lililobaki kwa Watanzania
katika harakati za ukombozi wa awamu ya pili, kutafuta mabadiliko ya
kimfumo na kiutawala nchini kwa ajili ya maendeleo ya watu.

Wilayani Nzega, kikao cha kiutendaji kiliwavua uongozi aliyekuwa Mwenyekiti
wa Jimbo, Tito Onesmo kutokana na kupata nafasi hiyo kinyume cha utaratibu
na Katibu Mwenezi, Shaaban Mohamed kwa kosa la kughushi barua. Wote
walipewa karipio kali na kutakiwa kuandika barua ya maelezo kwa nini
wasichukuliwe hatua kali zaidi. Mohamed baada ya kubanwa na kukosa utetezi
wa makosa yake, aliamua kurejesha kadi ya uanachama mbele ya kikao hicho.

Katika Wilaya ya Bariadi, Katibu Mkuu alifutilia mbali kile kilichoitwa
uongozi wa Mkoa wa Simiyu kwani kwa taratibu za chama mkoa huo bado haupo,
hivyo uchaguzi ulikuwa batili tangu mwanzo.

Viongozi wa Wilaya ya Bariadi waliohusika katika kuitisha uchaguzi huo,
akiwemo Mwenyekiti Mwenyekiti wa Wilaya Limbu Ntalima, Katibu wake Elias
Maduka Kaselabantu na Mwenyekiti wa Vijana wa Wilaya, Khamis Rajab, na
Bwana Kube Kube aliyechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Mkoa, walipewa onyo kali,
kuwekwa chini ya uangalizi maalum kwa kipindi cha miezi 12, kuangalia
mwenendo wao ndani ya chama, huku pia Kube akitakiwa kuandika barua ndani
ya siku 30 kueleza kwa nini alikuwa nyuma ya suala hilo.

Mbali ya kufutilia mbali uongozi huo, kikao hicho kiliwaondoa madarakani
viongozi wa wilaya waliochukua madaraka isivyohalali aliyekuwa Mwenyekiti
wa Wilaya Limbu Ntalima, Katibu wake Elias Maduka Kaselabantu na Mwenyekiti
wa Vijana wa Wilaya, Khamis Rajab kwa kukiuka katiba ya chama na kukihujumu
katika uchaguzi mdogo wa kutafuta Diwani wa Kata ya Legangabilili, ambapo
CHADEMA ilikuwa ikipewa asilimia kubwa ya kuibuka mshindi.

Viongozi hao waliomba radhi na kuahidi mbele ya kikao kuwa mara moja
watakwenda kufuta kesi waliyofungua mahakamani kuhoji uhalali wa Kamati
Maalum (task force) iliyoundwa kwa ajili ya kuongoza chama wilayani Bariadi
kwa muda.

Katika Wilaya ya Kahama, Baraza la Mashauriano lilikubaliana kwa kauli moja
Charles Dotto Lubala, Anastazia Kanyanda na Justine Mganga wavuliwe
uanachama, huku wenzao 12 wakiwekwa chini ya uangalizi maalum kwa kosa la
kusababisha mgogoro ndani ya chama wilayani humo, hali iliyosababisha chama
kushindwa kufanya kazi ya kuwatumikia wananchi katika maeneo mbalimbali
kama vile ngazi ya vitongoji, vijiji na kata ambako wananchi waliichagua
CHADEMA kuwatumikia.

Katika Jimbo la Busanda, Mkutano Mkuu wa Jimbo uliamua kwa sauti moja,
baada ya kupiga kura, kumuachisha uanachama aliyekuwa Diwani wa Kata ya
Katoro, Gervas Daudi, akikabiliwa na tuhuma kadhaa ikiwemo kukihujumu chama
hicho. Ngazi husika za chama zitawasilisha taarifa ya maamuzi husika kwa
ajili ya uamuzi wa mwisho kwa mujibu wa katiba na kanuni za chama.

Mbele ya kikao hicho, Daudi alituhumiwa kukihujumu chama hicho kwa kuzuia
uongozi wa Serikali ya Kijiji cha Katoro ambayo inaongozwa na Chadema
kutekeleza ilani ya chama hicho katika kuwaletea maendeleo wananchi wa eneo
hilo, hasa katika kusimamia rasilimali za wanakijiji, huku akishiriki vikao
vya kuizushia tuhuma za kutengeneza.

Alituhumiwa kuzuia utekelezaji wa miradi ya maendeleo kama vile ujenzi wa
sekondari, kituo cha magari na urekebishaji wa mikataba mibovu ya upangaji
wa vibanda vya biashara mali ya kijiji hicho ambayo iliingiwa wakati wa
uongozi  wa CCM katika Serikali ya Kijiji cha Katoro kabla ya uchaguzi
uliokiondoa madarakani chama hicho katika eneo hilo.

Tuhuma zingine ni kuwachangisha fedha wananchi 9 kiasi cha shilingi laki 5
kinyume na taratibu, akiwaahidi kuwatoa waume zao ambao wanashikiliwa
mahabusu wakituhumiwa kwa kosa la mauaji, pia alituhumiwa kushiriki vikao
na wafanyabiashara, viongozi na wanachama wa CCM wakipanga kuipindua
serikali ya kijiji hicho na pia kuwapindua viongozi wengine wa vitongoji
wanaotokana na CHADEMA.

Daudi pia amesimamishwa nafasi zake zingine ndani ya chama hicho, ikiwemo
Uenezi Jimbo la Busanda, Uenyekiti Wilaya ya Geita, ambapo Kamati Tendaji
ya Wilaya ya Geita imeagizwa kukaa haraka kuteua mtu atakayeziba nafasi ya
Daudi kisha jina hilo litumwe na kujadiliwa Kamati Kuu ya chama hicho
inayotarajiwa kuketi hivi karibuni.

Halikadhalika katika Wilaya ya Geita, Baraza la Mashauriano kwa kauli moja,
baada ya kupiga kura lilifikia uamuzi wa kuvuliwa uanachama kwa viongozi wa
Baraza la Vijana (BAVICHA); aliyekuwa Mwenyekiti wa BAVICHA Jimbo la Geita,
Emmanuel Otto, Katibu wake, Vincent Paul na Mratibu wa Uhamasishaji
Philibert Msiba. Pia uongozi mzima wa baraza hilo ngazi ya jimbo
uliondolewa. Diwani wa Marceline Simbasana aliandikiwa barua ya karipio
kali kwa mwenendo wake kinyume na taratibu za chama.

Baraza la Mashauriano katika Wilaya ya Sengerema liliamua kwa kauli moja
kuvunja Baraza la Uongozi la Wilaya, pia uongozi wa Mabaraza yote, yaani
BAVICHA, BAWACHA na Baraza la Wazee katika majimbo mawili ya Buchosa na
Sengerema ulivunjwa baada ya kuonekana haukidhi mahitaji ya kikatiba,
kanuni na taratibu za chama.

Halikadhalika uongozi wa CHADEMA Jimbo la Sengerema wote ulivunjwa, ambapo
ilikubaliwa kuwa viongozi wote waliohusika katika kuvunja katiba, kanuni na
taratibu katika kusimamia shughuli za chama ikiwemo kuwafukuza wenzao
uanachama wasihusike katika mchakato wa kujaza nafasi za uongozi wakati
uchaguzi wa kukaimisha na pia katika uchaguzi wa ndani unaotarajiwa kuanza
hivi karibuni na kukamilika mwaka 2013.

Katibu Mkuu, Dkt. Slaa amesema kuwa hatarudi nyuma katika kuendesha
‘safisha safisha’ hiyo kwani akiwa Mtendaji Mkuu wa chama anatekeleza
azimio la Kamati Kuu iliyoazimia kuwa ofisi yake ifanye uhakiki wa uongozi
na utendaji wa chama ili kujenga chama na kukagua uhai wa chama kuanzia
ngazi ya chini, Msingi mpaka juu.

*Imetolewa leo Aprili 26, 2012, Dar es Salaam na; *

*Tumaini Makene*

*Afisa Habari wa CHADEMA*

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7051,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: CHADEMA YAZUNGUMZIA ZIARA YA DK SLAA MIKOANI
CHADEMA YAZUNGUMZIA ZIARA YA DK SLAA MIKOANI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlq2mQhLJIUedNs6xyGWDfKIyzcNmcyNvIqVq22l6hI06D8eHz6RJzBqQ19UMbhN5zYMOXtIiQVmgcD8MEnOppNcqJWlrDPJg1UGHXc_BeVb_p9PHvRhMEsvVBRXZHwW1_9dYOP0863LWo/s320/SLAA.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhlq2mQhLJIUedNs6xyGWDfKIyzcNmcyNvIqVq22l6hI06D8eHz6RJzBqQ19UMbhN5zYMOXtIiQVmgcD8MEnOppNcqJWlrDPJg1UGHXc_BeVb_p9PHvRhMEsvVBRXZHwW1_9dYOP0863LWo/s72-c/SLAA.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/04/chadema-yazungumzia-ziara-ya-dk-slaa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/04/chadema-yazungumzia-ziara-ya-dk-slaa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy