Mkuu wa wilaya ya Dodoma betty Mkwasa akiwa na binti huyo ambaye anamhifadhi nyumbani kwake MTOTO wa miaka 10 aliyeozwa kwa mahar...
Mkuu wa wilaya ya Dodoma betty Mkwasa akiwa na binti huyo ambaye anamhifadhi nyumbani kwake |
MTOTO
wa miaka 10 aliyeozwa kwa mahari ya mbuzi 12 na Sh. 100,000 ameokolewa kutoka
mikononi mwa mumewe Joshua Mnamba (25), baada ya majirani kutilia shaka
vilio vya mtoto huyo nyakati za usiku licha ya mumewe awali kudai binti huyo
alikuwa ni ndugu yake.
Tukio
hilo la aina yake, limetokea katika Kijiji cha Ibihwa Wilaya ya Bahi mkoani
Dodoma ambapo binti huyo (jina linahifadhiwa) alisema aliingia kwenye ndoa hiyo
baada ya kushinikizwa na mama yake na bibi yake.
Jeshi
la Polisi Wilaya ya Bahi Mkoani limekiri kupokea taarifa za tukio hilo ambapo
mara ya kwanza liliripotiwa Februari 9, mwaka huu na kuanza upelelezi na
hatimaye kuwatia mbaroni watuhumiwa wote.
Watuhumiwa
hao leo wanatarajiwa kufikishwa mahakamani watuhumiwa akiwemo baba wa mtoto
huyoStephano Mkuta na mama yake Juliana Gidion (50) kujibu tuhuma
zinazowakabili.
Mtoto
huyo amedumu kwenye ndoa kwa wiki mbili.
Majirani
na nyumba alimokuwa akiishi mtuhumiwa wanasema mara baada ya kufika na binti
huyo walikuwa wakihoji binti huyo ni nani lakini alikuwa akijibu kuwa ni ndugu
yake cha kushangaza walikuwa wakiishi peke yao kama mume na mke.
Majirani
hao ambao hawakutaka kutaja majina walisema walikuwa wakisikia kelele
usiku wa manane za mtoto ambaye alikuwa akilia jambo ambalo liliwashangaza.
“Usiku
tulikuwa tukisikia kelele za mtoto akilia ikabidi tujihoji iwapo ni mtoto
anayeishi na mtuhumiwa huenda alikuwa akimlazimisha kufanya nae mapenzi usiku”
Lakini
baadaye majirani hao waligundua kuwa Mnamba alikuwa ameoa mtoto mdogo wa miaka
10 kwa mahari ya mbuzi 12 na fedha taslimu Sh. 100,000.
Jambo
hilo lilionekana kuwakera wananchi ambapo mmoja wao, alitetajwa kwa jina la
Dominick alienda Ofisi ya Kijiji akachukua mgambo akakamatwa na kufikishwa
katika kituo cha polisi cha Bahi ambapo alichukuliwa maelezo yake.
Mtoto
huyo ambaye kwa sasa amepata hifadhi kwa aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bahi,
Betty Mkwasa anasema hajui kusoma wala kuandika kwani wazazi wake hawakumpeleka
shule na alikuwa akikaa nyumbani kulea wadogo zake.
“Sijapelekwa
shuleni nina wadogo zangu sita mimi ndio mkubwa na wazazi wangu na bibi ndio
walikuwa wakitaka niolewe lakini nilikuwa nikikataa mimi ni mdogo” alisema
Alisema
alikuwa akiishi na wazazi wake eneo la Bahi sokoni na baada ya kuolewa
alipelekwa Ibihwa kwa mumewe.
“Baba,
mama na bibi walisema nenda ukaolewe, niliondoka lakini nguo niliziacha kwa
mama nikakuta Mnamba anaishi peke yake tukawa tukawa tunaishi wote na tunalala
pamoja” alisema
Alisema
baadaye mumewe alikuja kukamatwa na polisi kwani alikuwa ameoa mtoto mdogo.
“Nilikuwa
sipendi kuolewa lakini walinilazimisha” alisema.
Mtoto
huyo alisema kwenye fedha za mahari ambazo zilitolewa na mtuhumiwa bibi yake
alipata mgao wa Sh. 10,000
Aliyekuwa
mkuu wa Wilaya ya Bahi, Mkwasa ambaye kwa sasa ni mkuu wa Wilaya ya Dodoma
Mjini ambaye anamhifadhi mtoto huyo nyumbani kwake anasema tatizo la ndoa za
utotoni katika wilaya hiyo ni kubwa lakini wananchi wamekuwa wakitoa ushirikiano
mkubwa kwa kutoa taarifa wanapoona kuna ndoa ya aina hiyo.
“Ninashukuru
hamasisho langu limezaa matunda na wananchi wamehamasika na sasa wanatambua
madhara ya ndoa za utotoni na wamekuwa mstari wa mbele kupinga” alisema
Alisema
tatizo kubwa la ndoa hizo katika Wilaya ya Bahi linasababishwa na mila na
desturi za kabla la wagogo ambapo wasichana huolewa wakiwa bado wadogo.
“Sasa
hii ya kumuoa mtoto wa miaka 10 ni kiboko maana mtoto mwenyewe hata maziwa hana
ana umbo dogo inasikitisha sana” alisema
Alisema
tatizo hilo pia limekuwa likichangiwa na mwamko finyu wa elimu kwani wananchi
wengi ni wafugaji wanajali zaidi mifugo kuliko binadamu na hata umaskini
umekuwa ukichangia.
“Baba
ana mtoto wa miaka 10 na anataka kupata fedha akaamua kumuoza binti yake ili
apate mbuzi na fedha lakini haangalii madhara ambayo mtoto Yule anaweza
kupata.” Alisema.
Hata
hivyo mtuhumiwa, Mnamba alisema alilazimishwa ndoa hiyo na bibi wa mtoto
aliyetajwa kwa jina la Ntolwa ambaye alisema mtoto huyo ni mkubwa na anaweza
ndoa jambo ambalo lilifanya amchukue na kwenda kuishi nae.
“Mimi
nilikaa na yule mtoto lakini alikuwa hatoshi, nikaenda nikamwambia bibi
namrudisha mtoto kwani hatoshi, nikamrudisha kwa bibi yake lakini bibi
akamrudisha tena kwangu” alisema mtuhumiwa.
Source>Sifalubasi:
http://dodomamatukio.blogspot.com/
COMMENTS