NI nadra sana kupata burudani na mafunzo kwa wakati mmoja kama ilivyotokea katika filamu ya Diana iliytolewa na nyota wa filamu katika...
NI nadra sana kupata burudani na mafunzo kwa wakati mmoja
kama ilivyotokea katika filamu ya Diana iliytolewa na nyota wa filamu
katika tasnia ya filamu Single Mtambalike al maarufu kama ‘Richie’.
Filamu hii yenye kumleta tena usoni mdada Halima Yahaya ‘Davina’
ambaye alikuwa amepotea kwa muda kutokana na kuwa katika masuala ya lazima ya
binadamu, uzazi, inazungumza sana kuhusu maisha ya ndoa urukaji na hasara ya
kuruka.
Mwenyewe Richie anasema kwamba filamu hiyo kwake ni ya bashashi
yenye kulenga kuleta fikira mpya kuhusu ndoa na mikikimiki yake, huku akiamini
kwamba wandoa watakaotaka kuponya ndoa zao wana kila sababu ya kunua Diana.
Amesema filamu ya 'Diana' ni fundisho kwa wanaume wote wanopenda
kuvamia wanawake wa nje wakati wana wake zao, tena wanaowapenda sana.Richie
ambaye amesema ameangalia matatizo yanayowakuta watu wanaofanya hivyo amesema
ameitengeneza kwa namna ambayo sit u inatoa fundisho bali inatoa na burudani
inayotakiwa kwa wapenzi wa sinema.
Kwa maneno yake mwenyewe Richie kutembea nje ya ndoa
huleta mitihani katika Ndoa na kuharibu mahusiano katika familia na akatoa
masikhara ya uchawi kama moja ya maeneo yanawakuta watu wengi, ambao huwa na
wanewake zaidi ya mke wake aliye nyumbani.
Dhana ya uchawi imetazamwa kwa namna mbaya zaidi kwa kuwa
inaonesha kwamba mke mwenza anataka kummaliza mwenye nyumba ili yeye abaki kuwa
kijogoo kwa namna yake.
“Filamu ya 'Diana' ni kipimo cha ndoa kwani inaonyesha jinsi
matatizo ambayo yanaweza kutokea kwa kuwa na Nyumba ndogo na
kusalitiwa” anasema Richie ambaye nmke wake katika sinema alirogwa na
mchuchu wake na kama zali alijikuta pia akipoteza kazi kutokana na kuendekeza.
Anasema simulizi lake hilo linalowapeleka katika raha,
mahangaiko na majuto na unamalizia katika hali ambayo kiu yako inaendelea kuwapo
ukiuliza kama njingelikuwa mimi nini hasa kingelitokea.
Richie anaamini ujio wa filamu hiyo unatoa nafasi ya tafakari
kwa watu wengi hasa ikizingatiwa kwamba ndoa nyingi sasa zina tofauti kubwa
kutokana na kutokuwa na muda wa kupima mambo yao.
Kimsingi 'Diana’ ambayo inaonekana miongoni mwa sinema za Richie
zilizobora imetoka kidogo katika mistari ya kawaida ya sinema za Richie kwani
Diana ikiwa ni kipimo cha ndoa bora inatoka tofauti na swahiba, mahabuba na
sinema nyingine.
Maneno ya Mtambalike kuhusu kampuni yake ya filamu ya Bulls
tutayapata katika raundi ijayo kama Mungu akitupa nafasi lakini kw aleo
inatosha kusema kwamba sinema kadhaa zilizotengenezwa na Richie bado zinaonesha
kwamba anajua nini nachofanya hasa kw akucheza na hisia za wapenzi wa sinema,
watu wazima katika sebule zao.
Nasema hivyo kwa kuwa sinema mama Tamaa Yangu,Diana, Gentlemen,
Jesica, Mtaani Kwetu,Kimya,Basilisa,Unexpected Truth,Solemba,Lerato,Mahabuba ni
sehemu tu ya sinema ambazo sebule ya watu makini unazikuta kwa kuwa ushiriki wa
watu na nnamna inavyokwenda ni raha tupu.
Richie ambaye amecheza sinema hizi na kuziongoza katika
mazungumzo yetu alisemamaisha ingawa ni mtihani mkubwa ipo haja ya kuangalia
namna watu wanavyoshughulikia mitihani ya maisha kwani ni heri tu kujua
maisha lakini si kuyafanyia masikhara kama alivyofanya katika sinema hiyo.
Inakuaje unapokuwa na nyumba yako ndogo halafu ikaendesha
usaliti na kukuacha wewe ukihemea juu kwa juu, sina uhakika kama Richie
ameshawahi kukumbana na kadhia hiyo ingawa anasema kwamba anayaona kwa watu na
anadhani ni vyema kuangalia jamii katika hali hiyo.
Unapoteza mwelekeo kwa sababu ya kimada, Richie lazima awe na
masikhara katika hili, anakuwa na masikhara kwa kuwa anamtazama mwenye ndoa
katika jicho la kawaida la watu wa dini wanafalsafa wa maisha hawatazami hayo
kwani inaonekana kuwa bahati mbaya lakini kwa Richie si bahati mbaya ni
makusudi yenye dhamira iliyopotofu.
Katika mazungumzo Richie alisema katika filamu hiyo,
imeshirikisha wasanii mbalimbali wakiwemo wakongwe na chipukizi, ili kuleta
ladha tofauti.
Haya ndiyo mambo ya Richie ambaye akichez akupenda unaweza
kupagawa, lakini akipagawa unaweza kukimbia, mudi tofauti kwa kazi tofauti na
ukiangalia filamu za sasa pasi shaka unaona kwamba libeneke linaaanza kupata
pumzi inayostahiki.
mwisho
filamu mpya mtaani
Tamaa Yangu
Ni kazi ya Deogratus Shija kama Dairekta ambapo ndani ya
filamu anayatafakari Maisha kama safari ndefu ambayo binadamu hujua mwanzo na
sio mwisho . mwisho anajua Mungu kama mwanzo ya awali anavyoijua kutokana na
ukweli kuwa hata kama usiku usingekuwa mrefu lakini asubuhi lazima itaonekana
tu, maisha ni tofauti sana unaw2eza kufikiria unataka iweje mwishoni lakini
huna uhakika na kama hukuwa na akili yatakukuta yaliyomkuta Rado. Ndio kusema
kama Rado angeyafahamu hayo yote mauti yasingemfika
Ukiangalia filamu hii unauafiki ule msemo wa Kibiblia kwamba
Msiyasumbukie mambo ya kesho maana kesha itajisumbua yenyewe.
Ngoma hii
iliyochezwa na Single Mtambalike, Simon Mwapangata, Regina Mroni, Deogratus
Shija imesimuliwa na Simon J. Mwapangata, ikazalishwa na Simoni J. Mwapangata
na kuongozwa na Deogratus Hija ikiwa ni kazi rasmi ya Epic Entertainment.
"THE HOUSE MAID"
WAPENZI wa muigizaji ambaye anapenda kujiita dada mdogo ,
Jeniffer Kyaka (Odama), wanasubiri kwa namna inayofaa kuona kw autamu
unaokusudiwa wa filmu mpya yenye kufundisha, kuadabisha na kuelimisha ya the
house Maid.
wote mnajua wasaidizi hawa inakuaje kuaje katika majuumba yenu
hasa wanapozidi kupendeza na nyie mkakosa namna ya kufanya.
kWa mujibu wa mtandao wa RUMAAFRICA (www.rumaafrica.blogspot.com) Odama anafanyia
vitu vidogo sinema hiyo na kwamba ikiwa gado itatumbukizwa katika mpangilio wa
sinema zake na nyie kuendelea kujidia huku akiwaandalia kitu kingine.
Anasema kwamba filamu hiyo inaandaliwa na kampuni yake ya J-FILM
4 LIFE na itatoka kwa kiwango cha juu.
Crazy tenant
Ni moja ya filamu ambazo zinaweza kukufanya uwe kichaa na halafu
ukafikiria nini hasa kimepangwa katika filamu hii ambapo washiriki wake ni
majina makubwa na simulizia lenyewe bonge la komedi.
jamani pigeni kelele ohoo nilidhani muziki kumbe ni fujo za
kwenye sinema hii.Promo lake lina siku 44 katika You Tube nasubiri tu asijui
imetoka?
Wewe na babangu ndio vipi... ha ha nadhani hupigi mswaki domo
lako heee! hayo mambo, wanakula na kutoka ghorofani unakamua nguo ha ha
COMMENTS