Mwezeshaji wa MCT Jackie Shirima,David Mbulumi na kaka Mkubwa talking notes Warsha ya maadili ya uandishi na azimio la Dar es sala...
| Mwezeshaji wa MCT Jackie Shirima,David Mbulumi na kaka Mkubwa |
talking notes
Warsha ya
maadili ya uandishi na azimio la Dar es
salaam kuhusu uhuru na uwajibikaji wa vyombo vya habari (Defir) kwa mkoa wa Mbeya
23-25Agosti 2012
Maana na umuhimu wa maadili ya uandishi wa habari
Kianzio:
Kuzaliwa kwa baraza la habari Juni 30,1995 kulilenga kutoa mwelekeo
mpya kwa waandishi wa habari kutenga mashauri yao wenyewe na pia kuwa alama
mahususi ya kitaaluma inayotoa mwelekeo ili kulinda weledi na ufanisi katika
taaluma ya habari.
Aidha juhudi ya kuwapo kwa MCT kulikofanywa na watu takribani
13 kunatokana na hofu ambayo I dhahiri ya serikali kutaka kumeza uhuru wa
habari kwa kutengeneza sheria ambazo zinatoa nguvu kubwa kwake na kukandamiza
uhuru wa habari.
Hofu iliyotanda miongoni mwa watendaji wa serikali ilifanya
Baraza hili kuchelewa kusajili hadi miaka miwili baadae na baada ya patashika
kubwa. Baraza lilisajiliwa Mei 22,1997 na uzinduzi ulifanyika Agosti 16,1997
huku wadau wakisaini kuheshimu katiba ya baraza na kufanya kazi kwa mujibu wa katiba za baraza na kuheshimu maamuzi ya baraza .
Kitu kikubwa ni maadili ya uandishi wa habari na kuheshimu maamuzi ya baraza kwa kuwa ni la
hiari.
Maadili nini?
Maadili au kw akimombo ethics ni mambo ya msingi ambayo
yanatawala tabia ya kikazi katika taaluma. Kanuni hizi husaidia jamii husika
kutambua baya na zuri na kujenga misingi ya utendaji bora wa shughuli husika.
Tunaweza kusema kwamba ethics hutambulisha fanya hiki usifanye
kile.
Mathalani mwandishi ameenda mahali amepewa fedha na chanzo cha
habari. Katika maamuzi yake ana haya yafuatayo:.
Anaweza kuchukua fedha na kuamua asiandike habari
Anaweza kuchukua fedha na kuandika habari
Anaweza kukataa fedha na habari asiandike na
Anaweza kukataa fedha na akaandika habari
Ethics zinamtaka mwandishi wa habari afanye lililobora kabisa.
Kwa hiyo katika hali ya kawaida kabisa atakataa kuchukua fedha na ataandika
habari hiyo objectively.
Ufafanuzi zaidi kuhusu maadili:
Hakuna makubaliano ya kidunia kuhusu dhana hii ya maadili ya habari katika tasnia
ya habari, kila mtu anafanya kivyake akizingatia zaidi haja na utamaduni wa
eneo. Kwa maneno mengine hakuna sheria Fulani mahususi katika fani hii kuhusu
maadili katika dunia kwa ujumla wake.
Baadhi ya watu na taasisi zinasema wazi kwamba mazingira
yalivyo duniani, vyombo vya habari haviwezi kupatana kuhusu hili la kanuni za
maadili huku wanasheria wakionya kuhusiana na kanuni hizi, wakisema ipo hatari
zinapotengenezwa na kufanyiwa kampeni za kutawala maisha na mazingira ya
waandishi, wadau, serikali , wenye vyombo mpaka walaji.
Lakini katika miaka ya 1980 wakati wa mapitio ya Unesco kuhusu
mabaraza ya habari ilibainika kwamba kuna mambo Fulani yanaingiliana duniani,
lakini yanagusa hasa msingi wa maamuzi yaani ni ya kimoral zaidi.
Ipo msingi inayotawala Falsafa ya maadili . Kimsingi unaweza
kusema inatokana na maagizo ya Mungu kwa Mungu kuna uzuri na kudai kufanyika kw
amazuri; na pili wanafalsafa akina Plato ambao walisema ipo standadi yana
uwiano wa mambo mazuri nje kabisa ya nadharia ya uzuri wa mungu, shida ni kuwa
huo uwiano upo wapi? Msingi mwingine ni kuwa maadili yanatofautiana na
mazingira, watu na utamaduni kinachoweza kufanyika nchi za magharibi si kile
kinachofanyika nchi za kiarabu.
Lakini ukitazam kwa yote yanayofanya maadili kimsingi na
matukio ya uwiano wa mvutano wa mbali na karibu wa mambo ambayo yanaitofautisha
jamii na wapuuzi wengine ya kuwajibika na kujisikia vibaya unapokosa kutekeleza
wajibu wako kiuhalali na bila woga na kwamba ndani yake kuna uzuri usiotakiwa kukoswa.
Mambo hayo ni kama:
1)
Honesty and fairness
2)
Duty to seek the views of the subject of any
critical reportage in advance of publication or broadcast, duty to correct
factual errors
3)
Duty not to fasify pictures or to use them in
misleading fashion
4)
Duty to provide an opportunity to reply to
critical opinion as well as to critical factual reportage
5)
Respect to privacy
6)
Duty to distinguish between facts,opinions and conjecture
7)
Duty not to discriminate or to inflame hatred on
such grounds as race, nationality or gender
8)
Duty not to use dishonest means to obtain
information except in special circumstances
9)
General standard of decency and taste
10) Duty not
to divulge confidential sources and
11)
Duty not to prejudice the guilt of an accused
person and publish the dismissal of charges against or acquittal of any one
about whom the paper/tv/radio previously report that charges had been filed or
that a trial had commences
Na haya ndiyo yanatakiwa
kuangaliwa na mwandishi wa habari ambaye ndiye anaeyewakilisha taaluma nyingine
katika kufanikisha uchakataji wa habari
Kuna maelezo mengi ya nani ni mwandishi wa habari na katika
hili inatupasa kuelewa kuwa wanadamu
wote ni waandishi wa habari kimsingi. Lakini ninapozungumzia mwandishi wa
habari katika mafunzo haya, namzungumzia mtu ambaye amefunzwa namna ya kukusanya
habari, kuzichakata na kuzisambaza kw akuzingatia kanuni na misingi ya uandishi
wa habari.
Misingi hiyo inamtaka mwandishi wa habari kutekeleza majukumu
yake kwa kuzingatia ukweli, uadilifu, umahiri na weledi pamoja na umakini na uwajibikaji wa hali ya juu kwa umma, ili
kujenga imani na uaminifu machoni kwa umma.
Ni wajibu pia wa msingi kwa wanahabari kuepuka tabia za uchochezi wa vurugu, chuki na kukuza
heshima ya binadamu.
Hiyo inatokana na ukweli kuwa Tasnia ya habari ipo kuhudumia
umma. Na ndio maana pamoja na wafanyabiashara kuanzisha makampuni ya habari kupata faida, vyombo vyao
vinatakiwa kuhudumia maslahi ya umma
kwani tasnia ya habari ni mali ya umma.
Ili kutoa huduma hii kwa ufanisi wadau katika chumba cha
habari kuanzia waandishi ,wahariri na wakuu wa vyombo vya habari wanapaswa kujua
maana na umuhimu wa maadili katika fani
yao ili kudumisha na kuendeleza ubora wa kazi ya kupasha habari na kujenga
imani kwa watu wanaowasoma au kuwasikiliza na hata kuwaona.
Maadili yakifuatwa
Kinachopaswa kudumishwa hapa ni maadili na kanuni za kazi
yenyewe ambapo kama yatafuatwa ni dhahiri kutaepusha msuguano na kuleta uwiano
sawa wa upashanaji habari kwa manufaa ya umma na taifa bila kujali chombo
kinachotumika ni cha mfanyabiashara, dola au cha umma.
Ukiangalia kwenye azimio la Dar es salaam (DEFIR) kifungu cha nane na tisa waandishi wa
habari wakiwa na majukumu makubwa ya kuhabarisha wengine, wanatakiwa kutekeleza
wajibu wao na majukumu yao ya kijamii kwa uadilifu mkubwa, umakini na umahiri
unaolingana na viwango vya kitaalamu na maadili na kuelewa wakati wote kuwa
wajibu na uwajibikaji wao ni kwa umma na kuwa wao ni watendaji wa umma wanaotoa
huduma katika Nyanja nyeti ya utumishi kwa umma kwa minajili ya kujenga jamii
ya kidemokrasia isiyo na ukandamizi isiyo na ubaguzi kwa misingi ya rangi,ukabila,
jinsia na ulemavu na isiyo na uvunjaji wa haki za binadamu.
Mfano mahojiano ya Clouds na mwanafunzi aliyeandika mistari ya
bongo fleva nini manufaa yake kwa taifa,mahojiano yalionesha kumtetea huyu
mwanafunzi wa kidato cha nne, yumkini
maneno yake yakashawishi wanafunzi zaidi kudharau elimu kama msingi wa
kuwa mtu bora katika fani chagua. Kama wazo lilikuwa kuonesha udhaifu wa mtoto
mapokeo ya watoto ni tofauti sana kisaikolojia, pengine katika mahojiano
walistahili kuwepo wazazi na wataalamu wa saikolojia.
Au kusema kwamba polisi hawana mawasiliano kunasaidia nini
jamii kuweka wazi kwamba polisi ni kama wako watupu nahawawezi. Je hiyo
kimantiki haiwezi kuchochea uhalifu? Kama ungelikaa kimya ukaiandika kama
changamoto kwamba wanatakiwa kusaidiwa zaidi vifaa inakuaje. Isije ikawa
kuongezeka kwa uhalifu kwa asilimia 3.9 kunatokana na kuweka wazi wazi matatizo
ya lojistiki ya jeshi la polisi.
Maadili kwa misingi mingine unaweza kusema ni utekelezaji wa matakwa ya taaluma ili
kuweka bayana ukweli, usahihi, haki na uhuru
bila kuonea upande wowote kwa kuzingatia miiko ya taaluma na bila
kuumiza maslahi ya jamii.
Tujikumbushe
Mwandishi wa habari ni nani?
|
N
|
i mtu aliyefunzwa kitaalamu namna ya kukusanya habari na
kuziandaa kwa ajili ya vyombo mbalimbali huku akiwajibika kwa umma.Anatakiwa:
a)
Kuleta usawa : hii kuelezea pande mbili
zinazohusika na habari
b)
Kutofanya upendeleo yaani kuelezea upande mmoja wa
habari
c)
Kuwa mwaminifu kwa kupunguza madhara bila kudhuru
wengine
d)
Kutoa haki kwa kuhakikisha kila upande
(unaolalamikiwa na ule unaolalamika) nafasi au huduma sawa ya kusema na
kujitetea
e)
Kuhakikisha kuwa habari ina manufaa kwa umma,
inahusu ustawi kwa ujumla wa maisha ya watu ni kusema ni public interest.
Juu ya yote waandishi wa habari
lazima daima kukataa madai yasiyokuwa na mashiko kwa umma ambayo hutengeneza
mitazamo finyu na kusababisha kufikiri kimakundi na kujifunga kimawazo.
>>Madhara ya kupinda maadili
Adhabu ya kutofuata kanuni na kuheshimu maadili hupatikana
papo hapo mwandishi anapovunja. Adhabu hiyo ni kusongwa na moyo na kukosekana
kwa amani kwamba amefanya makusudi na
pia kuivunjia heshima tasnia ya habari na pia kuiletea kashifa na madeni
kampuni kwani ikishtakiwa inaweza kulipa na pia
kuonekana chombo kuwa cha hovyo na kinachokwenda kinyume na umuhimu wa
tasnia ya habari.
Kwa waandishi upo uwezekano wa kushtakiwa na katika hili
waandishi wapo waliofikishwa mahakamani kwa makosa ya maadili na wapo
wanaosubiri maafa kwani shauri lao linaangaliwa.
Pia mashauri yaliyopo barazani, kufa kwa baadhi ya magazeti
kutokana na watu kuyashtaki na mengine kwa kukosa wasomaji kutokana na uandishi
mbovu na wenye chuku.
NDIO KUSEMA
Mwandishi wa habari ambaye amefunzwa kitaalamu juu ya namna ya
kukusanya habari na kuziandaa kwa ajili ya vyombo mbalimbali huku akiwajibika
kwa umma.Anatakiwa:
a)
Kuleta usawa : hii kuelezea pande mbili
zinazohusika na habari
b)
Kutofanya upendeleo yaani kuelezea upande mmoja wa
habari
c)
Kuwa mwaminifu kwa kupunguza madhara bila kudhuru
wengine
d)
Kutoa haki kwa kuhakikisha kila upande (unaolalamikiwa
na ule unaolalamika) nafasi au huduma sawa ya kusema na kujitetea
e)
Kuhakikisha kuwa habari ina manufaa kwa umma,
inahusu ustawi kwa ujumla wa maisha ya watu ni kusema ni public interest.
| Lidia mapunda akiperuzi gazeti wakati wa kuchambua habari zisizo na viwango katika magazeti.Picha kwa hisani ya KALULUNGA.BLOGSPOT.COM kwa mapicha zaidi tembelea huko |
Juu ya yote waandishi
wa habari lazima daima kukataa madai yasiyokuwa na mashiko kwa umma ambayo
hutengeneza mitazamo finyu na kusababisha kufikiri kimakundi na kujifunga
kimawazo. JE TUNAFANYA HAYA/ AU TUNANG’ANG’ANIA kuvunja maadili kwa habari za
makundi au watu binafsi au kujinufaisha wenyewe?
mwisho
COMMENTS