BARAZA LA VIJANA LA CHADEMA (BAVICHA) IRINGA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Mkoa wa Iringa limesikitis...
BARAZA LA VIJANA LA CHADEMA (BAVICHA) IRINGA
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Mkoa wa Iringa limesikitishwa na kitendo
cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda kujivika jukumu la
kupachika raia vyeo ambavyo haviko kwenye utaratibu wa CHADEMA wala BAVICHA
ilili kutimiza lengo la kujaribu kukipaka matope CHADEMA na BAVICHA.
Tunapenda kuufahamisha umma kuwa taarifa zilizotolewa na Bwana Kamuhanda, RPC wa
Iringa na na kunukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa Bwana Athanas Mongo
(mtuhumiwa wa ujambazi) ni Kamanda wa Vijana wa CHADEMA Mkoa wa Iringa ni uongo
na uzushi wenye hila za makusudi za kujaribu kuharibu taswira ya BAVICHA na
CHADEMA kwa umma.
Bwana Mongo anayetuhumiwa kwa ujambazi si Kamanda wa BAVICHA Mkoa wa Iringa na
wala Muongozo wa Mabaraza ya chama unaosimamia mabaraza yote likiwemo BAVICHA
kwa upande mmoja na Katiba ya CHADEMA kwa upande mwingine haina na wala
haitambui cheo ambacho RPC Kamuhanda kamvisha bwana Mongo.
Tunavyojua sisi hicho ni cheo kinachotumika na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Sasa
labda RPC Kamuhanda ni mzoefu wa kukariri vyeo vya CCM. Yeye anajua hilo.
Mongo ni mwanachama wa kawaida wa CHADEMA na BAVICHA na asiyekuwa na cheo
chochote ndani ya BAVICHA wala CHADEMA. Ni Mtanzaniamwenye haki ya kuwa
mwanachama wa chama chochote cha siasa. Kutuhumiwa kwake kwa masuala ya uhalifu
hakupaswi wala hakuwezi kuhusiswa na CHADEMA wala BAVICHA.
BAVICHA tunamuonya RPC Kamuhanda kuacha mara moja tabia ya kukurupuka na
kutokuwa makini katika utendaji kazi kiasi cha kuingilia na kujaribu kubaka
Katiba ya CHADEMA na Kanuni za BAVICHA ili tu kukidhi haja yake ya kuipaka
matope CHADEMA baada ya kushindwa hila hizo kwenye tukio la mauaji ya Mwandishi
wa habari, marehemu Daudi Mwangosi kule Nyololo.
Bila shaka ni ukurupukaji na kukosa umakini kama huu, ndiyo uliosabisha RPC
Kamuhanda akakiuka misingi ya utawala bora kama ilivyoelezwa na Ripoti ya
Uchunguzi ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala juu ya mauaji ya Mwangosi.
Uchunguzi huo wa THUB ambacho ni chombo cha serikali chenye majukumu ya kikatiba
na kisheria kuhusu masuala ya haki za binadamu ulibaini kuwa RPC Kamuhanda mnamo
tarehe 02/09/2012 alikiuka Sheria ya vyama vya siasa (Cap 258 RE. 2002) kifungu
cha 11(a) na (b) na sheria ya Polisi (Sura ya 322) kwa kuingilia kazi za OCD wa
Mufindi na kutoa amri ya kuzuia shughuli za CHADEMA wakati yeye hakuwa “Officer
In-charge” wa polisi wa eneo husika. Kwa maana hiyo amri aliyoitoa haikuwa
halali kwa kuwa ilitolewa na mtu ambaye hakuwa na mamlaka kisheria kutoa amri
hiyo. Haya ni matumizi mabaya ya mamlaka, hivyo ni ukiukwaji wa misingi ya
utawala bora.
Kimsingi baada ya taarifa hiyo ya uchunguzi uliofanywa na chombo cha serikali,
unaoonesha kuwa utendaji mbovu wa Kamuhanda, RPC huyo pamoja na polisi wenzake
walioshiriki katika tukio la Nyololo kumuua mwandishi wa habari, kisha wakaanza
kufanya propaganda za kuipaka matope CHADEMA ili kuwanusuru wao, alipaswa kuwa
amejizulu au amefukuzwa kazi na kushtakiwa mahakamani kutokana na tukio hilo la
mauaji ya Mwangosi, kama ambavyo CHADEMA imeshauri mara kadhaa, ikiwemo kuandika
barua kwa Rais Jakaya Kikwete.
Imetolewa na leo tarehe 10/04/2013 Mkoani Iringa na:
Joseph Nzala Lyata
Mwenyekiti BAVICHA
Mkoa wa Iringa
0757925514
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Baraza la Vijana wa CHADEMA (BAVICHA) Mkoa wa Iringa limesikitishwa na kitendo
cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa Michael Kamuhanda kujivika jukumu la
kupachika raia vyeo ambavyo haviko kwenye utaratibu wa CHADEMA wala BAVICHA
ilili kutimiza lengo la kujaribu kukipaka matope CHADEMA na BAVICHA.
Tunapenda kuufahamisha umma kuwa taarifa zilizotolewa na Bwana Kamuhanda, RPC wa
Iringa na na kunukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa Bwana Athanas Mongo
(mtuhumiwa wa ujambazi) ni Kamanda wa Vijana wa CHADEMA Mkoa wa Iringa ni uongo
na uzushi wenye hila za makusudi za kujaribu kuharibu taswira ya BAVICHA na
CHADEMA kwa umma.
Bwana Mongo anayetuhumiwa kwa ujambazi si Kamanda wa BAVICHA Mkoa wa Iringa na
wala Muongozo wa Mabaraza ya chama unaosimamia mabaraza yote likiwemo BAVICHA
kwa upande mmoja na Katiba ya CHADEMA kwa upande mwingine haina na wala
haitambui cheo ambacho RPC Kamuhanda kamvisha bwana Mongo.
Tunavyojua sisi hicho ni cheo kinachotumika na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Sasa
labda RPC Kamuhanda ni mzoefu wa kukariri vyeo vya CCM. Yeye anajua hilo.
Mongo ni mwanachama wa kawaida wa CHADEMA na BAVICHA na asiyekuwa na cheo
chochote ndani ya BAVICHA wala CHADEMA. Ni Mtanzaniamwenye haki ya kuwa
mwanachama wa chama chochote cha siasa. Kutuhumiwa kwake kwa masuala ya uhalifu
hakupaswi wala hakuwezi kuhusiswa na CHADEMA wala BAVICHA.
BAVICHA tunamuonya RPC Kamuhanda kuacha mara moja tabia ya kukurupuka na
kutokuwa makini katika utendaji kazi kiasi cha kuingilia na kujaribu kubaka
Katiba ya CHADEMA na Kanuni za BAVICHA ili tu kukidhi haja yake ya kuipaka
matope CHADEMA baada ya kushindwa hila hizo kwenye tukio la mauaji ya Mwandishi
wa habari, marehemu Daudi Mwangosi kule Nyololo.
Bila shaka ni ukurupukaji na kukosa umakini kama huu, ndiyo uliosabisha RPC
Kamuhanda akakiuka misingi ya utawala bora kama ilivyoelezwa na Ripoti ya
Uchunguzi ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala juu ya mauaji ya Mwangosi.
Uchunguzi huo wa THUB ambacho ni chombo cha serikali chenye majukumu ya kikatiba
na kisheria kuhusu masuala ya haki za binadamu ulibaini kuwa RPC Kamuhanda mnamo
tarehe 02/09/2012 alikiuka Sheria ya vyama vya siasa (Cap 258 RE. 2002) kifungu
cha 11(a) na (b) na sheria ya Polisi (Sura ya 322) kwa kuingilia kazi za OCD wa
Mufindi na kutoa amri ya kuzuia shughuli za CHADEMA wakati yeye hakuwa “Officer
In-charge” wa polisi wa eneo husika. Kwa maana hiyo amri aliyoitoa haikuwa
halali kwa kuwa ilitolewa na mtu ambaye hakuwa na mamlaka kisheria kutoa amri
hiyo. Haya ni matumizi mabaya ya mamlaka, hivyo ni ukiukwaji wa misingi ya
utawala bora.
Kimsingi baada ya taarifa hiyo ya uchunguzi uliofanywa na chombo cha serikali,
unaoonesha kuwa utendaji mbovu wa Kamuhanda, RPC huyo pamoja na polisi wenzake
walioshiriki katika tukio la Nyololo kumuua mwandishi wa habari, kisha wakaanza
kufanya propaganda za kuipaka matope CHADEMA ili kuwanusuru wao, alipaswa kuwa
amejizulu au amefukuzwa kazi na kushtakiwa mahakamani kutokana na tukio hilo la
mauaji ya Mwangosi, kama ambavyo CHADEMA imeshauri mara kadhaa, ikiwemo kuandika
barua kwa Rais Jakaya Kikwete.
Imetolewa na leo tarehe 10/04/2013 Mkoani Iringa na:
Joseph Nzala Lyata
Mwenyekiti BAVICHA
Mkoa wa Iringa
0757925514
COMMENTS