‘Mbuzi Mmoja tu Anaweza Kuleta Mabadiliko’ Watoto wakishindana kuvuta kamba wakati wa mashindano ya mbio za mbuzi ya his...
‘Mbuzi Mmoja tu Anaweza Kuleta Mabadiliko’
![]() |
| Watoto wakishindana kuvuta kamba wakati wa mashindano ya mbio za mbuzi ya hisani ya mwaka jana. (picha: maktaba) |
Matayarisho ya mwisho ya Mashindano ya 12 ya Mbio
za Hisani za Mbuzi yatakayofanyika Septemba 1 mwaka huu jijini Dar es Salaam
yanaendelea.
Tukio hilo la kifamilia linalofanyika kila mwaka tayari
limeshafanikiwa kukusanya kiasi cha Shilingi milioni 544 (zaidi ya dola 345,000)
kutoka kwa karibu makundi 50 ya wahisani wa ndani tangu lilipoanza mwaka 2001.
(Tazama maelezo chini kwa mbio za mwaka huu.)
Zaidi ya watu 3,000 hushiriki kila mwaka, huku pia
wakijifurahisha kwa kutabiri mbuzi atakayeshinda, wakishiriki kwenye mashindano
ya mavazi yenye muonekano wa aina yake na kujiaribu ladha ya vyakula mbalimbali
vya kiasili na vinywaji wakiwa na familia na marafiki zao.
Yeyote anaweza kushiriki na kushinda zawadi
mbalimbali za kuvutia, ikiwa ni pamoja na zawadi kubwa kwa mwaka huu kutoka
Shirika la Ndege la Uingereza (British Airways) tiketi ya kwenda na kurudi Uingereza.
(Tazama orodha nzima ya zawadi chini.)
Watoto, kuanzia wanaotambaa na kuendelea, nao
watapata fursa nzuri ya kufurahi kwenye eneo maalumu lililodhaminiwa na Game kwa
kila wakitakacho. Kutakuwapo michezo ya kufurahisha, kupakwa rangi usoni,
michezo ya sanaa, mashindano ya mavazi ya watoto na burudani kutoka Kituo cha Kigamboni
Community Centre (tazama maelezo).
Mwanzilishi wa mbio za Dar Charity Goats Race, Paul
Joynson-Hicks anasema: “Nadhani inafurahisha kuona kuwa wazo la kuchekesha kama
hili la mbio za mbuzi Iimegeuka na kuwa tukio kubwa hapa Dar.
“Si tu kwamba tunakusanya mamilioni ya fedha kwa
ajili ya shughuli mbalimbali za hisani na kusaidia makundi mbalimbali, kubadilisha
kabisa maisha ya watu, lakini pia tunalifanya tukio hili kwa namna ambayo
inavuta hisia za wengi huku likiwafurahisha.”
Mashindano ya mwaka huu yatafanyika kuanzia saa
sita mchana hadi saa 11.30 jioni, kwenye viwanja vya The Green, Barabara ya Kenyatta.
‘Dar Charity Goat Races’ inaandaliwa na kamati ya
watu waliojitolea, pamoja na mkazi wa siku nyingi wa jiji hili, Bi. Karen
Stanley ambaye ndiye kinara wa tukio hili.
Mama huyo alisema: “Ninafuraha sana kushuhudia
jambo hili likiendelea kukua mwaka hadi mwaka likiwa na muonekano wa kuvutia
kwa sasa.
“Ukarimu wa wadhamini, wakubwa kwa wadogo, unamaanisha
kuwa tunaweza kukusanya kiasi kikubwa cha fedha ambacho baadaye hutolewa kwa
watu ambao kweli wanahitaji kusaidiwa.
“Haya yasingeweza kufanyika bila wao, hasa wale
wanaolipa ili wamiliki mashindano haya. Wamiliki wa mbio za mwaka huu ni Southern
Sun, British Airways, Coca-Cola, Tanzanian Breweries Limited, British Gas,
aetna na Mantra Tanzania.”
Tiketi moja ni Shilingi 5,000 na zitauzwa getini. Kwa
maelezo zaidi tembelea tovuti www.goatraces.com, au tuma barua pepe: goatraces@goatraces.com
au piga simu 0755 555 900.
Kwa waandishi wa habari wasiliana na Peter Mgongo kwa
simu 0784 765454 au barua pepe mgongo@gmail.com.
Lakini kwa ujumla unaweza kuwasiliana na Emma Pearson (mjumbe wa kamati
anayeshugulikia vyombo vya habari na mawasiliano ya umma) kwa simu 0768 912933 au
barua pepe ekpea@yahoo.co.uk
Maelezo
kwa Wahariri:
- Mwenyekiti wa Kamati ya ‘Goat Races’, Karen Stanley anapatikana kwa mahojiano ikiwa itahitajika.
- Picha pia zinapatikana kwa maombi rasmi.
- Jinsi mbio hizo zinavyofanyika:
*Kuna aina saba za
mashindano. Kila moja hudhaminiwa na wamiliki wa mbio hizo ambao kwa mwaka huu
ni Southern Sun, British Airways, Coca-Cola, Tanzania Breweries Limited,
British Gas, aetna na Mantra Tanzania.
*Hawa humlipia mbuzi
mmoja katika shindano moja. Mbuzi wao akishinda, wanakuwa na nafasi ya kupata
zawadi kubwa. Wengi huungana na rafiki au jamaa zao na kuwa wamiliki wa pamoja
wa mbuzi.
*Wote hupata nafasi ya
kuingia kwenye eneo maalumu na kupata nafasi nzuri ya kumshangilia mbuzi wao, na
kupata vinywaji na chakula bure kwa hisani ya Southern Sun Hotel, Tanzania
Breweries Ltd, Tanzania Distilleries Ltd, RednWhite na Coca-Cola.
- Wahisani wa mwaka huu ni:
·
Africa's Children - Africa's Future
·
BibiJann's Centre
·
Diocese of Central Tanganyika
·
Foxes' NGO
·
Kidzcare Tanzania
·
Kigamboni Community Centre
·
Molly's Network
·
United Planet
·
Zanzibar Outreach Program
- Kituo cha Kigamboni Community Centre – Hushughulikia umasikini na masuala ya afya kwa kutoa elimu ya bure kwa watoto walio kwenye mazingira magumu. Wana mambo mengine kadhaa wanayoyafanya ikiwa ni pamoja na masuala ya utamaduni kama maigizo, ngoma za asili na za kisasa, soka, muziki na sarakasi.
- Zawadi za mwaka huu ni:
·
British Airways – Tiketi mbili za kwenda London na
kurudi.
·
Blue Bay Beach Resort, Zanzibar – nafasi ya watu
wawili kwenda mapumzikoni Zanzibar kwa siku tatu pamoja na tiketi ya ndege
kutoka Dar kwenda Zanzibar kwa Zanair
·
Uhuruone – Mwaka mmoja wa kutumia bure ‘internet’
na vifaa vyake, kuvifunga na kuhudumiwa (ndani ya eneo linalopata mtandao wa Uhuruone).
·
Selous Great Water Lodge – Kifurushi cha safari
fupi kwa watu wawili, pamoja na usafiri wa kutoka Dar na kurudi, kusafari kwa
boti mtoni, kutembelea mbuga kwa siku nzima (na kuingia mbugani), kutembea kwa
miguu msituni na kulala kwenye hoteli kubwa kwa siku mbili.
·
Coastal Travels and Sea Cliff Hotel & Spa,
Zanzibar – Tiketi za kwenda Zanzibar na kurudi kwa watu wawili, pamoja na
malazi ya siku mbili kwa watu wawili kwenye hoteli ya Sea Cliff Zanzibar.
·
Selous Safari Company – Malazi ya siku mbili kule Ras
Kutani kwa watu wawili (vigezo kuzingatiwa).
·
Paragon Enterprises Ltd – Vocha ya dola 500 ya Tanzanite.
·
Begi la kisasa kutoka Toyota.
·
Colosseum Hotel and Fitness Club –Uanachama wa
miezi miwili kwa watu wawili ama Arena Gym, Palm Residence au The Colosseum
Gym.
·
Red ‘n’ White – Mfuko wa kisasa wa chapa ya Freixenet.
·
Watoto kupiga picha na Maretha L Pienaar.

COMMENTS