hadithi:Utamu wa Sukari Guru-1

Myspace Graphics Na Beda Msimbe ILIKUWA jioni sana  kwa maana kuku walikuwa wameanza kuingia katika mabanda yao huku, jua likitengeneza ...

Love Graphics for Myspace
Myspace Layouts & HTML Codes
Myspace Graphics


Na Beda Msimbe
ILIKUWA jioni sana  kwa maana kuku walikuwa wameanza kuingia katika mabanda yao huku, jua likitengeneza rangi ya hudhurungi likionesha wazi kwamba usiku unaingia.
Kila kiumbe kinachotumia mchana kwa ajili ya kazi zake za maendeleo kilikuwa kinajiandaa kurejea kwenye kiota. Katika kundi hilo alikuwapo msichana mmoja mwenye umri wa miaka 18 mwenye urembo wa haja.
Kibua mwenye urefu unaomuondoa katika maumbile ya mabinti wa Kiluguru kwa  mbali, alikuwa kiasi anakimbia kutokana na kulazimika kushuka kwa kasi katika miambao ya milima ambamo barabara imechongwa.
Kibua ambaye alikuwa  ni binti wa pekee nyumbani kwao alikuwa ameshika chupa ya mafuta ya kula ambayo wenyeji wa huku wanayaita uto, akiharakisha kurejea nyumbani.
“kibua” alisikia mtu akimuita, hakutaka kugeuka kwani maeneo aliyokuwa akiyapita ya masarawe kipindi cha jioni huwa na vituko sana.Akakazana tu akasikia tena sauti hiyo, akakazana akasikia tena, sasa akafanikiwa

kuigundua akageuka . Mvulana mmoja katika miaka yake ya 20 hivi au zaidi alikuwa anakimbia kumfuatilia.
Akasimama ajue kulikoni.
Akamfikia hima.
“Mimi naitwa Luwanda, kwetu ni Nyandira naweza kuzungumza nawe kidogo” alisema kwa Kiluguru cha kujiumauma.
Kibua hakumjibu alimkazia macho yake makubwa na kumwangalia.
“Mbona unanitazama hivyo”
Hakumjibu, akageuka na  kuelekea nyumbani kwake sasa akiwa anakimbia kidogo kidogo manake, ilikuwa lazima ale kona ya milima kabla jua halijazama kabisa. Mvulana akaona atalazimika nay eye kuvuta hatua angalau

apate miadi
“Kibua mbona unafanya shida katika hili”
“Unanichelewesha nikusaidie nini”
“Kama hutajali,napenda kuzungumza nawe”
“Kuna shida? Haya zungumza”
“Punguza mwendo basi”
“Siwezi nimechelewa na mama yangu atanipa shida bure”
“Mkubwa wewe. Nitakusindikiza”
“Mimi?Wewe unanijua mimi?”
“Sikujui ndio maana nataka kukujua.Nitakupeleka. Nizungumze nawe kidogo”
“Kunipeleka huwezi. Lakini kama una shida fika kesho saa za mchana katika jabali la Mikongowe nitakuwa nachota maji”
“Kwani hatuwezi kuzungumza hapa”
“Unaelewa au?”
“Basi Kibua mimi si mwenyeji huku kwenu”
“Kama hu mwenyeji umenijuaje?”
“Nimeelekezwa tu.”
“Kama umeelekezwa, rejea ukaelekezwe tena”
Alikuwa anakaribia kona,akaikata kisha akasema:”usipende kufuata watu usiowajua wewe”
Akasimama akaduwaa.
Alifika nyumbani na  kumkuta mama yake akimsubiri.
“Mhh Kibua ushaota mapembe. Yaani hapa na Msewe ni safari ya kwenda Morogoro au Yule mwanaharamu wako amerudi”
“Mamah nini tena unazungumza?”
“Nasema hivi kwanini umechelewa”
“Mafuta nimeyapata mbele zaidi mama sio Msewe!”
“Mwanangu taratibu!” alisema mama.
Kibua alienda zake jikoni na kuanza kuandaa chakula cha jioni akamshangaa mama yake na kelele za mwanaharamu wake. Mwanaharamu wake! Akaguna.
Alipomaliza kupika, akatenga chakula akamuita mama yake wakaenda kula. Hawakuwa na cha kuzungumza siku ile kwani Kibua alimuogopa mama yake,kwani mama yake akishaanza salamu za huyo anayemuita mwanaharamu

wake, huwa akijibu hakuchi, maneno mpaka anakasirika.
Mama yake alikuwa anamzungumzia mvulana aliyemtoa ushamba wakati akiwa darasa la saba ambaye ameenda mjini na wala hajaleta barua tena ingawa alisema kwamba atarejea kumuoa.
Amekataa wachumba wengi, kiasi cha mama yake kukereka na kumwambia wazi kwamba moyo wake ulikuwa umekufa kwa mtoto wa Peter aliyekuwa anakaa Midolowela. Miaka imepita na kwa kuwa hakupata nafasi ya

kwenda sekondari alibaki nyumbani akimsubiri mchumba aliyeondoka.
Baada ya kuona kwamba mchumba mwenyewe harudi alijaribu hapa na pale akaona kila mahali pachungu, pana mwiba na zaidi wavulana waliopatikana walikuwa na haraka sana.
Haraka zao zikawa haja zao na kila anapobaini kwamba wana haraka aliwaacha, akaenda kujilalia
Agosti ya mwaka 1970 saa nne asubuhi, akiwa nyumbani kwake anaota jua  alifika msichana mmoja jirani.
"Dada kuna mtu yupo  kule kisimani kwenye jabali anasema anaitwa Luwanda ana ujumbe wako"
"Luwanda? Unasemaje Chilua"
"Anasema anaitwa Luwanda anatoka huko sokoni" akakumbuka
"Asante mdogo wangu"
Alitoka pale na kuelekea kwenye lile jabali.
Alizunguka  kibonde na kumuona mvulana mmoja aliyempa mgongo, akadhani ndiye aliyemsimamisha jana.
Luwanda alionekana kujiketia kiuvivu kabisa katika jabali hilo kubwa.
Katika eneo lile lenye upweke mkubwa, alionekana kuigeukia mimea inayochoma ambayo kwao walikuwa wakiita siru.
hakujua kufika kwa Kibua pale, kwani mawazo yake yalikuwa yanamtazama mjusi mmoja wa rangirangi akipita kivivu katika mimea ile ambayo ukifanya masikhara ikakuchoma, basi mguu wako ukipona nenda katambike.
Yule mjusi wa rangi alimrukia mdudu mmoja na kummeza, akamshutumu kwa kummeza mdudu yule, mjusi alitoa ulimi wake nje akajilamba, kama anayemcheka.
Ahh! mjusi yule alimtibua na mimacho yake na kujilamba kwake baada ya kumuua mdudu. Aliamua kunyanyuka kuona kama mtu wake anakuja au angoje zaidi.
Alinyanyuka kivivu kabisa huku akiangalia chini ya milima akatazama mji wa Kilima kutoka pale Mikongowe, alipogeuka macho yake yakakutana moja kwa moja na ya Kibua ambaye alikuwa amejaza uso wenye bashasha.
"Nimekuja. Habari za asubuhi Luwanda"
"Nzuri.Umenishtua sikukusikia ukija"
"Mimi si mchawi Luwanda  wewe mwenyewe ulikuwa umejizamia wapi sijui. mjusi alikuwa anakuchanganya, marangirangi yake hayo.Ninapokuwa nimechoka kabisa huja hapa jioni kuona mijusi inavyoota jua la jioni.karibu

nimefika nina muda mfupi sana mama yangu atarudi"
"Nimefika hapa tuzungumze" aliingiza mkono mfukoni akatoa ua la mbaazi.
"Ua la mange? una lako jambo"
 “Una mwili mzuri!”
“Hauwezi kuushindana wa kwako”
“Hapana una uzuri ambao mimi siwezi kuwa nao.”
“Nambie Luwanda umekuja hapa kunambia hilo?”
“Nimekutunuku”
“ Luwanda hii si habari mpya na mimi si mtu mpya kuambiwa hivyo nawe”
“ Kweli kabisa ila ni hadithi ndefu,waweza nisikiliza .”
“Sawa.”
 “Mimi nafikiri tuketi ndio tuzungumze”
“Hapana. Nina kazi nyingi pale na nina muda mfupi sana wa kukusikiliza”
“ sawa”
“Tunazungumzia kitu gani hasa”
“Labda nijitambulishe.Mimi naitwa Luwanda, mtoto wa John Nyau”  alipomtamkia jina akataka kukimbia,mzee anayeogopwa sana maeneo ya Nyandira.
“Naona umeshtuka.Sikuja kwa mabaya.Nimekuja kwa heri kutaka mkono wa heri”
“Nambie wewe ndiwe mtoto wake wa Dar wanayejivunia?”
“Unataka kujua ukweli?”
“Ndio” macho yakiwa yamemtoka.
“Hapana.”
“hapana nini?Duhh, haya nambie”
“Nasikia watu wanasema mzee mchawi halafu ananiringia mimi.Najua wanavyosema lakini nataka nikuthibitishie ni upuuzi. Halafu mimi sikai dar”
 “Kwanini”
Hakumjibu akamwangalia.
“Nisaidie kitu hiki.Uliniona wapi?”
“Nilikuona jana ukiulizia mafuta pale. Nikasema dahh bonge la mtoto”
“Kisha”
“Sikia kibua sikuja hapa kupoteza wakati.Nataka kujua kama nina nafasi”
“Nafasi.Sisi hatupangishi bwana”
“ Mbona nimeambiwa, huna shida”
“Mhh nimekuwa jamvi la wageni”
“unasemaje?”
“Nimekuwa jamvi la wageni”
Hakusema na kweli ndicho alichoambiwa.
 “Unanijua mimi kikwelikweli”
“Labda sikujui”
“mimi sukari guru, unaijua sukari guru wewe”
“kama nikijua?”
“Huwezi kuila. Sikia umekuja hapa kunitongoza.Nikuambie kwamba mimi ni sukari guru huwezi kuipikia chai lakini unaweza kuila kwa saladi.Wewe unataka chai au saladi.?”
“Asubuhi sana kula saladi”
“Kwa hiyo unataka chai.Sijawahi kuambiwa hata na mwanaume mmoja duniani hasa, za dizaini zenu kuhusu sukari guru na saladi.Chai ina masharti yake. Nenda sikufai kwa kula wala kulumwagia.”
Akamtazama macho makavu kabisa.
“nakutaka kwelikweli”
“Wewe mtoto mzuri usitake kulala na majamvi huwezi kuyajua kama yanachawa au kunguni”
“nikuambie neon”
“Sema”
“ Sijaguswa nitakuwa zawadi kwako. “
Akacheka.
“Hili nalo linaongeza sababu nyingi zaidi za kukukataa.Sitaki washamba , sitaki kufundisha mtu”
 “Nataka nikuoe ili unifundishe”
“Nenda kafundishwe kwanza ukishakuwa mwalimu nitakuangalia”
 “Kwanini?”
“Sitaki kutoa wanafunzi wanaopita walimu halafu wende kufundisha wengine”
 “Kibua masikhara hayo”
 “Mimi sihitaji mume,kama wewe ndiwe unataka kuwa mume poa sana kwanza unapendeza pili unaonekana kichwani wamo,yaani naomba ufikirie tu kwenda kuoa kwingine usitafute maradhi usioweza kuyatibu”
 Itaendelea

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: hadithi:Utamu wa Sukari Guru-1
hadithi:Utamu wa Sukari Guru-1
http://www.fillster.com/images/graphics/186c.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2014/09/hadithiutamu-wa-sukari-guru-1.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2014/09/hadithiutamu-wa-sukari-guru-1.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy