Bia ya Safari Lager, inayotengenezwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) imeibuka kinara kwa kuwa mshindi wa kwanza katika mash...
Bia
ya Safari Lager, inayotengenezwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL)
imeibuka kinara kwa kuwa mshindi wa kwanza katika mashindano ya Ubora wa bia
barani Afrika.
com
Editha Mushi, Communications & Media Manager, +255767266420, editha.mushi@tz.sabmiller.com
Ushindi
huu unafuatia zoezi lililoendeshwa na Taasisi ya Utengenezaji wa Bia na Vileo
“Institute of Brewing and Distilling (IBD), ambapo mashindano hayo ya kuangalia
na kupima ubora wa bia yalifanyika, yakihusisha zaidi ya Bia 50 kutoka
makampuni maarufu yanayotengeneza bia Barani Afrika.
IBD
ilikusanya wataalamu huru kutoka katika mabara matatu tofauti ili kuonja bia na
kutoa maamuzi yasiyo na upendeleo wowote.
Wataalamu
hawa kwa pamoja wana uzoefu wa jumla ya zaidi ya miaka 500 katika kazi hii.
Katika mashindano haya bia hizi zilipimwa katika makundi tofauti kama vile, bia
zinazotengenezwa kwa kutumia malighafi zinazopatikana sehemu inapotengenezwa
bia yenyewe, bia zenye kiwango cha kilevi cha chini ya asilimia 5, na pia kundi
la bia zenye kiwango cha kilevi cha zaidi ya silimia 5.
Tuzo
ya juu kabisa ya tuzo za bia za Afrika ni tuzo ya ubingwa wa jumla wa bia zote
zilizoshiriki, ambayo imenyakuliwa na bia yetu ya Safari Lager, na mnamo Tarehe
07 Mwezi Machi 2013 Jijini Accra, Ghana Taasisi hiyo ikaitangaza Bia ya Safari
Lager kuwa ndio Bia Bora Kuliko Bia zote za Afrika.
Akizungumza na waandishi
wa habari jijini Dar es salaam, Meneja wa Bia ya Safari Lager Bw. Oscar
Shelukindo alisema; Huu ni ushindi mkubwa sana na wa kujivunia sio tu kwa Bia
hii ya Safari Lager, au Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) bali kwa Taifa zima la
Tanzania, kwani umeleta heshima kwa Bara zima la Afrika na Ulimwengu kwa ujumla
kuwa Watanzania wanaweza kutengeneza bidhaa bora na zenye kukidhi viwango vya
Kimataifa.
Bia hii ya Safari Lager
imeweza kuzidondosha bia zote za Afrika na kukamata namba moja katika Ubora,
hii inathibitishwa na ukweli kuwa hata hapa nyumbani, Bia hii ya Safari Lager
ndio inayoongoza kwa mauzo kuliko bia nyingine yoyote tangu ilipozinduliwa
mwaka 1977. Alisema Oscar.
Akizungumzia mikakati
iliyowekwa na Bia ya Safari Lager, katika kuhakikisha kuwa Ubingwa huu
unafahamika kwa Watanzania Bw. Shelukindo alisema; Tumejipanga kufikisha habari
hizi njema kwa Watanzania wote, na leo tumeanza na hatua hii moja muhimu ya
kuongea na vyombo vya Habari, ambavyo bila shaka vinawafikia watanzania wote
hata walio nje ya mipaka ya nchi yetu. Hatua hii itafuatiwa na safari ya
kupeleka kikombe hiki cha ushindi Bungeni siku ya Alhamisi wiki hii. Kama
tunavyofahamu, wabunge ni wawakilishi wa wananchi wote hivyo itakuwa fursa
nzuri kufikisha kombe hili ambapo Bunge litatoa baraka zake nasi tutaanza
kulizungusha kombe katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu. Ujumbe mkuu katika
ziara hii utakuwa ni kuutangaza ushindi huu mkubwa wa Bia hii ya Kitanzania,
inayotengenezwa na Watanzania. Lakini pia tutahamasisha Watanzania kuwa na
uzalendo, kuziamini na kutumia bidhaa zinazozalishwa hapa nchini. Tunaamini
kuwa ziara hii itaongeza hamasa kwa watanzania kupenda bidhaa za nyumbani na
hatimaye kusaidia kukuza uchumi wetu.
Bia ya Safari Lager pia
imeshinda jumla ya Tuzo sita za Dhahabu katika mashindano maarufu Duniani
yajulikanayo kama “Monde Selection”
-MWISHO-
Kwa Maelezo zaidi wasiliana na:
Oscar Shelukindo, Brand Manager, +255767266833, victoria.kimaro@tz.sabmiller.Editha Mushi, Communications & Media Manager, +255767266420, editha.mushi@tz.sabmiller.com
Dorris Malulu, Public Affairs Administrator, +255767266049, doris.malulu@tz.sabmiller.com
Kuhusu TBL
Tanzania Breweries Limited (TBL) inatengeneza,
kuuza na kusambaza bia, vinywaji vyenye ladha ya matunda vilivyo na kilevi na
vinywaji visivyo na kilevi hapa Tanzania. TBL pia ndiyo kampuni mama ya
Tanzania Distilleries Limited pamoja na kampuni shiriki ya Mountainside Farms
Limited.
Bia zinazotengenezwa na kampuni ya TBL ni pamoja na
Safari Lager, Kilimanjaro Premium Lager, Ndovu Special Malt, Castle Lager,
Vinywaji vingine vinavyotengenezwa na kundi la makampuni ya TBL ni Konyagi Gin,
Amarula Cream, Redd’s Original na Grand Malt.
Kundi la makampuni ya TBL limeorodheshwa kwenye
Soko la Hisa la Dar es Salaam, limeajiri watu wapatao 1,300 na linawakilishwa
nchi nzima na viwanda vinne vya bia, kiwanda kimoja cha kutoneshea, kimoja cha
kutengenezea kimea pamoja na bohari nane za kusambazia bia.
Kuhusu SABMiller
SABMiller plc moja kati ya makampuni makubwa ya bia
duniani ikiwa na mikataba ya kutengeneza na kusambaza bia kwenye nchi zaidi ya
60 katika mabara matano. Bia zake ni pamoja na zile za kimataifa kama Miller
Genuine Draft, Peroni Nastro Azzurro na Pilsner Urquell vilevile na bia
nyingine zinazoongoza kwenye masoko ya ndani ya nchi mbalimbali. Nje ya
Marekani, SABMiller ni moja ya kati ya makampuni makubwa yanayotengeneza
vinywaji vya Coca-Cola duniani. Hivi karibuni SABMiller plc ilinunua kampuni ya
bia ya Foster’s pamoja na shughuli zake za uzalishaji nchini India.
SABMiller imeorodheshwa kwenye masoko ya hisa ya
London na Johannesburg.
COMMENTS