MAONI YA AWALI YA MWENYEKITI WA CUF KUHUSU RASIMU YA KATIBA MPY A (NAYAFAGILIA SANA)

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: 09/06/2013 MAONI YA AWALI YA MWENYEKITI WA CUF KUHUSU RASIMU YA KATIBA MPYA UTANGULIZI; Kwan...



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI:
09/06/2013
MAONI YA AWALI YA MWENYEKITI WA CUF KUHUSU RASIMU YA KATIBA MPYA
UTANGULIZI;
Kwanza naipongeza Tume ya Jaji Warioba kwa kazi kubwa waliofanya ya kuratibu maoni na kuja na mapendekezo ya katiba mpya ambayo hayakushinikizwa na matakwa ya Chama tawala cha CCM. Tume imeonyesha ujasiri mkubwa na hakika wahafidhina wa chama hicho watachukia sana.
Mambo mengi yaliyopendekezwa na Chama Cha Wananchi CUF yameingizwa katika Rasimu ya Katiba. Mambo hayo ni pamoja na mfumo wa Muungano wa serikali tatu, kuruhusiwa mgombea binafsi, Rais kutangazwa kushinda akipata zaidi ya asilimia 50 ya kura zote zilizopigwa la sivyo uchaguzi urudiwe kwa wale wawili walio ongoza kwa kura, Tume huru ya uchaguzi, Mawaziri kutokuwa wabunge, Spika kutokuwa mbunge, haki za watu wenye ulemavu, haki za binadamu na mengine mengi.
Hata hivyo mambo mengi muhimu kama vile umilikaji wa ardhi, maliasili na rasilimali za nchi kutumiwa kwa manufaa ya wananchi wote, elimu, afya, mazingira ya kukuza uchumi unaoleta neema kwa wananchi wote, wajibu, uwezo na uhuru wa serikali za mitaa hayajaingizwa ndani ya katiba kikamilifu kwani rasimu ya katiba imeshughulikia mambo ya muungano.
Mambo ya Muungano ni saba: Katiba na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ulinzi na Usalama wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Uraia na Uhamiaji, Sarafu na Benki Kuu, Mambo ya Nje, Usajili wa Vyama vya Siasa na Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano.
Mwongozo wa Tume kuhusu utoaji wa maoni ulijikita katika maeneo yafuatayo; Misingi na Maadili ya Kitaifa,  Madaraka ya Wananchi, Muundo wa Nchi na Taifa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Haki za Binadamu na Wajibu wa Wananchi, Ardhi, Maliasili na Mazingira, Mihimili ya Nchi (Ardhi, Watu na Utawala), Mihimili ya Utawala (Serikali, Bunge na Mahakama), Serikali za Mitaa, Muundo na Mamlaka yake, Vyombo vya Ulinzi na Usalama. Mambo mengi muhimu kwa mwananchi wa kawaida ikiwa ni pamoja na serikali za mitaa, umilikaji wa ardhi, haki za huduma za afya na elimu, na matumizi ya maliasili hayajaingizwa katika katiba hii na yanatarajiwa kuingizwa kwenye katiba ya Tanzania Bara. Rasimu ya katiba kwa wananchi wa Tanzania Bara haijakamilika mpaka Rasimu ya katiba ya Tanzania Bara itakapokuwa tayari. Hotuba ya uzinduzi wa katiba ya Jaji Warioba haikulifafanua suala hili. Hakuna mantiki ya kupigia kura ya maoni katiba ya jamhuri ya muungano bila kuwa na katiba ya Tanzania Bara kwa upande wa bara na marekebisho ya katiba ya Zanzibar isikinzane na katiba ya jamhuri ya muungano kwa upande wa zanzibar. Katiba ya Tanzania Bara na katiba ya Zanzibar iwe ni sehemu ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.
Kuwepo kwa rasimu ya katiba ya Tanzania Bara kutasaidi kuondoa kuweka asasi mbili au tatu zinazofanya kazi moja. Kwa mfano Tume ya Uchaguzi, Jeshi la Polisi, Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali, Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa ya serikali ya Muungano ikafanya kazi pia kwa serikali ya Tanzania Bara ikiwa wananchi wa Tanzania Bara hawana tatizo na utaratibu huo.
MAPENDEKEZO YA JUMLA;
1.     Pendekezo langu la msingi ni kwamba, kura ya maoni isubiri kukamilishwa kwa rasimu ya katiba ya Tanzania Bara na zote zikajadiliwa na wananchi kwa pamoja. Sina pingamizi kuwa Wajumbe wa Tume wa Tanzania Bara waandae rasimu ya Katiba ya Tanzania Bara, na wajumbe wa Zanzibar waandae mapendekezo ya marekebisho ya katiba ya Zanzibari ili isikinzane na katiba ya Jamhuri ya Muungano. Muda wa kuyatekeleza haya na kubadilisha sheria zifuate matakwa ya katiba mpya kabla ya uchaguzi mkuu wa 2015 haupo. Serikali imeeleza kuwa haina nia na Rais Kikwete hataki kabisa kujiongezea muda kwa kisingizio cha kukamilisha utaratibu wa katiba mpya. Wananchi pia wamechoka wanataka mabadiliko.

2.     Katika masuala ya haki za binadamu ningependa Katiba itamke wazi kuwa mwanamke mjamzito ana haki ya kupata lishe bora na huduma za afya wakati wa ujauzito na kujifungua. Vile vile watoto bila kujali uwezo wa wazazi wao wana haki ya lishe bora, huduma za msingi za afya na elimu inayomuandaa mtoto kukabiliana na changamoto za maisha.

3.     Pendekezo la Rasimu ya Katiba ya kuwepo Tume Huru ya Uchaguzi ni la msingi. Pendekezo hili lianze kufanyiwa kazi mara moja ili kufanya mabadiliko ya sheria ya uchaguzi na Tume ya uchaguzi ili uchaguzi wa 2015 uendeshwe na Tume iliyo Huru kweli. Mchakato wa mabadiliko ya katiba utaendelea baada ya uchaguzi mpaka ukamilike na sheria husika kufanyiwa mabadiliko.

4.     Siyo lazima Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi wawe watu waliyewahi kushika wadhifa wa Jaji wa Makakama ya Juu, Mahakama ya Rufani au Mahakama Kuu na ameshika wadhifa huo kwa kipindi kisichopungua miaka mitano kama Rasimu ya Katiba inavyoelekeza katika kifungu 181 (4). Masuala ya kusimamia uchaguzi ni ya utawala na uendeshaji kuliko ya kutafsiri sheria. Majaji siyo wasimamizi na mameneja wazuri wa utawala na logistics. Nchini Ghana mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ambaye kafanya vizuri siyo Jaji bali ni Profesa wa sayansi ya siasa – Jaji Lewis Makame kwa miaka zaidi ya 15 na hakufanikiwa kujenga Tume ya Uchaguzi yenye uwezo na kuaminika. Ni vyema wigo wanaoweza kuomba kuwa wenyeviti wa Tume ukapanuliwa na kuingiza wenye uzoefu wa utawala na logistics. Tume ina mwanasheria wake ambaye ataelekeza na kushauri masuala yahusiyo sheria.


5.     Kasoro kubwa ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ni kwamba haina nyenzo za kutimiza malengo muhimu ya katiba yenyewe. Ibara ya 6(b) imeeleza kuwa “lengo kuu la Serikali litakuwa ni maendeleo na ustawi wa wananchi.” Mambo ya uchumi yote isipokuwa Benki Kuu na sarafu hayamo katika orodha ya mambo ya Muungano. Hata suala la uratibu wa sera za uchumi halimo. Ibara ya 7(2) inaeleza “mamlaka ya nchi na vyombo vyake vinawajibika kuelekeza sera na shughuli zake zote kwa lengo la kuhakikisha kwamba: (c)Serikali itahakikisha kuwa shughuli zinazofanywa zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine; (d)ardhi ikiwa rasilimali kuu na msingi wa Taifa, inalindwa, inatunzwa na kutumiwa na wananchi wa Tanzania kwa manufaa, maslahi na ustawi wa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo; (e)maendeleo ya uchumi wa Taifa yanapangwa na kukuzwa kwa ulinganifu na kwa pamoja na kwa namna ambayo inawanufaisha wananchi wote; (f)kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli yoyote ya halali inayompatia mtu kipato chake; (j)utajiri wa rasilimali na maliasili za Taifa unaelekezwa katika kuleta maendeleo, kuondoa umaskini, ujinga na maradhi”. Serikali ya Muungano haina nyenzo ya kusimamia mambo hayo.

6.     Ibara ya 11 inazungumzia utekelezaji wa malengo ya taifa. Kifungu (2) kinaeleza “Serikali itatoa taarifa Bungeni si chini ya mara moja katika kila mwaka, kuhusu hatua zilizochukuliwa na mamlaka ya nchi ili kuhakikisha utekelezaji wa malengo ya Taifa yaliyoainishwa katika Katiba hii. (c) kiuchumi, Serikali inachukua hatua zinazofaa ili: (i) kuwaletea wananchi maisha bora kwa kuondoa umaskini; (ii) kuhakikisha kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kuwa utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu mwingine; (iii) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kuanzisha na kuendeleza vyombo vya uwakilishi wa wakulima, wafugaji na wavuvi; (iv) kuweka mazingira bora ya kufanya biashara na kukuza fursa za uwekezaji; (v) kuweka mazingira bora kwa ajili ya kukuza kilimo, ufugaji na uvuvi kwa kuhakikisha kuwa wakulima, wafugaji na wavuvi wanakuwa na ardhi na nyenzo kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao; (vi) kuweka mazingira bora ya uzalishaji wa mazao kwa wakulima, wafugaji na wavuvi, utafutaji na uendelezaji wa masoko ya mazao yao; (vii) kuweka utaratibu mzuri wa upangaji na usimamiaji wa mizania ya bei za mazao na pembejeo; (viii) kuimarisha na kuendeleza uwekezaji wa ndani, upatikanaji wa pembejeo za kilimo, maeneo ya ufugaji na vifaa vya uvuvi; (ix) kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa fursa na nafasi za wazi kwa watu wote na kuanzisha shughuli za kiuchumi na kukuza mazingira yaliyo bora kwa ajili ya kuhamasisha sekta binafsi katika uchumi; (x) kuhakikisha kuwa kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anapata fursa ya kufanya kazi, kwa maana ya kufanya shughuli yoyote halali inayompatia kipato; (xi) kuweka utaratibu unaofaa kwa ajili ya kufanikisha utekelezaji wa haki ya mtu kujipatia elimu na kuwa huru kupata fursa sawa ya kutafuta elimu katika fani anayoipenda hadi kufikia upeo wowote kulingana na stahili na uwezo wake. Mambo yote haya siyo ya muungano”. Serikali ya Muungano itawezaje kutoa taarifa Bungeni kwa mambo ambayo haiyasimamii.

7.     Ukizingatia mambo ya Muungano yaliyoorodheshwa na Rasimu, Serikali ya Muungano haina vyanzo vya mapato ya kodi. Ibara ya 215 imeeleza Vyanzo vya mapato ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano vitakuwa: “(a) ushuru wa bidhaa; (b) maduhuli yatokanayo na taasisi za Muungano; (c) mchango kutoka kwa Washirika wa Muungano; na (d) mikopo kutoka ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano”. Katiba haizungumzii taasisi yeyote ya kukusanya kodi. Jambo la saba la muungano ni Ushuru wa bidhaa na mapato yasiyo ya kodi yatokanayo na mambo ya Muungano. Mambo sita ya Muungano hayalipi ushuru wa bidhaa. Biashara siyo jambo la Muungano kwa hiyo ushuru wa forodha, kodi za ongezeko la thamani (VAT), excise duty, kodi ya mauzo haziwezi kuwa suala la Muungano. Mwaka wa fedha wa 2010/11 Mapato ya serikali Asilimia 34.3 ushuru wa forodha na VAT katika bidhaa zinazoagizwa toka nje, Asilimia 18.6 kodi (VAT na Excise duty) za bidhaa zinazozalishwa ndani ya nchi. Asilimia 29 kodi ya mapato. Kodi na tozo nyingine asilimia 10.5, Mapato ya halmashauri asilimia 2.8. Kodi ni chanzo cha mapato ya serikali lakini pia ni sera ya uchumi. Viwango gani vya kodi havina athari kubwa kwa wananchi maskini na kupunguza motisha ya uzalishaji na uwekezaji? Serikali za washirika wa Muungano hawatakubali Serikali ya Muungano kutoza kodi katika maeneo ambayo siyo ya muungano. Katiba haina muongozo wowote wa michango toka washirika wa Muungano. Rasimu hii ilivyo ikipitishwa kutakuwa na mgogoro mkubwa wa fedha za kuendeshea serikali ya Muungano na hatma yake itakuwa Muungano kuvunjika.

8.     Katika mambo ya uchumi Tume haikufanya uchambuzi wa kina wa kuwa na katiba inayojenga mazingira mazuri ya kukuza uchumi unaoleta maendeleo kwa wote. Katiba haiibani serikali iwe na utaratibu mzuri wa bajeti. Katika mambo ya usimamizi wa matumizi ya serikali na kazi za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali rasimu hii ime –“copy” na ku-“paste” katiba ya sasa bila kutathmini kama mfumo wa hivi sasa unafanya kazi. Eneo hili linahitaji kufanyiwa uchambuzi zaidi.


9.     Ibara za 213 na 214 zinawapa uwezo Serikali ya Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mshirika wa Muungano “zitakuwa na mamlaka ya kukopa fedha ndani na nje ya Jamhuri ya Muungano kwa ajili ya kugharamia shughuli zilizo chini ya mamlaka yake.” Katika utaratibu huu nchi inaweza kughubikwa na madeni ikiwa serikali tatu zitashindana kukopa ndani na nje ya nchi. Lazima pawe na mwongozo wa kudhibiti mikopo na kuongezeka kwa deni la taifa. Nchi inaweza kuingizwa katika mgogoro wa madeni. Uhuru wa serikali zote tatu kukopa ndani na nje ya nchi inaweza kusababisha kukua kwa madeni kupita kiasi. Serikali za washirika zina vyanzo vya mapato serikali ya muungano haina. Kwa Rasimu ya Katiba hii serikali za washirika ndizo zinazokopesheka na siyo serikali ya muungano.

10.   Rasimu ya Katiba bila kusema hivyo inapendekeza kuwepo na Benki Kuu tatu. Ibara ya 217 inaeleza “Kutakuwa na Benki Kuu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania itakayojulikana kuwa “Benki Kuu” ambayo itakuwa na majukumu yafuatayo: (a) kutoa sarafu, kudhibiti na kusimamia mzunguko wa sarafu; (b) kuandaa na kusimamia Sera na Mipango inayohusiana na sarafu; (c) kudhibiti na kusimamia masuala ya fedha za kigeni; na (d) kusimamia Benki za Washirika wa Muungano.” Ibara ya 218 inaeleza “Serikali za Washirika zitakuwa na Benki zitakazokuwa najukumu la kutunza akaunti ya fedha za Serikali husika, kusimamia Sera za Kifedha na benki za biashara katika mamlaka zao.” Kazi ya Benki Kuu ni kusimamia Benki za Biashara, sera za fedha na hasa riba, na mfumo wa malipo. Kazi hizi zitafanywa na Benki za Washirika wa Muungano. Moja ya chanzo cha mgogoro wa Euro ni kutokuwepo usimamizi wa pamoja wa Benki za biashara. Hivi sasa Ukanda wa Euro unajaribu kuandaa utaratibu wa pamoja wa kuifanya Benki Kuu ya Ulaya (ECB) kusimamia Benki za Biashara. Kama tuna sarafu moja tuwe na Benki Kuu moja. Benki Kuu isiposimamia benki za biashara haitaweza kudhibiti na kusimamia ujazi wa fedha (money supply)
11.   Ibara ya 105 inaeleza “(2) Wajumbe wa Bunge watakuwa wa aina zifuatazo: (a) Wabunge waliochaguliwa kuwakilisha majimbo ya uchaguzi; (3) Kwa madhumuni ya Ibara ya ndogo (2)(a), kila mkoa kwa upande wa Tanzania Bara na wilaya kwa upande wa Zanzibar, itakuwa ni jimbo la uchaguzi”.
Nini vigezo vya kufanya mikoa na wilaya kuwa majimbo ya uchaguzi? Utaratibu wa kuanzisha mikoa na wilaya ni wa serikali washirika au wa Serikali ya Muungano? Hata hivyo ibara ya 180 (a) inaeleza “mamlaka zinazosimamia uchaguzi kutangaza majimbo kwa madhumuni ya uchaguzi wa wabunge.” Majimbo ya uchaguzi yataundwa na Tume au tayari yameishatajwa na katiba?

12.   Mamlaka ya Bunge katika kuisimamia serikali katika masuala ya bajeti ni madogo. Ibara ya 107 (2) inaeleza, “katika kutekeleza majukumu yake, Bunge litakuwa na madaraka yafuatayo: (c) kujadili mgawanyo na kuidhinisha matumizi ya fedha kwa Wizara, taasisi na mashirika ya Serikali; (d) kujadili utekelezaji wa kila Wizara wakati wa Mkutano wa Bunge wa kila mwaka wa bajeti; (e) kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali katika Jamhuri ya Muungano; (f) kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango wowote wa muda mrefu au muda mfupi”. Hata hivyo Mambo ya Muungano hayahusishi Mpango wa Maendeleo wa taifa.

13.   Ibara ya 177 inaeleza “Bila ya kuathiri masharti ya Katiba hii, utumishi wa umma na uongozi katika Jamhuri ya Muungano utazingatia misingi kwamba utoaji wa ajira na uteuzi wa viongozi utakuwa kwa uwiano baina ya Washirika wa Muungano, kwa kuzingatia weledi na taaluma katika eneo au nyanja husika.” Nini maana ya uwiano? Je maana yake nusu ya wafanyakazi watoke Zanzibar na nusu watoke Tanzania Bara?

14.   Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa ni muhimu iwemo ndani ya Katiba. Rasimu haina asasi hii muhimu ya usimamizi na uwajibikaji. Tunarudia pendekezo letu kuwa Katiba ieleze kuwepo kwa Tume ya Kupambana na Kuzuia Rushwa na kueleza kazi zake. Tume hii iwe na uhuru wa kupeleka kesi mahakamani bila idhini ya Mkurungezi wa Mashtaka ya Umma (DPP).

15.   Katiba imejaa imani kuwa vyeti vya shule na vyuo ndiyo elimu na hekima na kwa kutumia sifa za vyeti vya elimu inawanyima haki wananchi wengi kushiriki na kuwania uongozi katika ngazi mbalimbali. Ibara ya 75(f) inaeleza sifa moja ya Rais kuwa “anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi.” Cheti cha shahada siyo kipimo kizuri cha elimu, hekima na uwezo wa kuongoza. Bill Gates hakumaliza masomo yake ya shahada ya kwanza Chuo Kikuu cha Harvard. Aliona anapoteza muda akaanzisha kampuni ya Microsoft. Kama Bill Gates angekuwa Mtanzania, Rasimu ya Katiba ingemzuia kugombea Urais kwa kuwa hana cheti cha shahada. Steve Jobs pia hakumaliza na kupata shahada badala yake alifanya masomo aliyoyaona muhimu na kuanzisha kampuni ya Apple. Hapa Tanzania sidhani kama Said Salim Bakhresa ana shahada yeyote. Taarifa iliyoko Wikipedia na gazeti la Forbes inaeleza aliacha shule akiwa na miaka 14 na akaanza biashara ya kuuza potato mix. Kama taarifa hii ni kweli basi huenda hata darasa la 8 hakumaliza. Lakini uwezo, uzoefu na elimu itokanayo na uzoefu wa kazi ni kubwa kuliko hata mtu mwenye PhD ya biashara. Mzee Bakhresa hana sifa ya kugombea Urais kwa kuwa hana shahada ya kwanza. Sina uhakika kama Freeman Mbowe ana shahada. Ikiwa hana siyo haki kumzuia kugombea Urais kwa sababu hiyo. Mwache agombee na wengine wajenge hoja hana maadili na uwezo wa kuongoza nchi. John Major alikuwa Waziri Mkuu wa Uingereza mwaka 1991 – 97 hana shahada ya Chuo Kikuu. Kuna watu wengi wenye shahada nyingi lakini hawana hekima wala busara. Vyeti vingi vys siku hizi ni vya kughushi na inawezakana kabisa usiweze kugundua kuwa vimeghushiwa. Sifa ibakie kusoma na kuandika kiswahili. Wache wapiga kura waamue kuwa elimu ya mgombea haitoshi kumfanya kuwa Rais. Sifa ya elimu ya mgombea ubunge ni kidato cha nne. Rasimu itamzuia Mzee Bakhresa hata kugombea ubunge kwa sababu hana cheti cha kidato cha nne. Kuna Watanzania wengi waliomaliza darasa la nane au la saba la zamani wenye elimu bora kuliko aliyemaliza kidato cha nne hivi karibuni. Kuna watu wengi wamemaliza darasa la 7 wana uzoefu mzuri na wana uwezo wa kuwawakilisha wananchi katika Bunge. Vigezo vya vyeti vya elimu visitumiwe kuwanyima wananch haki zao za kisiasa. Kigezo cha shahada pia kimeingizwa katika uteuzi wa Mawaziri. Watu wenye uzoefu na uwezo wa uongozi lakini hawana vyeti vya shahada hawawezi kuteuliwa kuwa mawaziri. Nastaajabu hii obsession na vyeti imetoka wapi?

16.   Ibara ya 31 inazungumzia Dini. (1) Kila mtu anao uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya imani ya dini na anao uhuru pia wa kubadilisha dini, imani yake au kutokuwa na imani na dini. Kifungu cha (5) Ni marufuku kwa mtu, kikundi au taasisi ya dini kutumia uhuru wa kutangaza dini kwa kukashifu imani na dini nyingine, kujenga chuki au kuchochea vurugu na ghasia kwa madai ya kutetea imani au dini”. Tatizo ya ibara hii ni tafsiri ya kukashifu. Imani za dini zina tofauti. Imani ya msingi ya dhehebu moja inaweza kuwa kufuru kwa dhehebu lingine na ikatafsiriwa kuwa ni kukashifu. Kuna masuala ambayo jamii inapaswa kujenga maelewano ya kuvumiliana na kuheshimiana na kukubali tofauti za imani bila kugombana. Kuliweka katika katiba inaweza kujenga chuki na ikatafsiriwa kuwa inalenga kundi fulani. Ibara na 5 imelenga kikundi au taasisi ya dini. Je vikundi ambavyo siyo vya dini vinaruhusiwa kukashifu imani na dini?

17.   Serikali ya Muungano itakuwa na Jeshi la ulinzi, Polisi na Usalama wa Taifa. Serikali za washirika zinaruhusiwa kuwa na polisi na usalama wa taifa. Inawezekana serikali ya Muungano ikaongozwa na Chama A, Serikali ya Zanzibar ikaongozwa na chama B na serikali ya Tanzania Bara ikaongozwa na chama C. Serikali zote zina polisi na usalama wa taifa wake, haitakuwa kasheshe ndani ya nchi? Sina uhakika katiba imeweka bayana utaratibu wa kuzuia migongano kati ya vyombo vya Muungano na vyombo vya Washirika.
Haya ni mapendekezo ya awali tu, mapendekezo mengine yataendelea kutolewa kwa kadri ambavyo tutazidi kuichambua rasimu hii ya katiba. Natoa wito kwa Watanzania wote kuhakikisha kuwa wanaitafuta rasimu hii bila kuchoka, kuisoma na kuielewa na kuendelea kutoa mapendekezo yao kwa tume ya mabadiliko ya katiba iwe ndiyo lengo kuu.
Kwa sababu tume imetangaza kuwa itachapisha rasimu katika magazeti ya serikali kwa maana ya HABARI LEO na ZANZIBAR LEO, tunaona kama huku ni kuififisha rasimu isiwafikie watanzania wengi zaidi.
Kuna haja ya dhati, tume ikaitangaza rasimu katika magazeti mbalimbali ya kila wiki na ya kila siku ili kuhakikisha kuwa rasimu imefikiwa na imesomwa na watanzania wengi. Na nakala zitakazobakia “returns” baada ya mauzo ya magazeti husika tume izinunue nakala hizo na izisambaze kwa utaratibu maalum mikoani na vijijini.
Ni ushauri wetu kwa Tume pia kwamba baada ya kazi kubwa waliyoifanya, wasikubali kuyumbishwa na wahafidhina wasiopenda mabadiliko wanaotokana na CCM. Tume iwe na msimamo na iangalie wananchi wanataka nini na itetee masuala ya msingi na ya maslahi ya wananchi ambayo inaona ni muhimu yakatetewa kwa maslahi ya taifa na hasa kwa kuzingatia matakwa ya wananchi.
Na mwisho, Tume ihakikishe kuwa masuala haya tunayoyashauri kwa awamu yanapewa uzito na tafakuri pana ili kuipata katiba itakayokuza uchumi imara, kuongeza ajira kwa vijana na kuinua maisha ya wananchi wa kipato cha chini.
“Mungu Ibariki Tanzania”

Prof. Ibrahim Haruna Lipumba.
Mwenyekiti,
09 Juni 2013, Dar Es Salaam.

COMMENTS

Name

Anga,12,Arusha,27,batiki,1,Burudani,447,burundani,2,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,78,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,287,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,haba,1,habar,3,Habari,7051,habari dodoma,39,habari. dodoma,32,habaria,1,hadithi,23,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,52,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,6,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,739,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,miochezo,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,376,muziki na fasheni,20,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,9,SAYANSI ANGA,12,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,17,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,urembo,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTALII,1,UTAMADUNI,4,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: MAONI YA AWALI YA MWENYEKITI WA CUF KUHUSU RASIMU YA KATIBA MPY A (NAYAFAGILIA SANA)
MAONI YA AWALI YA MWENYEKITI WA CUF KUHUSU RASIMU YA KATIBA MPY A (NAYAFAGILIA SANA)
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVc4-8DH8PHxvnEJsvd1eLbL6-bSa0Qy-VHdS6U0Wo7-a_SOcmL9wD_s8zLFYUlxqqQmiHfdw6IsWCD8lGuMVlj284Lzt2dg7YY2mmoQ4JwiMecueKKrv-Hdq9x2GTCS_f2YxL23EOhD53/s1600/IBRAHIM+LIPUMBA.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgVc4-8DH8PHxvnEJsvd1eLbL6-bSa0Qy-VHdS6U0Wo7-a_SOcmL9wD_s8zLFYUlxqqQmiHfdw6IsWCD8lGuMVlj284Lzt2dg7YY2mmoQ4JwiMecueKKrv-Hdq9x2GTCS_f2YxL23EOhD53/s72-c/IBRAHIM+LIPUMBA.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2013/06/maoni-ya-awali-ya-mwenyekiti-wa-cuf.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2013/06/maoni-ya-awali-ya-mwenyekiti-wa-cuf.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy