TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Shilingi bilioni 620 za Deni la Taifa hazina maelezo Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serika...
TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
Shilingi bilioni 620 za
Deni la Taifa hazina maelezo
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali ametoa taarifa yake ya mwaka 2011/2012 na kuonyesha kuwa
kuna skandali kubwa sana katika akaunti ya Deni la Taifa.
Nanukuu ‘Uhakiki wa mchanganuo wa madeni ya Taifa kama
ulivyokuwa tarehe 30 Juni, 2012 ulibaini kuwepo kwa marekebisho ya deni ya
shilingi
619,803,554,183.91 ambayo
uongozi haukuweza kutoa maelezo ya kuridhisha.’
(Taarifa ya CAG, Ripoti
ya Serikali Kuu 2011/2012 uk 158). Mwisho wa Kunukuu
Katika Taarifa yake hiyo
CAG anaendelea kuonyesha kuwa Deni la Taifa linazidi kukua na mwaka unaoishia
mwezi Juni 2012 deni lilikuwa kwa asilimia 17 kutoka mwaka unaoishia mwezi Juni
2011.
Kukosekana kwa maelezo ya
kuridhisha kuhusu zaidi ya nusu trilioni za Deni la Taifa ni jambo linalopaswa
kutiliwa mashaka makubwa, kuchunguzwa na kupata majawabu stahiki. Tafiti
mbalimbali duniani zinaonyesha kuwa kuna mahusiano makubwa sana kati ya Deni la
Taifa la utoroshaji wa fedha kwenda kwenye mabenki ya ‘offshore’.
Katika kitabu cha ‘Africa’s
Odious Debts: How Foreign Loans and Capital flight bled a continent’
kilichoandikwa mabwana
Leonce Ndikumana na James Boyce imeonekana kwamba Deni
la Taifa huchochea
utoroshwaji wa Fedha kwenda kuficha nje ya Tanzania.
Mabilioni haya kwenye
akaunti ya Deni la Taifa yanashtusha sana. Kambi ya Upinzani Bungeni kwa miaka
miwili mfululizo imekuwa ikitaka ukaguzi maalumu kwenye akaunti za Deni la
Taifa lakini Serikali imeshindwa kufanya hivyo. Nikiwa Mwenyekiti wa Kamati ya
PAC pia nimemtaka CAG
afanye ukaguzi huu
maalumu. Kambi ya upinzani Bungeni ilisema hivi katika
Bajeti yake kivuli
2012/13:
DENI LA TAIFA
Mheshimiwa Spika, Kambi
ya Upinzani inasikitika kwa serikali kuendelea kutengeneza
madeni kwa Taifa kwa
kuendelea kukopa zaidi kwa matumizi ya kawaida ya
serikali. Wakati Serikali
inasisitiza kwamba Deni letu linastahmilika, Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa
Serikali anaonyesha mashaka makubwa sana kutokana na kasi ya
kukua kwa Deni la Taifa. Taarifa
ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali inaonyesha
kuwa Deni la Taifa linazidi kuongezeka kwa asilimia 38% kutoka shilingi
trillion 10.5 mwaka 2009/2010 hadi shilingi trillion 14.4 mwaka 2010/2011. Kwa
mujibu wa Waziri wa
Fedha Deni la Taifa
limefikia shilingi trillion 20.3 mpaka ilipofika mwezi
Machi mwaka 2012. Ukisoma
taarifa ya Mwezi wa Mei 2012 ya Benki Kuu ya
Tanzania, Deni la Taifa
sasa limefikia shilingi trillion 22.
Mheshimiwa Spika, Suala
hapa sio ustahmilivu wa Deni kama inavyodai Serikali bali ni kwamba tunakopa
kufanyia nini? Bajeti ya Mwaka 2012/13 inayopendekezwa inaonyesha kwamba
Serikali itakusanya shilingi trilioni 8.7 kama makusanyo ya ndani na itatumia
shilingi trilioni 10.6 kama
matumizi ya kawaida. Ni
dhahiri kwamba sehemu ya mikopo ambayo serikali
inachukua sasa itakwenda
kwenye matumizi ya kawaida. Hatutaki mikopo kwa ajili
ya matumizi ya kawaida ya
posho, kusafiri, magari nk. Tuchukue mikopo kuwekeza
kwenye miradi itakayokuza
uchumi na kuzalisha kodi zaidi. Bajeti inaonyesha kwamba
Serikali itakopa shilingi
takribani trillion 5 mwaka 2012/13. Serikali
ikubalikutekeleza
mapendekezoya
Kambi ya Upinzani ya
kuimarisha ukusanyaji wa kodi na kupanua wigo wa kodi katika
maeneo muhimu kama sekta
ya
madini na mawasiliano,
kuzuia misamaha ya kodi, kutokomeza ukwepaji kodi, na
kuepuka matumizi mabaya
ili kuepuka madeni yasiyo ya lazima.
Mheshimiwa Spika, Kambi
ya Upinzani inapenda
kusisitiza kwamba Bunge
lifanye ukaguzi maalumu kuhusu akaunti ya Deni la Taifa
ili kuweza kubaini ukweli
kuhusu ustahmilivu wa Deni na mikopo ambayo Serikali
inachukua kama inakwenda
kwenye Maendeleo na miradi ipi na kama miradi hiyo ina
tija. Vilevile
tumependekeza kwamba Mikopo yote ambayo Serikali inachukua iwe
inapata idhini ya Kamati
ya Bunge ya Fedha na Uchumi au Bunge litunge sharia
ili kiwango cha juu cha
kukopa ambacho Serikali haipaswi kuvuka. Kuiacha
Serikali inaendelea
kukopa bila mpango ni kuliweka Taifa rehani na kupeleka
mzigo wa kulipa madeni
haya kwa kizazi kijacho. Hatuwezi kukubali Wazee wetu waishi
maisha yao, waishi maisha
yetu na pia wakope maisha ya watoto wetu. Mwisho wa
kunukuu.
Kambi ya Upinzani
inarejea kutaka ukaguzi maalumu kuhusu akaunti za Deni la Taifa na maelezo ya
kina ya Serikali kuhusu shilingi 620 bilioni ambazo hazina maelezo kwenye Deni
la Taifa.
Hatuwezi kukaa kimya
kuona Watanzania wanabebeshwa madeni ambayo kimsingi ni
madeni bandia
yanayotajirisha watu wachache wenye uwezo na ujasiri mkubwa wa
kuiba, kupora nakufisidi
hazina ya Taifa letu.
Kabwe
Zuberi Zitto,Mb
Waziri Kivuli Fedha na
Uchumi
COMMENTS