Baba askofu Isuja kuzikwa Paulo wa Msalaba Jumatano

Mhasdhamu Isuja akiwa na rais Mstaafu wakati wa sherehe za miaka 40 ya uaskofu ASKOFU wa kwanza Mzalendo  na wa tatu kwa jimbo kato...


Mhasdhamu Isuja akiwa na rais Mstaafu wakati wa sherehe za miaka 40 ya uaskofu

ASKOFU wa kwanza Mzalendo  na wa tatu kwa jimbo katoliki Dodoma, Mhashamu Mathias Isuja Joseph  ( 86) amefariki dunia akitibiwa katika hospitali ya misheni ya Mtakatifu Gaspar, Singida.
 Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Uongozi wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma,Mhashamu Isuja ambaye alistaafu kazi hiyo ya uaskofu mwaka 2005 atazikwa kanisa kuu la Jimbo katoliki Dodoma la Paulo wa Msalaba Jumatano ijayo.
 Mhashamu Isuja aliteuliwa kuwa askofu wa Dodoma Juni 26 1972 akichukua nafasi ya  Askofu Anthony Jeremiah Pesce ambaye alifariki Desemba 20 1971. Kabla ya askofu Pesce ambaye aliteuliwa Mei 10,1951 alikuwapo  askofu Stanislas dell’Addolorata ambaye aliteuliwa Juni16 1937 na kufariki 1941. 
Jimbo Katoliki Dodoma lilianzishwa mwaka Januari 28,1935.
 Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Askofu Mkuu Beatus kinyaiya aliyeteuliwa Novemba  6,2014 kuchukua nafasi ya Askofu Gervas John Mwasikwabhila Nyaisonga ambaye alikwenda kuwa Askofu wa Mpanda. Askofu Nyasionga alichukua nafasi ya Askofu Jude Thadeus Ruwa’ichi ambaye 2010 alichaguliwa kuwa askofu wa Mwanza.
 Askofu Isuja, ambaye wengi walizoea kumwita “Babu”, amefariki dunia akiwa ametumikia utumishi wa Mungu kwa miaka 55 ya huduma ya Upadre na miaka 43 ya Uaskofu huku akibahatika kuona Jimbo Katoliki Dodoma likizaa Jimbo Katoliki la Kondoa na hatimaye, kupandishwa hadhi kuwa Jimbo kuu la Dodoma.
 Katika uhai wake Askofu Isuja tangu akiwa Padre hadi Askofu alikuwa chachu kubwa katika masuala ya elimu Jimboni Dodoma,kupambana na umasikini lakini pia alisistiza wakazi wa mikoa ya kanda ya kati kukabili umaskini kwa kujikita katika kilimo cha zabibu.
 Askofu Isuja alikuwa pia kipenzi cha watoto wa Shirika la Utoto Mtakatifu Kipapa ambapo mara nyingi alikuwa akiwasisitiza kupeleka neno kwa watoto wenzao huku akiimba sisi ni Christopher.
Askofu Isuja alizaliwa Agosti 14,1929 katika kijiji cha Haubi Kondoa,alipata daraja takatifu la Upadre Desemba 24,1960 Parokiani Kondoa na Septemba 17,1972 alipata daraja takatifu la Uaskofu Jimboni Dodoma.
Aidha mwaka 2005 Askofu Isuja alikabidhi utawala wa kichungaji kwa Ruwaichi kwa mujibu wa sheria za Kanisa pamoja na kwamba aling’atuka.
Askofu Isuja ni mtoto wa Mzee Joseph Chundu na mama Odilia Mbula alizaliwa Agosti 14, 1929 katika kijiji  cha Haubi Wilayani Kondoa.
Alisoma shule ya msingi Kondoa na Bihawana kuanzia mwaka 1942 hadi 1948, mnamo mwaka 1949 hadi 1953 alichaguliwa kujiunga na elimu ya Sekondari katika Seminari  ya Bihawana.
Mwaka 1953 hadi 1955 alijiunga na seminari ya Tosamaganga kwa elimu ya falsafa na mwaka 1956 hadi mwaka 1960 alijiunga na seminari ya Kibosho kwa elimu ya theology.
Mnamo mwaka 1960 alitunukiwa daraja la upadri katika parokia ya Kondoa mara baada ya kupewa daraja la upadri alitumwa parokia ya Kibakwe kuwa paroko mwaka 1961 hadi 1963 na mwaka 1963 hadi mwaka 1969 aliteuliwa kuwa katibu wa elimu na ilipofika mwaka 1966 hadi mwaka 1971 aliteuliwa kuwa makamu wa askofu  huku akiendele na nafasi yake ya katibu wa elimu na mwaka 1971 hadi mwaka 1972 aliteuliwa kuwa msimamizi wa kitume wa jimbo la Dodoma.Aliwekwa wakfu na Kardinali Laurean Rugambwa mwaka 1972.
Pia katika uongozi wake taasisi mbalimbali zilianzishwa ikiwemo Bihawana seminari, nyumba ya malezi ya waseminari wa jimbo Miyuji, chuo cha ufundi Mpwapwa-magogo,Chuo cha ufundi veyula, chuo cha Ufundi cha John Bosco, Seminari na chuo cha walimu cha wasalesiani, sekondari ya wasichana ya masista wa Huruma, kituo cha watoto walemavu Mlali, kituo cha watoto wenye mtindio wa akili (Cheshire Home Miyuji).
Vile vile vyuo vya kilimo Ipala na Chikopelo, Holy cross centre, hospitali ya masista wa Mtakatifu Gemma Galgani Miyuji, Kituo cha Hija Mbwanga, hosteli ya mapadri Kondoa, nyumba ya watoto yatima Kondoa, nyumba mpya ya Askofu na Ofisi ya Jimbo.
Askofu Isuja atakumbukwa pia kwa ushauri alioutoa Julai mwaka 2014 kwamba watanzania wanapaswa kuheshimu hadhi na mamlaka aliyonayo Rais wa Jamhuri ya Muunganao wa Tanzania Dk Jakaya Mrisho Kikwete, kwa kuthamini na kuzingatia mwongozo na ushauri mbalimbali anaoutoa kwa wananchi kwani mamlaka hayo yanatoka kwa Mungu.
Kauli hiyo  ambayo aliitoa katika mahubiri yake maalum wakati wa ibada ya misa ya jumapili katika Parokia ya Makole, Jimbo Katoliki la Dodoma, iliyokuwa na lengo la kuchangia ujenzi wa kanisa la kiaskofu  Jimbo la Kondoa, alisisitiza Watanzania waombe Mungu ajalie busara na hekima katika kutenda na kuamua mambo mbalimbali yahusuyo nchi yakiwemo malumbano yaliyokuwa yakifanyika nchini kote kuhusu mchakato wa kupata Katiba Mpya.
Askofu huyo alisema hafurahishwi na jinsi makundi mbalimbali ya Watanzania yalivyokuwa yanalumbana na kubeza hata miongozo inayotolewa na Rais Kikwete.
Wakati wa wakati wa sherehe ya miaka 40 ya Uaskofu wa Mhashamu baba Askofu  Mathias  Isuja, Septemba 18 ,2012, Rais  wa awamu ya tatu Benjamini William Mkapa  aliwataka kuachwa kwa mtazamo wa mbaya  wa kuwabeza viongozi wastaafu ambao wameitumikia nchi.
 “Kustaafu si kuchoka, sio uwe legelege lakini kwa imani unatakiwa kutoa mchango wako kwa kutumiza wajibu wako katika jamii” alisema
Alisema kuwa tatizo kubwa lililo katika jamii ni kutotaka kuheshimu mamlaka kwani kila mtu anajifanya kuwa mjuaji maishani, haambiliki.
Aidha Rais mstaafu Mkapa alishawahi kusikika akisema kwamba  anamheshimu Askofu huyo kutokana na kutosikia malumbano ya dini.
Alisema kuwa,Katika kipindi alichokuwa waziri wa mambo ya nje na hata alipokuwa rais hakuwahi kusikia malumbano yoyote ya kidini mkoani Dodoma na hilo ni jambo la kujifunza katika umoja na mshikamano wa madhehebu ya dini ya kikristo na kiislam.
“Tutamuenzi Askofu Isuja kwa kuzingatia kauli mbiu yake na ngao yake ya mapendo, haki na amani.” Alisema.
Naye Askofu Mkuu Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo alisema kuwa askofu Isuja atakumbukwa kwa mchango wake kwa kuboresha huduma za afya na ujenzi wa shule na zahanati. 
Source: Sifa Lubasi, Habarileo Dodoma





COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: Baba askofu Isuja kuzikwa Paulo wa Msalaba Jumatano
Baba askofu Isuja kuzikwa Paulo wa Msalaba Jumatano
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6Umtj7VnudaB961ymAeFRTV-3vjI-759E5zXsXX48ZADPZy59re_CgE1ilDb80j54uj0te-jKNgoEH3t6wk4szmdS6DiN2_ZAxurpA2gbYzpGVlUcxqd1LklHSiWBmPUxauaXHJM6YJg/s320/mkapa+na+isuja.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6Umtj7VnudaB961ymAeFRTV-3vjI-759E5zXsXX48ZADPZy59re_CgE1ilDb80j54uj0te-jKNgoEH3t6wk4szmdS6DiN2_ZAxurpA2gbYzpGVlUcxqd1LklHSiWBmPUxauaXHJM6YJg/s72-c/mkapa+na+isuja.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/04/baba-askofu-isuja-kuzikwa-paulo-wa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/04/baba-askofu-isuja-kuzikwa-paulo-wa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy