MAGARI AINA YA NOAH HAYASTAHILI KUTOA HUDUMA YA USAFIRI WA UMMA

Huduma ya usafirishaji wa abiria kwa kutumia magari aina ya Toyota NOAH nchini Tanzania, ulianzia katika mikoa ya Kaskazini   ya Kilimanj...


Huduma ya usafirishaji wa abiria kwa kutumia magari aina ya Toyota NOAH
nchini Tanzania, ulianzia katika mikoa ya Kaskazini  ya Kilimanjaro,
Arusha na Manyara ambapo magari hayo yalipewa leseni za kutoa huduma ya
usafiri katika njia zote, leseni ambayo hutolewa kwa magari ya
kusafirisha watalii tu.  
 
Hata hivyo wamiliki wa magari hayo hawakuzingatia  masharti ya leseni ya
usafirishaji kwani badala ya kusafirisha watalii walijiingiza kwenye
biashara ya usafiri wa umma na hivyo kuzusha migogoro kati ya
wasafirishaji wa magari makubwa katika njia hizo na wamiliki wa Noah.  
 
Migogoro hiyo ilitokana na magari hayo kutokuwa na leseni ya njia maalum
na hivyo kusababisha vurugu za mara kwa mara katika utoaji wa huduma ya
usafirishaji abiria katika maeneo husika.  
 
Kwa kuzingatia kuwa tayari kulikuwa na mgogoro wa wasafirishaji,
Mamlaka ya SUMATRA iliona ni vyema kukutana na wadau  wa usafiri katika
mikoani husika kwa lengo la kujua hali halisi ya usafiri katika mikoa
hiyo pamoja na kujua kero za wananchi kwa ujumla na kuzitafutia
ufumbuzi. 
 
Katika mikutano hiyo, changamoto mbalimbali za masuala ya usafirishaji
zilijadiliwa zikiwemo, ajali za barabarani, upandishwaji holela wa nauli
pamoja na   vurugu za mara kwa mara  zinazosababishwa na  waendeshaji wa
magari ya Noah ambayo hayakuwa na leseni za usafirishaji.
 
Baada ya kutathmini changamoto mbalimbali zilizojadiliwa kwenye mikutano
hiyo, Mamlaka ilifanya tathmini ya utendaji kazi wa aina hii ya magari
ya Noah na kubaini kuwa kulikuwa na malalamiko mengi kutoka kwa abiria
na wasafirishaji wa mabasi makubwa wanaotoa huduma ya usafiri katika
maeneo ambayo magari ya Noah yakitoa huduma. 
 
Baadhi ya malalamiko yaliyotolewa na abiria waliotumia huduma ya magari
ya Noah ni pamoja na abiria kutozwa nauli kubwa zaidi ya viwango
vilivyoridhiwa na Mamlaka; abiria kuhoji umbali unaoruhusiwa kwenda
magari hayo pamoja na uimara wa bodi ya magari hayo kwa kubeba abiria;
mizigo ya abiria kuachwa kwenye vituo kutokana na kutokuwa na nafasi ya
kuhifadhia na magari hayo kutoa huduma bila kufuata njia maalum kama
ilivyoainishwa kwenye leseni zao. Malalamiko mengine yalihusisha magari
ya Noah kukwama mara kwa mara sehemu za vijijini hasa wakati wa mvua;
mwendo kasi ambao ni hatari kwa maisha ya abiria na madhara makubwa kwa
abiria na mali zao ajali zinapotokea kutokana na uhafifu wa bodi zake
 
 
 
Baadhi ya wasafirishaji wanaotoa huduma ya usafiri mijini na kati ya mji
na mji, wamelalamikia magari ya Noah kuwa magari hayo yemekuwa yakitoa
huduma ya usafirishaji bila ya kufuata utaratibu wa kupakia abiria wa
kufuata foleni kama ulivyo utaratibu wa watoa huduma kwa mikoa ya
Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Baadhi ya vyama vya wasafirishaji
viliwahi kuandika malalamiko yao na kuonyesha wasiwasi wa kuzorota au
kudidimia kwa sekta ya usafirishaji kutokana na wasafirishaji wenye
uwezo wa kuagiza mabasi makubwa kuacha kufanya hivyo na kununua magari
ya Noah ili kujipatia faida haraka pasipo kuangalia maslahi na usalama
wa wasafiri. 
 
 Baada ya Mamlaka ya SUMATRA kupokea malalamiko hayo Mamlaka  ilifanya
tathmini iliyoshirikisha Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani
pamoja na Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na kubaini kuwa uwezo wa
magari hayo kutumika kama usafiri wa umma ni mdogo na hivyo kuifanya
biashara ya usafirishaji kwa kutumia magari hayo kutokuwa na tija;
magari  ya aina hiyo madirisha yake ni madogo na hayana milango ya
dharura. Aidha, magari hayo hayakidhi matakwa ya kifungu namba 4.4.3 cha
Kiwango Na. 598:1999 pamoja na Kifungu Namba 5.2.1 - 5.3.5 Kiwango TZS
598 (Part 3): 2010 cha Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa magari ya
abiria. Vifungu hivyo vinaeleza viwango vya bodi, madirisha na urefu
katika gari la abiria.
 
Zaidi ya hiyo matumizi ya magari hayo yana hatari ya kudumaza au
kudidimiza sekta ya usafirishaji kwa waagizaji wa mabasi makubwa kuacha
kuagiza mabasi hayo yenye uwezo mkubwa (Economies of Scale) wa kubeba
abiria wengi kwa pamoja na kuagiza magari mengi ya Noah yenye uwezo wa
kubeba abiria wachache. Aidha ilibainika kuwepo kwa uwezekano mkubwa wa
msongamano wa magari kwenye miji ya mikoa hiyo pamoja na abiria kukosa
haki ya msingi ya kusafiri na mizigo usiozidi kilo 20 ambapo ni kinyume
na Kanuni Na. 23 (1) ya kanuni za leseni za usafirishaji magari ya
abiria mwaka 2007.
 
Kutokana na hali hiyo SUMATRA ilifikia  uamuzi wa kusitisha utoaji wa
leseni hizo, baada ya  ya kutathminini malalamiko na hoja mbalimbali
zilizotolewa na wadau wa usafiri. 
 
 maamuzi hayo yanazingatia jukumu la SUAMTRA katika kusimamia sekta ya
usafirishaji abiria kwa njia ya barabara kama yalivyoainishwa katika
Kifungu Namba 5(b)(c)(d) cha Sheria ya SUMATRA, ambapo  Mamlaka ilitoa
maamuzi kuwa kuanzia tarehe 10/01/2012 hakutakuwa na utoaji wa leseni za
usafiri wa umma kwa msafirishaji mpya anayemiliki gari la Noah. Aidha
magari ya aina hiyo ambayo yatahitaji kufanya biashara ya usafirishaji
abiria yataruhusiwa kwa kupewa leseni ya kutoa huduma ya usafiri kwa
watalii tu.
 
Kwa mmiliki wa Noah mwenye leseni ya usafirishaji, ataruhusiwa
kuendeleza leseni hiyo na mwisho tarehe 30/06/2012 ambapo matumizi ya
leseni itakayo endelezwa kuanzia tarehe hiyo mwisho wake wa kutumika
utakuwa tarehe 29/06/2013.  
 
Pia iliamuliwa kuwa wasafirishaji wote wa leseni za Noah, watakao
endeleza leseni zao kila moja itaishia kwa utaratibu wake kwa kipindi
cha mwaka mmoja kwa leseni hizo kama kanuni inavyoelekeza. Mfano leseni
iliyotolewa tarehe 1/4/2012 itaishishia tarehe 30/03/2013, leseni
iliyotolewa tarehe 10/08/2011 itaishia tarehe 09/08/2012 na
haitaendelezwa tena. Utaratibu huo utafuatwa mpaka leseni ya mwisho
itakapoishia tarehe 29/06/2013. 
 
 Misingi ya Uamuzi wa SUMATRA imezingatia kifungu Namba 5 cha Sheria ya
SUMATRA, Sura ya 314, Mamlaka inalo jukumu la kisheria la kulinda
maslahi ya watumiaji pamoja na watoa huduma wa sekta inazozidhibiti. 
 
 Aidha, kifungu Namba 6 cha Sheria hii, kinaipa Mamlaka wajibu wa
kuhakikisha kwamba  huduma zinazotolewa na sekta inazozidhibiti,
zinatolewa katika ubora (quality) unaokubalika, gharama zinazostahili
(cost effective) na zinakidhi viwango (Standards) vilivyowekwa na
Mamlaka husika.
 
 Kwa kuzingatia jukumu na kazi  za Mmalaka katika udhibiti wa usafiri wa
nchi kavu, Mamlaka ilifikia uamuzi wa kusitisha leseni za Noah kwa
kuzingatia hasa mambo makuu yafuatayo: 
 
 
(a).              Sababu za Kiuchumi
Uwezo mdogo wa mabasi yaliyotajwa hapo juu katika kubeba abiria na hivyo
kuifanya biashara ya usafirishaji kwa kutumia mabasi hayo kutokuwa na
tija. Noah inabeba abiria saba tu wa kulipa kwa nauli ya Sh 300/= kwa
abiria kwa umbali wa chini ya kilomita 10 haiwezi kukidhi gharama za
uendeshaji.
 (b).             Sababu za Kiusalama
 
Magari ya Noah hayakidhi viwango vya usalama kwa magari ya umma
(commuter buses). Aidha, magari hayo hayakidhi matakwa ya kifungu namba
4.4.3 cha Kiwango Na. 598:1999 cha Shirika la Viwango Tanzania (TBS) kwa
magari ya abiria. Magari hayo yameundwa kwa shughuli za kifamilia na
burudani.
(c)        Umuhimu wa kusimamisha magari ya Noah kwa awamu (Gradual
phasing out)
 
            Utaratibu wa kusimamisha leseni kwa gari mojamoja kadiri
muda wa leseni husika unapoisha linaondoa uwezekano wa kutokea
msongamano wa wamiliki wa magari ya Noah siku ya mwisho wa huduma endapo
wote wataruhusiwa kuendesha biashara zao mpaka tarehe ya mwisho.
Msongamano wa wamiliki wengi ambao wote leseni zao zinaisha muda wake
kwa siku moja utachochea mgogoro mkubwa utakaoathiri utulivu kwenye
shughuli za usafirishaji nchini.
(d)       Wakati SUMATRA inaendelea kuondoa mabasi madogo yaani vipanya
(mini buses) na kuhamasisha matumizi ya mabasi makubwa yenye faida
kiuchumi (economies of scale) kwa mtoa huduma na mtumia huduma, matumizi
ya magari madogo zaidi ya vipanya (micro bus) ni jambo lisilokubalika.
Kwa maelezo hayo, Mamlaka ya SUMATRA inapenda kuuhakikishia Umma kwamba
nia ya Mamlaka katika kutekeleza hatua hii ni kuepusha madhara
yanayolikumba na yanayoweza kulikumba Taifa kutokana na utumiaji wa aina
hii ya usafiri ambayo si salama kwa maisha ya abiria lakini vile vile
hauleti tija katika kuboresha sekta hii ya usafirishaji wa umma kwa njia
ya barabara. 
 
 
David Mziray
Public Affairs Manager
SUMATRA
P.O.Box 3093
Dar es Salaam
Tel: +255 22 2197521
Mob: 0767 250 550
Website: www.sumatra.or.tz <http://www.sumatra.or.tz> 
Email: davymzy@yahoo.com <mailto:davymzy@yahoo.com> 

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7051,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MAGARI AINA YA NOAH HAYASTAHILI KUTOA HUDUMA YA USAFIRI WA UMMA
MAGARI AINA YA NOAH HAYASTAHILI KUTOA HUDUMA YA USAFIRI WA UMMA
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2012/09/magari-aina-ya-noah-hayastahili-kutoa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2012/09/magari-aina-ya-noah-hayastahili-kutoa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy