TAARIFA
KWA UMMA KUHUSU
TAHADHARI
YA KUWEPO KWA UGONJWA MPYA WA MAHINDI
Tumepokea
taarifa kutoka kwa ubalozi wa Tanzania nchini Kenya na Shirika la Kilimo na
Chakula (Food and Agriculture Organization) juu ya kuwepo ugonjwa mpya
wa mahindi unaojulikana kwa jina la “Maize Lethal Necrotic Disease (MLND)”.
Ugonjwa huo unasababishwa na virusi vinavyojulikana kitaalamu “Maize
Chlorotic Mottle Virus (MCMV)” na “Sugarcane Mosaic Virus (SCMV)”.
Katika
nchi jirani ya Kenya, ugonjwa huo ulianzia katika eneo la Bomet lililopo katika
Bonde la Ufa ambapo ulisababisha asilimia 100 ya uharibifu kwa zao la mahindi
lililokuwepo shambani. Kulingana na taarifa hiyo, hadi sasa ugonjwa umesambaa
katika eneo kubwa ndani ya bonde la ufa na umeenea katika wilaya 22
ambapo jumla ya hekta 16,000 za zao la mahindi zimeathirika. Hasara kutokana na
ugonjwa huo inakadiriwa kuwa kati ya asilimia 60 hadi 90.
Ili
kukabiliana na hatari ya uwezekano wa ugonjwa huo kuingia nchini Tanzania,
Wizara inawaarifu wadau wote wa kilimo nchini kuzingatia yafuatayo:
(i)
Kwa kuwa inasemekana kuwa ugonjwa huo unaenezwa na mbegu na kwa kuwa
Tanzania inaagiza kiasi kikubwa cha mbegu kutoka nje ya nchi, vibali vyote
vinavyotolewa kuingiza mbegu hizo lazima ziwe hazina vimelea vya “Maize Lethal
Necrotic Disease baada ya kufanyika kwa uchunguzi wa maabara.
(ii)
Vilevile mbegu hizo kabla hazijaingizwa nchini sampuli ichukuliwe na
kupelekwa kituo cha karantini cha Tropical Pesticide Research Institute
(TPRI) kilichopo Arusha kwa ajiri ya kuhakiki. Kwa kufanya hivyo,
tutaweza kuthibiti ugonjwa huo kuingia nchini.
(iii)
Halmashauri za Wilaya kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo Chakula na
Ushirika zitatoa elimu ya jinsi ya kutambua ugonjwa huo na mbinu za kukabiliana
nao.
(iv)
Wakuu wote wa Mikoa, Wadau wote wa mbegu, Wakulima na wananchi kwa
ujumla katika mikoa inayolima mahindi kwa kutegemea umwagiliaji au kilimo cha
msimu cha kutegema mvua wanapaswa kutoa taarifa mapema endapo dalili zisizo za
kawaida zitaonekana katika mashamba ya mahindi.
(v)
Wakulima wote wanashauriwa kununua mbegu zilizothibitishwa ubora na
Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu (Tanzania Official Seed Certification
Institute - TOSCI). Sambamba na agizo hili, wauzaji na wasambazaji wa mbegu
nchini wanaagizwa kuzingatia Sheria ya Mbegu ya Mwaka 2003, kinyume chake watachukuliwa
hatua kali za kisheria.
(vi)

Wananchi wote waliopo mipaka wanashauriwa kutokuhamisha au kubeba mahindi kiholela kutoka nchi jirani bila kufuata taratibu za kisheria.

Wananchi wote waliopo mipaka wanashauriwa kutokuhamisha au kubeba mahindi kiholela kutoka nchi jirani bila kufuata taratibu za kisheria.
WIZARA
YA KILIMO CHAKULA NA USHIRIKA








0 comments:
Post a Comment