Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji imeridhishwa na matumizi ya fedha kiasi cha shilingi Bilioni 141 zilizotolewa na ...
Kamati ya Kudumu ya Bunge
ya Kilimo, Mifugo na Maji imeridhishwa na matumizi ya fedha kiasi cha shilingi
Bilioni 141 zilizotolewa na Serikali kugharamia mradi mkubwa wa ujenzi wa bomba
la maji kutoka Mtambo wa Ruvu Chini,wilayani Bagamoyo kwenda jijini Dar es
salaam kufuatia ujenzi wake kukamilika.
Akizungumza mara baada ya
Kamati hiyo kutembelea maeneo mbalimbali ya mradi huo ikiwemo mtambo wa Maji wa
Ruvu Chini, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Hanan'g
Mhe. Mary Nagu amesema kuwa kamati kamati yake
imeridhishwa na ubora wa kazi
iliyofanyika chini ya Usimamizi wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka Dar es
salam ( DAWASA).
Amesema mradi huo wenye
urefu wa kilometa 56 umekamilika na
kueleza kuwa itakua historia kwa wananchi
wa Dar es salaam waliounganishwa na mtandao wa mabomba ya DAWASCO kukosa
maji.
Amesema kama kamati
wamejiridhisha kuwa kiasi cha maji kinachozalishwa kwa siku lita milioni 270
kutoka mtambo wa Ruvu Chini ni kingi na
kueleza kuwa kiwango hicho kitaongezwa kwenye uzalishaji wa awali.
"Sisi kama Kamati ya
Bunge tumeridhishwa na kazi nzuri iliyofanyika, tumeshuhudia wenyewe maji
yanayozalishwa ni mengi tunaipongeza Serikali kwa kusikia kilio cha muda mrefu
cha wakazi wa jiji la Dar es salaam" Amesema Mhe.Nagu.
Amesema kazi iliyopo sasa
kwa Serikali na mamlaka zinazohusika ni kuhakikisha kuwa inakabiliana na na
changamoto ya usambazaji wa maji hayo ili wakazi wengi zaidi wa jiji hilo
wanaunganishwe na mtandao wa mabomba ya DAWASCO.
Amewataka DAWASCO kuifanya
kazi hiyo kwa kasi pia kuangalia upya
gharama za usambazaji wa maji pia kuwaangalia upya mawakala waliowekwa
kusimamia usambazaji wa maji ili kuwadhibiti wale wasiowaaminifu ili wananchi
waweze kupata maji kwa bei nafuu na kuepuka kutumia maji yasiyo salama ambayo
yamekuwa chanzo cha milipuko ya magonjwa ikiwemo kipindupindu.
Aidha,ametoa wito kwa
wananchi kulinda na kutunza vyanzo vya maji ili upatikanaji wa maji hayo uwe
endelevu huku akitoa wito kwa Wizara kulifanyika kazi suala la kuwapatia maji
wananchi wote wanaoishi kuzunguka miundombinu mikubwa ya maji kote nchini ili
kuimarisha ulinzi na usalama.
Kwa upande wake Waziri wa
Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge akizungumza mara baada ya kukamilika
kwa ziara ya wabunge hao kwenye mtambo wa Maji wa Ruvu Chini amesema kuwa
kukamilika kwa mradi huo kutalifanya jiji la Dar es salaam kupata maji.
Amesema katika kuchukua
hatua za kukabiliana na uhaba wa maji Serikali iliamua kufanya maboresho
makubwa mifumo ya maji kwa kujenga mipya na kurekebisha ile ya zamani ili
kuendana na kasi ongezeko la uhitaji wa maji.
Amesema kazi kubwa ambayo
inaendelea sasa ni kuhakikisha usambazaji katika maeneo yenye mitandao ya
mabomba na ile ambayo haikuwa na mitandao ya mabomba ili kuwapatia maji ya
uhakika.
" Naishukuru kamati
kwa kuja kutembelea mradi wetu wametupa changamoto ya kuhakikisha maji yanafika
kwa wananchi, sisi kama serikali tuna mpango wa kuhakikisha tunaondoa mifumo
yote chakavu katika jiji la Dar es salaam kwa kuweka mipya na hii tunaendelea
nayo kwa kasi" Amesisitiza.
Amesema kazi ya kuweka
miundombinu ya usambazaji maji katika jiji
la Dar es salaam imeshaanza akifafanua kuwa Serikali imeingia mikataba na
wakandarasi kuhakikisha kuwa kazi hiyo inafanyika kwa viwango.
Aidha, amesema kuwa baadhi
ya maeneo ya jiji ikiwemo eneo la Kimara kazi inaendelea huku maeneo ya
katikati ya jiji miundombinu yake ni chakavu inaendelea kubadilishwa ili iweze
kuhimili wingi na nguvu ya maji inayosukumwa
Ametoa wito kwa wananchi
na wenye viwanda kutumia maji hayo ili kulinda afya za walaji kwa kuwa maji
hayo ni salama na yamepita kwenye vipimo vya ubora ili kuepuka kutumia maji
yasiyo salama ambayo yamekuwa chanzo cha magonjwa.
" Tumeshatoa
maelekezo viwanda vyote vya Dar es salaam vihakikishe kuwa vinatumia maji haya,
sasa tuna maji ya kutosha, waje tuwaunganishe na maji haya japo baadhi yao wamekuwa
wakijiunganishia maji kiholela na kutumia visima wanavyochimba ambavyo si
salama".
Kuhusu Serikali
kuhakikisha ulinzi wa mtandao wa bomba hilo lenye urefu wa Kilometa 56 amesema
kuwa kazi hiyo inafanywa na DAWASCO ikiwahusisha viongozi na wananchi ambao
mradi unapita katika maeneo yao.
" Ni kweli ulinzi wa
bomba hili ni muhimu,DAWASA wanaendelea kutoa elimu kwa wananchi katika maeneo
linakopita bomba, pia tumeshaweka matoleo kwa ajili ya kuhakikisha
tunawafikishia huduma ya maji wananchi wanaoishi kuzunguka bomba hili ili nao
wawe sehemu ya walinzi wa mradi wao" Amesema.
Mhe. Lwenge ameongeza kuwa
Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASCO) litaweka mfumo wa
ulinzi wa kieletroniki ili kulinda bomba hilo, mfumo huo utakua unapima kiwango
cha msukumo wa maji yanayotoka Ruvu Chini kisha kutoa taarifa kwenye vituo
vitakavyoanzishwa endapo itatokea hitilafu ya miundombinu hiyo.
Baadhi ya wajumbe wa
kamati hiyo ambao ni Wabunge wakizungumzia kukamilika kwa mradi huo wamesema
kuwa wameridhishwa na kazi kubwa iliyofanywa na serikali na kwamba itaondoa
kero ya maji katika jiji la Dar es-slaam.
Mbunge wa jimbo la
Itirima, Mhe. Njalu Silanga ambaye ni
mmoja wa wajumbe wa Kamati hiyo ameeleza kuwa ameridhishwa na kazi nzuri
iliyofanywa na Serikali kwa kuwa mradi huo umejengwa katika viwango vya hali ya
juu na kuongeza kwamba wakazi wa Dar es salaam sasa watarajie kupata maji Safi
na Salama.
"Naipongeza sana
Serikali kwa kufanikisha mradi huu,kweli
wamefanya kazi kubwa sana, mimi na wabunge wenzangu tumeona na
tumeridhishwa na utendaji wa Serikali katika kuhakikisha jiji la Dar es salaam
linapata maji safi na salama"
Ameiomba Serikali kuweka
msisitizo katika uimarishaji wa miundombinu ili kuwezesha maji kufika kwa
urahisi katika makazi ya watu.
Naye Mhe. Dkt.Sware
Semesi, Mbunge wa viti maalum mkoa wa Dodoma akiuzungumzia mradi huo amesema
kuwa ameridhishwa na miundombinu imara iliyojengwa na kuiomba serikali
kusimamia usambazaji wa huduma hiyo kwa wananchi.
" Mimi pamoja na
wabunge wenzagu tumeshuhudia mradi huu ni mkubwa,kilichobaki kwa mamlaka
zinazohusika ni kujipanga na kuhakikisha kunakuwa na mgawanyo mzuri wa maji
haya,kufanyika kwa Uhakiki na ukusanyanji wa ankara za wateja unaoendana na
matumizi halisi ya maji hayo ili huduma hii iwe endelevu" Amesema.
Aidha, ametoa wito kwa
DAWASCO kusimamia kikamilifu usambazaji wa lita milioni 270 zinazozalishwa kwa
siku na mtambo wa Ruvu chini kwenda
matangi ya maji yaliyoko Chuo
Kikuu Ardhi
Source: Aron Msigwa -
MAELEZO.
COMMENTS