SIKIKA:Serikali isikwepe kulipa malimbikizo ya madeni MSD kuokoa maisha ya Watanzania!

Taarifa kwa Vyombo Vya Habari, 30 Octoba 2014 Sikika imesikitishwa na tamko lililotolewa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Ja...




Taarifa kwa Vyombo Vya Habari, 30 Octoba 2014



Sikika imesikitishwa na tamko lililotolewa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, kuhusiana na kushindwa kwa vituo vya huduma za afya kununua dawa MSD kutokana na kuongezeka kwa deni. Ni wazi kuwa waziri hajalipa tatizo hili uzito unaotakiwa na kutambua kuwa baadhi ya wagonjwa wanaweza kupoteza maisha kutokana na tatizo hili.

Sikika inatambua kuwa, mapato yatokanayo na uchangiaji katika huduma za afya ni moja tu ya vyanzo vinavyotumika katika kuongeza upatikanaji wa dawa na vifaa tiba nchini. Na pia inatambua kuwa chanzo hiki pekee hakiwezi kuziba pengo kubwa la ufinyu wa bajeti ya dawa na vifaa tiba muhimu ambao hauendani na mahitaji halisi. Kwa mfano, makadirio ya mahitaji ya dawa nchini kwa mwaka wa fedha 2014/15 ni shilingi bilioni 500 lakini bajeti iliyopangwa na kupitishwa ni shilingi bilioni 70.5 ambayo inakidhi mahitaji kwa asilimia 14 tu!

Sikika inapenda kuikumbusha Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kuwa, takribani asilimia 75 ya wagonjwa  wanaopata huduma katika hospitali za Manispaa wapo katika kundi la msamaha wa huduma za afya. Kundi hili linahusisha wajawazito, watoto chini ya miaka mitano, wazee, watu wenye magonjwa sugu, watu wasiojiweza pamoja na watu wenye ulemavu. Hii inamaanisha kuwa Serikali inategemea asilimia 25 tu ya wagonjwa wanaoweza kuchangia huduma  kama chanzo  kikuu cha fedha za dawa zitokanazo na uchangiaji. Serikali inatakiwa kuwajibika katika hili na sio kuwatupia mzigo wananchi wachache.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii atambue kuwa, kuzitaka hospitali kulipa deni la MSD kwa kutumia fedha za uchangiaji badala ya kutumia fedha hizo kununua dawa kutokana na ufinyu wa bajeti, ni chanzo cha kuzifanya hospitali hizo kuendelea  kukopa zaidi na hivyo kuendelea kukuza tatizo badala ya kutafuta suluhu. Tunamkumbusha kwamba hili ni tatizo linalotokana mfululizo wa upangaji wa bajeti finyu kwa makusudi. Baadhi ya hospitali hizi zimekuwa zikitumia fedha za uchangiaji kununua dawa lakini bado zina madeni. Kwa hiyo, agizo la Waziri halitakuwa na tija katika kutatua tatizo hili kwa sasa.

Hii sio mara ya kwanza kwa Wizara ya Afya kuzitaka hospitali kupeleka MSD asilimia 50 ya mapato yao uchangiaji. Agizo hili limekuwa likijirudia tangu mwaka 2012 bila ya kuwa na usimamizi katika utekelezaji na ufuatiliaji. Kwa mfano, mwezi Julai 2014, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii aliziagiza hospitali zote kupeleka MSD asilimia 50 ya mapato yao. Kwa kuwa agizo hili limekuwa likishindwa kutatua tatizo la upatikanaji wa dawa, tulitarajia mbinu mbadala kutoka serikalini.

Sikika ingependa pia kujua ni jinsi gani hospitali ya Taifa, za rufaa na maalumu ambazo zinachangia asilimia kubwa ya deni (67%) katika kundi la madeni ya vituo vya huduma za afya zitalipa deni hilo, kwani agizo la waziri lililenga hospitali za wilaya na mikoa pekee. Vile vile, tungependa kujua Wizara imeweka mipango gani katika kulipa deni lake ambalo ni zaidi ya asilimia 70 ya deni lote ambalo MSD wanadai. Deni hilo la Wizara linatokana na gharama za kugomboa, kuhifadhi na kusambaza bidhaa za miradi misonge (vertical programs).


Mbali na hilo, tamko la Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kwa Umma la tarehe 27 Oktoba 2014 linaeleza kuwa, Serikali imekuwa ikilipa Deni la MSD kwa awamu. Hata hivyo, Waziri hakuweka wazi kwamba pamoja na kulipa kwa awamu, deni limekuwa likiongezeka kwa sababu serikali inalipa kiwango kidogo na kukopa kiwango kikubwa. Kwa mfano, mwaka 2013 deni lilikuwa kiasi cha Tsh. bilioni 76.4 lakini kufikia Septemba 2014 deni limekuwa na kufikia kiasi cha Tsh. bilioni 102 ingawa serikali ilifanya malipo ya Tsh. bilioni 10 .

Sikika ingependa kupata ufafanuzi kutoka kwa Waziri wa Afya na Naibu Waziri wa Wizara ya Fedha, Mh. Mwigulu Nchemba ambaye hivi karibuni alinukuliwa na baadhi ya magazeti akisema kuwa kiasi cha fedha zilizotolewa kwa ajili ya dawa katika mwaka 2013/14 ilikuwa Tsh. bilioni 47 lakini ni Tsh. bilioni 7 tu ndizo zilitumika katika kununua dawa. Sikika, pamoja na watanzania wote, ingependa kujua ni wapi  fedha hizi zimepelekwa na ni kwa sababu zipi  hususan katika kipindi hiki cha uhaba wa dawa na vifaa  tiba katika vituo vya huduma za afya.

Sikika pia ingependa kutoa ufafanuzi kwa umma kwamba misaada iliyositishwa na wafadhili ni kwenye bajeti ya kuu tu (General Budget support) na si kwenye mfuko wa pamoja wa sekta ya afya (Health Basket Fund). Kwa kipindi cha Julai-Septemba 2014, zaidi ya Tsh bilioni 20 zilitolewa na wafadhili kwa ajili ya kusaidia halmashauri zote nchini ambapo kwa kawaida, theluthi moja ya fedha hizo inapaswa kutumika kwa ajili ya manununzi ya dawa na vifaa tiba muhimu.

Sikika inatambua juhudi za serikali kujumuisha sekta ya afya katika mpango wa matokeo makubwa sasa (BRN), ambao kwa kiasi unaweza kuchangia kupunguza uhaba  sugu wa  dawa na vifaa tiba katika vituo vya huduma za afya vya umma. Hata hivyo, mpango huo utaanza kutekelezwa rasmi mwaka wa fedha 2015/16, hivyo hauwezi kutatua tatizo la sasa la dawa. Waziri atambue kwamba wagonjwa wanateseka na pengine baadhi kufariki kwa sababu ya ukosefu huu wa dawa na vifaa tiba.

Mwisho, Sikika inaitaka Wizara ya afya na Ustawi wa Jamii kuchukua hatua za haraka katika kutatua tatizo hili sugu la ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika vituo vya huduma za afya vya umma. Uhaba wa dawa unawanyima wananchi kupata haki ya huduma bora za afya ambazo huweza kusababisha vifo. Serikali inapaswa kulipa deni la MSD na kuwezesha upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kwa dharura na haraka. Sio haki kwa serikali yoyote kuacha wananchi wake wakiteseka ama kupoteza maisha kutokanana sababu zinazoweza kuzuilika.
Mr. Irenei Kiria,
Executive Director of Sikika,
P. O. Box 12183 Dar es Salaam,
Tel: +255 222 666355/57, Fax: 2668015, Email: info@sikika.or.tz, Twitter: @sikika1, Facebook: Sikika Tanzania, Website: www.sikika.or.tz

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: SIKIKA:Serikali isikwepe kulipa malimbikizo ya madeni MSD kuokoa maisha ya Watanzania!
SIKIKA:Serikali isikwepe kulipa malimbikizo ya madeni MSD kuokoa maisha ya Watanzania!
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdQTwVAck3M61NXu_5zY_7hpRFvYsi7s1s_gpmlNbW2IDoLD_iXICaHpDuAJJmnYcHR4ZuGRhhaSwqcov-nHGVz7b8XnBAepFDiHDC9nX1ZyDHdT8xmybhdB_Xp-pcmT8IELVCza8QRmE/s1600/irenei.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdQTwVAck3M61NXu_5zY_7hpRFvYsi7s1s_gpmlNbW2IDoLD_iXICaHpDuAJJmnYcHR4ZuGRhhaSwqcov-nHGVz7b8XnBAepFDiHDC9nX1ZyDHdT8xmybhdB_Xp-pcmT8IELVCza8QRmE/s72-c/irenei.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2014/10/sikikaserikali-isikwepe-kulipa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2014/10/sikikaserikali-isikwepe-kulipa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy