MAELEZO YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI AKIJIBU HOJA ZA WABUNGE KUHUSU HOTUBA YA BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKU...
MAELEZO
YA MHESHIMIWA MIZENGO P. PINDA (MB), WAZIRI MKUU, WAKATI AKIJIBU HOJA ZA
WABUNGE KUHUSU HOTUBA YA BAJETI YA OFISI YA WAZIRI MKUU NA TAASISI ZAKE KWA
MWAKA WA FEDHA 2013/2014
UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika,
·
Niruhusu nianze kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa
kunipa Afya njema hadi leo ninapohitimisha Majadiliano ya Bajeti ya Ofisi ya
Waziri Mkuu; Ofisi ya Waziri Mkuu - Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa;
Taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na Ofisi ya Bunge kwa mwaka
2013/2014.
Mheshimiwa Spika,
·
Katika mjadala huu, jumla ya Waheshimiwa Wabunge 217 Walichangia. Waheshimiwa Wabunge 119
waliochangia kwa kuzungumza moja kwa moja hapa Bungeni na Waheshimiwa Wabunge 98 wamechangia kwa njia ya maandishi.
·
Kama ilivyo miaka yote Idadi ya Wachangiaji ni
kubwa. Hii inaonesha dhahiri jinsi ambavyo Waheshimiwa Wabunge mnavyoweka
umuhimu katika majukumu yanayotekelezwa na Ofisi ya Waziri Mkuu na Taasisi
zilizo chini yake.
·
Waheshimiwa Mawaziri na Naibu Mawaziri wamejitahidi
kujibu hoja mbalimbali lakini bado zimebaki nyingi. Kama ilivyo ada
tutajitahidi kujibu hoja zilizosalia kwa njia ya maandishi.
MAJIBU
YA HOJA
Mheshimiwa
Spika,
·
Kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge, Kanuni ya
99(9) inayohusu kujadili Bajeti ya Wizara, nichukue nafasi hii sasa kujibu na
kufafanua baadhi ya hoja zilizotolewa na Waheshimiwa Wabunge kama ifuatavyo.
VIPAUMBELE VYA SERIKALI
VYA MPANGO WA MAENDELEO WA MIAKA 15 NA MIAKA MITANO
Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani, Mheshimiwa Freeman A. Mbowe (Mb.)
anasema kuwa:
“Tatizo kubwa la
Serikali inayoongozwa na CCM ni kukosa Weledi wa kutekeleza kikamilifu
Vipaumbele vyake pamoja na kuviainisha kupitia Mpango wake wa Miaka Mitano,
Bajeti na Programu”
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
·
Serikali ilikwishaandaa Mpango Elekezi wa Maendeleo
wa Miaka 15 wa kutekeleza Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2025 ambao umegawanyika
katika vipindi vya miaka Mitano Mitano.
·
Mpango wa kwanza wa Maendeleo wa Miaka Mitano
kuanzia mwaka 2011/2012 hadi 2015/2016 uliokuwa na Vipaumbele vya kufungulia
fursa za ukuaji wa Uchumi wa Tanzania ulijadiliwa hapa Bungeni mwaka 2011/2012
na tukapata maoni ya Wabunge ambayo tuliyazingatia yakawa sehemu ya Mpango huo.
·
Ndani ya Mpango Elekezi wa Miaka 15, tulikubaliana
kuanza kutekeleza Mpango wa kwa wa Maendeleo wa Miaka Mitano (2011/2012 –
2015/2016) ambao ndio tunaoendelea nao hivi sasa.
·
Katika Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano na ule
wa Miaka 15, Vipaumbele vya Msingi vimefafanuliwa waziwazi na ambavyo ni
vifuatavyo:
i)
Miundombinu hasa uwekezaji mkubwa katika miundombinu ya Nishati, Usafirishaji, TEHAMA, Maji Safi na Majitaka na Umwagiliaji;
ii)
Kilimo
kwa shabaha ya kuleta Mapinduzi ya Kilimo kwa tafsiri pana inayojumuisha Kilimo Mazao, Mifugo, Uvuvi, Misitu na
Ufugaji Nyuki;
iii)
Maendeleo
ya Viwanda hasa vile vinavyotumia malighafi zinazopatikana
hapa Nchini, Viwanda vinavyoongeza thamani ya Mazao, Madini pamoja na kujenga
Viwanda vikubwa vya Mbolea, Saruji, Viwanda vya Kielektroniki na vinavyohusiana
na TEHAMA pamoja na vile vya maeneo maalum ya kiuchumi kwa ajili ya kutengeneza
bidhaa za Soko la Ndani, Kikanda na Kimataifa;
iv)
Maendeleo
ya Rasilimali Watu na ujuzi kwa kutilia mkazo maendeleo ya Sayansi,
Teknolojia na ubunifu pamoja na kuimarisha mafanikio yaliyopatikana katika
upatikanaji wa huduma za Jamii (Elimu,
Afya na Maji);
·
Maeneo haya ya Vipaumbele vya Kimkakati ndiyo
tuliyokubaliana ili kuleta matokeo ya haraka katika ukuaji wa uchumi na kwa
namna ambayo ni shirikishi ya kujumuisha Sekta Binafsi na Wadau wengine.
·
Katika Hotuba yangu, nimeeleza kuwa Vipaumbele vya
Mpango wa Maendeleo ya Miaka Mitano ndivyo vinavyotuongoza. Hata hivyo hii
haina maana kuwa maeneo mengine yanapuuzwa, bali hii ni katika kuhakikisha
tunafikia malengo tuliyojiwekea ya Kukuza Uchumi na Kuondoa Umaskini kwa
haraka.
·
Hivyo inashangaza, msemaji Mkuu wa Upinzani
Mheshimiwa Freeman Mbowe (Mb.) kwa niaba ya CHADEMA anadiriki kusema Serikali
haina Weledi. Hivi tusingekuwa na Weledi tungekuwa hapa.
·
Tumeshuhudia Mataifa Makubwa yanatupongeza kwa
jinsi tunavyosukuma maendeleo yetu. Inashangaza kwamba sisi wenyewe Watanzania
hususan Viongozi wa baadhi ya Vyama vya Siasa hatuoni hivyo.
·
Kwa kifupi nitoe mifano michache.
(a)
VIASHIRIA
VYA UCHUMI JUMLA
-
Uchumi umeendelea kukua kwa kasi ya kuridhisha
ambapo kwa mwaka 2012 ulikua kwa Asilimia 6.9;
-
Bajeti ya Serikali imeendelea kuongezeka kutoka
Shilingi Trilioni 4.2 mwaka
2005/2006 hadi Shilingi Trilioni 16.7
mwaka 2013/2014;
-
Makusanyo ya Kodi yameongezeka kutoka Wastani wa
Shilingi Bilioni 117 kwa mwezi mwaka
2005/2006 hadi Wastani wa Shilingi Bilioni 680
kwa mwezi mwaka 2012.
(b)
MIUNDOMBINU
(Barabara, Reli, Bandari, Viwanja vya Ndege na Mawasiliano)
BARABARA
Mheshimiwa
Spika,
·
Hadi
kufikia mwaka 2000, kulikuwa na barabara kuu za lami zenye urefu wa Kilometa 3,904
tu Nchini. Serikali ya Awamu ya Tatu, ilianzisha Miradi 14 ya ujenzi wa barabara zenye urefu wa jumla ya Kilometa 1,226.
Kati ya Miradi hiyo, Miradi saba (7) ya barabara zenye urefu wa Kilomita 403 ilikamilika katika kipindi cha Awamu ya Tatu kufikia mwezi
Desemba 2005. Hivyo, Serikali ya Awamu
ya Nne ilipoingia madarakani ilirithi Miradi saba (7) iliyokuwa bado kukamilika
yenye urefu wa jumla ya Kilometa 823 na
kuikamilisha.
·
Pia
Serikali ya Awamu ya Nne ilianzisha Miradi mipya 26 ya ujenzi wa Barabara zenye urefu wa Kilometa 1759.6. Kati ya Miradi hiyo, jumla ya
Kilometa 1270.8 sawa na Asilimia 72 zimekamilika kwa kiwango cha lami
kufikia mwezi Machi 2013. Kwa Miradi ya barabara zenye urefu Kilometa 488.8 zilizobaki, inaendelea
kutekelezwa katika hatua mbalimbali.
Hivyo, Serikali ya Awamu ya Nne (4) imejenga barabara kuu mpya zenye
urefu wa Kilometa 2093.8 katika
kipindi cha miaka saba iliyopita.
·
Sambamba
na ujenzi wa barabara mpya, Serikali pia imeendelea kufanya ukarabati mkubwa wa barabara kuu za
lami. Kati ya mwaka 2006
na 2013, Serikali ya Awamu ya Nne imetekeleza
Miradi 10 ya ukarabati mkubwa wa barabara kuu za lami zenye urefu wa jumla ya
Kilometa 841.2. Kati ya hizo jumla ya Kilometa 650, sawa na Asilimia 77 zimekamilika. Serikali inaendelea
kukamilisha Miradi ya barabara zenye urefu wa Kilometa 191.2 zilizobakia kabla ya mwisho wa mwaka huu.
·
Vilevile, pamoja na ujenzi unaoendelea katika
Miradi hiyo, kuna Miradi mingine 43
iliyobuniwa katika Awamu ya Nne yenye urefu wa jumla ya Kilometa 5,739 ambayo inaandaliwa kwa ajili ya
kuanza ujenzi. Kati ya Miradi hiyo, Miradi 16 yenye urefu wa jumla ya Kilometa 3,817, ipo katika hatua mbalimbali za
kukamilishwa Usanifu, na Miradi 27
yenye urefu wa jumla ya Kilometa 1,921
usanifu wake umekamilika na inatafutiwa Makandarasi. Lengo ni kuunganisha kwa
awamu Miji Mikuu ya Mikoa yote Nchini kwa barabara za lami ifikapo mwaka
2017/2018.
Mheshimiwa Spika,
·
Maendeleo
ya ujenzi wa barabara yamepunguza kwa kiasi kikubwa kero iliyokuwepo ya usafiri
wa Barabara Nchini. Sambamba na hatua hizo za ujenzi wa barabara mpya kwa
kiwango cha lami, Serikali ya Awamu ya Nne imeendelea kuzingatia umuhimu wa
kuimarisha mtandao wa barabara zote Nchini kwa kufanya matengenezo kwa viwango
vinavyotakiwa kwa kuongeza Bajeti ya Matengenezo ya Barabara kupitia Mfuko wa
Barabara.
·
Mfuko
huo uliimarishwa kwa kuuongezea fedha kwa asilimia 155 kutoka Shilingi Bilioni 85.74 mwaka 2006/07 hadi Shilingi
Bilioni 218.47 mwaka 2007/08 na
kiwango cha fedha cha Mfuko kimeendelea kuwa cha wastani huo kila mwaka hadi
sasa. Pamoja na mafanikio hayo, Serikali inakusudia kuongeza fedha za Mfuko wa
Barabara ili kufidia pengo lililopo hivi sasa la mahitaji ya Shilingi Bilioni 435 kwa mwaka kwa ajili ya Matengenezo
ya Mtandao wa Barabara Nchini, kutoka kwenye wastani Shilingi Bilioni 222 kwa mwaka zinazotolewa hivi sasa.
UJENZI WA MADARAJA
Mheshimiwa Spika,
·
Sambamba na ujenzi wa barabara za lami, Serikali
imetilia mkazo ujenzi wa madaraja ambayo kutokuwepo kwake, imekuwa kero ya muda
mrefu kwa Wananchi wa maeneo husika.
Kati ya mwaka 2006 na 2013 Serikali ya Awamu ya Nne imetekeleza miradi
mingi ya ujenzi wa madaraja makubwa na madogo.
Baadhi ya madaraja makubwa yaliyokamilika na yanayoendelea kujengwa ni
pamoja na: Daraja la Umoja na Madaraja ya Nangoo na Nanganga (Mtwara); Daraja
la Ruvu (Pwani); Daraja la Mwatisi (Morogoro); Daraja la Ruhekei (Ruvuma);
Daraja la Sibiti (Singida); Daraja la Mbutu (Tabora); Daraja la Malagarasi (Kigoma);
Daraja la Kigamboni (Dar es Salaam);
Daraja la Kilombero (Morogoro) na Daraja la Kimataifa la Rusumo (Kagera)
linalounganisha Tanzania na Rwanda.
UJENZI WA VIVUKO VIPYA
Mheshimiwa Spika,
·
Vivuko
vipya 10 vimejengwa na Serikali ya Awamu ya Nne kati ya mwaka 2006 na 2013
kwa ajili ya kuvusha Wananchi na mizigo yao kwenye Mito, Maziwa na Bahari.
Vivuko hivyo ni vifuatavyo: Mv. Kilombero (Morogoro); Mv. Ruhuhu (Ruvuma); Mv.
Misungwi (Mwanza); Mv. Magogoni (Dar es
Salaam); Mv. Kome (Mwanza); Mv. Pangani ( Tanga); Mv. Utete (Pwani); Mv.
Ruvuvu (Kagera), Mv. Ujenzi (Musoma) na Mv. Kalambo (Mtwara).
USAFIRI
WA RELI
Mheshimiwa
Spika,
·
Katika Dira ya Maendeleo ya Taifa kufikia mwaka
2025 na katika Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano 2010/2011 hadi 2014/2015,
suala la uwekezaji wa kutosha kwenye Miundombinu ya Reli Nchini limepewa
kipaumbele.
Kuimarisha
Reli ya Kati
Mheshimiwa
Spika,
·
Mnamo mwezi Machi 2010, Serikali iliamua kuchukua
Hisa Asilimia 51 zilizokuwa zinamilikiwa na Kampuni ya RITES katika TRL hivyo
kuiwezesha Serikali kuchukua jukumu la kuendesha Kampuni hiyo. Aidha, ili kuimarisha usafiri katika Mtandao
wa Reli unaohudumiwa na TRL, Serikali ilitenga jumla ya Shilingi Bilioni 101 katika mwaka 2011/2012 na imetenga
Shilingi Bilioni 135 katika mwaka
2012/2013 kwa ajili ya kununua injini za treni na mabehewa (Rolling Stock).
·
Katika kuimarisha Njia ya Reli ya Kati, Serikali
ilikarabati njia ya Reli, kati ya Kilosa na Gulwe iliyoharibiwa na Mafuriko kwa
gharama ya Shilingi Bilioni 26.36
kati ya mwaka 2009 na 2012. Aidha,
Serikali ilitumia Mkopo wa Dola za Marekani Milioni 33 kununulia Sleepers,
mataruma ya Reli na vifaa vya kufungia na hivyo kuwezesha kuanza kwa kazi ya kubadilisha
Reli zenye uzito mdogo wa Ratili 45
kwa yadi hadi Ratili 80 kwa yadi
kati ya Kitaraka na Mlongwe (km 89). Kazi hii ilianza mwezi Septemba
2012 na itakamilika ifikapo mwezi Septemba 2013. Kazi ya kubadilisha njia ya
Reli kutoka Igalula hadi Tabora (km 32)
itaendelea katika mwaka 2013/2014.
Ujenzi
wa Reli Mpya ya Kati
Mheshimiwa
Spika,
·
Serikali ya Tanzania imeingia makubaliano na
Serikali za Rwanda na Burundi ya kutekeleza Mradi mkubwa wa ujenzi wa Reli Mpya yenye urefu wa Kilometa 1,661
kutoka Dar es Salaam – Isaka – Keza – Kigali hadi Musongati (Burundi).
Upembuzi yakinifu wa Mradi huu ulikamilika mwaka 2009 na usanifu wa kina wa
Mradi huu ulianza mwaka 2011/2012.
Reli
ya TAZARA
Mheshimiwa
Spika,
·
Serikali za Tanzania na Zambia zimepata mkopo wa Dola za Marekani Milioni 39.9
kutoka Serikali ya China kwa ajili ya kuboresha Njia ya Reli kwa ukarabati
pamoja na ununuzi wa Injini na Mabehewa katika Reli ya TAZARA.
Mipango
ya Ujenzi wa Reli Mpya
i)
Ujenzi
wa Reli Mpya ya Tanga - Arusha – Musoma - Kampala
·
Serikali imeanza kufanya upembuzi Yakinifu kwa
ajili ya kuboresha Reli ya Tanga hadi Arusha kuanzia mwaka 2011/2012. Lengo ni
kuimarisha Reli hiyo ili iweze kuunganishwa na Reli Mpya iliyopangwa kujengwa
kati ya Arusha – Musoma hadi Kampala. Mkataba wa Makubaliano kuhusu ujenzi wa
Reli hii ulitiwa mwezi Juni 2011 kati ya Serikali ya Tanzania na Uganda. Mradi
huu utajumuisha pia ujenzi wa Bandari za Tanga, Musoma na Bandari iliyopo upande
wa Uganda.
ii)
Ujenzi
wa Reli ya Ukanda wa Mtwara
·
Serikali imekamilisha kazi ya Upembuzi yakinifu wa
Reli Mpya itakayotoka Bandari ya Mtwara hadi Mchuchuma na Liganga. Kazi hii
imegharimiwa na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na hivi sasa Serikali inamtafuta
mwekezaji kwa ajili ya ujenzi wa Reli hii.
USAFIRI
WA MAJINI NA UIMARISHAJI WA BANDARI
Bandari
Mpya ya Bagamoyo
Mheshimiwa
Spika,
·
Upembuzi yakinifu kuhusu upanuzi wa Bandari ya Dar
es Salaam umebaini kuwa ili kujenga Bandari itakayokuwa Kitovu (Hub) kwa ajili
ya kuhudumia Nchi Jirani, bandari kubwa ya kisasa itapaswa kujengwa katika eneo
la Mbegani, Bagamoyo ambapo Hekta 2,518
zimetengwa. Upembuzi yakinifu wa Bandari Mpya ya Bagamoyo ulikamilika mwezi
Julai 2010. Aidha, tayari Serikali ya Tanzania na Serikali ya China kupitia
Kampuni ya China Merchants zimeingia
Mkataba wa Makubaliano ya ujenzi wa Bandari hiyo kwa utaratibu wa Ubia wa Sekta
ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).
Bandari
ya Mtwara
Mheshimiwa
Spika,
·
Serikali imetenga eneo kubwa la Ardhi yenye ukubwa
wa Hekta 2,647 litakalotumika kwa
ajili ya upanuzi wa Bandari ya Mtwara.
Hivyo, Serikali imenza upembuzi yakinifu wa Mradi wa Upanuzi wa Bandari ya
Mtwara tangu mwaka 2011/2012 na kazi hiyo itakamilika katika mwaka huu wa 2013.
Mkongo wa Taifa wa
Mawasiliano Nchini
Mheshimiwa
Spika,
·
Mojawapo
ya Mafanikio makubwa ya Serikali ya Awamu ya Nne ni ujenzi wa Mkongo wa Taifa
wa Mawasiliano (National ICT Broadband Backbone). Utekelezaji wa awamu ya I na
II ya ujenzi wa Mkongo huo umekamilika. Mkongo huo una jumla ya Kilomita 7,560 zikiwemo Kilomita 5,448 zilizojengwa na Serikali na
Kilomita 2,112 zilizojengwa na
TANESCO. Mkongo huo umejengwa kwa
kiwango cha ubora wa Kimataifa ambao unakidhi mahitaji ya ndani na nje ya Nchi.
Mkongo huo una mizunguko (rings)
mitatu ya Kaskazini, Kusini na Magharibi. Hivyo kunaufanya Mkongo
kuwa na huduma ya uhakika isiyotetereka kirahisi kwani hata pale inapotokea
Mkongo kukatika upande mmoja huduma itaendelea kuwepo bila ya matatizo yoyote.
Kuunganisha Mkongo na Zanzibar na Mikoa
Mheshimiwa
Spika,
·
Mkongo
wa Taifa Mawasiliano wenye urefu wa Kilometa 7,560 umeunganishwa na Makao Makuu
ya Mikoa 24 ya Tanzania Bara.
·
Kwa
upande wa Zanzibar, Pemba imeunganishwa na Mkongo kwa kutumia Msongo wa Umeme wa TANESCO kutokea Tanga
wakati Unguja itaunganishwa kwa kutumia Msongo wa Umeme kati ya Dar es Salaam
na Unguja. Uwekaji wa Mkongo huu umeanza hivi sasa.
Kuunganisha Mkongo na Nchi Jirani
Mheshimiwa
Spika,
·
Vituo
tisa (9) vya Mkongo (Cross-border
Connectivity Stations) vimejengwa mpakani na Nchi jirani za Rwanda,
Burundi, Uganda, Kenya, Malawi, na Zambia. Hivi sasa nchi za Rwanda, Burundi,
Malawi, na Zambia zinatumia huduma ya Mkongo wa Taifa kwa malipo kwa ajili ya
kuunganishwa na Mikongo ya Kimataifa ya Baharini ambayo ni SEACOM na EASSy.
·
Mradi
wa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano
umelenga kuunganisha Makao Makuu ya Mikoa na Wilaya zote Tanzania Bara
na Visiwani. Mkongo ukifika Wilayani watoa huduma za mawasiliano na TEHAMA
watasambaza huduma hizo hadi Vijijini kwa haraka na kwa gharama nafuu, hivyo
kuharakisha ukuaji wa uchumi na maendeleo ya Taifa kwa kuwa Wananchi watapata
fursa ya kutumia TEHAMA katika juhudi za kupambana na umaskini na kujiletea
maendeleo kwa kasi zaidi. Manufaa ya Mkongo huo yameanza kuonekana kutokana na
kupungua kwa gharama za mawasiliano ya simu Nchini kwa zaidi ya Asilimia 60 hivi sasa.
MAFANIKIO
KATIKA MATUMIZI YA MITANDAO YA MAWASILIANO
Mheshimiwa
Spika,
·
Tangu Serikali ya Awamu ya Nne iingie madarakani,
matumizi ya Simu za Mkononi na mawasiliano kupiti Mtandao wa Internet
yameongezeka sana.
Simu
za Mikononi
·
Kiwango cha matumizi ya Simu za Mezani na Mkononi
kimeongezeka kutoka Watumiaji 3,118,157
sawa na Asilimia 10 ya idadi ya Watu
Nchini mwaka 2005 hadi Watumiaji 27,395,650,
sawa na Asilimia 61 ya Watu Nchini
mwaka 2012.
Mtandao
wa Internet
Mheshimiwa
Spika,
·
Matumizi ya Mtandao wa Internet yameongezeka kutoka
Watumiaji 1,681,012, sawa na
Asilimia 4.5 mwaka 2005 hadi
Watumiaji 7,519,078, sawa na
Asilimia 16.8 mwaka 2012.
NISHATI
MPANGO WA KUONGEZA UZALISHAJI WA UMEME NCHINI
Mheshimiwa Spika,
·
Kwa sasa (2013) uwezo wa kuzalisha umeme MW 1,438. Lengo ni kuzalisha MW 2,780
hadi MW 3,000 ifikapo mwaka 2015. Ipo miradi mingi inayotekelezwa na Serikali
ili kufikia lengo hilo. Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na ifuatayo:
(i)
Ujenzi wa Mitambo ya kusafisha Gesi Asilia na Bomba
la kusafirisha Gesi Asili kutoka Mnazi Bay hadi Mtwara na Songosongo Kisiwani
(Lindi) kupitia Somanga Fungu hadi Dar es Salaam. Gharama za Mradi huu ni Dola za Marekani Milioni 1,225.3, sawa na Shilingi Trilioni 1.96. Kati ya fedha hizo Asilimia 95 ni Mkopo Nafuu
kutoka Benk ya Exim ya China na Asilimia 5
itachangiwa na Serikali.
(ii)
Serikali inatekeleza mradi wa kujenga Mtambo wa
Kufua Umeme wa Kinyerezi I
utakaozalisha MW 150 na Kinyerezi II wa MW 240.
(iii)
Serikali imekamilisha Mradi wa Ujenzi wa Mtambo wa
kufua umeme wa MW 105 wa Ubungo II, Dar es Salaam. Vilevile, Serikali inatekeleza mradi wa
ujenzi wa Mtambo wa kufua umeme wa MW 60
Nyakato, Mwanza.
(iv)
Miradi mingine ni Mradi wa Somanga Fungu
unaotekelezwa na Kampuni ya Kilwa Energy unaotarajiwa kuzalisha MW 320.
(v)
Mradi mwingine ni ule wa kufua umeme wa Mchuchuma
wa kuazalisha MW 600 na Mradi wa
Makaa ya Mawe wa Ngaka utakaozalisha MW
40.
·
Miradi hii ikikamilika itaongeza uwezo wa
uzalishaji umeme Nchini na kuondoa tatizo lililopo kwa kiwango kikubwa.
Mafanikio
mengine katika Sekta ya Nishati
·
Serikali imefanikiwa kusambaza Umeme katika Wilaya 117 (sawa na Asilimia 89) kati ya Wilaya 133 zilizopo Nchini.
·
Idadi ya Watanzania wanaopata umeme imeongezeka
kutoka Asilimia 10 mwaka 2005 hadi Asilimia 14.5 mwaka 2012/2013.
·
Kutokana na kuhamasisha uwekezaji katika Sekta ya
Nishati, Makampuni makubwa yamefanya utafiti na Kugundua Gesi Asilia kiasi cha
Fiti za Ujazo Trilioni 32 kwenye
kina kirefu cha bahari.
·
Serikali inatekeleza Mradi mkubwa wa ujenzi wa
Bomba la Gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ambao ukikamilika utatuwezesha
kuwa na uhakika wa Umeme Nchini na wa bei nafuu. Hatua hii itasaidia kuokoa
Dola za Kimarekani Milioni 850 kwa mwaka kwa kutumia Gesi Asilia
badala ya Mafuta kuzalisha Umeme.
(c)
KILIMO
Mafanikio ya Sekta ya Kilimo
Mheshimiwa
Spika,
·
Katika kipindi cha mwaka
2006/2007 hadi 2012/2013, Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali zenye
lengo la kuimarisha Sekta ya Kilimo na kuleta Mapinduzi ya Kijani hapa Nchini.
Hatua hizo ni pamoja na kutekeleza programu ya kuendeleza Sekta ya Kilimo
(ASDP), azma ya KILIMO KWANZA, Mipango wa Ruzuku ya Pembejeo za Kilimo na
Mifugo, Kuanzishwa kwa mpango wa kukopesha wakulima Matrekta, Uanzishwaji wa
Benki ya Kilimo, kuanzisha Mpango wa Kuendeleza Kanda za Kilimo (SAGCOT) na
kadhalika.
·
Mpango wa Uwekezaji wa Ukanda wa Kusini (SAGCOT). Huu ni mpango wa kilimo ambao unashirikisha
Sekta binafsi wakiwemo Wadau wa Maendeleo, Wawekezaji wa Ndani, Wawekezaji wa
Kimataifa na Taasisi mbalimbali za ndani na nje ya Nchi.
·
Wakati Mpango wa SAGCOT
unaanza mwaka 2010/2011, jumla ya wakulima walikuwa takriban 265 tu walijiunga na Mpango huo,
kutokana na usimamizi mzuri wa Mpango huu hadi mwaka 2012/2013 idadi ya
wakulima imeongezeka hadi kufikia 3,000.
·
Tayari matokeo ya awali
ya kutia moyo yameshaanza kuonekana ambapo Wakulima
wadogo wameweza kuvuna kiasi cha Tani 8 za mpunga kwa Hekta kutoka Tani 1.5
walizokuwa wanavuna kabla ya kujiunga na Mpango wa SAGCOT na wameweza kuzalisha
mara mbili ya wakulima wakubwa wanaowazunguka ambao wanavuna Tani 4 tu kwa
Hekta). Haya ni mafanikio makubwa ambayo Serikali yetu inapaswa kujivunia.
Benki ya Kilimo
Mheshimiwa Spika,
·
Serikali imekamilisha
maandalizi ya kuwepo kwa Benki ya Kilimo ambayo inatarajiwa kuanzishwa katika
mwaka wa 2013/2014 ili kuwawezesha wakulima kupata mikopo kwa riba nafuu. Aidha, Benki hiyo tayari imeshasajiliwa na
Serikali imeshateua Wakurugenzi wa Bodi wa muda na Mtendaji Mkuu wa muda.
Nafasi za kazi kwa watendaji wakuu wa Benki hiyo zimeshatangazwa.
Pembejeo na zana za Kilimo
Mheshimiwa Spika,
·
Utaratibu wa utoaji wa
Ruzuku ya Pembejeo umewezesha jumla ya Kaya takriban Milioni 2 kunufaika na Mpango huo.
·
Kutokana na juhudi hizi
za Serikali matumizi ya mbolea yameongezeka kutoka Tani 73,000 mwaka 2006/2007 hadi kufikia Tani 240,350 mwaka 2012/2013, na matumizi ya Mbegu bora yameongezeka
kutoka Tani 11,056 mwaka 2006/2007
hadi Tani 30,443 mwaka 2012/2013.
Matumizi ya Zana za Kilimo
Mheshimiwa Spika,
·
Kutokana na juhudi za
kuhimiza matumizi ya zana bora za
kilimo, Matrekta yameongezeka kutoka Matrekta Makubwa 7,823 na Madogo 3,400
mwaka 2010 hadi kufikia Matrekta Makubwa 8,466
na Madogo 4,571 mwaka 2011.
Serikali za mikoa zilifanya kazi nzuri sana ya kuwasaidia wakulima kupata
matrekta hayo jambo lililofanya matrekta ya mkopo kuchukuliwa yote. Sasa hivi
Serikali imeshaandaa mpango wa kuingiza Matrekta yapatayo 3,000 kutoka India kwa ajili ya kuwakopesha Wananchi.
Kilimo cha Umwagiliaji
Mheshimiwa Spika,
·
Eneo linalotumika kwa
Umwagiliaji limeongezeka kutoka Hekta 233,398
mwaka 2006/2007 hadi kufikia Hekta 450,392
mwaka 2012/2013. Kwa vile skimu nyingi zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi,
Serikali inaamini kuwa eneo la umwagiliaji litaongezeka maradufu katika siku za
usoni.
(d)
VIWANDA
Mheshimiwa Spika,
·
Ukuaji wa Sekta ya Viwanda umeongezeka kutoka
Asilimia 8.4 mwaka 2005 hadi
Asilimia 9.9 mwaka 2008. Licha ya
kutokea Mdororo wa Kiuchumi mwaka 2008/2009 na matatizo ya umeme, ukuaji wa
Sekta ya Viwanda umeendelea kuwa juu ya Asilimia 8.2 kwa mwaka.
·
Viwanda vikubwa vya Saruji, Bia, Karatasi, Sigara,
ambavyo vilibinafsishwa katika miaka ya 1990 vimeongeza uzalishaji mara dufu.
·
Katika kuhamasisha na kuvutia Uwekezaji, jumla ya
Wawekezaji 59 tayari wameanzisha
Viwanda vya kuzalisha bidhaa mbalimbali na wamewekeza Mtaji wa Dola za
Kimarekani Milioni 792.2.
·
Mauzo ya bidhaa nje za Viwanda yameongezeka kutoka
Dola za Marekani Milioni 156.1 mwaka
2005 hadi Dola za Marekani Milioni 861.5
mwaka 2011/2012.
(e)
MAENDELEO
YA RASILIMALI WATU (Elimu, Afya na Maji)
MAFANIKIO YA ELIMU
(i)
Elimu
ya Msingi
Mheshimiwa Spika,
·
Idadi ya Shule za Msingi imeongezeka kutoka Shule 14,400 mwaka 2006 hadi 16,331 mwaka 2012.
·
Idadi ya Wanafunzi imeongezeka kutoka Wanafunzi
Milioni 7.9 mwaka 2006 hadi
Wanafunzi 8.3 mwaka 2012.
·
Idadi ya Walimu imeongezeka kutoka Walimu 135,013 mwaka 2005 hadi kufikia 180,987 mwaka 2012 na uwiano wa Mwalimu
kwa Mwanafunzi umeimarika kutoka 1:51
mwaka 2010 hadi 1:46 mwaka 2012.
(ii)
Elimu
ya Sekondari
Mheshimiwa
Spika,
·
Idadi ya Shule za Sekondari imeongezeka kutoka
Shule 1,845 mwaka 2006 hadi Shule 4,528 mwaka 2011/2012.
·
Idadi ya Wanafunzi wanaojiunga na Kidato cha Kwanza
imeongezeka kutoka Wanafunzi 196,391
mwaka 2006 hadi Wanafunzi 517,993
mwaka 2012.
·
Idadi ya Walimu wa Sekondari imeongezeka kutoka
Walimu 23,805 mwaka 2005/2006 hadi
Walimu 65,086 mwaka 2012.
(iii)
Vyuo
vya Ualimu
Mheshimiwa
Spika,
·
Hivi sasa Mafunzo ya Elimu ya Ualimu ngazi ya Cheti
na Stashahada yanatolewa katika Vyuo vya Ualimu 34 vya Serikali na Vyuo 82
visivyo vya Serikali vyenye uwezo wa kudahili Wanachuo 47,898 kwa wakati mmoja. Uandikishaji kwa mwaka katika Vyuo hivyo
ni takriban Wanachuo 43,258.
(iv)
Elimu
ya Juu
Mheshimiwa Spika,
·
Idadi ya Vyuo Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki
imeongezeka kutoka Vyuo 26 mwaka
2005 hadi Vyuo 46 mwaka 2012 vya
Serikali na Binafsi.
·
Kati ya Vyuo hivyo vipya, ni Chuo Kikuu cha Dodoma
kinachoendelea kujengwa ambacho kikikamilika kitakuwa na Wanafunzi 40,000 na hivyo kuwa ndicho kikubwa
kuliko vyote Nchini.
·
Wanafunzi wanaojiunga na Vyuo Vikuu vilivyopo
Nchini imeongezeka kutoka Wanafunzi 40,719
mwaka 2005/2006 hadi 166,484 mwaka
2011/2012.
·
Fedha za mikopo ya Elimu ya Juu zimeongezeka kutoka
Shilingi Bilioni 56.1 mwaka
2005/2006 hadi Shilingi Bilioni 326
mwaka 2012/2013.
·
Idadi ya Wanafunzi wanaopata mikopo ya Elimu ya Juu
imeongezeka kutoka 55,584 mwaka 2006
hadi Wanafunzi 98,772 mwaka 2012.
AFYA
Mheshimiwa Spika,
·
Serikali imeongeza uwezo wa ndani wa kutibu Maradhi
mbalimbali yakiwemo ya upasuaji wa Moyo ambapo hadi sasa zaidi ya Wagonjwa 450 wamepatiwa huduma hiyo.
·
Serikali imekarabati kwa kiwango kikubwa Hospitali
mbalimbali Nchini, ikiwemo Hospitali ya Saratani ya Ocean Road kwa kuongeza
uwezo wake kutoka Vitanda 120 hadi 270. Pia, jengo maalum la kutoa huduma ya
Saratani katika Hospitali ya Bugando limekamilishwa.
·
Kutokana na juhudi za kuhamasisha matumizi ya
Vyandarua na udhibiti wa Mazalia ya Mbu, kiwango cha Malaria Nchini kwa Watoto
walio na umri wa chini ya miaka Mitano kimepungua kutoka Asilimia 18 mwaka 2007 hadi Asilimia Tisa (9) mwaka 2012.
·
Jumla ya Vyandarua vilivyowekwa Viuatilifu vya muda
mrefu ambavyo vimesambazwa kwa Kaya zenye Watoto walio na umri chini ya Miaka 5
na Wanawake Wajawazito imefikia Milioni
43.
·
Jitihada za kudhibiti Malaria zimechangia kupunguza
Vifo vya Watoto Wachanga kutoka Vifo
99 kwa kila Watoto 1,000 mwaka 1999
hadi Vifo 51 kwa kila Watoto 1,000
mwaka 2010.
·
Vilevile, vifo vya Watoto wenye umri chini ya miaka
5 vimepungua kutoka Vifo 147 kwa kila Watoto 1,000 mwaka
1999 hadi Vifo 81 kwa kila Watoto
1,000 mwaka 2010.
·
Aidha, Vifo vya Mama Wajawazito vitokanavyo na
Uzazi vimepungua kutoka 578 kwa kila
Vizazi hai 100,000 mwaka 2004/2005 hadi Vizazi 454 mwaka 2010.
·
Idadi ya Wanafunzi wanaodahiliwa katika Sekta ya
Afya wa ngazi ya Cheti, Stashahada na Uzamili imeongezeka kutoka 5,365 mwaka 2010/2012
hadi 7,458
mwaka 2011/2012. Kati ya Wanafunzi hao, wapo
Wauguzi 3,136, Wataalam wa Sayansi
Shiriki 2,257 na Wataalam mbalimbali
wa ngazi ya Shahada wapatao 1,320.
·
Maambukizi ya UKIMWI yamepungua kutoka Asilimia 5.7 mwaka 2007/2008 hadi Asilimia 5.1 mwaka 2011/2012.
MAJI
·
Hadi mwaka 2012/2013 zaidi ya miradi 138 ya maji ilikuwa imekamilika katika
Halmashauri mbalimbali Nchini.
·
Mpaka kufikia mwaka 2012/2013 upatikanaji wa maji
Vijijini uifikia Asilimia 58 na kwa
upande wa Mijini ulifkia Asilimia 86.
·
Kukamilika kwa mradi mkubwa wa maji kutoka Ziwa
Victoria kwenda Mikoa ya Shinyanga na Kahama.
Mheshimiwa Spika,
Kama
Serikali ya Awamu ya Nne isingekuwa na Weledi, je mafanikio haya yangepatikana!
Wahenga
wanasema
“Mnyonge mnyongeni
lakini haki yake mpeni” Serikali inafanya kazi nzuri.
HOJA: TUME YA MABADILIKO YA KATIBA NA
MCHAKATO WA KATIBA MPYA
Mheshimiwa Spika,
·
Mheshimiwa Mbowe kwa niaba ya CHADEMA amekuja na
vipaumbele vyake ambavyo havijumuishi miundombinu, kilimo, Maendeleo ya Viwanda
wala Maendeleo ya Rasilimali Watu n.k. Kipaumbele
chake kikubwa alichoanza nacho katika hotuba yake ni Tume ya Mabadiliko ya Katiba na Mchakato wa Katiba Mpya. Mimi nadhani Mheshimiwa Mbowe ameanza
kuchanganya mambo na kupagawa na Uchaguzi wa 2015 wa nani atakuwa Rais 2015. Katika hotuba yake yapo maneno yanayosema “Tume ya Mabadiliko ya Katiba imethibitisha
haina Weledi wa kusimamia mchakato huru usiofungamana na upande wowote”. Mimi nadhani hii siyo lugha ya kiungwana
kwa Tume ambayo imeundwa kwa mujibu wa Katiba na yenye Watu wanaoheshimika sana
Nchini.
·
Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba wanaotokana
na orodha ya majina yaliyopendekezwa na Vyama vya siasa vyenyewe. Katika Tume hii, wapo Wajumbe Wawakilishi
kutoka CHADEMA, wenye Weledi mkubwa wengine ni Maprofesa. Siamini kama Mheshimiwa Mbowe anashindwa
kutambua kwamba Mjumbe wake katika Tume hii ni Profesa Mwesige Baregu. Sasa ni
Weledi upi anaozungumzia ambao Profesa Baregu hana.
Mheshimiwa
Spika,
·
Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba waliteuliwa
na Mheshimiwa Rais kutokana na orodha ya majina yaliyopendekezwa na Vyama Siasa
vyenye usajili wa kudumu. Aidha, Jumuiya za Kidini, Asasi za Kiraia,
Jumuiya/Taasisi zisizo za Kiserikali na makundi ya watu wenye malengo
yanayofanana. Uteuzi wa Wajumbe ulizingatia sifa zilizoanishwa kwenye kifungu
cha 6 (3) (a, b, c) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83.
·
Kwa
kuzingatia utaratibu huo, inaonyesha kuwa Wajumbe wa Tume wana sifa na Weledi
wa kutosha kutekeleza majukumu waliyokabidhiwa na Taifa.
Hoja: Tume kutokuwa na nia na dhamira ya
kusimamia mchakato huru wa Katiba.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Tume inafanya kazi kwa mujibu wa Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba, (Sura ya 83) ambayo imeainisha Majukumu na Hadidu za
Rejea. Hivyo, kwa muhtasari ni kwamba:
i)
Utendaji kazi wa Tume unazingatia majukumu ya Tume
kwa mujibu wa Hadidu za Rejea kama
zilivyoanishwa kwenye Vifungu vya 9, 17 vya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba,
Sura ya 83;
ii)
Katika utekelezaji wa majukumu yake, Tume imepokea
na kukusanya maoni ya Wananchi kuanzia mwezi Julai, 2012 na kukamilika mwezi
Januari, 2013;
iii)
Kwa mujibu wa Kalenda ya Tume, hivi sasa Tume
imefanya kazi ya uchambuzi wa maoni yaliyokusanywa ili kutayarisha Rasimu ya
Ripoti na Rasimu ya Katiba ambayo itawasilishwa kwa Wananchi kupitia Mabaraza
ya Katiba ya Wilaya ambayo uundwaji wake unaendelea hivi sasa;
iv)
Kwa mujibu wa Ratiba ya Utekelezaji wa Kazi za Tume
hadi kufikia Mwezi Aprili, 2014 Tanzania itakuwa na Katiba Mpya;
Mheshimiwa
Spika,
·
Tunaposema
Tume haina nia na dhamira ya kweli ni kuwavunja nguvu, kuwakatisha tamaa na
kuwadharau watu tuliowaamini na kuwapendekeza sisi wenyewe na bila kuzingatia
mazingira magumu wanayokumbana nayo katika utekelezaji wa kazi tuliyowapatia.
·
Napenda kutumia fursa hii pia kuwapa moyo Wajumbe
wote wa Tume na Sekretarieti yake kuendelea na kasi na ari waliyonayo katika
kufanikisha jukumu kubwa walilokabidhiwa na Taifa la kuhakikisha kuwa, kufikia
mwaka 2014, tunapata Katiba Mpya iliyotokana na maoni ya Wananchi.
·
Nawasihi wasife moyo, kwani Wananchi wanatambua juhudi zao za dhati katika kutekeleza jukumu
walilokabidhiwa. Hivyo, Kauli iliyotolewa na Kambi ya Upinzani Bungeni kuwa
Tume hii haina weledi na dhamira ya kweli kusimamia mchakato huru wa Katiba, ni
kuwavunja moyo kuwakatisha tamaa na kuwadharau Watu tuliowaamini na
kuwapendekeza sisi wenyewe na bila ya kuzingatia mazingira magumu wanayokumbana
nayo katika utekelezaji wa kazi nzito tuliyowawakabidhi.
Hoja kuhusu: Mchakato wa Mabadiliko
ya Katiba yaliyokusudiwa yanaelekea kuilinda CCM na Serikali yake na kuendeleza
baraka za “Status Quo”.
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
·
“Status Quo” inayozungumziwa ni ipi? Kwa
maana, Wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba hawatokani na wana CCM peke
yake. Wajumbe wale ni mchanganyiko wa watu waliopendekezwa kutoka Vyama vya
Siasa vyenye usajili wa kudumu, Jumuiya za Kidini, Asasi za Kiraia,
Jumuiya/Taasisi Zisizo za Kiserikali na makundi ya watu wenye malengo
yanayofana. Hivyo, siyo kweli kwamba Tume inaelekea kutengeneza Katiba
itakayoilinda CCM.
·
Kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura
ya 83, mchakato wote wa kupatikana kwa
Katiba Mpya umekuwa ukiwahusisha na utaendelea kuwahusisha Wananchi katika
hatua zote:
i)
Kwa kuzingatia Kifungu cha 9 (1) Tume ilitumia njia mbalimbali katika kukusanya
maoni ya Wananchi;
ii)
Kwa mujibu Kifungu cha 18 (1), (2), (3) cha Sheria
ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, Rasimu ya Katiba yenye maoni ya Wananchi
itawasilishwa kwa Mwananchi kupitia Mabaraza ya Katiba ya Wilaya ambapo
Wananchi watapata fursa ya kuijadili na kuitolea maoni Rasimu
iliyoandaliwa kutokana na maoni yao
wenyewe;
iii)
Kwa mujibu wa Vifungu vya 25 (1), 26 (2) Wabunge wa
Bunge la Jamhuri ya Muungano na wale wa Baraza la Wawakilishi ambao ni
Wawakilishi wa Wananchi watapata fursa ya kuipitia kuijadili na kuipitisha au
kuikataa Rasimu ya Katiba na wanaweza kuifanyia mabadiliko kama watakavyoona
inafaa;
iv)
Kwa mujibu Kifungu cha 36 cha Sheria ya Mabadiliko
ya Katiba, Sura ya 83, Katiba iliyopendekezwa itapelekwa kwa Wananchi ili
waweze kuipitisha au kuikataa kwa kupiga kura ya “Ndiyo” au “Hapana”;
v)
Mchakato huo unashirikisha Wananchi wa Vyama vyote
na wasiokuwa na vyama. Siyo sahihi
kusema kuwa Mabadiliko ya Katiba yataendelea kuibeba CCM. Yote yanayofanywa na yatakayofanywa na Tume
ya Mabadiliko ya Katiba ni kwa mujibu wa
Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inayoainisha mchakato ambao ulipitishwa na Bunge
hili na kisha kuwekwa mezani katika Baraza la Wawakilishi Zanzibar.
Hoja: Tume haikuwa na utaratibu madhubuti wa kutoa
elimu kwa Wananchi juu ya masuala yote yanayohusu Katiba Mpya na kwamba
haikutoa elimu ya kutosha kwa Wananchi ili kuwaandaa kuchangia maoni yao kwa
Tume wakiwa na uelewa wa kutosha.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Katika suala la kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu Mchakato wa Katiba Mpya, Tume
iliandaa program mbalimbali za Elimu kwa kutumia:
i)
Vyombo vya Habari [Redio, Luninga, Magazeti];
ii)
Kutoa machapisho mbalimbali yakiwemo:
Ø Katiba
ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Lugha Nyepesi;
Ø Sheria
ya Mabadiliko ya Katiba kwa Lugha nyepesi;
Ø Sheria
ya Mabadiliko ya Katiba Sura ya 83;
Ø Hadidu
za Rejea za Tume ya Mabadiliko ya Katiba;
Ø Kazi
za Tume ya Mabadiliko ya Katiba;
Ø Maswali
yanayoulizwa Mara kwa mara.
·
Tume imehakikisha kuwa Machapisho hayo pamoja na
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar yalisambazwa Nchi
nzima kabla Tume haijafika kukusanya
maoni ya Wananchi. Naamini kwamba, Waheshimiwa Wabunge, ninyi ni mashahidi wa
suala hili kwani Tume iliwapatia nyaraka hizo ikiwa ni pamoja na Wananchi
katika Majimbo yenu.
·
Mheshimiwa
Mbowe pia, analinganisha mchakato wa Katiba Mpya baina ya Tanzania na Kenya. Eti Tume ya Katiba ya Kenya ilitoa elimu kwa
miezi sita kabla ya kuanza kukusanya maoni ya Wananchi.
Mheshimiwa
Spika,
·
Mimi nisingependa kutumia Kenya kama mfano. Kwa
sababu Tume ya Katiba ya Kenya ilikwenda kwa Wananchi mara mbili. Mara ya kwanza ilikwenda kutoa Elimu ya Katiba,
na mara ya pili ilikwenda kwa
Wananchi kukusanya maoni. Baada ya hapo Tume hiyo haikurudi tena kwa wananchi
hadi wakati wa kura ya maoni. Matokeo
yake ni kwamba, eneo na idadi ya wananchi wa Kenya waliofikiwa na Tume ilikuwa
ndogo.
Mheshimiwa
Spika,
·
Hadi kufikia hatua ya kupata Katiba mpya, Tume ya
Mabadiliko ya Katiba itakwenda kwa Wananchi mara nne kupata maoni yao. Kwanza
ni wakati wa kuwaelimisha na kukusanya maoni yao; Pili ni kupitia Mabaraza ya Katiba ya Wilaya; Tatu ni kwa kupitia Bunge Maalum la Katiba kwa Wananchi
kuwalikishwa na Wawakilishi wao ikiwa ni pamoja na Waheshimiwa Wabunge na Waheshimiwa
Wawakilishi wa Baraza la Wawakilishi la SMZ na Nne ni kwa Wananchi kushirikishwa katika kuiridhia rasimu ya Katiba
kwa kupiga Kura ya Maoni.
·
Ni wazi kuwa Tume yetu itawafikia Wananchi wengi
kuliko Tume ya Katiba ya Kenya. Hivyo Tume ya Kenya haina vigezo vya
kulinganishwa na yetu.
Hoja Kuhusu: Muda
uliowekwa na Tume wa kukusanya maoni ni mdogo ukilinganishwa na ukubwa wa Nchi
na Wingi wa Wananchi. Wananchi walipewa dakika 5 kuwasilisha maoni yao kwenye
Mikutano
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
·
Kwa mujibu wa Kifungu cha 9 (1) (a) Sheria ya Mabadiliko
ya Katiba Sura ya 83, Tume imepewa jukumu la kuratibu na kukusanya maoni ya Wananchi.
Katika kutekeleza jukumu hilo Tume iliweka utaratibu wa kutumia njia mbalimbali
za kuratibu na kukusanya maoni ya Wananchi. Njia hizo ni:
i)
Kukusanya maoni kwenye Mikutano ya hadhara
iliyoitishwa na Tume kwenye Mikoa yote, Wilaya zote na Mamlaka za Serikali za
Mitaa zote Tanzana Bara na Zanzibar;
ii)
Pale ambapo mwananchi hakuweza kumaliza kutoa maoni
yake kwa kuongea alipewa Fomu maalum za Tume ili aweze kuandika maoni yake
yaliyobakia;
iii)
Katika Mikutano ya hadhara, Mwananchi yeyote
aliyetaka kutoa maoni yake kwa njia ya maandishi alipewa fomu maalum iliyotayarishwa na Tume;
iv)
Kupokea maoni kupitia Sanduku la Barua 1681 Dar es Salaam
na 2775 Zanzibar;
v)
Kupokea maoni kupitia Mitandao ya Kijamii ya barua
pepe ya katibu @katiba.go.tz,
facebook yenye anuani ya “tumeyamabadilikoya katiba”, Tovuti ya Tume yenye
anuani ya www.katiba.go.tz;
vi)
Makala
mbalimbali kutoka kwenye Magazeti; na
vii)
Katika njia ya ujumbe mfupi wa simu.
·
Mimi najiuliza hivi ni Nchi gani ambayo Tume
imeweza kuzunguka kila kitongoji?. Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, hakuna
Tume yoyote iliyoweza kuwafikia Wananchi wengi, kukusanya maoni mengi, kutumia
njia nyingi za kukusanya maoni na kufika katika kila Wilaya Nchini na katika
baadhi ya Vijiji. Tume nyingine zimetumia “sample”
katika baadhi ya maeneo
·
Ingawa idadi ya waliotoa maoni ni muhimu lakini
suala la msingi ni uzito wa maoni yaliyopatikana. Kwa mujibu wa Tume, Wananchi
wametoa maoni katika maeneo yote muhimu ya Katiba. Sasa kwa utaratibu huu, utaratibu wa hovyo utakaozaa
Katiba hovyo anaouzungumzia Mheshimiwa Mbowe ni upi?
·
Hivyo,
kutokana na Taratibu nzuri zilizowekwa na Tume kukusanya maoni, tunastahili
kuipongeza kwa kazi inayofanya na siyo kuanza kuishambulia, kuishutumu na
kuibeza kwa kazi ambayo tuliwatuma kupitia Sheria tuliyoipitisha sisi wenyewe.
Mheshimiwa Spika,
·
Aidha, Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni pia ametoa tishio la kuitisha maandamano Nchi
nzima na kuwataka Wananchi wagomee mchakato wa Katiba.
·
Niwaombe Wananchi wote kupitia Bunge lako Tukufu
kutokubali kurubuniwa na baadhi ya Wanasiasa wasiokuwa na nia safi na wenye
agenda zao za siri zenye kulenga kuvuruga mchakato huu ambao ni muhimu kwa
mustakabali wa Taifa letu. Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
aliwahi kusema kuwa “Akili za Kuambiwa, Changanya na zako”. Napenda kuwakumbusha kuwa, kila maandamano
yanayofanyika, wanaoathirika ni Wananchi na sio Viongozi wanaoshinikiza
maandamano hayo.
Hoja kuhusu: Tume kutokuwa
huru au kuutafsiri uhuru vibaya na kutoa Taarifa zake kwa Mheshimiwa Rais.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Kifungu cha 10 cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba
Sura ya 83 kinatoa Mamlaka na Uhuru kwa Tume katika utekelezaji wa Majukumu
yake bila ya kuingiliwa na Mtu au Mamlaka yoyote.
·
Tangu ilipoanza kutekeleza majukumu yake, Tume
imekuwa na utaratibu wa kutoa taarifa kuhusu jambo lolote linalopangwa
kutekelezwa na baada ya utekelezaji wake. Taarifa hizo hutolewa kupitia
Mikutano na vyombo vya habari, magazeti, majadiliano katika Redio na Luninga na
mitandao ya Kijamii.
·
Katikati ya mwezi Desemba, 2012 Mwenyekiti wa Tume
aliongea na vyombo vya habari ambapo pamoja na mambo mengine alitoa taarifa ya
utekelezaji wa kazi za Tume pamoja na ratiba ya kazi za Tume zinazotarajiwa
kutekelezwa kipindi kijacho. Hivyo, hotuba ya Rais ya mwishoni mwa mwaka 2012
ilitokana na taarifa ya Mwenyekiti wa Tume alipoongea na Vyombo vya Habari na
alifanya hivyo kwa kutambua kuwa Watanzania wengi huwa wanasikiliza kipindi
hicho cha Rais.
·
Katiba
siyo siri. Kwa maana hiyo, Mheshimiwa Rais kuongea na
Wananchi na kutumia taarifa iliyotolewa kwa Vyombo vya Habari Mimi sioni kama
ina ubaya. Mheshimiwa Rais amekuwa wazi
kwa kuonesha kuwa Hotuba yake ilitokana na Taarifa ya Tume, kosa lake ni
nini?. Aidha, Mheshimiwa Rais ndiye
msemaji Mkuu wa Nchi. Sasa najiuliza
kama yeye ana kosa kwa kuzungumza na Wananchi kuhusu kazi za Tume.
·
Aidha, kupitia Kalenda zilizotolewa na Tume ya
Mabadiliko ya Katiba za mwaka 2013, Tume imeainisha ratiba ya utekelezaji wa
shughuli zote za Tume kwa kuainisha aina ya jukumu, muda utekelezaji na tarehe
ya mwisho ya utekelezaji. Kalenda hizo zimegawanywa kwenye Taasisi za Serikali,
Vyama vya Siasa, Jumuiya za Kidini, Asasi za Kiraia, Jumuiya/Taasisi zisizo za
Kiserikali, Makundi mbalimbali na kwa Wananchi. Hivyo, ratiba ya utekelezaji wa
shughuli za Tume siyo siri. Kwa msingi
huo, Kauli ya Kambi ya Upinzani kwamba Tume inatoa taarifa zake za utendaji kwa
Rais na Serikali tu siyo sahihi bali taarifa za Tume hutolewa kwa Umma wote wa
Tanzania kwa ujumla. Suala linalotakiwa kwa kila mmoja wetu ni kuwa makini
kusikiliza taarifa mbalimbali zinazotolewa na Tume, kwani utendaji wao ni wa
wazi.
Hoja kuhusu: Tume ya Mabadiliko
ya Katiba kutowajibika kwa Bunge
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
·
Tume ya Mabadiliko ya Katiba ni Taasisi huru
inayotekeleza majukumu yake chini ya Wizara ya Katiba na Sheria.
·
Katika uwajibikaji wake kwa Bunge kwa maana ya
kutoa taarifa za mapato na matumizi, utekelezaji wa kazi zake, mafanikio na cha
changamoto, Tume ya Mabadiliko ya Katiba hupitia Wizara ya Katiba na Sheria
ambayo ndiyo Wizara Mama inayowasilisha maombi ya fedha za kazi za Tume na kutoa
Taarifa ya Utekelezaji.
·
Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba
anawajibika kwa Tume yenyewe na siyo kwa Taasisi au Mamlaka nyingine yoyote.
·
Katibu
wa Tume akiwa ndiye Mtendaji Mkuu wa Tume, anawajibika kuwasilisha taarifa za
utekelezaji wa masuala ya fedha kwa Katibu Mkuu – Wizara ya Katiba na Sheria
ambaye kupitia Waziri wa Katiba na Sheria anawasilisha taarifa hizo Bungeni.
·
Sisi hatudhani kwamba Tume imekosea kwa hali yoyote
ile. Kwa hiyo siyo busara Kambi ya Upinzani kuitumbukiza Tume katika mgogoro na
Taasisi au Mhimili mwingine yaani Bunge.
Kimsingi Tume haijakataa kuhojiwa na Bunge. Taratibu zipo kupitia Wizara
ya katiba na Sheria.
Hoja : Tume imetengeneza utaratibu wa Mabaraza ya Kikatiba ambao kwa
ushahidi wa mwanzo inaonyesha kuwa hayo ni Mabaraza ya CCM na siyo Mabaraza ya
Watanzania; kutokana na Wajumbe hao kuchaguliwa na Kamati ya Maendeleo ya Kata.
Mheshimiwa
Spika,
·
Katika kuwapata Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya
Wilaya, Tume ilitumia Muundo wa Serikali za Mitaa na taratibu za Mikutano
katika ngazi hizo ikiwa ni katika Vijiji, Mitaa na Kata. Muundo huu si ubunifu
wa Tume bali umeainishwa katika Sheria
za Serikali za Mitaa zikiwa ni Sheria zilizotungwa na kuridhiwa na Bunge
hili.
·
Waheshimiwa Wabunge, mkiwa Wajumbe wa Mabaraza ya
Halmashauri katika maeneo yenu, naamini mnafahamu kwamba, katika ngazi ya Kata,
tofauti na ilivyo katika ngazi ya Mtaa na Kijiji, Chombo kinachotambuliwa
Kisheria kutoa maamuzi kwa niaba ya Wananchi, ni Kamati ya Maendeleo ya Mtaa
(WDC). Hivyo, maamuzi ya kutumia Chombo hicho, yana msingi katika Sheria za
Serikali za Mitaa. Aidha, propaganda zinazoeleza kuwa, Mabaraza hayo ni ya CCM,
na si Mabaraza ya Katiba ya Watanzania wote, siyo za kweli, bali zimelenga
kujenga chuki na kupotosha Umma wa Watanzania. Uanachama au kutokuwa Mwanachama
wa Chama cha Siasa haikuwa sifa mojawapo ya kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya.
Madai yaliyotolewa na Mheshimiwa Mbowe kuwa
Wagombea wasiokuwa wa CCM walienguliwa katika Chaguzi hizo si za kweli na yamelenga
kupotosha Umma. Kwa mujibu wa Mwongozo, Wananchi walitakiwa kuomba kwenye
ngazi za Vijiji na Mitaa kwa Tanzania Bara na Shehia kwa Zanzibar.
Mheshimiwa
Spika,
·
Kwa
Tanzania Bara: Mikutano Mikuu ya Vijiji/Mitaa ilitumika kuwapigia
Kura ya Siri Wananchi walioomba kuwa Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya
bila kujali itikadi za Vyama vyao.
·
Aidha, majina ya Wananchi waliochaguliwa kwenye
ngazi ya Vijiji /Mitaa yaliwasilishwa kwenye Kikao cha Kamati ya Maendeleo ya
Kata ili yapigiwe Kura za Siri na Wajumbe kwa utaratibu wa uchaguzi wa kawaida.
·
Utaratibu wa Kamati za Maendeleo za Kata kuhusika
katika uchaguzi huu, haujaanzishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba. Kamati hizo
zimekuwa zikitumika kuchagua Wajumbe mbalimbali katika ngazi ya Kata, kama vile
Kamati za Maji, Shule, Ukimwi, Afya, Mazingira, n.k.
·
Suala la Wajumbe wa Kamati za Maendeleo za Kata
kuwa na Wajumbe wengi kutoka Chama kimoja ni matokeo ya maamuzi ya Wananchi waliowachagua.
·
Hoja kwamba Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya
wachaguliwe na Wananchi moja kwa moja katika ngazi ya Kata, hilo HALIWEZEKANI. Mantiki yake ni kwamba,
kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa Na. 7 na 8 na Mamlaka za Wilaya na
Miji za mwaka 1982 hakuna Mkutano wa uchaguzi unaowahusisha Wananchi wote
katika ngazi ya Kata.
Hoja: Tume kukataa kubadilisha Muundo wa Mabaraza
ya Katiba hata baada ya kupewa maoni na Wadau.
Mheshimiwa Spika,
·
Baada ya kuandaa Rasimu ya Mwongozo kuhusu Muundo,
Utaratibu wa kuwapata Wajumbe wa Mabaraza ya Katiba ya Wilaya, Tume iliusambaza
Mwongozo huo kwa Wadau mbalimbali na kuutangaza kwenye Vyombo vya Habari
ikiwemo Magazeti, Luninga na katika Tovuti ya Tume ambapo ilitoa muda kwa Wadau
kuwasilisha maoni yao kuhusu Rasimu hiyo.
·
Tume ilipokea maoni mbalimbali kutoka kwa Wadau na
kwa kiwango kikubwa maoni hayo yalizingatiwa na kuingizwa kwenye Mwongozo. CHADEMA haikutoa maoni yake kwenye Tume
kuhusu Rasimu ya Mwongozo. Badala yake ilitoa maoni yao katika Mikutano ya
hadhara baada ya Mwongozo kuchapishwa na kusambazwa.
·
Uzoefu unaonesha kwamba, lipo tatizo kwa upande wa
CHADEMA kushinikiza kila jambo wanalolitoa Bungeni au katika Mikutano yao ya
hadhara, bila ya kuzingatia kuwa lina maslahi ya Taifa au la, wakitaka
litekelezwe na Serikali au Taasisi zake. Serikali imekuwa ikiwasikiliza mara nyingi,
lakini inapotokea kuwa masuala wanayoyashinikiza yasipotekelezwa na Serikali
kwa sababu za msingi, Chama hicho kimekuwa na tabia kupitia kwa Viongozi wake
kutishia kuchukua hatua kadhaa ikiwemo kuitisha maandamano Nchi nzima na
kususia masuala mbalimbali ya Kitaifa.
·
Hali hiyo pia ilijitokeza hata wakati wa mchakato
wa awali wa kutunga Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, ambapo licha ya kususia
vikao vya Bunge vilivyokuwa vikijadili Muswada wa Sheria hiyo, bado Mheshimiwa
Rais aliwapa fursa ya kuwasilikiza na kuchukua baadhi ya
maoni yao. Hivyo, si sahihi kuisema
Serikali ya CCM kuwa si sikivu na isiyojali maoni ya Wadau. Nawashauri CHADEMA
kufuata na kuzingatia masharti ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba ambayo kama
nilivyosema hapo awali kuwa, si taratibu zilizoanzishwa na Tume.
Hoja: Sheria ya Marekebisho ya
Katiba imefanyiwa marekebisho mara moja tu kinyume na Makubaliano ya CHADEMA na
Mheshimiwa Rais.
Mheshimiwa Spika,
·
Utakumbuka kuwa, tarehe 10 Februari, 2012 Bunge
lako Tukufu lilipitisha Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba, 2011; na hatimaye Mheshimiwa Rais kuridhia Marekebisho hayo tarehe 20
Februari, 2012. Baada ya Marekebisho hayo, Mheshimiwa Rais aliteua Tume ya
Mabadiliko ya Katiba ambayo ilianza kutekeleza majukumu yake rasmi tarehe 01
Mei, 2012.
·
Marekebisho hayo yalitokana na maoni kutoka
Serikalini, pamoja na Wadau mbalimbali wakiwemo Vyama vya Siasa (CHADEMA, CUF
na NCCR MAGEUZI) na Asasi mbalimbali za Kijamii; ambapo wote walipata fursa ya
kukutana na Mheshimiwa Rais na kujadiliana naye kuhusu mapendekezo ya
marekebisho ya Sheria hiyo.
·
Katika majadiliano hayo, Wadau hao kwa pamoja walikubaliana na Serikali kwamba,
Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, yafanywe kwa Awamu tatu. Awamu
ya kwanza ikihusu Tume ya Mabadiliko ya Katiba na masuala mengine
yanayohusiana nayo, ikiwa ni pamoja na Utaratibu wa kuwapata Wajumbe wa Tume na
kuruhusu Wanasiasa kuteuliwa kuwa Wajumbe wa Tume. Vilevile ilikubaliwa kuwa, Awamu ya Pili ya marekebisho itahusu
Bunge Maalum la Katiba pamoja na masuala yote yanayohusiana nayo. Aidha, Awamu ya Tatu na ya mwisho itahusu
masuala yote ya Kura ya Maoni.
·
Kutokana na utaratibu huo, Awamu ya Kwanza ya
Marekebisho ilishafanyika, na hivyo kutoa nafasi sasa kwa majadiliano ya Awamu
ya Pili ya marekebisho. Hivyo, mwezi Januari 2013, Vyama vya Siasa vya CHADEMA,
CUF na NCCR MAGEUZI viliwasilisha kwa maandishi maoni yao yanayohusu
mapendekezo ya marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Serikalini. Kwa
nyakati tofauti, tarehe 04 - 08 Machi 2013, Wawakilishi wa Vyama vya CHADEMA,
CUF na NCCR - MAGEUZI walikutana na Serikali chini ya Uongozi wa Mheshimiwa
Waziri wa Nchi OWM (Sera, Uratibu na Bunge) na Mheshimiwa Mwanasheria Mkuu wa
Serikali kujadili mapendekezo ya Vyama hivyo. Katika vikao hivyo ilipendekezwa
kuwa, mapendekezo kuhusiana na Bunge
Maalum la Katiba ndiyo yatakayojadiliwa huku yale yanayohusu Kura ya Maoni
yatajadiliwa katika Awamu ya Tatu kwa kuwa, kabla ya zoezi hilo la Kura ya
Maoni, Sheria mahsusi kuhusu Kura ya Maoni itatungwa kwa ajili ya mchakato huo.
Mheshimiwa Spika,
·
Katika majadiliano hayo, yapo maeneo ambayo
Serikali na Wadau walikubaliana na hivyo kuchukuliwa na kuingizwa katika
Muswada wa Marekebisho ya Sheria hiyo. Ninapenda kuliarifu Bunge lako Tukufu
kuwa, Muswada huo wa Marekebisho
unatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge hili la Bajeti.
Hoja: Bado haijulikani Wajumbe 166
watakaotokana na Taasisi mbalimbali zilizotajwa na Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba watateuliwa kwa utaratibu gani na nani atakayefanya uteuzi huo.
Mheshimiwa Spika,
·
Suala hili lilishabainishwa na kufanyiwa kazi na
Serikali tangu awali, ambapo miongoni mwa marekebisho yanayotarajiwa kufanyika,
Serikali imependekeza utaratibu utakaotumika kuwapata Wajumbe 166 waliotajwa katika Kifungu cha 22(1)(c) kutoka katika Taasisi
mbalimbali kabla ya majina yao kuwasilishwa kwa Rais kwa majadiliano na Rais wa
Zanzibar kwa ajili ya uteuzi.
·
Utaratibu uliopendekezwa ni kuazima maneno yaliyopo
chini ya Kifungu cha 6(6) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, 2011
yatumike katika kualika Asasi hizo kupendekeza majina ya Wajumbe kwa ajili ya
uteuzi utakaofanywa na Mheshimiwa Rais kama ilivyokuwa wakati wa uteuzi wa
Wajumbe wa Tume.
Mheshimiwa
Spika,
·
Kwa maelezo hayo, utaratibu huo utatumika mara
baada ya Bunge lako Tukufu kupitisha Marekebisho ya Pili ya Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba.
Hoja: Hakuna muafaka juu ya
uhalali wa idadi kubwa ya Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kutoka Zanzibar
kushiriki katika mjadala wa Katiba Mpya kwenye masuala yasiyokuwa ya Muungano.
Mheshimiwa Spika,
·
Suala hili pia lilijitokeza katika majadiliano;
ambapo CHADEMA walitoa hoja ya kuwa, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi wasiwe
Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Walieleza kuwa, kwa kuwaruhusu Wajumbe wa
Baraza la Wawakilishi kushiriki katika Bunge Maalum, kutaiongezea CCM na CUF
idadi ya Wajumbe katika Bunge Maalum wakati CHADEMA ikibakiwa na idadi yake ya
sasa katika Bunge la Muungano.
Mheshimiwa Spika,
·
Naomba kusisitiza kuwa, Wajumbe wa Baraza la
Wawakilishi wataendelea kuwa Wajumbe katika Bunge Maalum la Katiba kama
ilivyobainishwa katika Sheria. Hii ni kwa sababu Baraza la Wawakilishi ndicho
Chombo mahsusi kinachowawakilisha Wananchi wa Tanzania Zanzibar katika masuala
ya Muungano na yasiyo ya Muungano.
·
Aidha, kwa mujibu wa Kifungu cha 26(2) cha Sheria ya Mabadiliko ya
Katiba, msingi wa maamuzi katika Bunge Maalum la Katiba utafanywa kwa
kuzingatia theluthi mbili ya idadi ya
Wajumbe wote wa Bunge Maalum kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili kutoka
Tanzania Zanzibar. Hivyo, idadi yoyote ya Wabunge kutoka Zanzibar
haitaathiri maamuzi ya Wajumbe kutoka Tanzania Bara.
Hoja: Hakuna Sheria inayompa Mheshimiwa Rais Mamlaka ya kuliitisha upya
Bunge Maalum la Katiba na kulielekeza kuboresha masharti ya Katiba Mpya mara
baada ya Bunge hilo kuipitisha.
Mheshimiwa
Spika,
·
Maelezo kuhusu Hoja hii yameainishwa bayana katika Kifungu cha 28 (2) cha Sheria ya
Mabadiliko ya Katiba, 2011. Kifungu hiki kinachotoa fursa kwa Mheshimiwa Rais
kuliitisha tena Bunge baada ya kuvunjwa au kukoma kwa lengo la kuboresha
masharti yaliyomo katika rasimu ya Katiba inayopendekezwa kabla na baada ya
Kura ya Maoni, hususan pale atakapoona kuna umuhimu wa kufanya hivyo kwa
maslahi ya Taifa.
·
Kwa maelezo hayo, utaona kuwa Sheria tangu awali
ilishatoa muongozo kuhusu suala hili muhimu kwa kufanikisha azma ya Taifa ya
kupata Katiba mpya.
Hoja: Haujulikani uhalali upi wa Kisheria utakaoiruhusu Tume ya Taifa ya
Uchaguzi kusimamia na kuendesha kura ya maoni ya kuhalalisha Katiba Mpya.
Mheshimiwa Spika,
·
Sheria kama ilivyo sasa, chini ya Sehemu ya Sita imetoa uhalali na
muongozo wa Kisheria kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushirikiana na Tume ya
Uchaguzi ya Zanzibar kuendesha na kusimamia zoezi zima la Kura ya Maoni kwa
Rasimu ya Katiba Mpya. Hivyo, uhalali wa Tume hizi kuratibu zoezi hilo upo
katika Sheria ya Mabadiliko ya Katiba.
Mheshimiwa Spika,
·
Hata hivyo, ili zoezi hili lifanyike kwa ufanisi,
Serikali pia imekwishaandaa Muswada wa
Sheria ya Kura ya Maoni ambao nao unatarajiwa kuwasilishwa katika Bunge
hili la Bajeti. Hivyo, ninawasihi Waheshimiwa Wabunge sambamba na maoni yao
kuhusu Muswada huo na maoni mengine kwa ajili utaratibu mzima wa Kura ya Maoni
katika Sheria iliyopo, tushirikiane kuyaandaa kwa ajili ya Awamu ya Tatu ya
Marekebisho ya Sheria hii kama ilivyokubaliwa na Mheshimiwa Rais na Wadau
mbalimbali wakiwemo Wawakilishi wa Vyama vya Siasa.
MATOKEO HAFIFU YA
KIDATO CHA NNE MWAKA 2012
Hoja: Elimu sio kipaumble cha Taifa kwa CCM na
Serikali yake
Jibu:
Mheshimiwa
Spika,
·
Msemaji Mkuu wa Kambi ya Upinzani katika eneo hili
la Elimu ameanza kwa kumnukuu Rais wa 55 wa Marekani John Kennedy (1917- 1963
kuhusu maendeleo ya elimu katika Nchi yetu. Mimi nadhani hakuna haja ya kwenda
mbali mpaka Marekani miaka hiyo ya nyuma ndiyo sisi Tanzania tupate suluhisho
la matatizo ya elimu katika Nchi yetu. Jambo la msingi hapa ni kujua sisi
tunasemaje. Mheshimiwa Mbowe anasema tufanye nini, siyo nadharia ya John
Kennedy wa miaka hiyo.
·
Katika hotuba yangu nilieleza juu ya uwekezaji
mkubwa uliofanywa na Serikali kwenye Sekta ya Elimu katika kipindi cha mwongo
mmoja uliopita. Ni ukweli usiopingika pia kwamba, tulianza kupanua elimu ya
Msingi na Sekondari kwa kasi sana mwaka 2006.
Kipaumbele kiliwekwa katika Sekta ya Elimu ambapo Bajeti ya Elimu
ilichukua nafasi ya kwanza kwa miaka nane mafululizo. Aidha, fedha zilizokuwa zinatengwa zilikuwa zinaongezeka
mwaka hadi mwaka.
Bajeti ya Elimu Kuanzia Mwaka 2005/2006 hadi
2012/2013
ilikuwa inaongezeka kama ifuatavyo:
MWAKA
|
BAJETI
|
ASILIMIA YA BAJETI YOTE
|
2005/2006
|
Bilioni 669.5
|
16%
|
2006/2007
|
Bilioni 891.2
|
18.4%
|
2007/2008
|
Bilioni 1,086
|
17.9%
|
2008/2009
|
Bilioni 1,430
|
19.8%
|
2009/2010
|
Bilioni 1,743.9
|
18.3%
|
2010/2011
|
Bilioni 2,045.3
|
20.3%
|
2011/2012
|
Bilioni 2,283
|
19.7%
|
2012/2013
|
Bilioni 2,890
|
23.4%
|
·
Matokeo ya uwekezaji huu hayawezi kuonekana mara
moja na kwamba pamoja na umuhimu wake upanuzi wa elimu ya Msingi na Sekondari
umekuja na changamoto zake, kama vile upungufu wa walimu, vyumba vya madarasa,
madawati, vitabu na vifaa vingine vya kufundishia na kujifunzia. Nilieleza pia kwamba, Serikali inaendelea
kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo hatua kwa hatua.
Hoja
kuhusu: Elimu ya Tanzania
imeporomoka kwa kiasi kikubwa cha sasa kuhatarisha mustakabali wetu kama Taifa
hasa kutokana na kufeli kwa kutisha kwa Wahitimu wa Kidato cha Nne mwaka 2012.
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
·
Ni kweli kwamba, Matokeo ya Mitihani ya Kidato cha
Nne mwaka 2012 yameonesha kuwa kiwango cha ufaulu kimeshuka kwa kiwango kikubwa
ikilinganishwa na miaka ya hivi karibuni. Matokeo yaliyotangazwa yanaonesha
kwamba kati ya Wanafunzi 397,132
waliofanya Mtihani huo, Watahiniwa 126,851
ndio waliofaulu. Katika idadi hii, Wanafunzi waliofaulu katika daraja la I-III
ni 23,520 na daraja la daraja la IV
ni 103,327. Watahiniwa 240,903 sawa na Asilimia 65.5 wamepata daraja la sifuri.
Mheshimiwa Spika,
·
Kutokana na matokeo hayo, Serikali iliunda Tume
inayoongozwa na Prof. Sifuni Mchome kama Mwenyekiti kufuatilia suala hilo ni
Huru na inafanya kazi kwa mtazamo tofauti sana.
Ina wajumbe kutoka Vyuo vya Elimu ya Juu; Baraza la Wawakilishi;
Mashirika Yasiyo ya Kiserikali; Madhehebu ya Dini; Chama cha Walimu, Muungano
wa wenye Shule Binafsi na Muungano wa Walimu Wakuu wa Sekondari.
·
Hadidu za Rejea za Tume hiyo ni kama ifuatavyo:
i)
Kubainisha sababu za matokeo mabaya ya Mtihani wa Kidato
cha Nne mwaka 2012;
ii)
Kubaini sababu za kushuka kwa kiwango cha ufaulu
katika Mitihani ya Kidato cha Nne kuanzia kipindi cha mwaka 2005 hadi 2012;
iii)
Kutathmini nafasi ya Halmashauri katika kusimamia Elimu
ya Sekondari katika Halmashauri zake;
iv)
Kuanisha sababu nyingine zinazoweza kuwa
zimechangia hali hii ya matokeo;
v)
Kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua mara moja
kwa Wanafunzi 240,903 waliopata Daraja
la Sifuri katika Mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2012; na
vi)
Kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukua kukabiliana
na tatizo la mwenendo wa kushuka kwa kiwango cha elimu mara moja, kipindi cha
muda mfupi, kati na kipindi cha muda mrefu;
·
Kazi hii itafanyika kwa kipindi maalum kuanzia
tarehe 1 Machi, 2013, Tanzania Bara na Zanzibar na kuwasilisha taarifa yake kwa
Serikali mara baada ya kukamilisha kazi hiyo.
·
Napenda kusisitiza kwamba Serikali ina dhamira ya
dhati ya kupata ufumbuzi wa kudumu wa
changamoto zinazoikabili sekta ya elimu kwa kuwashirikisha wadau wote. Naomba tuiache Tume hii huru ifanye
kazi. Ifikiri nje ya sanduku na itupe
mtazamo mpya. Baada ya hapo
ndipo tuweze kusema kweli kama hakukuwa na sababu
ya Tume hiyo. Nawaomba pia Waheshimiwa Wabunge tuangalie
sana kauli zetu tusije tukakuta wakati mwingine tunawachochea walimu. Tuwape moyo wafanye kazi yao wakati
tukishughulikia changamoto zinazowakabili.
HOJA: Serikali iliunda Tume ya kushughulikia
suala la kuporomoka kwa elimu nchini 2010 hatua gani zimechukuliwa kufuatia
mapendekezo ya Tume hiyo.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Mwaka 2011, Serikali iliunda Kikundi Kazi cha Serikali ambacho kilifanya utafiti wa
kubaini chanzo cha wanafunzi kutofanya vizuri kwenye mitihani ya Kidato cha Nne
mwaka 2010. Kikundi hicho kilikamilisha
kazi na kuwasilisha taarifa yake mwezi Juni, 2011. Mapendekezo yaliyotolewa yanahitaji
utekelezaji wa muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu. Serikali ilianza
kutekeleza mapendekezo hayo hatua kwa hatua kuanzia mwaka 2012/2013. Kwa mfano,
idadi ya walimu imeongezeka kutoka 40,517
mwaka 2010 hadi 78,055 mwaka 2013. Kwa mwaka huu wa fedha (2012/2013) peke yake
Serikali imeajiri jumla ya walimu 12,969.
Aidha, Mfumo wa kuwapangia vituo vya kazi unazingatia mahitaji (ikama) kwa
shule zote. Ujenzi wa maabara, nyumba za walimu na hosteli za wanafunzi
unaendelea katika Shule mbalimbali za Sekondari Nchini.
·
Hata
hivyo, bado mwelekeo wa ufaulu wa wanaomaliza Kidato cha Nne unapungua mwaka
hadi mwaka. Jambo kubwa zaidi safari hii ni kushuka kwa ufaulu hata katika
Shule za Mashirika ya Dini na Watu Binafsi zilizokuwa zinafanya vizuri sana. Hizi
ni dalili kuwa hatujapata ufumbuzi wa tatizo hilo. Ndiyo maana, Serikali iliona ni vema kuunda
Tume ambayo ni shirikishi zaidi na yenye kufanyakazi kwa kina zaidi kuliko Kikosi
Kazi.
·
Tume
iliyoundwa na Serikali hivi karibuni, ni tofauti na Kikundi Kazi cha mwaka 2011
kwa sababu inajumuisha Wadau mbalimbali wa Sekta ya Elimu kama
nilivyokwishaeleza. Aidha, hadidu za
rejea za Tume hii ni pana zaidi kuliko zile za Kikundi Kazi cha mwaka 2011.
HOJA: Serikali imechukua hatua gani kuwawajibisha
viongozi wanaohusika na Sekta ya Elimu kufuatia kufeli kwa kutisha kwa wahitimu
wa Kidato cha Nne mwaka 2012.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
- Kwa sasa bado tunatafuta chanzo cha tatizo. Matokeo ya Tume iliyoundwa itaonesha chanzo cha tatizo. Serikali itajielekeza zaidi katika kupata ufumbuzi wa kudumu wa tatizo linalotukabili, kuelezana tulipokosea na kwa pamoja kurekebisha makosa na kusonga mbele katika safari ya maendeleo ya Elimu Nchini.
Hoja: Ushiriki wa Wanafunzi wa Elimu ya Juu
katika Siasa unaonekana kuelekea upande wa kukipendelea CCM.
Jibu:
Mheshimiwa
Spika,
·
Kwa mujibu wa Sheria ya Vyuo Vikuu Kifungu Na. 52
ni kosa kuendesha harakati za kisiasa katika mazingira/maeneo ya Vyuo
Vikuu. Kifungu hiki hakiwazuii Wanafunzi
kuwa Wanachama wa vyama mbalimbali au kuwa na itikadi tofauti na ya Chama
Tawala. Kinachokatazwa na Sheria hii ni
kufungua matawi, kufanya kampeni, kufanya mikutano au kuandikisha Wanachama
katika maeneo ya Vyuo Vikuu.
·
Kimsingi Vyama vya Siasa vimetumia mbinu nyingi
kupata Wananchama. Chama cha Mapinduzi
kimeamua kuanzisha Mkoa wa CCM katika Vyuo Vikuu lakini kwa kuweka msisitizo
kuwa shughuli zake za kichama zifanyike nje ya mazingira ya Chuo/Vyuo. Vyama vingine havijakatazwa kutumia njia
mbalimbali kupata Wanachama ili mradi shughuli zote zifanyike nje ya maeneo ya
Chuo/Vyuo na kwa kufuata matakwa ya Sheria.
Kuruhusu moja kwa moja harakati za kisiasa kufanyika Vyuoni kutaleta
athari zikiwemo uvunjifu wa amani, kuathiri shughuli za kitaaluma. n.k. Napenda kusisitiza kuwa katika hili hakuna
upendeleo wowote kwa Chama Tawala.
·
Ili kudhibiti harakati za kisiasa katika maeneo ya
Vyuo Vikuu, Sheria ndogo ndogo (By-laws) na Hati Idhini za Vyuo hivyo hutumika
katika kudhibiti masuala ya kisiasa ambayo yanaweza kuleta athari na kuathiri masuala
ya kitaaluma.
·
Wanafunzi wanao uhuru wa kutoa maoni yao bila
kubugudhiwa kwenye warsha, mikutano, kongamano na semina zinazofanyika katika
maneo ya Vyuo.
Hoja: Vigezo vinavyotumiwa na Bodi ya Mikopo
kutoa mikopo kuwa vinawapaendelea matajiri.
Jibu:
Mheshimiwa
Spika,
·
Vigezo vya utoaji mikopo havitoi mwanya wa
upendeleo kati ya Watoto wanaotoka katika familia zenye vipato tofauti. Uchambuzi wa waombaji unafanywa na mfumo
ambao unatoa majibu kulingana na taarifa alizojaza mwombaji mkopo bila kumwangalia
mhusika usoni, dini au kabila lake. Hata
Mwanafunzi anayekosa mkopo anapewa nafasi ya kukata rufaa kwenye Bodi ya
Mikopo, na ikishindikana anayo nafasi ya kukata rufaa kwa Waziri mwenye dhamana
ya Elimu.
- Tofauti ya kiasi cha mkopo anaopewa Mwanafunzi inategemea, pamoja na mambo mengine kama mwombaji anachukua programu ya kipaumbele cha Taifa pamoja na ukomo wa Bajeti.
Hoja: Bodi ya Mikopo imetumia gharama kubwa
kununua mfumo wa uchambuzi wa utoaji mikopo ambao haujaleta tija hadi sasa.
Jibu:
Mheshimiwa
Spika,
·
Ni kweli kwamba Serikali kupitia iliyokuwa Wizara
ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu, ilinunua mfumo wa utoaji mikopo kabla
ya Bodi ya Mikopo kuanzishwa mwaka 2004/2005.
Baada ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kuanzishwa, ililazimika
kuboresha mfumo huu ili kuzingatia changamoto zilizojitokeza kama vile wingi wa
waombaji, mabadiliko ya mara kwa mara ya vigezo vya utoaji mikopo pamoja na
programu za vipaumbele vya Taifa. Hata
hivyo, mfumo huu umeleta mafanikio makubwa hasa kwa kuweza kupokea maombi,
kuchambua, kupanga viwango vya mikopo na hatimaye kutoa mikopo kwa waliotimiza vigezo vyote
vya kupewa mikopo.
Mfumo
huu ambao kwa kiasi kikubwa unatumia “Online Loan Applicagtion System (OLAS)”
umesaidia kuepuka kutumia makaratasi pamoja na kuokoa muda.
Hoja: Kuna ucheleweshwaji wa Mikopo kwa
Wanafunzi waliopo Vyuoni jambo ambalo linasababisha migomo katika Taasisi za
Elimu ya Juu.
Jibu:
Mheshimiwa
Spika,
·
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu
imejipanga kuhakikisha kuwa Wanafunzi wanapata mikopo kwa wakati kwa
kushirikiana na wadau wote wakuu kama vile TCU, NACTE, Vyuo pamoja na Wanafunzi
wenyewe. Wadau hawa wanatakiwa
kuwasilisha taarifa sahihi na kwa wakati kwenye Bodi ya Mikopo ili utoaji wa
mikopo uweze kufanyika kwa wakati. Kwa upande wa Serikali, tumejipanga kutoa
fedha kwa wakati ili taratibu za utoaji mikopo ziweze kufanyika kwa
wakati. Kuanzia mwaka wa fedha 2012/2013, Serikali imetoa fedha kwa muda
muafaka na walengwa wameweza kunufaika na mikopo hiyo. Aidha, kila Chuo kimeajiri Afisa Mikopo
ambaye ni kiungo kati ya Wanafunzi, bodi ya Mikopo na Menejimenti za Vyuo
husika ili kuwezesha Wanafunzi kujikita zaidi kwenye masuala ya Kitaaluma
badala ya kutumia muda wao kushughlikia mikopo.
Hoja: Kuna kasi ndogo ya urejeshwaji wa mikopo
kutoka kwa wanufaika kwa vile Serikali na Bodi haikuzingatia ushauri wa Kambi
ya Upinzani kwenye Bajeti ya 1012/2013.
Jibu:
Mheshimiwa
Spika,
·
Ushauri wa Kambi Rasmi ya Upinzani kuhusu utumiaji
wa Mifumo ya Mawasiliano katika urejeshwaji mikopo umezingatiwa na Serikali
pamoja na Bodi ya Mikopo. Kwa mwaka wa
masomo 2012/2013, Bodi ya Mikopo imetumia mifumo hii (Tigo pesa, Airtel Money
na M – Pesa) kulipia gharama za kutuma maombi ya Mikopo. Kwa mwaka wa masomo 2013/2014, Bodi ya Mikopo
ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu itatumia mifumo hii katika kurejesha fedha za
walionufaika na mikopo. Mazungumzo
yanaendelea kati ya Bodi, Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa, Mamlaka za Mifuko
ya Hifadhi za Jamii na TRA ili kuweza kuwabaini walionufaika na hivyo kuwa
katika nafasi ya kuwabana kurejesha mikopo.
·
Bodi vilevile, imeanza kuwafikisha Mahakamani
wanufaika waliokaidi kurudisha mikopo baada ya kuhitimu na kumaliza “grace period”. Nitumie fursa hii, kuwasihi wote walionufaika
na mikopo, kuwa na moyo wa uzalendo kuanza kurudisha mikopo badala ya kusubiri
kutafutwa.
DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA
HOJA: Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama
vya Siasa unaotegemewa kuletwa Bungeni kwa ajili ya kuufanyia marekebisho,
usubiri hadi Katiba Mpya itakapokuwa imeanza kutumika.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Kwa kuwa shughuli za Vyama vya Siasa zinafanyika
wakati wote ni vizuri Sheria hii ikafanyiwa Marekebisho bila kuathiri mfumo na
taratibu zitakazoletwa na Katiba Mpya. Vilevile, kutokuleta marekebisho hayo kutadumaza demokrasia kwa kuingoja
Katiba Mpya.
HOJA: Tume ya
Taifa ya Uchaguzi iandae Daftari la Kudumu la Wapiga Kura litakalotumika kwa
uchaguzi wa Wabunge huko Zanzibar.
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
Kwa hivi sasa,
Tume inazingatia Sheria ya Taifa ya Uchaguzi (Sura ya 343) iliyopitishwa na Bunge hili Tukufu
inayoelekeza kuwa Tume itatumia Daftari
lililoandaliwa kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Zanzibar katika Uchaguzi wa
Wabunge huko Zanzibar. Kwa msingi huo, Tume ya Taifa ya Uchanguzi hutumia Daftari
lililoandaliwa na Tume ya Uchanguzi ya Zanzibar katika uchaguzi wa Wabunge huko
Zanzibar.
TUME
YA TAIFA YA UCHAGUZI
HOJA: Tume
ya Taifa ya Uchaguzi ina mpango wa siri wa kuandaa Daftari la Kudumu la Wapiga
Kura kwa kutumia mfumo wa ‘biometric’.
Mipango imeanza bila ya kushirikishwa Vyama vya Siasa.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Tume ya Uchaguzi haina mpango wa siri wa kuandaa
Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa kutumia mfumo wa ‘biometric’. Hata hivyo, Tume ipo katika hatua ya awali ya kuandaa
Uboreshaji wa Daftari kwa utaratibu wa kawaida na Tume itawashirikisha wadau.
HOJA: Sheria gani inaruhusu uboreshaji wa
Daftari la Wapiga Kura kwa njia ya ‘biometric’?
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka
1977, inaipa Tume ya Uchaguzi mamlaka ya kuandaa na kurekebisha Daftari la
Kudumu la Wapiga Kura kwa utaratibu/mfumo unaofaa.
·
Kwa sasa Nchi karibu zote za SADC, Afrika
Mashariki, Kati na Magharibi zinatumia mfumo wa ‘biometric’ na Nchi nyingine mbalimbali Duniani zinatumia mfumo wa ‘biometric’ katika kuandikisha wapiga
kura na kuanzisha Daftari la Uraia. Uamuzi wa kutumia mfumo wa ”Biometric” au la utafanyika kwa uwazi
na kwa kuwashirikisha Wadau wote ikiwa ni pamoja na kuifanyia marekebisho
Sheria husika.
SALAAM
ZA POLE KWA WATU WALIOPATA MAAFA NA AJALI
HOJA: Mheshimiwa
Waziri Mkuu alieleze Bunge ni kwa nini kwenye Hotuba yake hakutoa pole kwa Watu
walipoteza maisha kutokana na ajali za barabara na majini wakati Watu wengi
wamepoteza maisha kutokana na ajali hizo.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Katika Hotuba yangu kwenye Aya ya 5 ukurasa wa 3 na
4 nimetoa Pole kwa Watu mbalimbali
waliopatwa na matukio ya Majanga na Maafa mbalimbali yaliyojitokeza mwaka
2012/2013.
·
Wakati nawasilisha Hotuba yangu Aya hiyo sikuisoma kutokana
na makubaliano yetu hapa Bungeni ya kuongeza ufanisi katika kutunza muda.
SENSA
YA WATU NA MAKAZI
HOJA: Serikali itekeleze ahadi yake Bungeni ya
kuwalipa Posho Watendaji wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji waliohusika kuwasaidia
Makarani katika zoezi la Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Katika Makadirio ya Bajeti ya Sensa ya Watu na
Makazi, malipo ya Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na Mitaa hayakuwepo kwa kuwa
hapo awali waliopangwa kufanya kazi ya kuwaongoza Makarani na Wasimamizi wa Sensa
walikuwa ni Watendaji wa Kata (WEO) na Watendaji wa Vijiji na Mitaa (VEO). Hata
hivyo, wakati wa Zoezi la Sensa ilionekana kuwa Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji
na Mitaa ni muhimu wawepo kusaidia kuwaongoza Makarani na Wasimamizi wa Sensa.
·
Viongozi hao walifanya kazi hiyo vizuri na
walistahili kulipwa takriban Shilingi
4,292,501,555.
·
Hivyo, katika Kikao cha Kamati Kuu ya Taifa ya
Sensa ya Watu na Makazi kilichokutana tarehe 26 Machi 2013, Zanzibar kilijadili
suala hilo na kuielekeza Wizara ya Fedha kuhakikisha kuwa malipo ya Wenyeviti
wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji walioshiriki katika zoezi la Sensa yanafanyika
kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha. Taratibu za kupata fedha hizo
zinaendelea na Wahusika wote watalipwa.
HOJA: Serikali iwapatie Waheshimiwa Wabunge
nakala ya Taarifa ya Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2012 katika
Mkutano wa Bunge la Bajeti. Aidha,
Serikali itoe Taarifa ya Sensa ya Watu na Makazi ikionyesha wazi mchanganuo wa
Idadi ya Watu Kimkoa.
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Tarehe 5 Aprili, 2013 nilipata fursa ya kuzindua Ripoti
ya Idadi ya Watu kwa ngazi za Utawala kuanzia ngazi ya Mkoa, Wilaya na Kata/Shehia.
·
Ripoti hiyo ya kwanza ni moja kati ya Machapisho ya
Sensa zaidi ya 18 yatakayotolewa na
Ofisi ya Taifa ya Takwimu kuanzia mwezi Aprili, 2013 hadi Juni, 2014 kuonyesha mchanganuo
wa Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya 2012.
·
Serikali
itaiagiza Ofisi ya Taifa ya Takwimu kusambaza kwa Waheshimiwa Wabunge wote
Nakala za Taarifa mbalimbali za Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi
kila mara zinapotoka. Nakala za Toleo la Kwanza la Taarifa za Matokeo ya Sensa
ya Watu na Makazi zitasambazwa kabla ya mwisho wa Mkutano huu wa Kumi na Moja
unaojadili Bajeti ya Serikali.
·
Taarifa zenye mchanganuo wa Matokeo ya Sensa ya
Watu na Makazi zitasambazwa kwa Wadau wote wa ndani na nje kwa kutumia Wavuti
(Website) ya Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Mtakwimu Mkuu wa Serikali Zanzibar.
Aidha, Taarifa hizo pia zitasambazwa kwa Viongozi na Watendaji wa Mikoa, Wilaya
na Halmashauri kupitia Kamati za Sensa ya Watu na Makazi za ngazi ya Mikoa na
Wilaya.
MAKAZI
BORA KWA ASKARI WA JESHI LA POLISI
Hoja: Serikali iwapatie Askari Polisi Makazi bora
yenye staha hususan kwa kuanzisha mfuko wa ujenzi wa Nyumba za Askari
JIBU:
Mheshimiwa
Spika,
·
Serikali inaendelea kutekeleza Programu Endelevu ya
Kuboresha Makazi ya Askari Polisi kwa kujenga nyumba mpya na kuzifanyia
ukarabati zile zilizopo ili kuweza kukidhi mahitaji ya nyumba bora za kuishi
kwa Askari wetu. Askari Polisi nchini
wanahitaji jumla ya Nyumba 41,000 na
Nyumba zilizopo ni 10,479 ambapo
Nyumba 582 ni nzima na zingine
zinahitaji matengenezo makubwa na madogo.
·
Ili kukabiliana na uhaba wa nyumba za kuishi Askari
Polisi Nchini, Serikali kuanzia mwaka 2006 hadi sasa imekamilisha kujenga jumla
ya Nyumba 458 katika maeneo ya Dar
es Salaam, Unguja, Pemba, Arusha, Mwanga (Kilimanjaro), Bahi (Dodoma) na
Kigoma. Serikali pia, inaendelea na ujenzi wa Nyumba 76 za Polisi katika miji ya Mwanza, Bukoba, Musoma, Kwimba na
Ludewa.
·
Aidha, Serikali inatarajia kuanza kujenga Nyumba 350 za Polisi katika eneo la
Osterbay, Jijini Dar es Salaam pamoja na kufanya mazungumzo na Serikali ya
Jamhuri ya Watu wa China ili kupata mkopo nafuu utakaofanikisha ujenzi wa
nyumba nyingi maeneo mbalimbali Nchini.
·
Katika Mpango wa Muda Mrefu, Serikali imepanga
kutumia utaratibu wa PPP kujenga makazi bora ya Askari wetu na kuongeza Bajeti
ya maendeleo kwa Jeshi la Polisi kila mwaka ili kukabiliana na mahitaji ya
nyumba na Ofisi.
·
Katika mwaka 2013/2014, Bajeti iliyotengwa kwa
Miradi ya Maendeleo pamoja na ujenzi wa Nyumba ni jumla ya Shilingi Bilioni 8.
·
Aidha, Jeshi la Polisi limeanzisha Shirika la
Uchumi - The Corporation Sole (Police Force) kwa tangazo la Serikali
Namba 66 la tarehe 29 Machi, 2013.
Shirika hilo pamoja na masuala mengine, litalijengea uwezo Jeshi la Polisi
katika kutekeleza Mikakati na Programu mbalimbali ya muda mfupi na mrefu ikiwa
ni pamoja na kujenga nyumba za makazi, Vituo na Ofisi za Polisi Nchini.
Hoja: MASUALA YA UDINI, AMANI NA UTULIVU
JIBU:
Mheshimiwa Spika,
·
Suala la Udini na Amani na Utulivu limezungumziwa
kwa kirefu katika hotuba ya Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hotuba yake kwa Wananchi ya tarehe 31
Machi, 2013. Tumefika mahali ambapo kama Viongozi na Waumini wa dini kusisitiza
umuhimu wa Waislamu na Wakristo kuishi pamoja kidugu, kwa upendo, ushirikiano
na kuvumiliana vinginevyo Nchi yetu itaacha kuwa kisiwa cha amani na kuingia
katika orodha ya Nchi zenye migogoro na hata vita vya wenyewe kwa wenyewe. Hatutaki
kufikia hatua hiyo kwa namna yoyote ile.
Ni lazima sote tulivalie njuga suala hili kuhakikisha kwamba Nchi yetu
inaendelea kuwa na mshikamano na upendo kati ya Waislam na Wakristo.
·
Aidha, katika siku za hivi karibuni kumejitokeza
matukio mbalimbali yanayoashiria uvunjifu wa hali ya amani na utulivu Nchini.
Katika maeneo mengi kumeibuka chokochoko za kidini ambazo zimeleta madhara
makubwa.
·
Vilevile, kutokana na Uhuru na Demokrasia pana
iliyopo, baadhi ya Wanaharakati na Vyama
vya Siasa wamekuwa wakihamasisha Wanachama wao kuendeleza vitendo vya uvunjifu
wa amani na kujenga chuki na uhasama miongoni mwa Jamii na kwa Serikali halali
iliyopo Madarakani. Mmeshuhudia katika maeneo mengi kuna baadhi ya Watu hasa
wale wa Vyama vya Siasa ambao badala ya kueleza Sera za Vyama vyao na
kuhamasisha maendeleo, wao wanataka kubomoa Umoja wa Taifa letu kwa kuendeleza
Vitendo vya uvunjifu wa amani na utulivu. Vitendo hivyo ni pamoja na kufanya
maandamano kinyume cha Sheria, na kuitisha mikutano ya kutukana, kubezana,
kushutumiana na kuzomeana. Chokochoko hizi si dalili nzuri kwa mustakabali wa
Nchi yetu inayopenda kudumisha amani na utulivu.
·
Serikali iliyopo Madarakani inayo dhamira njema ya
kujenga Umoja wa Kitaifa, Mshikamano, Amani na Utulivu. Hii ni kwa sababu tunatambua kuwa Amani
na Utulivu uliopo Nchini ni mazingira wezeshi ya kusaidia kila mmoja wetu kufanya shughuli zake za
kijamii na kiuchumi na kujiletea maendeleo.
Bila Amani na Utulivu hakuna maendeleo ya kweli ya Wananchi wetu.
·
Natoa Wito kwa Viongozi wote wa Vyama vya Siasa
kuacha tabia ya kuchochea Wananchi kwa kisingizio cha nguvu ya Umma badala yake
kuhimiza suala la kupitia Kamati za Ulinzi na Usalama.
·
Katika muda si mrefu, tumepanga kukutana na
Viongozi na Wadau mbalimbali katika Mikoa/Wilaya ikiwemo Vyama vya Siasa,
Madhehebu ya Dini, Vyombo vya Habari, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali,
Wanataaluma; Viongozi wa Wazee, Viongozi wa Makundi ya Vijana, n.k. kuzungumzia
suala hili na kuchukua hatua za kudumisha Umoja wa Kitaifa na Amani na Usalama
Nchini.
·
Aidha, Serikali itaendelea kuwaelimisha Wananchi
wote kuzingatia na kuheshimu Utawala Bora wa Sheria, Kanuni na Taratibu
zilizopo na hususan ‘Utii wa Sheria Bila Shuruti’ ili kudumisha Amani na
Utulivu tuliojijengea kwa muda mrefu.
·
Nirudie kuwakumbusha tena Wakuu wa Mikoa na Wilaya
na Wakuu wa Vyombo vya Usalama kutekeleza Agizo la Mheshimiwa Rais kwa kuacha
ajizi katika kutimiza wajibu wao kwenye suala la ulinzi na usalama. Tuhakikishe kamba Nchi yetu inabaki na amani
na utulivu ili Wananchi wetu waendelee kufanya shughuli za maendeleo. Serikali pia inawahakikishia kuwachukulia
hatua kali wale wote wanaotumia udini kwa maslahi ya vyama vyao ili kudumisha
amani na utulivu Nchini.
HITIMISHO:
Mheshimiwa
Spika,
·
Kama nilivyosema, hoja ni nyingi. Pamoja na
kurekebisha Kanuni zetu bado hatuwezi kumaliza kuzijibu hoja zote kwa muda huu
niliopangiwa. Baadhi ya hoja hizo zitajibiwa na Wizara za Kisekta wakati wa
kuwasilisha Hotuba zao za Bajeti.
·
Nawashukuru sana!
·
Naomba kutoa hoja!
COMMENTS