DAR ES SALAAM, Alhamisi , Aprili 7 2016 – TUKIO kufanyika kwa mbio za kwanza mnamo mwaka 2001 Mbio za Mbuzi...
DAR
ES SALAAM, Alhamisi , Aprili 7 2016
– TUKIO kufanyika kwa mbio za kwanza mnamo mwaka 2001 Mbio za Mbuzi za Hisani
Dar es Salaam zimechangisha zaidi ya shs bilioni 1 kwa ajili vituo vya hisani
vya hapa nchini, na katika mwaka wake wa
16 mbio hizo zipo tayari kuendelea kukusanya fedha.
Mbio za Mbuzi za Hisani Dar es Salaam
2016 zinatarajiwa kufanyika Septemba 10 mwaka huu kuanzia saa sita mchana
kwenye Viwanja vya The Green, Barabara ya Kenyatta jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti Mwenza wa Kamati ya Mbio za
Mbuzi za Hisani Dar es Salaam, Rachel Carlin anasema msaada usio na kifani kwa
Mbio za Mbuzi unaotoka katika jamii ni wenye thamani ya kipekee.
“Kila mwaka tunaweza kuandaa tukio hili
kutokana na misaada kwa wafadhili na bila kusahau watu wanaohudhuria katika
siku yenyewe ya mbio za mbuzi,” alisema.
“Na kutokana na haya tunahamasisha watu
na mashirika kumiliki mbuzi kwa ajili ya tukio la mbio za mbuzi.
“Kumiliki mbuzi ni jambo lenye bashasha
nyingi, hususan akishinda lakini pia ni vyema kuwa mmoja wa wawezeshaji wa mbio
hizo kwani hutusaidia kukusanya fedha,” akaongeza Bi. Carlin.
Kutokana na idadi ya mbuzi kuwa ndogo
wanaopenda kumiliki mbuzi wanahamasishwa kutembelea tovuti na kupakua fomu ili wasijeambulia patupu.
Kwa wale wanaotaka kujaribu bahati zao
kushiriki mashindano ya mavazi ya kupendeza kauli mbiu ya Mbio za Mbuzi kwa mwaka
huu ni; ‘Wakati katika Mbio’ inayoleta
motisha wa aina tofauti. Kauli hii ipo wazi kwa tafsiri mbalimbali ilimradi
ilete msisimko na tukio la kupendeza.
“Wakati
ikiwa ni kuleta furaha, sababu tunaandaa tukio hili kila mwaka ni kuchangisha
fedha kwa ajili ya vituo vya hisani vya kitanzania, hivyo naviomba vituo vyote
hapa nchini vilivyosajiliwa kutembelea tovuti yetu na kupakua fomu ya maombi,”
anasema Janine Deetlefs, mmoja wa viongozi wa kamati ya mbio za mbuzi.
Help2kids
ni asasi isiyo ya kiserikali inayosaidia
mahitaji ya kielimu ya watoto wenye mahitaji maalumu kwa kuwapatia nyenzo
muhimu kuwawezesha kuendelea na elimu ya msingi na sekondari.
“Mbio
za Mbuzi za Hisani Dar es Salaam zimeisaidia help2kids kukamilisha malengo yao
ya kujenga jengo la bafu na choo katika shule ya msingi tulio na ushirika
nayo,” anasema Justine LeDonne, Meneja miradi wa Help2kids.
“Mbio
za Mbuzi za Hisani huwezesha mashirika madogo na makubwa kama sisi kuboresha
miradi inayoendelea Dar es Salaam. Kwa gharama za uendeshaji za kila siku,
kipaumbele katika mafanikio ya shirika dogo kupata maendeleo makubwa katika
miradi kunaweza kuchukua miaka mingi endapo hapatakuwemo na uwezeshaji makini.
Mbio za ,Mbuzi huwezesha mipango hiyo na miradi kufikia ukamilifu,” akaongeza.
Kamati ya watu wanaojitolea huandaa
tukio la Mbio za Mbuzi za Hisani Dar es Salaam, na wengi tu hujitolea kutuunga
mkono siku ya mbio za mbuzi.
“Mwisho mbio za mbuzi zisingeweza
kufanyika kama tusingekuwa na wafadhili, na kama wakati wa nyuma idadi kubwa ya
mashirika imekuja tena kusaidia mbio za mbuzi mwaka huu.
“Ningependa
kwa namna ya kipekee kutambua mchango wa wafadhili wetu ambao ni: Hoteli ya Southern
Sun Hotel, Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Kampuni ya vinywaji baridi ya
Coca-Cola (Kwanza), Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo, Benki ya Stanbic,
Toyota Tanzania, Regent Tanzania Ltd, Shirika la Ndege la Uswisi, na Kampuni ya
Continental Outdoor,” Bi. Deetlefs akahitimisha.
Wale wanaopenda kununua mbuzi au
kusaidia siku ya tukio wanahamasishwa kuwasiliana na Kamati ya Mbio za Mbuzi
Dar es Salaam.
MWISHO.
Taarifa
kwa Wahariri: Picha
zenye ubora za mashindano ya mwaka 2015
zinaweza kupatika hapa:http://bit.ly/1F8OUf7
Fomu ya kuomba msaada inaweza
kupakuliwa hapa; www.goatraces.com
Kwa taarifa zaidia au kuandaa
mahojiano, tafadhali wasiliana na:
Mbio za Mbuzi +255 712 575 747 au barua
pepe: goatraces@goatraces.com
Peter Mgongo kwenye +255 767 765 454 au
barua pepe: mgongo@gmail.com
Kuhusu Mbio za Mbuzi.
Tokea mbio za mbuzi za kwanza mnamo
mwaka 2001, Mbio za Mbuzi za Dar es Salaam zimekua haraka hata kuwa tukio kubwa
la hisani jijini Dar es Salaam.
Wazo la mbio za mbuzi lilianza Uganda
mwaka 1993 wakati jumuiya ya wafanyabiashara walipobuni njia ya kipekee ya
kuchangisha fedha kwa kuanzisha mbio za mbuzi labda wakiongeza ubunifu
wakifananisha na mbio za farasi za kifalme nchini Uingereza lakini huku Afrika
Mashariki wakitumia mbuzi.
Kila mwaka Mbio za Mbuzi za Dar es
Salaam hukusanya mamilioni ya shilingi kuwezesha mashirika madogo ya kitanzania
na vituo vya hisani kusaidia jamii yao.
Mbio za Mbuzi za Hisani za Dar es Salaam
zinapenda kuwashukuru kila mmoja, kuanzia wafadhili wetu, wote waliomiliki
mbuzi, walioshiriki katika mchezo wa kubahatisha na kutabiri mbuzi mshindi au
wale waliokuja tu ili kupata burudani, kwa michango yao iliyowezesha kuleta
mabadiliko makubwa katika maisha ya watanzania wengi.
Kamati ya watu wanaojitolea kuandaa mbio za mbuzi
2016 ni pamoja na:
Rachel Carlin (Mwenyekiti mwenza),
Janine Deetlefs (Mwenyekiti mwenza), Danielle Kidd Fanning (Hisani)Karen
Stanley (Katibu), Paul Backhurst (Mhazini),
Kerri Mramba (Uwanjani), Kurstii Perks
(Bahati nasibu), Hiren Soni (Getini) Alan Sutton (Uwanjani).
COMMENTS