Naam ugomvi kati ya Kibua na Semie umeshamalizika na kwa maneno yake mwenyewe Kibua amekubali yaishe.Je kuna jipya gani litazuka hasa...
Naam ugomvi kati ya Kibua na Semie umeshamalizika na kwa
maneno yake mwenyewe Kibua amekubali yaishe.Je kuna jipya gani litazuka hasa
ukizingatia kwamba Kibua anajua baba yake amemkataa. Kumbuka safari iliyopita
kuliletwa kondoo pale nyumbani kwa akina Kibua.Ambatana name kwenye simulizi
hili lenye mihemko ya mapenzi.
KIBUA aliporejea nyumbani kutoka kwa akina Semie alikuwa
amechoka sana.Hii ilitokana na ukweli kuwa alikuwa ametumia nguvu za ziada
kumwadhibu Semie na mume wake.Ni matumizi ya nguvu hizo zilimfanya arejee
nyumbani pale kimya kimya, akamsalimia mama yake na kwenda kulala bila kuoga.
Katikati ya usiku ndoto zilimwamsha, zilikuwa si ndoto
rafiki akakumbuka kwamba katika maisha
yake hajawahi kulala na janaba na ndio maana akili ilimcheza, akatoka akaenda
jikoni akakuta mama yake ameinjika maji katika chungu na vijinga vya moto
vilikuwa bado vinawaka.Asingeliweza kulala hadi asubuhi, kwani mwili wa Kibua
ulikuwa si wa kawaida, uligombana mno na uchafu.
Akachukua maji yale akayachanganya vyema na kuelekea uani,
mwanga wa mbalamwezi ulimpa kampani kubwa akaamua kujiogea nje kwani hakuna
haja ya kwenda bafuni katika usiku huo mkubwa.Akasaula nguo zake akazitupa
upenuni, akaanza safari ya kujiogesha, ilikuwa safari ndefu na aliifanya kwa
utaratibu sana.
Pale alipokua akiogea palikuwa karibu sana na chumba ambacho
mama yake analala, zile kelele za maji zilimwamsha bi mkubwa Yule.Huku
akipepesuka kwa usingizi alikwenda
kufungua mlango wake akatoka nje na kuona mlango wa nje umesindikwa
tu.Akaufungua na kumuona mtoto wake akioga kwa taratibu sana, hakutaka kumshtua
kwani alionekana kama vile yuko mbali sana. Kila kata ya maji ilionekana kuwa
na kusudio fulani katika mwili wake.
Alimsubiri amalize, lakini ilionekana kwamba itamchukua muda
mrefu sana. Alipoona sasa anakwenda kasi akajua kwamba akili imemrejea na
akaamua kumuita.
“Kibua”
“Unasemaje mama” alijua ni mama yake.
“mbona chilo chikulu (usiku mkubwa)vipi mwanangu?”
“mama nilirudi nimechoka sana, nikasema nijipumzishe kumbe
ndio nimelala.Nimeshtuka nikiwa naota ndoto mbaya sana,nikagundua ahaa kunbe
sijaoga ndio naoga mama”
“umechukua muda mrefu sana mama kuoga”
“Ha mama yaani kumbe muda wote huoupo unaniangalia tu?Nimekuwa
mwanasesere?”
“Kwangu mimi wewe ni mwanasesere, kwa wengine wewe ni mtoto na kwa wanaume wewe ni mwanamke.Haya tuache hayo.Nilikuwekea ugali na mboga ya beze ikichanganyika na konge.Konge lakini lipo peke yake .Utahitaji kula si vyema kulala na njaa, bado sijafa.Kabla sijasahau kesho kuna ugeni hapa nyumbani usiondoke.”
“Kwangu mimi wewe ni mwanasesere, kwa wengine wewe ni mtoto na kwa wanaume wewe ni mwanamke.Haya tuache hayo.Nilikuwekea ugali na mboga ya beze ikichanganyika na konge.Konge lakini lipo peke yake .Utahitaji kula si vyema kulala na njaa, bado sijafa.Kabla sijasahau kesho kuna ugeni hapa nyumbani usiondoke.”
“Enhee kuna ugeni gani mama wa mwanasesere?”
“Kwani lazima uujue mama”
“Kwani lazima uujue mama”
“kweli kabisa si lazima niujue, lakini si unanijua mwanao
ninapokuwa na mambo yangu hakafu kuna vitu ambavyo si vya lazima kuvifanya?”
“Najua”
“Haya”
“Sikia Kibua nadhani hapana usitoke.Nadhani ni vyema
ukabaki.Nadhani kuna mambo baba yako anataka kusema nawe”
“Achana naye mama.Nimeenda kanizodoa, sina shida naye. Nimemjua,nimemwelewa.
Yangu kuanzia sasa ni macho tu”
“hapana mama nadhani kuna kitu anataka kukifanya kwako.Kaletwa
mnyama hapa ni dalili kwamba baba yako anataka kupata nawe.”
“Hapana mama nilimwambia kwamba kama yeye si baba yangu basi
amruhusu Siri alete posa, hiyo ni posa mama”
“Haiwezekani si posa! Wale ni wanyama wa tambiko walioletwa
hapa”
“Ndio mama, tambiko la kutenganisha ukoo,sijui nitazaa Mtitu
mimi Dah”
“kama hilo sitakubaliana nalo”
“Ndio maana nikasema wala usimsikilize alishamaliza mambo
yake”
Mama Kibua alimtazama mwanae akamuona ametulia sana.Akajua
kwamba sasa mwanae huyo wa pekee ataanza kufanya maamuzi kama aliyoyafanya yeye
na lile lilimpatia shida, hakuyapenda na hajawahi kupenda maamuzi yale.
“Sikiliza Kibua”
“Unasemaje mama?”
“Nenda kale, kisha kalale nina hakika mpaka kesho utajisikia vyema sana. Wala usiondoke tuwangoje tuwasikilize”
“Nenda kale, kisha kalale nina hakika mpaka kesho utajisikia vyema sana. Wala usiondoke tuwangoje tuwasikilize”
Hakusubiri amjibu aliondoka kurejea chumbani kwake akimwacha
Kibua akipiga mwayo huku naye akienda jikoni kupata chakula kama mama yake
alivyomshauri.
XXX
Huku Dar es salaam mambo hayakuwa kama vile yalivyokuwa
yakitarajiwa kuwa.Mtotobaba mwenye nyumba kama baba mwenyewe alivyokuwa alianza
kuchongeka. Na kikubwa alichokuwa anakifikiria ni jinsi alivyomkosa Kibua ,
mwanamke wa haja ambaye alidhani kwamba anafaa sana kuwa mtu wa kumkosha katika nafsi yake ya upweke
kwa jinsi binadamu walivyoumbwa.
Wakati wa mtoto anachongeka akiakili na kimwili kwa ajili ya
Kibua na hasa akitafakari maneno ya baba yake, kwamba Kibua ni mama yake mdogo na hana la
kufanya,baba mtu naye aliona miezi minne kama mwaka. Hali haikuwa njema ingawa
mkewe kwa mara ya kwanza alianza kuwapo nyumbani kwa muda mwingi sana kuliko
awali na alikuwa akijitahidi kupika walimu mtamu ambao yeyhe alijua kabisa
ameukozesha nazi.
Mama alijitahidi sana kuhakikisha kwamba tui analotengenezea
wali limekoza na lipo shatashata lakini mzee mzima kila akila wali ule alikuwa
kama vile anataka kuutema.Ilifika siku akaamua kumuondolea uvivu na kumchana
laivu.
“Enhee nambie kanali wa jeshi, komando” akajenga uso wa
tabasamu kisha akaendelea siriazi kidogo;” kuna tatizo gani siku hizi mbona
kila ukila unazidi kunyong’onyea?”
Alimtazama, yale macho ambayo baba mwenye nyumba anayajua, ya
baridi. Hakumuelewa.
“Sina tatizo lolote lile kwani vipi?”
“Asiyekujua atasema upo sawa, sisi wengine tunakujua.Tueleze
baba chanja tatizo nini?”
“sina tatizo mama”
“Kweli kabisa?”
“Ndiyo”
“Au ndio mawazo ya Kibua.Yule mtoto kakupa nini hasa?”
“ushaanza”
“Wala Mwaya!Lakini dawa ya maradhi yasikuue kwanza ni kuyakubali, kisha kutafuta
dawa yake, kuyakataa wakati yanakutesa si sahihi.Nataka kusema hivi baba chanja
dawa ya maradhi yako ni kukiri, usipofanya hivyo utakufa utaacha kila kitu
pamoja na Kibua mwenyewe”
“unanitaka nini?”
“Mimi nauliza Yule mtoto kakupa nini mpaka unachanganyikiwa?”
“Mbona hivyo mama watoto?”
“kuna mawili ama wewe ni mjinga ama hutaki kukubali hofu yako.Utakufa kw akihoro mpenzi”
“kuna mawili ama wewe ni mjinga ama hutaki kukubali hofu yako.Utakufa kw akihoro mpenzi”
“kama hakuna maongeze hapa sebuleni ila hayo, basi naomba
twende tukalale”
“huwezi wewe”
“Kwanini siwezi”
“Nikuambie ukweli?”
“Nambie”
“Nambie”
“Sasa hivi staili na miondoko ni ya Kibua. Umekwisha
wewe!Hufurukuti”
“Mhh”
“Mhh nini?Kila siku ukikolea unaliita jina lake na halafu
unasema hivi..” akaaenda kumnong’oneza sikioni.
“Sio kweli”
“Ukweli ni nini laazizi?Nambie basi”
“Ninachotaka kusema unachosema si cha kweli mimi si mvulana
bana”
“Unaona sasa?”
“Ninaona nini”
“Ninaona nini”
“mimi nishampoteza mpenzi na mapenzi yako kule.Siku zote hizi
unajisikia kuniamrisha kama jeshini fanya hivi, kaa hivi kama unapiga picha ya
mmodo khaa,”
“na wewe unafanya”
“na wewe unafanya”
“Nifanyeje na bwana mkubwa kesha jenga mazoea.Tusipofanya si
tutaharibu picha nzima”
“Mazoea?Mazoea gani”
“Hivyo unavyoagiza”
“Sikiza…” akakatwa kauli.
“Nisikilize mimi babachanja.Simchukii mtoto Yule! Lakini jinsi
unavyokwenda na damu changa ile utatuletea majanga nyumba hii! We endekeza tu”
akanyanuka kuelekea chumbani.
Hakujibu lilikuwa limepigwa chini ya mkanda mzee mzima ilibidi atulie kusikilizia maumivu.Akagundua kwamba hawezi tena kuficha mkewe alikuwa anamjua alipolala na alipoamkia.
Hakujibu lilikuwa limepigwa chini ya mkanda mzee mzima ilibidi atulie kusikilizia maumivu.Akagundua kwamba hawezi tena kuficha mkewe alikuwa anamjua alipolala na alipoamkia.
Itaendelea
COMMENTS