JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI Simu:022-2110146/2110150/2/211679 Faksi:022-2113271, Tov...
JAMHURI YA MUUNGANO WA
TANZANIA
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO
YA UFUNDI
Simu:022-2110146/2110150/2/211679 Faksi:022-2113271, Tovuti: www.moe.go.tz
NAFASI ZA MAFUNZO YA UALIMU NGAZI YA
STASHAHADA KWA MWAKA WA MASOMO 2014/2015
UTANGULIZI
Moja ya mikakati ya Wizara ya Elimu na
Mafunzo ya Ufundi katika kuandaa walimu mahiri ni pamoja na kuhakikisha kuwa
wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya Stashahada ni
wale wenye ufaulu mzuri katika mitihani ya kidato cha NNE na SITA. Ili
kufanikisha azma hii, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, itadahili wanafunzi
wenye ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi Daraja la Tatu tu.
Aidha, kutokana na upungufu mkubwa wa
walimu wa Sayansi na Hisabati wa takribani walimu 26,000 kipaumbele katika udahili kitatolewa
kwa waombaji waliofaulu masomo Sayansi
na Hisabati ili kuziba pengo hili. Nia ya Serikali ni kuwavutia wanafunzi
wengi wa masomo ya Sayansi na Hisabati. Kuanzia mwaka huu wa masomo 2014/15 wanafunzi
watakaojiunga na fani ya Ualimu kwa masomo ya Sayansi na Hisabati watagharimiwa
na Serikali kupitia mfumo wa ruzuku na mkopo. Wanafunzi watakaokuwa na ufaulu
wa Daraja la Kwanza watapatiwa Ruzuku na wale wenye Daraja la Pili na la Tatu
watapewa mkopo ili kuwasaidia katika masomo yao. Watakaofaulu mafunzo ya ualimu
katika masomo ya Sayansi/Hisabati watapatiwa ajira moja kwa moja kulingana na
taratibu za serikali.
VIGEZO
Vigezo vifuatavyo vitatumika kuchagua
wanachuo wa kujiunga na mafunzo ya ualimu mwaka 2014/15.
1: MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA
STASHAHADA: MASOMO YA SAYANSI/HISABATI NA UFUNDI: MUDA MIAKA 2.
(i)
Ualimu wa masomo ya Sayansi/Hisabati katika vyuo vya Dakawa, Kasulu,
Korogwe, Morogoro, Mpapwa, Tukuyu, Songea , Butimba, Kleruu na Monduli
Mwombaji awe
amehitimu:
Kidato cha VI kati ya mwaka
2004 na 2013 na awe na ufaulu wa ‘Principal
Pass’ mbili katika Masomo ya Sayansi
na Hisabati.
(ii)
Ualimu wa ufundi katika chuo cha ualimu Kleruu
Mwombaji awe
amehitimu:
a. Mafunzo ya FTC kati ya mwaka 2004
na 2010 kutoka Vyuo vya Ufundi, Au
b. Mafunzo ya ufundi katika
ngazi ya NTA Level 6 au sifa linganishi
(equivalent qualification) kati ya mwaka 2007 na 2013 kutoka chuo chochote cha
Ufundi kinachotambulika na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE).
(iii) Ualimu wa Kilimo katika chuo
cha ualimu Monduli
Mwombaji awe
amehitimu:
Kidato cha VI kati ya mwaka
2004 na 2013 na awe na ufaulu ‘Principal Pass’ mbili katika somo la
‘Agricultural science’ na ‘Biology’, ‘Chemistry’ au ‘Food and Nutrition’.
2: MAFUNZO MAALUM YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA KWA KIDATO CHA NNE MASOMO YA SAYANSI/HISABATI
NA ENGLISH: MUDA MIAKA 3
Ualimu wa masomo ya Sayansi/Hisabati
na English katika vyuo vya Butimba, Morogoro, Korogwe, Songea na Mpwapwa
Mwombaji awe amehitimu:
Kidato cha IV kati ya mwaka 2004 na
2013 na awe na ufaulu wa Daraja la Kwanza hadi la Tatu, na Credit mbili (yaani
A, B+, B au C) katika masomo ya Sayansi,
Hisabati na Kiingereza.
3: MAFUNZO YA UALIMU TARAJALI NGAZI YA STASHAHADA: MUDA MIAKA 2.
(i)
Ualimu wa masomo ya Sayansi Jamii katika vyuo vya Bunda, Dakawa Kasulu, Korogwe, Marangu, Morogoro, Mpwapwa,
Mtwara (K), Shinyanga, Songea, Tabora, Tukuyu.
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013
na awe na ufaulu wa kiwango cha ‘Principal Pass’ mbili
(ii)
Biashara katika vyuo vya Shinyanga na Kasulu
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013
na awe na ufaulu wa kiwango kisichopungua ‘Principal
Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja
(iii)
Sanaa za Ufundi, Sanaa za
Maonyesho, Muziki na Michezo katika chuo cha Butimba.
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013
na awe na ufaulu wa kiwango kisichopungua ‘Principal
Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja
Tanbihi: Masomo ya ‘Economics’,
Basic Applied Mathematics’, ‘General Studies’ na ‘Divinity’ hayatatumika kama kigezo cha kumchagua au kumdahili
mwombaji.
4: MAFUNZO YA UALIMU
TARAJALI STASHAHADA ELIMU YA MSINGI: MUDA MIAKA 3)
Ualimu wa Stashahada ya Elimu ya Msingi katika chuo cha Vikindu
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha IV
kati ya mwaka 2004 na 2013 wenye ufaulu wa Daraja la I Daraja la Tatu katika Mtihani
uliofanyika katika kikao kimoja.
Tanbihi: Kipaumbele kitatolewa kwa waombaji waliofaulu masomo ya ‘Mathematics’, ‘Biology’, ‘Physics’,
‘Chemistry’, ‘Agriculture’, ‘Food and
Nutrition’, ‘English’ na Kiswahili na
wahitimu wenye mahitaji maalumu.
5. MAFUNZO YA UALIMU KAZINI STASHAHADA:- MUDA MIAKA 2
Ualimu wa masomo ya Sayansi katika vyuo vya Dakawa, Kasulu, Korogwe,
Morogoro, Mpapwa, Tukuyu, Songea , Butimba, Kleruu na Monduli
Mwombaji awe amehitimu:
Mwalimu wa Daraja ‘A’ aliyehitimu Kidato cha VI na mwenye
ufaulu usiopungua ‘Principal Pass’
moja na ‘Subsidiary’ moja katika
Masomo ya Sayansi na Hisabati; na mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda
usiopungua miaka miwili.
6: MAFUNZO YA UALIMU
KAZINI STASHAHADA (SEKONDARI):- MUDA MIAKA 2.
(i)
Ualimu wa masomo ya Sayansi Jamii katika vyuo vya Bunda, Dakawa, Kasulu,
Korogwe, Marangu, Morogoro, Mpwapwa, Mtwara (K), Shinyanga, Songea, Tabora,
Tukuyu.
Mwombaji awe:
Amehitimu Kidato cha VI kati ya mwaka 2004 na 2013
na mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal
Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja katika masomo ya ‘Biology, ‘Chemistry’ na
‘Food and Nutrition
(ii)
Ualimu wa masomo ya Biashara katika vyuo vya Shinyanga, Kasulu
Mwombaji awe:
Mwalimu wa Daraja ‘A’ aliyehitimu Kidato cha VI na
mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal Pass” moja na ‘Subsidiary’ moja; na mwenye
uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.
(iii)
Ualimu wa masomo ya Elimu Maalumu katika chuo cha Patandi
Mwombaji awe:
Mwalimu mwenye Stashahada ya Ualimu fani ya
Sayansi; Au Sayansi ya Jamii na
uzoefu wa kazi ya ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili, Au
Mwalimu wa Daraja ‘A’ aliyehitimu Kidato cha VI na
mwenye ufaulu usiopungua ‘Principal
Pass’ moja na ‘Subsidiary’ moja;
na mwenye uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.
Tanbihi: Walimu wanaofundisha
watoto wenye mahitaji maalum kama wasioona, viziwi, wenye ulemavu wa akili,
n.k. ni sifa ya nyongeza (vithibitisho viambatishwe).
7: MAFUNZO YA UALIMU
KAZINI STASHAHADA ELIMU YA MSINGI: MUDA
MIAKA 2:
Ualimu wa Stashahada ya Elimu ya Msingi katika chuo cha Vikindu
Mwombaji awe:
Mwalimu wa Daraja ‘A’ mwenye
uzoefu wa kazi ya Ualimu kwa muda usiopungua miaka miwili.
MAELEZO MUHIMU
(i)
Vigezo vilivyoelekezwa kwa
waombaji wa mafunzo ya Ualimu ngazi ya Stashahada ni kwa ajili ya waombaji wa
mafunzo ya Ualimu katika Vyuo vya Ualimu
vya Serikali na visivyo vya Serikali;
(ii)
Muombaji wa chuo cha ualimu
cha Serikali anatatakiwa kuchagua vyuo visivyopungua vitano ambavyo angependa
kujiunga navyo akianzia kile anachokipendelea zaidi;
(iii)
Waombaji wa mafunzo ya Ualimu
walioajiriwa watakaopatiwa nafasi za mafunzo watapaswa kupata ruhusa (Release)
kutoka kwa waajiri wao;
(iv)
Majibu kwa watakaochaguliwa
kujiunga na mafunzo ya Ualimu katika vyuo vya Serikali yatatolewa kwenye Tovuti
za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi (www.moe.go.tz), OWM-TAMISEMI (www.pmoralg.go.tz) na NACTE
(www.nacte.go.tz)
(v)
Waombaji watakaochaguliwa
watatumiwa barua za kujiunga na mafunzo na Wakuu wa vyuo vya Ualimu
watakakokuwa wamepangwa kupitia anuani zao;
(vi)
Tangazo hili lipo pia katika
tovuti ya Wizara: www.moe.go.tz, OWM
TAMISEMI: www.pmoralg.go.tz na NACTE: www.nacte.go.tz na
kwenye ofisi za Makatibu Tawala (M) na vyuo vya ualimu;
Namna ya kutuma maombi:
a) Waombaji watume maombi yao kwa njia ya MTANDAO
(online application) kupitia tovuti zifuatazo: www.moe.go.tz AU www.nacte.go.tz
Maombi kwa njia ya mtandao yataambatana na ada ya shilingi
10,000 itakayolipwa kwa kutumia MPESA. Maelekezo ya kina kuhusu
namna ya kutuma maombi kwa njia ya mtandao yanapatikana katika tuvuti ya wizara
www.moe.go.tz
na Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi www.nacte.go.tz
Malipo ya
maombi yanaweza kufanyika kupitia MPESA kama ifuatavyo:
1.
Piga
*150*00#
2.
Chagua
4. (Lipa kwa MPESA);
3.
Chagua
1. (Weka LIPA Namba);
4.
Weka
LIPA Namba (ingiza namba 607070);
5.
Ingiza
kiasi (ingiza kiasi cha 10,000.00);
6.
Weka
Enter Reference No. ( ingiza 1234);
7.
Weka
namba ya SIRI (ingiza namba yako ya siri); na
8.
Ingiza
1 kuthibibitisha malipo.
AU
b) Barua kwa:
KATIBU
MKUU
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
S.L.P. 9121
DAR ES SALAAM (Aione: Mkurugenzi, Elimu
ya Ualimu)
COMMENTS