Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Mhe. Ban Ki Moon akiwa na Msaidizi wake wa Karibu, Dkt. Asha-Rose Migiro wakati wa tafrika ya kumshuk...
·
Ya mshukuru kwa mchango wake katika kutetea afya
ya wanyonge
·
Yasema alikuwa na mchago mkubwa sana katika vita
dhidi ya malaria, ukimwi, kifua kikuu na afya ya wanawake na watoto
·
Ban ki
Moon asema alikuwa si mtu wa makuu na mtu wa watu
Na Mwandishi Maalum
Mashirika ya Umoja wa Mataifa
yanayohusika na masuala ya Idadi ya Watu ( UNFPA),Ugonjwa wa Ukimwi (
UNAIDS) na Mpango wa kupambana na Ugonjwa wa Malaria ( RBM) jana
jumanne yaliandaa tafrija kamambe ya kumshukuru
na kumuaga Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dkt. Asha- Rose
Migiro.
Tafrija hiyo ya aina
yake na ambayo mgeni
rasmi alikuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa, Ban Ki Moon, akiambatana
na mke wake na kuhudhuriwa pia na
wadau mbalimbali akiwamo Mtendaji Mkuu wa UNDP Bi Helen Clark, mabalozi
wanaoziwakilisha nchi zao katika UM, sekta binafis na taasisi za kiraia imefanyika
hapa makao Makuu ya Umoja wa Mataifa.
Akizungumza wakati wa
tafrija hiyo, Katibu Mkuu Ban ki Moom ameleezea baadhi ya sababu
zilizomsukuma kumteua Dkt. Asha-
Rose Migiro kuwa msaidizi wake wa karibu.
“ Nilianza kumfahamu
Asha- Rose Migiro wakati huo sote tukiwa mawaziri wa mambo ya nje katika nchi zote. Uwezo wake na uelewa wake
wa mambo ulinivutia sana, lakini nilivutiwa zaidi pale nilipofahamu kwamba
aliwahi kuwa waziri anayehusika na masuala ya wanawake na watoto.
Nikajiridhisha kwamba huyu ndiye alikuwa ananifaa kuwa msaidizi wangu wa
karibu” akasema Ban Ki Moon na kuufanya umati ulihohudhiria tafrija hiyo kushangilia
kwa nguvu.
Kama hiyo haitoshi, Ban Ki Moon amemuelezea Dkt. Asha-
Rose Migiro kama msaidizi wake wa karibu ambaye licha ya kufanya kazi kwa
uadilifu mkubwa lakini ni mtu ambaye alikuwa hana makuu na wala hata siku moja
hakujikweza.
“ Katika kipindi chote
ambacho Migiro amekuwa msaidi wangu wa karibu, amenisaidia katika mambo mengi,
ni mtu muadilifu sana, ni mtu aliyekaribu sana na watu, aliyeamsha matumaini na
kuwapa tabasamu watu waliokuwa katika mazingira magumu. Daima amekuwa mstari wa mbele kunisaidia na hakuna hata siku moja alipojikwenza. Na
kwa sababu hii anastahili tafrija hii”
akasisitiza Ban Ki Moon.
Aidha Ban Ki Moon
akamuelezea Asha- Rose Migiro kama
kiongozi ambaye daima alitoa kipaumbele
cha aina yake katika masuala ya afya ya jamii eneo alilotumia uwezo wake wote, maarifa yake
yote kama naibu katibu mkuu kupigania afya ya wanawake na watoto na watu wote
walio katika mazingira magumu
Kwa upande wao
waandaaji wa tafria hiyo na wakizungumza
kwa nyakati tofauti wamemuelezea Naibu
Katibu Mkuu, kama kiongozi ambaye mchango
wake umesaidia sana katika
kuihamasisha jumuiya kimataifa kuweka mkazo wa aina yake katika
kushughulika afya ya jamii.
Bw. Michel Sidibe,
Mkurugenzi mtendaji wa UNAIDS yeyé
alimuelezea Asha- Rose Migiro kama dada yake ambaye sifa zake zinaazia mbali.
“ Asha- Rose Migiro ni
dada yangu, ni dada ambaye anasifa za kipekee, ni mwanamke wa kwanza aliyefaulu
kwa daraja la kwanza katika sheria kutoka chuo kikuu cha dar es Salaam, ni mwanamke wa kwanza kuwa waziri wa mambo ya
nje nchini Tanzania, na ni mwanamke wa
kwanza kutoka afrika kuwa naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa” akasema Bw.
Sidibe kauli iliyoamsha tena makofi kutoka kwa wageni waalikwa.
Hakuishia hapo, Michel
Sidibe akamuelezea Migiro kama kiongozi aliyefanya kazi kwa karibu na
Shirika lake katika kuhakikisha kwamba maambukizi ya
virusi vya ukimwi yalikuwa yakipungua ikiwa ni pamoja na kupatika kwa tiba ya uhakika
kwa waathirika.
“ Tunakila sababu leo hii
kumshukuru kwa namna alivyoshirikiana nasi, na ingawa unaondoka lakini tambua kwamba mchango wake
utaendelea kukumbukwa na kuenziwa” akasisitiza
Bw. Michel Sidibe.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Maifa la Idadi ya Watu, Dr. Babatunde Osotimehin
amesema juhudi kubwa zilizoonyeshwa
na Naibu Katibu Mkuu katika
kushughulikia masuala ya afya ya jamii, kumefanikisha kupunguza kwa
kiasi kikubwa idadi ya vifo vya wanawake vitokanavyo na uzazi hali kadhalika vifo vya watoto wachanga chini
ya miaka mitano.
“Katika kipindi cha uongozi wako, umefanikisha sana katika
kuhamasisha jumuia ya kimataifa
kuongeza misaada yao na kutoa kupaumbele
katika afya ya mama na mtoto, tunakushukuru sana kwa hili, na Mungu aendelee kukubariki” akasema Dr.
Babatunde Osotimehin.
Kwa upande wake, Bw. Herve Verhoosel, Mwakilishi wa
Mapango wa kupunguza Malaria, yeyé alimuelezea Dkt. Asha-Rose Migiro kwamba chini ya uongozi wa Ban Ki Moon, ameweza kujenga
misingi bora ya ushirikiano na muamko
miongoni mwa wadau mbalimbali katika kuhakikisha kwamba kunakuwapo na uhusiano kati ya sekta za umma
za zile za binafasi katika kutimiza malengo ya afya ya jamii ikiwa ni pamoja na
kasi ya kupunguza malaria
Akiwashukuru waandaji wa tafrija hiyo, Naibu
Katibu Mkuu amemshukuru Katibu Mkuu Ban Ki Moon kwa kumuamini kuwa msaidizi
wake wa karibu katika kipindi cha miaka mitano na nusu.
Akasema ingawa yeyé amejituma na kutekeleza majukumu yake kwa ukamilifu,
lakini amefanya hivyo kwa kuwa Ban Ki Moon alimuamini kwamba anaweza. Na kwamba
daima ataendelea kuienzi heshima hiyo.
Akatumia fursa hiyo
kumueelezea Ban Ki Moon kama kiongozi ambaye amekuwa mstari wa mbele
kuhakikisha kwamba kila mtoto angalau alikuwa analala kwenye chandarua, akina
mama wajawazito walikuwa hawapotezi maisha kutoka na uzazi.
Aidha Migiro amewashukuru kwa moyo wa dhati
wasaidizi wake wa karibu aliofanya nao
kazi akiwa naibu katibu mkuu na kwamba bila wao asingefika hapo alipo,
akawashukuri pia wadau mbalimbali wakiwamo mabalozi kwa ushirikiano wa hali na
mali waliompatiwa muda wote wa miaka mitano na nusu
COMMENTS