JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA MKAKATI WA KUDHIBITI BIASHARA YA MAZAO YA MISITU KINYUME ...
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WAKALA WA HUDUMA ZA MISITU TANZANIA
MKAKATI WA KUDHIBITI BIASHARA YA MAZAO YA MISITU KINYUME
CHA SHERIA PAMOJA NA KUBORESHA UKUSANYAJI MADUHULI
1.
UTANGULIZI
Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (Tanzania Forest
Services Agency) –TFS- umeanzishwa kwa kuzingatia Sheria ya Wakala wa Serikali
Namba 30 ya 1997 iliyorejewa 2009). TFS ilianza kazi rasmi Julai 1, 2011 ikiwa na
lengo la kutekeleza majukumu ya kiutendaji ya uhifadhi na usimamizi wa rasimali
za misitu na nyuki kwa ufanisi na tija zaidi.
Wakala
unatakiwa kuendesha shughuli za uhifadhi na usimamizi wa rasimali za misitu na
nyuki kwa kujitegemea kwa asilimia 100 pamoja na kuchangia fedha katika
mfuko mkuu wa Serikali yaani Hazina. Ili kufikia azma hii Wakala unajizatiti
katika kudhiti biashara haramu ya mazao ya misitu inayofanywa kinyume cha
sheria na kuboresha ukusanyaji wa maduhuli, kubaini mianya iliyopo ya ukwepaji
kulipa ushuru wa mazao ya misitu na kutafuta mikakati ya kuidhibiti.
2.
HATUA TULIZOCHUKUA
Wakala umefanya
ukaguzi maalum wa namna biashara ya mazao ya misitu na ukusanyaji maduhuli inavyosimamiwa
katika maeneo mbalimbali ili kubaini na kujionea hali halisi katika
kudhibiti biashara ya mazao ya misitu na
kukusanya maduhuli kwa nchi nzima kuanzia tarehe 7/05 – 21/05/2012.
Katika ukaguzi huo
makundi 11 yalifanya kazi katika maeneo mbalimbali kwa lengo la kuboresha ukusanyaji maduhuli, kuimarisha
makusanyo na kupunguza kasi ya uharibifu wa misitu nchini. Ukaguzi na uhakiki
wa nyaraka ulifanyika katika Ofisi za Maafisa Misitu Wilaya, Maafisa wa Vituo
vya Ukaguzi, maeneo ya uvunaji na kwa wafanyabiashara ili kuangalia kama
taratibu, kanuni na sheria dhidi ya kumiliki na kusafirisha mazao ya misitu
zinazingatiwa. Kazi hii ilifanyika usiku na mchana.
Ukaguzi umeokoa fedha
ambazo zilipaswa kukusanywa kama maduhuli ya Serikali pamoja na kukamata mazao
yalivyovunwa au kumilikiwa kinyume cha sheria pamoja na ada za makampuni ya
uchimbaji madini na minara ya simu. Katika zoezi hili jumla ya Shilingi 744,340,146/= zilikusanywa. Hali
kadhalika tuliweza kukamata mazao ya misitu kama mkaa, mbao na magogo
yaliyovunwa kinyume cha sheria yenye thamani ya Shilingi 33,068,390/=. Jumla Shilingi 777,408,536/=
fedha taslim na thamani ya mazao ya misitu yaliyokamatwa. Vile vile, kuna fedha shilingi 35,485,000/= ambazo zinatakiwa kulipwa
kama ada za kampuni za uchimbaji madini na minara ya simu.
Katika kipindi cha
mwaka huu wa fedha hadi Mei 2012, Wakala umefanikiwa kukusanya Jumla ya Shilingi 59,328,190,572.26 ambazo ni
sawa na asilimia 110 ya lengo la
mwaka huu wa fedha.
