IRENE SANGA: mcheza sinema,muigizaji,mwandishi na mwanamuziki

MSANII mwenye kariba ya kimataifa Irene Sanga anasema bado hajaachana na sanaa na kwamba zipo kazi nyingi amezifanya na nyingine zipo kati...


MSANII mwenye kariba ya kimataifa Irene Sanga anasema bado hajaachana na sanaa na kwamba zipo kazi nyingi amezifanya na nyingine zipo katika hatua mbalimbali na kwamba mashabiki wake watarajie kazi njema na zenye maana katika maisha yao. Beda Msimbe  amefanikiwa kuzungumza anaye Msanii huyu ambaye kwa sasa anatamba na mchezo wa jukwaani wa Africa Kills Her Sun ambao tayari umeoneshwa nchini marekani na Uganda. Fuatilia mahojiano haya:


SWALI:

 Ghafla haupo katika ulimwengu wa muziki wala sinema nini kimetokea? au majukumu ya uzazi yamezidi?
JIBU:
Hapana watoto wameshakuwa wakubwa ,mimi nafanya sanaa kama kawaida. Siku hizi naandika filamu. Nimeandika, Mikono salama ameprojuzi JB, nimeandika Kutakapo Kucha ameprojuzi Malalo na kuchezwa na Kitime; nimeandika Nyuma ya Pazia anaprojuzi Mtitu na ninafilamu inaitwa Mjomba ndio naendelea kuiandika pamoja na Nguvu ya Msamaha ipo katika drafti ya pili. Pia nina projekti ya Afrika inaua mwangaza wake ambayo tutaanza kuifanyia mazoezi kw amaonesho ya hapa nyumbani .Mara ya kwanza tulionesha Uganda Novemba mwaka jana
Aidha naandika  telebision series za Ubongo kids na kila kilenga. Pia nimeandika skripti za Babu Mbuyu za watoto bado zipo njiani kutoka chini ya kampuni ya Tanarea.

SWALI:
 Kumbe mwenzangu unahangaika katika sanaa mimi nadhani umetulia.
JIBU:
kweli kaka nipo sana na naandikaa vitu vingi mpaka muziki. kama unavyojua muziki upo damuni.

SWALI:
Naam naelewa mashairi yako huwa yanakuwa na moto mkali hasa katika jamii. Lakini kimya kirefu.
JIBU:
Si kirefu hivyoo.Ninamiziki miwili ipo Irie Production bado sijaimaliza ,mmoja unaitwa Enjoy mwingine unaitwa Africa Bara langu.Kiufupi bado nafanya sanaaaaaa tena sanaaaaa.

SWALI
Mengi tumeyaona lakini sikuwa najua kwamba wewe umo namna hii ndio maana nikauliza. Kuna vitu watu wanavifanya halafu wanapozungumza hawasemi kuhusu wamepata wapi vitu hivyo ili watu wajue kwamba katika sanaa mtu kutengeneza chakula kilichoandaliwa na mwingine. Haya reponse (Muitikio) ya filamu ulizoandika ( Je ni simulizi au andiko lenyewe ) ipi imeleta heshima sana mjini .Na hapo hapo nikuulize kwenye muziki tutarajie kama Mjomba au safari hii mapenzi hewani?
JIBU:
Mvuto uko katika Mikono salama.Watu wengi walinipigia simu na kusema wameipenda. Kutakapokucha pia, lakini unajua sisi waandishi huwa hatujulikani sana,watanzania hawana utamaduni wa kusoma washiriki ,filamu ikiisha tu televisheni huzimwa na wasanii wakisifiwa hawana utamaduni wa kumsifia mwandishi nadhani ni Tanzania tu ambayo ipo nyuma kwa vitu kama hivyo,watu hawapendi kumpa credit, mtu sijui ilitokea wapi hata sijui siku zote anayepika hasifiwi ila aliyenenepa baada ya kula (anacheka).Kitu kingine ni Nyuma ya pazia ninadhani itakuwa nzuri zaidi kwa sababu napenda sana kuzungumzia habari za ukweli na zinazoendelea nchini kwetu,hiyo inahusu rushwa na uadilifu kazini

SWALI:
Naam kwahiyo mwaka huu ni mwaka wetu.Haya kampuni yako inaendeleaje?
JIBU:
Namshukuru Mungu inaendelea vyema ,japo changamoto ni nyingi,kufanya kazi bila meneja ni ngumu sanaaaa

SWALI:
Hata mimi naamini hivyo lakini kwanini humtafuti meneja?
JIBU
Sijui nianzie wapi kila mara na wish (natamani) ningekuwa naye kwa sababu kazi zote hizo nilizo kwambia hakuna hata moja nilioitafutia wateja bali watu wananitafuta na ninajisikia vibaya kukaa na idea ( mawazo)  huku  sina wa kusaidia kuzipush (kufikia walengwa) ,unajikuta umekaa tu huna cha kufanya wakati nilitakiwa kuwa busy(anacheka).

SWALI
Lazima kuna kasoro. Ninavyokujua wewe ungelikuwa na nafasi kubwa ya kumpata mtu wa kufanya naye kazi au watu wa hapa wamejawa na Longolongo ?
JIBU
Kaka Msimbe  ukipata meneja niambie nikae naye tuweke miradi hadharani,namiss sana sanaa ya jukwaani nataka kuifanyia mkakati sana

SWALI:
Je kama leo mtu angelikuuliza una miaka mingapi katika sanaa na nini umekiona Tanzania ungelisema vipi?Yaani kama kioo msanii wa tanzania anakosa kitu gani
JIBU
Nina mika 15 katika sanaa. Ninavyoona mimi sanaa ya Tanzania imeingiwa na dosari ya kibiashara kuliko ubora. Kila mtu ni msanii,kila mtu anasaka pesa ,ukisimamia ubora inakula kwako.Sanaa mbovu zimejaa mtaani huku zikinunua airtime ili ziwe maarufu hasa upande wa muziki,upande wa filamu bila skendo hujawa msanii,utandawazi uhuru wa vyombo vya habarii umeifikisha sanaa hapa,tofauti na wenzetu nchi jirani mfano Kenya na Uganda pamoja na utandawazi sanaa yao inaubora sana.

SWALI:
ulizungumzia mchezo wa Afrika inaua Mwangaza wake, je hauna mpango  hasa wa kuonesha kwa watanzania katika matamasha makubwa ya sanaa?
JIBU:
Niliongea na Dk Martin Mhando wa tamasha la nchi za Majahazi nahisi naweza kuperfome Africa kills her sun ZIFF bado tunaangalia jinsi ya kufanya.

SWALI:
Hii naipenda zaidi ya kuonesha ZIFF, kuna haja kubwa ya sisi kuona kazi za wazawa wa nchi hii kwani wana mengi wanayasema.sasa nikuulize kuhusu msimamizi meneja anatakiwa awe na sifa zipi au meneja anatakiwa aweje, sifa zipi na yukoje.
JIBU:
Meneja anatakiwa auze mawazo kwa wadau mabalimbali wa sanaa,mfano tukifanya mazoezi ya mchezo ajue watazamaji watatoka wapi na kuwasaka na kutangaza kwa nguvu zote:kuwasiliana wa wafanya biashara ili waweze kuwekeza katika sanaa yetu na kadhalika. Tunafasi ndogo sana imaana tunahitaji mameneja ili wapigekelele watu waje waone ukweli ni kwamba hakuna sanaa nzuri kama ya jukwaani hasa ikuchanganywa na muziki, ngoma na ucheshi .

SWALI:
Swali hili ni la kizushi .Ulizaliwa wapi, ulisoma wapi, ulijifunza sanaa wapi, Nani role model, na kubwa zaidi mashabiki wako wategemee nini?
JIBU

Nimezaliwa hapahapa Dar, nimesoma Iringa girls na Ruvu ,nimesoma sanaa Chuo cha Bagamoyo na warsha katika nchi mbalimbali. Nampenda sana Kalola Kinashe,wanaonikubali waendelee kunikubali bado nakaza buti katika sanaa sijakata tamaa.

SWALI
bnado hujasema miaka yako?

JIBU
kaka beda nawe! Wanawake hatutaji miaka ya kuzaliwa ila kwetu Makete ,Mwenge ndio hasa nilizaliwa Ocean road hospital .
mwisho

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: IRENE SANGA: mcheza sinema,muigizaji,mwandishi na mwanamuziki
IRENE SANGA: mcheza sinema,muigizaji,mwandishi na mwanamuziki
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvFRpnmNIlpIhv1zKmYTw0emu0oR7lrckNAKtKzuEhyXoCNUQVliNRnBYTPC9Px5eRYa_Frtzi8ONhSMBeZNNgpuVmTAL6m3jX5IFmlbL-nqBzW0yloKJoFtikCXadv7d7IBNmQsg23t4/s1600/IMG-20141210-WA0030%5B1%5D.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgvFRpnmNIlpIhv1zKmYTw0emu0oR7lrckNAKtKzuEhyXoCNUQVliNRnBYTPC9Px5eRYa_Frtzi8ONhSMBeZNNgpuVmTAL6m3jX5IFmlbL-nqBzW0yloKJoFtikCXadv7d7IBNmQsg23t4/s72-c/IMG-20141210-WA0030%5B1%5D.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2015/03/irene-sanga-mcheza-sinemamuigizajimwand.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2015/03/irene-sanga-mcheza-sinemamuigizajimwand.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy