THE CIVIC UNITED FRONT
|
|
Office of TheYouth Secretary General
P.O. Box
10979
Dar Es Salaam, Tanzania
e-mail: juvcuf@yahoo.com
http://www.cuf-or.tz
CUF/DSM/JUVCUF/002/1A/2012/0105/09/2012
MAUAJI YA RAIA NI MUHIMU MTAALA WA MAFUNZO
YA POLISI KUANGALIWA UPYA.
SEKRETARIETI ya Vijana
Chama cha Wananchi –CUF (JUVCUF) Taifa tunataka Serikali kupitia upya MTAALA wa
Mafunzo wa Jeshi la Polisi kwa lengo la kuwapa elimu ya maadili mema katika utendaji
wao wakazi ikiwa ni pamoja na kuwapa mbinu na jinsi ya kukabiliana na
changamoto ndogondogo kamaza Maandamano ya Raia na Mikutano yahadhara inayofanyika
kwa Sasa, hasa kutokana na kukua kwa Demokrasia hapa nchini.
Tunaamini bila ya Serikali
kukaa na kuliangalia nini polisi wanatakiwa wafundishwe wanapokabiliana na raia
wasiokuwa na silaha wala kujua matumizi yake, hali itazidi kuwa mbaya hapa nchini
sababu Polisi wataendelea kukosa maadili, wataua na kujeruhi raia jambo litalowafanya
raia nao kutembea na silaha za moto kila watapokuwa kwenye mikutano yao ya hadhara
au Maandamano, na ikifikia hapo nchi itakuwa imepoteza amani yake iliyodumu kwa
nusu karne sasa na itasababisha nchi kuingia kwenye machafuko kama ilivyotokea katika
mataifa ya Afrika Kaskazini ambapo ilifika mahali vijana walichoshwa na vitendo
vya mauji ya raia na kuamua kuasi wakapambana
na Utawala hadi ukaanguka madarakani.
JUVCUF tunaamini kuwa Watanzania
wengi hasa vijana wamekuwa wakiishi kwa utulivu huku wakilinda amani ya Taifa hili
pamoja na matatizo makubwa ya umasikini yanowakabili kutokana na kukosekana kwa
ajira za uhakika na kudumu kunakosababishwa na mfumo mbaya wa utawala na
mipango hasi ya chama cha Mapinduzi.
Tunaiomba serikali kuwa makini
na iwajengee uadilifu watendaji wake waliopo kwenye vyombo vya ulinzi na
usalama kwa lengo la kuheshimu Mkataba wa kimataifa wa haki za Binadamu wa 1948
ili kulinda haki za msingi za binadamu hapa nchini.
Vijana wa CUF tunaendelea kulaani
mauaji hayo yanayoendelea kufanywa na Polisi kwa kuwa yamekiuka haki ya msingi ya
kuishi ya Marehemu Mwangosi kijana ambae alikuwa bado anahitaji kulitumikia Taifa
lake.
Hivyo tunaomba Tume iliyoteuliwa
iwe makini katika kuchunguza na kulifuatilia suala hili na iwe huru na yeyote aliyehusika atajwe na kufikishwa kwenye mikono ya sheria
bila kujali nafasi, umaarufu au uwezo wa kifedha alionao.
Tunawaomba Vijana wajiunge
na kushirikiana na CUF ili tulete mabadiliko yenye tija na manufaa kwa Vijana yatayolinda
haki ya kila kijana ndani ya nchi na kupambana na kuondoa uonevu kama huo unaofanywa
na polisi kwa maslahi ya watu wachache
Ashura
Mustapha
Mkurugenzi
wa Habari Secretarieti ya Vijana CUF-Taifa
0655
727341








0 comments:
Post a Comment