TAMKO LA TEF KUHUSU UONGOZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KUTOSHIRIKI MKUTANO WA WAHARIRI NA MCT MKOANI MOROGORO

TAMKO LA TEF KUHUSU UONGOZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KUTOSHIRIKI MKUTANO WA WAHARIRI NA MCT MKOANI MOROGORO ...


TAMKO LA TEF KUHUSU UONGOZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KUTOSHIRIKI MKUTANO WA WAHARIRI NA MCT MKOANI MOROGORO

Mwenyekiti wa Jukwaa Absalom Kibanda
UTANGULIZI
Juni 3 – 5, 2012, wahariri watendaji na waandamizi wa vyombo vya habari nchini walikutana mjini Morogoro katika Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka wa Mashauriano kati yao na Baraza la Habari Tanzania (MCT).
Mkutano huu ulioshirikisha wahariri kutoka katika vyombo vya serikali, binafsi na vile vinavyomilikiwa na vyama au taasisi za kidini pamoja na mambo mengine ulijadili hali na mwenendo wa vyombo vya habari hapa nchini kwa sasa na kwa siku zijazo.
Katika mkutano huo zilijadiliwa mada mbalimbali ambazo kwa ujumla wake zililenga kuwezesha kazi ya uandishi wa habari kufanyika kwa kuzingatia maadili, wajibu na weledi wa kitaaluma.
Pia mada hizo zililenga kuimarisha, weledi wa kitaaluma, uwajibikaji utendaji wa kazi, na uhuru wa vyombo vya habari na zaidi kujenga mfumo wa usimamizi wa maadili ndani ya vyombo vya habari.
Mbali ya hayo, wahariri na wadau wengine wa habari waliohudhuria mkutano huo walijadili kuhusu Mchakato wa Sheria ya Haki ya Kupata Habari na Huduma za Vyombo vya Habari nchini ambao umekuwa ukisuasua kwa takriban miaka 10 sasa.
Ifahamike kwamba, mkutano huu ulikuwa na uzito wa pekee hasa kwa kuzingatia ukweli kwamba, wahariri ndio wasimamizi na watoa uamuzi wa mwisho katika vyumba vya habari kuhusu masuala yote yanayohusu habari, makala na taarifa zinazotolewa katika vyombo wanavyofanyia kazi.
USHIRIKI WA SERIKALI
Kwa masikitiko makubwa, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Seth Kamuhanda hawakushiriki hata kwa kufungua mkutano huu kama walivyoombwa na Baraza la Habari Tanzania na wao wenyewe kuthibitisha kwa nyakati tofauti.
Kwa mshangao wa wahariri na wadau wengine waliohudhuria mkutano huo, viongozi hao wawili mbali ya kutumiwa rasimu ya hotuba ambayo ilipaswa kusomwa kwanza na waziri ambaye ndiye alipaswa kuwa mgeni rasmi, kabla ya yeye mwenyewe (waziri) kutoa taarifa MCT kwamba, angewasilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara hawakutokea katika mkutano huo wala kutuma mwakilishi mwingine yoyote, huku wakitoa udhuru kwamba walikuwa na kazi nyingine.
Hatua ya viongozi hao kushindwa kufika katika mkutano huo muhimu kwa maendeleo ya tasnia ya habari nchini ikiwa ni pamoja na kushindwa kwao kutuma mwakilishi mwingine kutoka wizarani, si tu iliwashtua wahariri, bali iliwasononesha na kuwashangaza.
Taarifa ambazo tulizipata zinaonyesha kuwapo kwa msuguano usio na afya kwa tasnia ya habari, kwa wizara na kwa serikali nzima kati ya Waziri na Katibu Mkuu. Kitendo cha wao kushindwa kutuma mwakilishi kutoka kwa viongozi na watendaji wengi waliojaa katika wizara hiyo ni ushahidi wa namna hali ilivyo mbaya na tete kimahusiano na kikazi katika wizara hiyo.
MTIZAMO WA WAHARIRI
Kitendo cha wiki hii kinatupa mashaka iwapo tunastahili kuendelea kuwa na uongozi wa Waziri na Katibu Mkuu wa sasa katika wizara hii. Tunasema hivyo kwani tuna shaka sana kama siku zijazo watatoa ushirikiano wa kutosha, hasa katika mchakato wa kupata sheria nzuri za Huduma za Vyombo vya Habari na ya Haki ya Kupata Habari.
Tukio hili kwetu wahariri limetupunguzia imani kwa viongozi hawa iwapo wataweza kutuvusha katika mabadiliko ya kitaaluma na yale ya kimfumo katika kukusanya na kutoa habari nchini.
Kwa maana hiyo tumeazimia kwamba kwanza; Tunatoa taarifa rasmi ili umma wa Watazania uweze kufahamu hali hii, lakini pili tutawasilisha rasmi malalamiko yetu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aweze kuingilia kati hali hii kwa nia ya kuiokoa tasnia ya habari, ambayo ni muhimu kwa ustawi na afya ya taifa hili.
Tunapenda kuwahakikishia Watanzania na Serikali kwa ujumla kuwa vyombo vya habari vimejizatiti na kujipanga kuwatumikia Watanzania kwa kuzingatia maadili na weledi wa hali ya juu pia kwa kuzingatia matakwa na maslahi ya umma.
Tunachoomba ni zana za kufanyia kazi hii. Zana hizi si nyingine bali ni Sheria ya Huduma za Vyombo vya Habari na Sheria ya Haki ya Kupata Habari, ambazo mchakato wake umedumu kwa zaidi ya miaka 10 sasa bila sheria hizi kupatikana.
Tunasema mikingamo inayokwamisha sheria hii imalizwe ili tuweze kupata sheria nzuri na kufanya kazi kwa uhuru na uhakika zaidi.
Hili la Waziri na Katibu Mkuu wizarani linaongeza wasiwasi wa kupatikana kwa sheria hizi.
Mungu ibariki Tanzania.
Neville Meena,
Katibu – Jukwaa la Wahariri (TEF)
Dar es Salaam,
Juni 07, 2012.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: TAMKO LA TEF KUHUSU UONGOZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KUTOSHIRIKI MKUTANO WA WAHARIRI NA MCT MKOANI MOROGORO
TAMKO LA TEF KUHUSU UONGOZI WA WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO KUTOSHIRIKI MKUTANO WA WAHARIRI NA MCT MKOANI MOROGORO
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhelbpv1wEzPP5sQZySQUf3xYp9lX5uSuC5qxaFGemJniTqk40aZHfk-aruSP5D2gQznRjYGxyv-wHxmymYl512jHN3lf0_-qeUNbE7jzn0jSMU92xg83ShPAX77Y5mWSgC4LyaJ6x-zlRs/s320/MWENYEKITI+wa+Jukwaa+la+Wahariri,+Absalom+Kibanda.JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhelbpv1wEzPP5sQZySQUf3xYp9lX5uSuC5qxaFGemJniTqk40aZHfk-aruSP5D2gQznRjYGxyv-wHxmymYl512jHN3lf0_-qeUNbE7jzn0jSMU92xg83ShPAX77Y5mWSgC4LyaJ6x-zlRs/s72-c/MWENYEKITI+wa+Jukwaa+la+Wahariri,+Absalom+Kibanda.JPG
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/06/tamko-la-tef-kuhusu-uongozi-wa-wizara.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/06/tamko-la-tef-kuhusu-uongozi-wa-wizara.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy