SWAHILIVILLA ANASEMA NINI KUHUSU VALENTINE DAY NI VYEMA UKASOMA

Na Mwandishi wetu Washington  Kila ifikapo tarehe 14 Februari nchini Marekani na sehemu nyengine Duniani husherehekewa Siku Ya Wapendan...

Na Mwandishi wetu Washington 
Kila ifikapo tarehe 14 Februari nchini Marekani na sehemu nyengine Duniani husherehekewa Siku Ya Wapendanao "Valentine's Day", au kama ijulikanavyo kwa jina jengine "Siku Ya Mtakatifu Valentine" (Saint Valentine's Day). Katika miaka ya hivi karibuni siku hii pia imeanza kusherehekewa katika maeneo ya Afrika Mashariki. Labda shukrani ziende kwa enzi za utandawazi. Lakini je Siku Kuu hii ilianzia lini?
Asili yake
Hakuna chanzo cha uhakika kuhusu asili na chimbuko la Siku ya Wapendanao. Hata hivyo inaaminika kuwa asili yake inarejea katika enzi za Himaya ya Warumi, na baadaye Kanisa Katoliki kuingiza katika Ukristo.
Kuna watu watatu katika historia ya Kanisa Katoliki ambao wanajulikana kama Mtakatifu Valentine au Valentinus, na wote inasadikiwa walikufa kama mashahidi kwa mujibu wa itikadi za Kikatoliki, na kwa hivyo Kanisa likaamua kuiadhimisha siku waliyonyongwa kama kuwaenzi watumishi hao.
Kuna nganu inayodai kuwa Valentine alikuwa ni Mchungaji aliyehudumu Roma katika karne ya tatu. Wakati huo, Mfalme Claudius Wa Tatu, alipitisha amri ya kupiga marufuku ndoa kwa vijana wa Kiume kwa vile alihisi kuwa wanaume wasio na wake au familia walikuwa askari bora zaidi kuliko waliokuwa kwenye ndoa.
Mchungaji Valentine hakukubaliana na amri hiyo ya Mfalme na akawa naendelea kufungisha watu ndoa kwa njia za siri. Mfalme Claudius alipogundua mpango huo, aliamuru Valentine anyongwe.
Simulizi nyengine zinadai kuwa Valentine huenda alinyongwa kwa kosa la kuwasaidia Wakristo kutoroka katika magereza ya Warumi ambako walikuwa wakiteswa vibaya.
Inadaiwa kuwa Valentine ndiye aliyetuma maamkizi ya mwanzo ya mapenzi (valentine) kumpelekea msichana aliyempenda ambaye alikuwa akimtembelea wakti akiwa gerezani.
Inadaiwa kuwa kabla ya kifo chake, aliandika barua na kuisaini "Kutoka kwa wako Valentine". Maneno hayo bado yanaendelea kutumika hadi leo katika kadi za maamkizi ya siku ya Wapendanao.
Kwa upande mwengine, inasadikiwa kuwa kuanzia tarehe 13 hadi 15 Februari, Warumi walikuwa na desturi ya kusherehekea siku iliyojulikana kwa jina la Lupercalia. Miongoni mwa ada za siku hii ilikuwa ni wanaume kuwapiga wanawake.
Mnamo karne ya tano, Baba Mtakatifu Gelasius wa Pili, alikoroga mambo kwa kuichanganya siku ya Mtakatifu Valentine pamoja na ile ya Lupercalia kwa lengo la kuizika ada hiyo ya kipagani ya Warumi.
Kadiri miaka ilipozidi kusonga mbele ndivyo kadiri siku ya Wapendanao ilivyozidi kusherehekewa, mpaka ikafikia enzi za Shakespeare na Chaucer, ambao waliipamba siku hiyo katika kazi zao za sanaa na hivyo kuipatia siku hii umaarufu zaidi. Katika karne za kati, kadi zilizotengenezwa kwa mikono ndizo zilikuwa zikitamba.
Hatimaye, utamaduni huo ukavuka bahari na kuingia nchini Marekani na sehemu nyingine ulimwenguni, na mnamo karne ya 19 mapinduzi ya viwanda yakachapuza katika uchapishaji wa kadi za makazi na kuipa umaarufu mkubwa zaidi siku hiyo. Katika mwaka 1913 shirika la Hallmark likaanza kuchapisha kadi za Siku ya Wapendao na kubadilisha mkondo wa kihistoria wa kuadhimisha siku hiyo.
Katika enzi za leo
Siku ya Wapendao si Sikuu Rasmi nchini Marekani. Watu huenda makazini kama kawaida, hata hivyo kama zilivyo Siku Kuu nyingi nchini humu, nayo pia imekumbwa na kimbunga cha biashara tangu pale Hallmark walipoanzisha kuzalisha kadi zao kwa wingi. Hii ni siku ya pili kwa ukubwa wa mauzo katika mwaka baada ya siku ya Christmas.
Inakadiriwa kuwa mauzo ya kadi hizo katika siku hiyo hufikia zaidi ya Dola Billioni 15. Baadhi ya watani wanasema kuwa "iwapo sherehe za siku ya Wapendanao zitapigwa marufuku nchini Marekani, basi shirika la Hallmark litafilisika"
Biashara nyengine inayochangamka katika siku hiii ni ya maua. Tani za maua huuzwa katika siku hii, na baadhi ya wauza-maua huajiri wafanyazi wa kiasi wiki moja kabla ya siku hii ili kukabiliana na ongezeko la wateja. Waridi ni nembo ya pili maarufu katika siku hii baada ya ile ya moyo.
Mbali na biashara hizo mbili, kuna zawadi aina kwa aina ambazo watu huwanunulia wale wawapendao, zikiwemo pipi, chokleti, na vitu vyengine vya kula na kunywa ambavyo ama hutengenezwa katika umbo la "moyo" kama ishara ya mapenzi, au kufungwa katika vifurushi vilivyopambwa katika mfumo kama huo.
Siyo Hallmark tu wanaofaidika katika siku hii, bali biashara nyingi mauzo yao huongezeka hususan mikahawa ambayo watu wanaotaka kudhihirisha mapenzi kwa wapenzi wao hujazana katika sehemu hizo na kudhihirisha mapenzi ya hali ya juu kwa kuagiza milo ya fahari.
Kwa ujumla Waswahili wanasema "Mtu hujikuna ajipatapo". Kwa hivyo, kuna wale ambao huwanunulia wapenzi zawadi hafifu kama vile kadi yenye thamani ya chini, na kuendelea mpaka kufikia vito vya thamani, magari, majumba na sema upendavyo.
Nchini Marekani, Canada na kwengineko, baadhi ya maskuli huandaa tafrija maalum za Siku ya Wapendanao ambapo wanafunzi hubadilishana zawadi na marafiki zao ambazo aghlabu huwa ni pipi, chokleti na kadi za maamkizi.
Wanaosherehekea na Wasiosherehekea siku hii.
Ingawaje siku hii huzalisha mabilioni ya Dola nchini Marekani, hata hivyo wako watu ambao hawasherehekei siku hii kutokana na sababu mbalimbali.
Wale wanaosherehekea wanaona kuwa ni siku iliyojaa upendo. "Siku ya Wapendanao ni siku iliyojaa upendo, anga yote huwa imejaa mapenzi", anasema Angie Bradlye, Msimamizi wa Uzalishaji katika kiwanda kimoja nchini Marekani, na kuongeza, "ingawa mume wangu amefariki, lakini katika siku hii hujihisi kama niko pamoja naye na moyo wangu hujaa furaha"
Naye Mae, anaona kuwa ni fursa kwa wanaume kudhihirisha mapenzi kwa wapendanao. "Ni siku muhimu kwa wanaume kudhihirisha mapenzi kwa wanawake wawapendao" alisema.
Kwa upande wa wale wasiosherehekea siku hii nao pia wana sababu zao.
Scotty ni Mmarekani mwenye asili ya Afrika na anasema "Mimi siadhimishi siku hii kwa sababu ni siku kuu iliyotengenezwa na Wazungu tu kwa ajili ya kujipatia pesa kutokana na mauzo ya biashara zao"
Hata hivyo, Blue, ni mwanamke wa Kizungu, lakini hasherehekei siku hii akisema "Huu ni upuuzi mtupu, si chengine chochote ispokuwa wanawake wasiokuwa na shukurani kujipatia zawadi wasizostahiki kutoka kwa mabwana zao"
Wengine huwa hawasherehekei kwa sababu hawana wapenzi wa kusherehekea nao, kama ambavyo Kendra Simpson kutoka Jimbo la Karolina Ya Kusini aliiambia Swahillivilla : "Mimi sisherehekei kwa sababu sina mpenzi kwa sasa, kama nina mpenzi na anapenda kuadhimisha siku hii, basi nitaingia naye pumbaoni". Hata hivyo alisisitiza kuwa kila siku inapaswa kuwa siku ya mapenzi kwa wapendao, na siyo siku hii moja tu.
Rai hiyo inaungwa mkono na Bi LaToya Bragg wa jimbo la Ohio, ambaye anasema "ni jambo la kushangaza kuona watu wanahemkwa na kupoteza mapesa katika siku hii moja, wakati ambapo mapenzi yanatakiwa kudumu kwa muda wote ambao watu wapendanao huwa pamoja katika uhai wao"
Athari mbaya za Kijamii.
Bi LaToya aliyeandika kitabu kwa jina "The Heart Of Me" pia haoni sababu ya kuadhimisha siku hii katika mfumo wake wa sasa kwa vile unaleta athari mbaya za kijamii. "Kuna watu wengine hali zao za kiuchumi siyo nzuri, kwa hivyo hawawezi kunnuua zawadi kwa wapenzi wao, na hivyo wapenzi wanaokosa zawadi kutoka kwa wapenzi wao, hujihisi duni mbele ya wenzao"
"Aidha huleta athari za kiuchumi kwa watu wenye kipato cha chini kwa kujikalifisha kuwanunulia wapenzi wao zawadi wazipendazo ambazo wakati mwnengine ziko nje ya uwezo wao, almradi tu na wao waonekani ni watu katika jamii"
Mbali na umaarufu wa siku hii, hata hivyo uchunguzi mdogo uliofanywa na Swahilivilla umeonesha kuwa, idadi kubwa ya watu hawajui asili, chimbuko na maana ya Siku ya Wapendanao. Kristy, ni afisa wa mapokezi na usafirishaji katika Shirika moja la vifaa vya magari anasema: "Ninavyojua siku hii ni ya wanaume kuwanunulia zawadi wapenzi wao, na kwa wanaume siku yao ni ile inayoitwa 'sweetest hearts day'.."
Naye Amanda Waleker anasema: "Sijui chochote kuhusu asili ya siku hii, watu wanasherehekea na kuadhimisha, lakini mimi si katika mambo yangu"

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: SWAHILIVILLA ANASEMA NINI KUHUSU VALENTINE DAY NI VYEMA UKASOMA
SWAHILIVILLA ANASEMA NINI KUHUSU VALENTINE DAY NI VYEMA UKASOMA
http://4hdwallpapers.com/wp-content/uploads/2013/02/valentine-day-roses.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/02/swahilivilla-anasema-nini-kuhusu.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/02/swahilivilla-anasema-nini-kuhusu.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy