Kaka mkubwa akitabasamu washiriki wakitoa hamasa kwenye karatasi Wakati wizara ya habari inafanya vitu vyake Dodoma mimi kaka mkub...
Kaka mkubwa akitabasamu washiriki wakitoa hamasa kwenye karatasi |
Wakati wizara ya habari inafanya vitu vyake Dodoma mimi kaka
mkubwa nilikuwa namie namalizia ngwe yangu ya kuzungumza na wanahabari wa
manyara katika mafunzo yaliyowezeshwa na baraza la habari nchini (MCT).
Niseme kuwa nimeyapata
mengi kwa kuwa darasa lilikuwa la kubadilishana na niliyoyapata ama hakika
yanatia simanzi na kuleta kiwi kubwa katika akili.
Katika mazungumzo wakati wa kujadili Azimio la Dar es salaam
kuhusu Uhuru wa uhariri na uwajibikaji wa vyombo vya habari (DEFIR) suala la
maslahi na upotofu wa madili kwa wahariri mpaka waandishi wa habari na
kuingiliwa na wenye vyombo vya habari vilichukua muda mwingi.
Wahariri walituhumiwa
kusababisha uvunjifu wa maadili na kanuni za vyombo vya habari kwa kutotetea
haki za waandishi wa habari, wao wenyewe kuomba rushwa anuai kutoka kwa
waandishi na wanasiasa kuwatumia vibaya waandishi wa habari.
Ni a kubwa ya
semina darasa hili pamoja na kuibua uozo wa wapiganaji na makamanda wao ilikuwa
kukumbushana na kuleta uelewa wa kiwango cha juu miongoni mwa wanahabari kuhusu
maadili ya uandishi wa habari.
Pamoja na hayo semina darasa hili lililenga kujenga
uwezo wa kuchambua maadili wakati wa utendaji kazi ili kufikia uamuzi sahihi
wenye kulenga maslahi ya umma kwa kufikia maamuzi sahihi ya utendaji.
Aidha Azimio la Dar es salaam kuhusu uhuru na
uwajibikaji wa vyombo vya habari (DEFIR) lilichambuliwa kwa kuona misingi yake,
dhana na umuhimu wa kuwepo kwake kuhakikisha kwamba maadili yanazingatiwa licha
ya changamoto zake na mitanziko iliyopo.
Baadhi ya washiriki wakimsikiliza mwezeshaji |
Vijana kwa wazee wadada kwa wakaka walichambua vipengele ndani
ya azimio la Dar es salaam ambapo kwenye
kifungu cha nane na tisa waandishi wa habari wakiwa na majukumu makubwa ya
kuhabarisha wengine, wanatakiwa kutekeleza wajibu wao na majukumu yao ya
kijamii kwa uadilifu mkubwa, umakini na umahiri unaolingana na viwango vya
kitaalamu na maadili na kuelewa wakati wote kuwa wajibu na uwajibikaji wao ni
kwa umma na kuwa wao ni watendaji wa umma wanaotoa huduma katika Nyanja nyeti
ya utumishi kwa umma kwa minajili ya kujenga jamii ya kidemokrasia isiyo na kandamizi
isiyo na ubaguzi kwa misingi ya rangi,ukabila, jinsia na ulemavu na isiyo na
uvunjaji wa haki za binadamu.
Misingi hiyo inamtaka mwandishi wa habari kutekeleza
majukumu yake kwa kuzingatia ukweli, uadilifu, umahiri na weledi pamoja na
umakini na uwajibikaji wa hali ya juu kwa
umma, ili kujenga imani na uaminifu machoni kwa umma.
Ni wajibu pia wa msingi kwa wanahabari kuepuka tabia
za uchochezi wa vurugu, chuki na kukuza heshima ya binadamu.
Hiyo inatokana na ukweli kuwa Tasnia ya habari ipo kuhudumia
umma. Na ndio maana pamoja na wafanyabiashara kuanzisha makampuni ya habari kupata faida, vyombo vyao
vinatakiwa kuhudumia maslahi ya umma
kwani tasnia ya habari ni mali ya umma.
NILISEMA: Ili kutoa huduma hii kwa ufanisi wadau katika chumba
cha habari kuanzia waandishi ,wahariri na wakuu wa vyombo vya habari wanapaswa kujua
maana na umuhimu wa maadili katika fani
yao ili kudumisha na kuendeleza ubora wa kazi ya kupasha habari na kujenga
imani kwa watu wanaowasoma au kuwasikiliza na hata kuwaona.
Kinachopaswa kudumishwa hapa ni maadili na kanuni za
kazi yenyewe ambapo kama yatafuatwa ni dhahiri kutaepusha msuguano na kuleta
uwiano sawa wa upashanaji habari kwa manufaa ya umma na taifa bila kujali
chombo kinachotumika ni cha mfanyabiashara, dola au cha umma.
>>Kama ni hivyo maadili nini?
Maadili ni mambo ambayo yameainishwa wazi kufanywa na
yasiyotakiwa kufanywa kwa mujibu wa heshima ya taaluma ya uandishi wa habari.
Maadili kwa misingi mingine unaweza kusema ni utekelezaji wa matakwa ya taaluma ili
kuweka bayana ukweli, usahihi, haki na uhuru
bila kuonea upande wowote kwa kuzingatia miiko ya taaluma na bila
kuumiza maslahi ya jamii.
washiriki wakikiangalia kazi za kuainisha baada ya kupigwa na dozi ya maadili |
Haya yanaweza kuangaliwa
pamoja na mambo mengine kama kumi na nne hivi LAKINI kubwa ni uadilifu
1—Uadilifu:
a) Hapa unakutana na
haja ya kujua sheria mama yaani katiba, kuiheshimu na kukubaliana na sheria za
nchi huku mwandishi akionesha mwenendo mzuri katika maish ayake binafsi.
b) Upendeleo usitawale
au kuhatarisha uadilifu wa kazi, uhuru na uwezo wake.
c) Kujiepusha na hali
ya kuonekana kwamba ametumiwa na watu wenye agenda za siri, rushwa au ajenda
binafsi isiyokuwa na mashiko kwa umma.
d) Ni lazima
kujitambulisha katika hali ya kuaminika anaweza kubadilika maslahi ya umma yanapotetereka.
2- Wizi wa maandishi/ mawazo
Mwandishi ni vyema akaeleza chanzo cha habari.
3- Ukweli na uhakika
Kwa kiuzingatia maagizo ya maadili ni lazima afanye kw
ausahihi na ukweli na kupambanua maoni na taarifa
4-Usawa na uaminifu
Pamoja na kutakiwa kuw amzalendo mwandishi haruhusi
kupendelea upande au kuzuia habari
isitoke labda kwa maslahi ya taifa. Na asimfiche mtu mwenye ushawishi mkubwa
kwa jamii katika utrekelezaji wa kazi yake.
5-Faragha
Waandishi watambue mipaka ya faragha za watu katika maisha yao
ili mradi hawaendi kinyume na maadili ya kazi zao.
6-ushawishi na mvuto wa watu binafsi
Usikubali kuvutwa na
ushawishi au mvuto wa mtu au familia katika utendaji wa kazi wasikubali
kushawishika kwa huruma zawadi au au manufaa ahadi
7-Uhuru wa waandishi wa habari
Unatakiwa kuelewa na kutetea maslahi ya umma kwa kutetea uhuru
a vyombo vya habari
Ukiangalia vipengele hivyo kiundani unatambua
kwamba ipo haja kwa mwandishi wa habari kujua
sheria mama yaani katiba,
TUKIRUDIA TENA:Ndio kusema mwandishi wa habari ili
atekeleze kazi yake vyema ni lazima awe mwadilifu,hafanyi wizi wa
maandiko,anatafuta ukweli na uhakika, anaamini katika usawa na uaminifu anakuw
a mzalendo (inapobidi) lakini si kwa kushurutishwa anaheshimu faragha, kuelewa
sheria ya watoto kupunguza madhara na wasikubali kuvutwa na ushawishi wa mtu au
familia.
>>Madhara ya kupinda maadili
Adhabu ya kutofuata kanuni na kuheshimu maadili hupatikana
papo hapo mwandishi anapovunja. Adhabu hiyo ni kusongwa na moyo na kukosekana
kwa amani kwamba amefanya makusudi na
pia kuivunjia heshima tasnia ya habari na pia kuiletea kashifa na madeni
kampuni kwani ikishtakiwa inaweza kulipa na pia
kuonekana chombo kuwa cha hovyo na kinachokwenda kinyume na umuhimu wa
tasnia ya habari.
Kwa waandishi upo uwezekano wa kushtakiwa na katika hili
waandishi wapo waliofikishwa mahakamani kwa makosa ya maadili na wapo
wanaosubiri maafa kwani shauri lao linaangaliwa.
Pia mashauri yaliyopo barazani, kufa kwa baadhi ya magazeti
kutokana na watu kuyashtaki na mengine kwa kukosa wasomaji kutokana na uandishi
mbovu na wenye chuku.
NDIO KUSEMA
Mwandishi wa habari ambaye amefunzwa kitaalamu juu ya namna ya
kukusanya habari na kuziandaa kwa ajili ya vyombo mbalimbali huku akiwajibika
kwa umma.Anatakiwa:
a)
Kuleta usawa : hii kuelezea pande mbili
zinazohusika na habari
b)
Kutofanya upendeleo yaani kuelezea upande mmoja wa
habari
c)
Kuwa mwaminifu kwa kupunguza madhara bila kudhuru
wengine
d)
Kutoa haki kwa kuhakikisha kila upande
(unaolalamikiwa na ule unaolalamika) nafasi au huduma sawa ya kusema na
kujitetea
e)
Kuhakikisha kuwa habari ina manufaa kwa umma,
inahusu ustawi kwa ujumla wa maisha ya watu ni kusema ni public interest.
Juu ya yote waandishi
wa habari lazima daima kukataa madai yasiyokuwa na mashiko kwa umma ambayo
hutengeneza mitazamo finyu na kusababisha kufikiri kimakundi na kujifunga
kimawazo. JE TUNAFANYA HAYA/ AU TUNANG’ANG’ANIA kuvunja maadili kwa ahabari za
makundi au watu binafsi au kujinufaisha wenyewe?
mwisho
COMMENTS