UNAPENDWA NA KUOGOPWA NA WATU WENGI DUNIANI ■ UKO HATARINI KUPOTEZA ASILI YAKE KABISA Na Onesmo Ngowi Masumbiwi au kwa maj...
UNAPENDWA NA
KUOGOPWA NA WATU WENGI DUNIANI
■UKO HATARINI KUPOTEZA ASILI YAKE KABISA
Na Onesmo Ngowi
Masumbiwi au kwa majina mwengine ndondi au ngumi na
kwa majina ya mitaani ndogwa, mawe n.k. ni mchezo unapoendwa sana na watu
wengi. Aidha mchezo huu ni kati ya michezo inayoogopwa sana duniani. Mchezo wa
ngumi uko hatarini kupoteza maana yake ya asili yaani kucheza kama burudani,
kuwakilisha nchi na kujenga ushupavu wa mchezaji. Mamilioni ya watu wanaojazana
kuutazama wasingependa kabisa kujiingiza kuucheza mchezo wa ngumi. Sasa
endelea………………………………….!
Mabondia wengi na
walio mabingwa wa dunia huajiri "cutman" kwa kipindi chote cha maisha
yao ya ngumi. Kutokana na umuhimu wa kumhudumia bondia wake vizuri ma-cutman
wengi wanalipwa fedha zaidi ya madaktari katika mpambano.
Katika mpambano wa
ngumi kuna washika vibao (Card Girls) vinaoonyesha raundi inayofuata. Mara
nyingi watu hawa huwa ni wasichana wanamitindo au waliobobea kwenye majukwaa
kama wanamuziki, wanamitindo, wacheza shoo n.k. Kila raundi inapoisha mshika
kibao huingia kwenye ulingo akitembea kwa maringo na kuonyesha raundi
inayofuata.
Mara nyingi mwendo
wake husaidiwa na musiki mororo unaopigwa na watazamaji hufuatilia kwa makelele
ya furaha. Wapo vile vile washika vibao ambao ni wanaume wanaofanya mazoezi ya
kutunisha musuli na haswa mpambano wenyewe unapokuwa ni wa wanawake.
Vile vile kuna
mtangazaji (Commentator) ambaye anatakiwa kutangaza mpambano wenyewe.
Mtangazaji wa mpambano hutangaza mpambano wenyewe kwa ujumla akianzia na aina
ya mpambano, wageni waliohudhuria na mabondia wahusika.
Pengine ni wakati
anapotangaza mabondia husika ndipo anapotakiwa kutumia madoido ya hali ya juu
kumnadi kila bondia. Kazi yake nyingine ni kutangaza matokeo ya kila mpambano
haswa inapozingatiwa kuwa mchezo wa ngumi unajumuisha mapambano mengi madogo
madogo (supporting bouts) kabla ya mpambano mkubwa.
Waliotajwa hapo juu
ndio wahusika muhimu mbali na promota na meneja kuendesha pambano la ngumi.
MIFUMO
YA NGUMI NA MADHARA YAKE KWENYE MAENDELEO YAKE
Mifumo ya ngumi
imekuwa inabadilika na wakati, tangu ngumi zilipoanza. Lakini nitaanzia na hapa
kwetu Tanzania. Ipo mifano mingi inayoonyesha namna mabondia wetu wa kitanzania
walivyo na uwezo mdogo wa maswala ya ngumi. Mfano mmoja ni jinsi Kamisheni ya
Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) ilivyokwisha jitahidi kutafuta vyanzo
mbalimbali vya fedha ili kuwawezesha baadhi ya mabondia kushindania tuzo
mbalimbali za kimataifa.
Kana kwamba ni kazi
ta TPBC kuhakikisha kwamba bondia bingwa wa tuzo hizi kuzitetea, mabondia hawa
wanaishia kupoteza mataji yote waliyoyashinda kwa gharama kubwa na juhudi hizi
za TPBC bila kuyatetea.
Baadhi yao wakitumiwa na wababaishaji wachache wanaojiita mameneja feki
wanaodiriki hata kuushutumu uongozi wa TPBC kwamba uliuuza mikanda yao ya
ubingwa. Kuna usemi wa kiswahili unaosema kwamba “akutukanaye hakuchagulii
tusi”. Ni kioja cha hali ya juu tena dhihaka isiyo na upeo kwa mtu kusema
kwamba mkanda wake umeuzwa.
Mkanda wa bondia ni
mali yake na haiwezekani tu mtu akajitokeza barabarani amevaa mkanda wa ubingwa
asiokuwanao. Kufanya hivi ni sawa na mtu kuvaa nguo za askari wa zima moto na
kwenda nazo disko.
Dhihaka kama hizi na nyingine nyingi zilnaufanya uongozi wa TPBC uachane na
kujishughulisha na maswala ya kupromoti na kumeneji. Kwa kuwa juhudi zake za
kuwasaidia mabondia pale ambapo mapromota na mameneja hawakuwepo zinachukuliwa
kama njia mbadala ya kujinufaisha kifedha, iliamua kukoma.
Mikanda ambayo TPBC
iliigharamia ili kuhakikishia mabondia wa kitanzania wanayashinda ni pamoja na
IBF/Afrika, CBC, ECAPBF na WBU.
Ni vizuri nieleze tu kwamba bondia anayeshinda mkanda wa ubingwa anatakiwa awe
ameutetea katika kipindi kati ya miezi minne na mwaka mmoja (Division ndogo
kuanzia Light Fly mpaka Super Light Weight wanatakiwa wawe wametetea katika
kipindi cha miezi sita, Kunzia Welterweight mpaka Heavyweight anatakiwa awe
ametetea katika kipindi cha mwaka mmoja husuan ubingwa wa dunia). Mashirikisho
mengi madogo mbali na IBF, WBA, WBO na WBC hayana sheria ngumu zinazomtaka
bondia atetee ubingwa wake katika kipindi hiki kilichotajwa hapo juu.
Hivyo huwapa muda
kati ya miezi sita mpaka mwaka mmoja an wakati mwingine bondi anakaa tu na
mkanda mpaka atakapojitokeza bondia mwingne anayeutaka.
Lakini mashirikisho
kama IBF, WBC, WBO na WBA ni lazima bondia bingwa acheze na bondia
anayemfuata kwenye viwango katika kipindi kilichotajwa cha miezi sita kwa
ubingwa wa bara (Continental) mpaka mabara (Intercontinental).
Sheria za mashirikisho haya zimeufanya mchezo wa ngumi kuwa na upinzani wa hali
ya juu. Bingwa anapotakiwa kutetea ubingwa na bondia anayemfuata kwenye viwango
na kwa muda uliotakiwa kunaufanya mchezo wa ngumi kuwa na upinzani wa hali ya
juu.
Bondia anaposhindwa
kutetea ubingwa wake katika kipindi hiki hunyanganywa ubingwa na kutangazwa
kuwa ubingwa wenyewe uko wazi. Ubingwa uliotangazwa kuwa wazi unawafanya
mabondia walio namba moja hadi nne kucheza mapambano ya mtoano (Elimination
Titles) ili kuwapata mabondia wawili watakaoshindania ubingwa.
Kwa ajili ya
upinzani na malipo mazuri mapambano yote ya mashirikisho haya hutangazwa kwa
njia ya tenda (bidding). Mapromota wanatakiwa watume ofa ya fedha watakazolipa
mabondia na atakayetoa donge nono ndiye anayeshinda katika tenda ya kupromoti
pambano husika.
Kwa wenzetu inakuwa
rahisi kwani mifumo yao wa kupromoti ngumi inamruhusu promota kuweza
kukubaliana na makampuni mbalimbali ya mitandao ya televisheni itakayomlipa
fedha za kupromoti. Anapopiga mahesabu yake na kuona kuwa anazo fedha za
kutosha na faida ndipo anapotuma tenda yake. Iaendelea………………………….!
Mwandishi wa makala haya ni; Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa
Tanzania (TPBC), Shirkisho la Ngumi za Kulipwa Afrika Mashariki na Kati
(ECAPBF), Shirikisho la Ngumi la Kimataifa bara la Afrika, Masharilki ya Kati,
Ghuba ya Uarabu na Uajemi (IBF/AFRICA) na Mkurugenzi wa Baraza la Ngumi la
Jumuiya ya Madola (CBC) E-mail: ibfafrica@yahoo.com
COMMENTS