3. CHANGAMOTO
3.1 MAMBO TULIYOJIFUNZA
Tathmini ya zoezi
hili imefanyika na kutuonyesha changamoto zinazotukabili katika maeneo
yafuatayo:-
(i)
Usimamizi wa rasilimali za misitu
(ii)
Mfumo wa Utendaji
(iii)
Watumishi na Vitendea Kazi mfano Usafiri na Nyaraka
3.2
MIKAKATI YA KUKABILI CHANGAMOTO
a) Kuimarisha uhifadhi na udhibiti wa Misitu ya Hifadhi
ya Asili pamoja na biashara ya Mkaa na Mbao
i)
Kutoa elimu kuhusu usajili, wajibu na
majukumu ya wakala, taratibu za kufanya biashara ya mazao ya misitu,
kukumbushana malengo na mafanikio yaliyofikiwa na TFS
ii)
Kufanya utambuzi wa Misitu – mipaka
kubainishwa
iii) Kudhibiti
uvunaji katika Wilaya ambazo hazina mpango ya uvunaji
iv) Kuweka
Maafisa Leseni za msitu katika maeneo muhimu
v)
Kuwa na vitabu vya regista za wateja,
na wilaya kupata orodha halisi ya wafanyabiashara waliosajiliwa
vi) Kuanzisha
stock register ya wateja itakayorahisisha ukaguzi
vii) Kuanzisha
bustani za upandaji miti
viii) Kuimarishe
Vizuia vya mipakani ili kuhakikisha mazao yanakotoka, kuwa na nyundo maalum kwa
ajili ya mazao yanayotoka nje ya nchi
ix) Kuhakikisha
taratibu za ushuru wa madini zinasimamiwa ili kuongeza udhibiti
b)
Kuimarisha
Mifumo ya ukusanyaji
Kuwa na hatua
za utekelezaji katika udhibiti kama
ifuatavyo:
(i)
Kuhakikisha biashara za mkaa na mbao zinadhibitiwa:
·
Kuhusu mkaa, ushuru uzingatie uzito na
uvunaji ufanyike kwenye maeneo yaliyoainishwa pamoja udhibiti katika idadi ya
magunia yanayozidi
·
Mbao/ Magogo yalipiwa kufuatana na
ujazo halisi
(ii)
Kuhakikisha elimu ya maadili inatolewa
kwa watumishi na wafanyabiashara wanaelimishwe kuhusu taratibu za biashara kwa
kufuata kanuni na sheria. Pia tutatoa hamasa na elimu ya teknolojia mbadala ya utengenezaji wa mkaa na
kutumia majiko banifu
(iii)
Kuwa na vituo vya ukusanyaji wa mkaa
(iv)
Kuhakikisha Wafanyabiashara wa mazao
ya misitu wanaunda vyama vyao;
(v)
Kudhibiti idadi ya mazao ya misitu
yanayosafirishwa kwa kuwa na jedwali la mahesabu
c)
Kuwapatia
motisha na vitendea kazi kwa watumishi
(i)
Kuhakikisha kuwa TFS kwa kushirikiana
na Halmashauri za wilaya zinakuwa na watumishi wake katika maeneo muhimu mfano
Rufiji, Kilwa, Liwale, Masasi, Ruangwa, Nachingwea, Tandahimba, Mtambawala na
Nanyumbu
(ii)
Kuongeza watumishi kwenye vituo vya
udhibiti (Kisosi na vizuia) vyenye upungufu
(iii)
Kujenga ushirikiano na mahusiano
mazuri kati ya watendaji wa vizuia, vikosi na halmashauri
(iv)
Kutoa motisha kwa watumishi pale
wanapofanya masaa ya ziada au kazi nzuri na kuwachukulia hatua za kisheria pale
wanapokiuka sheria
(v)
Kutoa elimu zaidi kuhusu sheria,
taratibu, miongozo na kanuni, elimu hiyo itolewe kwa vitendo (practical
training)
(vi)
Kuhakikisha nyaraka zote za makusanyo
zinapatikana kwa wakati vituoni
(vii)
Kupeleka vitendea kazi kama pikipiki kwenye
maeneo muhimu
(viii)
Kuhakikisha TFS inakuwa na waendesha
mashitaka wake, watu wenye nia na uwezo watabainishwa na kupelekwa kwenye
semina maalum kwa ajili ya kazi hiyo.
4
HITIMISHO
Kufuatana na
ukusanyaji maduhuli pamoja na mikakati ambayo tumeianzisha napenda kuwaambia
kwamba tutahakikisha tunaendeleza mikakati hiyo na kuifanya kuwa ya kudumu na
siyo ya mptio na kwamba taarifa mbalimbali zitaendelea kutolewa kuhusu
maendeleo ya utendaji wa wakala kila itakapobidi.
Juma S. Mgoo
Mtendaji Mkuu
Wakala wa Huduma za Misitu
Tanzania
05/06/2012
COMMENTS