Katika mpango mkubwa wa kutanua wigo wake wa wasikilizaji na watazamaji barani Afrika, BBC imetangaza kuzindua kipindi chake cha k...
Katika mpango mkubwa wa kutanua wigo wake wa
wasikilizaji na watazamaji barani Afrika, BBC imetangaza kuzindua
kipindi chake cha kwanza cha habari za dunia kwa lugha ya
Kiswahili
kiitwacho Dira ya Dunia. Kuanzia Jumatatu Agosti 27, kituo shirika
cha
BBC Idhaa ya Dunia nchini Tanzania, Star TV, kitarusha kipindi cha
Dira
ya Dunia cha BBC Idhaa ya Kiswahili. Matangazo hayo ni ya dakika
30
yakiwapa watazamaji fursa ya kupata habari motomoto za dunia na
uchambuzi yakinifu kutoka katika shirika hilo la utangazaji la
kimataifa
ulimwenguni.
Kipindi hicho ambacho kitakuwa kikirushwa kila Jumatatu hadi
Ijumaa
kitatoa chachu katika matangazo ya Star TV kwa kuwaletea
watazamaji
habari za kiwango cha hali ya juu kutoka katika kitovu cha habari
za
dunia cha BBC- Global News. Dira ya Dunia pia itawaletea
watazamaji
taswira na uchambuzi yakinifu kutoka kwa waandishi wa habari
waliotapakaa katika nchi 48 barani Afrika, na hivyo kuleta picha
halisi
ya bara zima kwa watazamaji wanaozungumza Kiswahili.
Kipindi cha radio cha Dira
ya Dunia ni kipindi maarufu sana kwa
mamilioni ya wasikilizaji katika eneo la Afrika Mashariki na Kati
na
hata wasikilizaji wanaoishi nje ya eneo hilo. Kwa kuzindua kipindi
cha
TV chenye jina kama hilo, BBC ina imarisha zaidi matangazo yake
hasa kwa
kutumia waandishi wake wa habari waliobobea - watangazaji Salim
Kikeke
na Charles Hilary, mhariri Mariam Omar pamoja na waandishi waliopo
Burundi, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Kenya, Nigeria, Rwanda,
Afrika
Kusini, Sudan Kusini, Tanzania, Uganda na Uingereza.
Mhariri wa BBC Idhaa ya Kiswahili, Ali Saleh anasema:
"Uzinduzi wa Dira
ya Dunia kupitia TV, ni kwenda na mabadiliko makubwa
tunayoyashuhudia ya
jinsi watu wanavyofuatilia habari barani Afrika, na pia mahitaji
wa
mashabiki wa BBC Ihdaa ya Kiswahili. Tunavyoarifu na kuchambua
habari za
eneo letu na hata duniani, iwe siasa, uchumi au utamaduni, Dira ya
Dunia
itatoa taswira halisi ya Afrika, tofauti na jinsi ambavyo bara
hili
limekuwa likiripotiwa kwa miaka mingi. Kipindi chetu kitakuwa
kinashirikisha watazamaji, na pia kuzigatia misingi ya BBC ya muda
mrefu
ya uhuru, uhakika na bila upendeleo"
Kinara wa Dira ya Dunia, Salim Kikeke ameongeza kwa kusema:
"Ni heshima
kubwa na nafasi ya kipekee kuwa katika mradi huu wa Idhaa ya
Kiswahili
ya BBC wa TV. Tumepitia mengi hadi kufika hapa, na kila sekunde ya
safari hiyo ilikuwa ni ya kuvutia.Ni imani yangu kuwa kipindi hiki
kipya
cha TV kitavutia wengi katika eneo la Afrika Mashariki na
Kati."
Uanzishaji wa Dira ya Dunia katika TV ni sehemu ya mabadiliko
makubwa ya
matangazo yaliyofanyika ndani ya BBC mwaka huu katika bara la
Afrika,
katika TV na redio. Uzinduzi huu umekuja muda mfupi baada ya
kuzinduliwa
kwa kipindi cha TV kwa lugha ya Kiingereza kwa Afrika, Focus on
Africa,
ambacho pia kinarushwa kupitia Star TV. Mwezi Julai, siku chache
kabla
ya kuanza kwa michuano ya Olimpiki jijini London, BBC Idhaa ya
Ulimwengu
ilizindua kipindi kipya cha redio, Newsday - Kipindi ambacho
kimelenga
zaidi wasikilizaji wa redio wa asubuhi barani Afrika.
Mhariri wa BBC wa eneo la
Afrika, Solomon Mugera, naye amesema: "Miongo
mingi ya utangazaji katika lugha mbalimbali barani Afrika, BBC
imejenga
uhusiano wa kipekee na wasikilizaji wetu wa redio, kwa kueleza ya
Afrika
duniani, na kuipeleka dunia barani Afrika. Kukua kwa njia za utangazaji
za BBC ni ushahidi wa kuwepo kwa mizizi ya muda mrefu na ufahamu
wa bara
la Afrika. Tunavyoanza safari hii mpya, kwa kweli tuna hamasa
kubwa hasa
kwa kushirikiana na mashirika ya utangazaji yenye hadi kubwa
katika eneo
letu."
Nathan Lwehabura, Meneja
mipango na utafiti wa SMG Ltd, anasema: " Ni
heshima kubwa kwa Star TV kujumuisha Dira ya Dunia katika vipindi
vyake
vya kila siku - tunaamini kipindi hiki kitavutia watu wengi.
Kipindi cha
BBC cha Kiingereza kilichozinduliwa hivi karibuni kupitia Star TV,
Focus
on Africa, kinazidi kujipatia umaarufu mkubwa, sio tu miongoni mwa
watazamaji wetu, bali pia hata miongoni mwa mashirika mengine
kutokana
na kuzingatia fani ya uandishi, utangazaji na ubora wa kipindi. Ni
matumaini yetu kuwa ushirika kati ya BBC na Sahara Media Group
utaimarisha matangazo yetu ya TV hasa tunavyoelekea katika
matangazo ya
kisasa ya mfumo wa digital."
Dira ya Dunia kutoka Idhaa
ya Kiswahili ya BBC itakuwa ikitangazwa
Jumatatu hadi Ijumaa, saa tatu usiku kupitia Star TV nchini
Tanzania.
Pia matangazo hayo yatapatikana kupitia wavuti wa BBC Idhaa ya
Kiswahili
- bbcswahili.com.
BBC ilirusha matangazo yake ya kwanza kabisa barani Afrika zaidi
ya
miaka 80 iliyopita. Idadi kubwa ya wasikilizaji kwa ujumla kupitia
redio
na TV inaifanya BBC kuwa shirika kubwa zaidi la kimataifa la
utangazaji
barani Afrika.
Kwa taarifa zaidi tafadhali wasiliana na:
BBC Global News Press Office
+44 207 557 2944; sophie.west@bbc.co.uk <mailto:sophie.west@bbc.co.uk>
COMMENTS