BAWACHA WASEMA WANASHANGAZWA NA MAUAJI YA RAIA

TAMKO LA BARAZA LA WANAWAKE WA CHADEMA  ( BAWACHA) KWA VYOMBO   VYA HABARI Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA), tunalaani...




TAMKO LA BARAZA LA WANAWAKE WA CHADEMA  ( BAWACHA) KWA VYOMBO  VYA HABARI

Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA), tunalaani kwa nguvu zote mauaji yanayoendelea nchini yakifanywa au kusababishwa na Jeshi la Polisi ambao tuliamini kuwa ni walinzi wetu na mali zetu, lakini wamegeukaa kuwa ndio wauaji wakubwa wa wananchi wasiokuwa na hatia.

Aidha, BAWACHA tumeshangazwa na kauli ya Msajili wa Vyama vya Siasa John Tendwa ya kufuta vyama vya siasa ambavyo mauaji yatatokea katika mikutano yao, wakati anajua kuweli kuwa mauaji hayo yanafanywa na Jeshi la Polisi.

BAWACHA tunatambua kuwa kauli hiyo inailenga CHADEMA ili kutekeleza dhamira ovu ya Tendwa aliyotumwa na Serikali inayooongozwa na CCM. Tunamtaka Tendwa awaeleze Watanzania iwapo kauli yake hiyo haitatumiwa na polisi na CCM kuua tena ili kukoleza sababu za kutaka kuifuta CHADEMA.

Tunashangazwa na utendaji kazi wa Jeshi la Polisi ambalo limefikia mahali linatumia nguvu kubwa na kuua wananchi ambao mbali ya kuwa hawana hatia yoyote, pia hawana silaha yoyote lakini ndio wanaopigwa na mabomu na risasi za moto. Baraza la Wanawake wa CHADEMA, tunalaani vitendo hivi vya kinyama vinavyoendelea nchini.

Kumekuwa na matukio mfululizo wa Jeshi la Polisi kutumia nguvu kubwa sana katika mikutano ya CHADEMA, mauaji ya Januari 5, 2011 Jijini Arusha, ambapo polisi waliua kwa risasi za moto watu watatu ambao hawakuwa na hatia wala silaha yoyote.

Hata katika matukio mengine yasiyohusiana na shughuli za kisiasa zinazofanywa na wananchi, polisi wamekuwa wakitumia nguvu kubwa kudhibiti mitafaruku inayotokea hali ambayo badala ya kutatua imekuwa ikiongeza ukubwa na ugumu wa tatizo. Tulishuhudia katika Jiji la Mbeya Watanzania wanaofanya shughuli za biashara ndogondogo (Wamachinga) walipigwa mabomu na risasi za moto kusababisha hasara kubwa,  ambapo pia katika tukio hilo waandishi wa habari ambao hawakuwa na silaha yoyote zaidi ya kalamu zao, waliathiriwa na matumizi hayo nguvu kubwa kutoka kwa askari bila sababu za msingi.

Tukio la karibuni kabisa ni lile lililotokea mjini Morogoro ambapo kijana mmoja, Ali Zona aliyekuwa akiendelea na shughuli zake pembeni mwa barabara, aliuawa na Jeshi la Polisi kwa kitu kinachoonekana kuwa ni risasi au bomu, lakini polisi wakatoa taarifa isiyokidhi kiu ya kutaka kujua, wakisema kijana huyo hakupigwa risasi bali alipigwa na kitu kizito.

Aidha BAWACHA inalaani vikali mauaji ya Mwandishi wa Habari wa Channel Ten, Hayati Daudi Mwangosi aliyeuawa kwa kushambuliwa kinyama na hatimaye  kulipuliwa kwa bomu na polisi mbele ya mashuhuda walioshuhudia jinsi mwandishi huyo akisambaratishwa mithili ya mnyama wakati akitimiza wajibu wake wa kuitumikia jamii. Mwangosi hakuwa na silaha yoyote zaidi ya vitendea kazi vyake vya uandishi wa habari, lakini bado askari walitumia nguvu kubwa kumshambulia na kumuua.

Mfululizo huu wa mauaji katika maeneo tofauti ya mikoa mbalimbali nchini  yanayofanywa na Jeshi la Polisi unathibitisha  kuwa hayafanyiki katika mikutano ya CHADEMA pekee, bali pia katika matukio mengine ya wananchi katika maeneo mengi nchini.

Hivyo BAWACHA inataka Watanzania kupuuza kauli iliyotolewa na CCM kupitia kwa Nape Nnauye ya kuwataka CHADEMA na viongozi kuwajibika kwa mauaji yaliyofanywa na Jeshi la Polisi mkoani Iringa na maeneo mengine nchini.

BAWACHA inatambua kuwa kauli hiyo ni ishara ya CCM kushiundwa kuongoza na kulinda mauaji yanayoendelea nchini. Ikiwa CCM ingekuwa inakerwa na mauaji hayo, badala ya kutaka CHADEMA iwajibike ingewawajibisha viongozi wake wa CCM na serikali, ambao wameongoza vikao vya Kamati za Ulinzi na Usalama kushawishi Jeshi la Polisi kuvuruga operesheni halali za CHADEMA na kufanya mauaji.


Tunapenda polisi wajue kuwa haya ni makosa makubwa kutumia vibaya madaraka waliyodhaminiwa na  wananchi, ambao pia ndiyo waliowasomesha, wanawalipa mishahara na kutimiza mahitaji yao muhimu ikiwemo vitendea kazi vyao kutokana na kodi wanazolipa lakini badala ya kuwatumikia, wanawaua kwa ukatili mkubwa.

Izingatiwe kwamba CHADEMA walikuwa hawaandamani wala kufanya mikutano ya hadhara bali walikuwa wanafungua matawi ya chama chao na kufanya vikao vya ndani.

Wamesababisha usumbufu mkubwa kwa Taifa, familia zao kuwakosa wapendwa wao, na si hivyo tu BAWACHA kama wanawake na wazazi tumeumia sana na vitendo vya kinyama vinavyofanywa na Jeshi la Polisi kote nchini. Tunasema tukiwa kama wazazi wenye uchungu na uzazi, tumechoka kusikia na kuona mauaji haya ya kinyama ya watu wasiokuwa na hatia.

BAWACHA tunasema kwa kuwa  Jeshi la Polisi limelifedhehesha Taifa na kutia doa nchi yetu inayojulikana dunia nzima kwamba ni kisima cha amani.

BAWACHA tunamtaka Waziri Emmanuel Nchimbi, IGP Said Mwema, Kamishna Paul Chagonja na RPC Michael Kamuhanda wajiuzuru haraka sana, ili wakati tume huru ya uchunguzi itakapoundwa kwa mujibu wa sheria kuchunguza tukio hilo na mengine, wao wahojiwe wakiwa hawako madarakani ili wasiharibu ushahidi.

Aidha BAWACHA  kwa ujumla tunasikitishwa kuona kwamba CCM na serikali yake, kwa kutumia Jeshi la Polisi sasa wameamua kutumia silaha kujibu nguvu za hoja za CHADEMA zinazochochea fikra na kuamusha ari ya mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala miongoni mwa Watanzania makini, ndani na nje ya bunge.

Lengo kubwa la Serikali ya CCM ni kuwafanya wananchi  washindwe kutambua  haki zao ili waweze kuwatala kwa urahisi, na kuifanya nchi kama mali yao binafsi wakiwa na hati miliki ya kutawala watakavyo.

Aidha BAWACHA tunalitaka Jeshi la Polisi Mkoani Iringa liwaambie wananchi ni nani aliyewashinikiza kwenda kuvuruga mikutano halali ya CHADEMA na kufanya mauaji.
Hizo ni mbinu za Chama Tawala cha CCM kuanzisha vurugu ili kuuhadaa umma na kutaka kuuaminisha kuwa CHADEMA ni chama cha vurugu. Tunawataka wajue katika mbinu hiyo pia hawatafanikiwa kama ambavyo hawajawahi kufanikiwa katika mbinu zao zingine.

BAWACHA  tunawasihi Watanzania wote waendelee kuiunga mkono CHADEMA katika kupaza sauti kutaka uwajibikaji wa Waziri Nchimbi, Said Mwema, RPC Michael Kamuhanda na Paul Chagonja wajiuzuru kwa maana wamelitia fedheha Taifa letu.

Aidha BAWACHA tunawaomba wanawake wote watuunge mkono kwani athari za mauaji haya yanayoendelea sasa ambayo yanafanywa na Jeshi la Polisi ni kubwa sana.

Watanzania tuungane kwa pamoja kuhakikisha haki inapatikana kwa kila mmoja wetu ili kudumisha na kulinda amani na utulivu katika nchi yetu.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

Subira  Waziri
Naibu  Katibu Mkuu
BAWACHA  - Taifa

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7051,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: BAWACHA WASEMA WANASHANGAZWA NA MAUAJI YA RAIA
BAWACHA WASEMA WANASHANGAZWA NA MAUAJI YA RAIA
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/09/bawacha-wasema-wanashangazwa-na-mauaji.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/09/bawacha-wasema-wanashangazwa-na-mauaji.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy