TABIA ya vijana wa sasa ya kuchukua fedha kutoka kwa wazee na kuwagawia vijana wenzao ili kurahisisha mambo kwa wazee hao, imeones...
TABIA ya vijana wa sasa ya kuchukua fedha kutoka kwa wazee na
kuwagawia vijana wenzao ili kurahisisha mambo kwa wazee hao, imeonesha
kumkera Rais Jakaya Kikwete
Akizungumza na vijana mjini hapa alisema vijana wa zamani walikuwa
tofauti na wa sasa, wakati vijana wakihakikisha mambo yanakwenda vyema
na hawatumiki vibaya, wa sasa ndio wanachukua fedha na kuwagawia
wenzao.
Alisema tabia ya baadhi ya viongozi wa vijana kutumika kugawa fedha za
wazee inaua demokrasia na maadili na kuingiza utamaduni wa hovyo
katika siasa.
“Kama ukiwa na viongozi wa vijana unapojihusisha na kugawa fedha,
vijana hamuwezi kugeuka makuwadi, hamuwezi kugeuka kuwa mawakala wa
kuhonga vijana wenzenu mtakuwa mmetoka kabisa kwenye mstari” alisema
Rais Kikwete alisema hayo jana wakati akifungua mkutano mkuu wa
kwanza wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu huku
akitamba kuwa CCM itaendelea kuongoza na wataisoma namba.
Aliwaasa vijana kuwa hatima ya CCM iko mikononi mwao na hivyo ni vyema
wakajiepusha na matendo ya rushwa na ukiukaji wa maadili.
“Hatma ya CCM iko mikononi mwa vijana, umoja wa vijana una kazi ya
kuandaa vijana nina masikitiko kwa haya yanayotokea” alisema
Alisema shirikisho ni kiungo muhimu kati ya CCM na wanafunzi kwani
wanachagua viongozi wa kutengeneza daraja kati ya wanafunzi na chama.
Alisema umoja wa vijana una kazi ya kuandaa vijana, kupata wanachama
wapya na kuimarisha umoja huo ili uwe na manufaa hapo baadaye.
Aliwataka kukaa na kuzungumza mustakabali wa chama, lakini chama
hakipendi kuona viongozi wa vijana wakifanya kazi ya kugawa hela za
wazee kwa vijana wenzao.
“Tunataka miaka 30 ijayo Rais lazima atoke miongoni mwenu lazima CCM
ifanye kazi ya kuandaa vijana, mimi na wenzangu tuliandaliwa kwenye
chama” alisema
Alisema Chama kinataka kuwe na umoja wa vijana wenye nguvu tofauti na
ilivyo sasa.
“Tunataka kila wanapokutana vijana wazee wawe na wasiwasi na maazimio
kila yanapotoka, lakini uhanaharakati wa vijana umenaza kupungua
kutokana na chama kuendeshwa vibaya lakini haiwezekani vijana
kujihusisha na kugawa fedha” alisema
Rais Kikwete alisema shirikisho hilo litatoa uhai na taswira mpya
kwani chama kina fursa ya kuandaa wanachama wa CCM kutoka elimu ya juu
ili kubeba jukumu la uongozi katika chama sasa na wakati ujao.
Alisema shirikisho hilo ni tanuru la kuoka viongozi wa baadaye na
taifa kwa ujumla kwa ajili ya maslahi mapana kwa taifa.
Alisema CCM itaendelea kushirikisha vijana kama miaka iliyopita
ambapo mwaka 2010 vijana walishirikishwa kutafuta wadhamini wa
wagombea, kwenye kampeni na kupangwa kwenye maeneo mbalimbali na
kwenye harakati za uchaguzi mwaka huu ushjiriki wa vijana utakuwa
mpana zaidi.
Aliwataka vijana kukaa na kutoa mapendekezo nini kifanyike ili
kuboresha maeneo ambayo yanawagusa moja kwa moja ikiwemo suala la
mikopo ya elimu ya juu,
“Kazi na mtoke na maazimio na hayo yote yatafanyiwa kazi” alisema
Wagombea nafasi ya Urais
Rais Kikwete alisema nafasi ziko wazi na chama kimesema wanaotaka
nafasi hiyo wajitokeze.
“Tunangoja siku ya kuchukuliwa kwa fomu watakaojitokeza ni wangapi,
sasa wako zaidi ya 20 wanaoutamani Urais” alisema
Alisema hakuna sababu ya kugombana na watu wala kuchukiana ila kila
moja anachotakiwa ni kufuata utaratibu.
“Kuongoza ni kuona mbali ni kufungua mabano, kitendaliwi na kufumbua
mafumbo, wanasiasa wanaamini ng’ombe anaweza kunenepa siku ya mnada”
alisema
Pia alitaka kutolewa kwa kadimpya za wanachama 30,000 ambapo
shirikisho hilo liliomba kwa ajili ya wanachama wake wapya.
Awali mlezi wa Shirikisho hilo Taifa, ambaye ni Naibu Waziri wa
Mawasiliano, sayansi na teknolojia, Januari Makamba shirikisho hilo
linaundwa na wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kutoka mikoa 21
nchini.
Alisema waliohudhuria mkutano huo ni wanachama kutoka matawi 137
ambapo idadu ya waliohudhuria ni 683 kati ya 685 ambapo shirikisho
hilo lina jumla ya wanachama 31,000.
Aliomba shirikisho hilo lipatiwe kadi 30,000 kutokana na mahitaji ya
kadi kuongezeka hali inayosababishwa na viajana wengi wasomi kujiunga
na shirikisho hilo.
Pia aliwataka vijana wapewe nafasi na kuambuliwa katika ofisi za
wilaya na mikoa kwani wamekuwa wakikosa ushirikiano huku akitaka suala
la mikopo kwa elimu ya juu liangaliwe tena ili kupunguza malalamiko
kwa wasomi hao.
Pia alimpongeza Rais Kikwete kwa kuendelea kuamini viajana hasa kwenye
uteuzi wa nafasi mbalimbali na kutaka upendeleo maalum wa ajira
utolewe kwa vijana wa CCm walio katika vyuo vya elimu ya juu.
Source: Sifa Lubasi,Dodoma
kuwagawia vijana wenzao ili kurahisisha mambo kwa wazee hao, imeonesha
kumkera Rais Jakaya Kikwete
Akizungumza na vijana mjini hapa alisema vijana wa zamani walikuwa
tofauti na wa sasa, wakati vijana wakihakikisha mambo yanakwenda vyema
na hawatumiki vibaya, wa sasa ndio wanachukua fedha na kuwagawia
wenzao.
Alisema tabia ya baadhi ya viongozi wa vijana kutumika kugawa fedha za
wazee inaua demokrasia na maadili na kuingiza utamaduni wa hovyo
katika siasa.
“Kama ukiwa na viongozi wa vijana unapojihusisha na kugawa fedha,
vijana hamuwezi kugeuka makuwadi, hamuwezi kugeuka kuwa mawakala wa
kuhonga vijana wenzenu mtakuwa mmetoka kabisa kwenye mstari” alisema
Rais Kikwete alisema hayo jana wakati akifungua mkutano mkuu wa
kwanza wa Shirikisho la Wanafunzi wa Vyuo vya Elimu ya Juu huku
akitamba kuwa CCM itaendelea kuongoza na wataisoma namba.
Aliwaasa vijana kuwa hatima ya CCM iko mikononi mwao na hivyo ni vyema
wakajiepusha na matendo ya rushwa na ukiukaji wa maadili.
“Hatma ya CCM iko mikononi mwa vijana, umoja wa vijana una kazi ya
kuandaa vijana nina masikitiko kwa haya yanayotokea” alisema
Alisema shirikisho ni kiungo muhimu kati ya CCM na wanafunzi kwani
wanachagua viongozi wa kutengeneza daraja kati ya wanafunzi na chama.
Alisema umoja wa vijana una kazi ya kuandaa vijana, kupata wanachama
wapya na kuimarisha umoja huo ili uwe na manufaa hapo baadaye.
Aliwataka kukaa na kuzungumza mustakabali wa chama, lakini chama
hakipendi kuona viongozi wa vijana wakifanya kazi ya kugawa hela za
wazee kwa vijana wenzao.
“Tunataka miaka 30 ijayo Rais lazima atoke miongoni mwenu lazima CCM
ifanye kazi ya kuandaa vijana, mimi na wenzangu tuliandaliwa kwenye
chama” alisema
Alisema Chama kinataka kuwe na umoja wa vijana wenye nguvu tofauti na
ilivyo sasa.
“Tunataka kila wanapokutana vijana wazee wawe na wasiwasi na maazimio
kila yanapotoka, lakini uhanaharakati wa vijana umenaza kupungua
kutokana na chama kuendeshwa vibaya lakini haiwezekani vijana
kujihusisha na kugawa fedha” alisema
Rais Kikwete alisema shirikisho hilo litatoa uhai na taswira mpya
kwani chama kina fursa ya kuandaa wanachama wa CCM kutoka elimu ya juu
ili kubeba jukumu la uongozi katika chama sasa na wakati ujao.
Alisema shirikisho hilo ni tanuru la kuoka viongozi wa baadaye na
taifa kwa ujumla kwa ajili ya maslahi mapana kwa taifa.
Alisema CCM itaendelea kushirikisha vijana kama miaka iliyopita
ambapo mwaka 2010 vijana walishirikishwa kutafuta wadhamini wa
wagombea, kwenye kampeni na kupangwa kwenye maeneo mbalimbali na
kwenye harakati za uchaguzi mwaka huu ushjiriki wa vijana utakuwa
mpana zaidi.
Aliwataka vijana kukaa na kutoa mapendekezo nini kifanyike ili
kuboresha maeneo ambayo yanawagusa moja kwa moja ikiwemo suala la
mikopo ya elimu ya juu,
“Kazi na mtoke na maazimio na hayo yote yatafanyiwa kazi” alisema
Wagombea nafasi ya Urais
Rais Kikwete alisema nafasi ziko wazi na chama kimesema wanaotaka
nafasi hiyo wajitokeze.
“Tunangoja siku ya kuchukuliwa kwa fomu watakaojitokeza ni wangapi,
sasa wako zaidi ya 20 wanaoutamani Urais” alisema
Alisema hakuna sababu ya kugombana na watu wala kuchukiana ila kila
moja anachotakiwa ni kufuata utaratibu.
“Kuongoza ni kuona mbali ni kufungua mabano, kitendaliwi na kufumbua
mafumbo, wanasiasa wanaamini ng’ombe anaweza kunenepa siku ya mnada”
alisema
Pia alitaka kutolewa kwa kadimpya za wanachama 30,000 ambapo
shirikisho hilo liliomba kwa ajili ya wanachama wake wapya.
Awali mlezi wa Shirikisho hilo Taifa, ambaye ni Naibu Waziri wa
Mawasiliano, sayansi na teknolojia, Januari Makamba shirikisho hilo
linaundwa na wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu kutoka mikoa 21
nchini.
Alisema waliohudhuria mkutano huo ni wanachama kutoka matawi 137
ambapo idadu ya waliohudhuria ni 683 kati ya 685 ambapo shirikisho
hilo lina jumla ya wanachama 31,000.
Aliomba shirikisho hilo lipatiwe kadi 30,000 kutokana na mahitaji ya
kadi kuongezeka hali inayosababishwa na viajana wengi wasomi kujiunga
na shirikisho hilo.
Pia aliwataka vijana wapewe nafasi na kuambuliwa katika ofisi za
wilaya na mikoa kwani wamekuwa wakikosa ushirikiano huku akitaka suala
la mikopo kwa elimu ya juu liangaliwe tena ili kupunguza malalamiko
kwa wasomi hao.
Pia alimpongeza Rais Kikwete kwa kuendelea kuamini viajana hasa kwenye
uteuzi wa nafasi mbalimbali na kutaka upendeleo maalum wa ajira
utolewe kwa vijana wa CCm walio katika vyuo vya elimu ya juu.
Source: Sifa Lubasi,Dodoma
COMMENTS