H 3424 page 10 Na John Gagarini, Kibaha MADIWANI wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani wameitaka Halmashauri kudhibiti upotevu wa f...
H 3424 page 10
Na John Gagarini, Kibaha
MADIWANI wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani wameitaka Halmashauri kudhibiti upotevu wa fedha sh bilioni 1.1 kwa mwaka kutokana makusanyo kuwa chini hivyo kushindwa kufikia malengo.
Wakizungumza kwenye baraza la madiwani la halmashauri hiyo, baadhi ya madiwani walisema upo upotevu wa fedha nyingi na kwamba endapo mianya hiyo itazibwa itasaidia kudhibiti hali hiyo.
Akizungumzia namna fedha hizo zinavyopotea, Diwani wa Kata ya Tumbi, Hemed Chanyika alisema madiwani walifanya utafiti kwenye vyanzo vya mapato na kugundua upungufu mkubwa katika ukusanyaji.
Chanyika alisema mfano ni mapato ya ushuru wa mchanga ambako waligundua magari yanayoingia yanachukua mchanga kwa siku ni 103 .
Alisema gari moja linalipia sh 3,000 kwa mwaka na mapato ni sh bilioni 1.1 ingawa makiso yaliyowekwa ni sh milioni 264.6 kwa mwaka huku kukiwa na tofauti ya sh milioni 900.
Alisema kwa upande wa stendi ya Maili Moja makisio yalikuwa ni sh milioni 320 kwa mwaka ambapo magari yanayopita ni zaidi ya 500 kwa siku ambayo yanaingiza takribani sh milioni 564 kwa mwezi. Upotevu unakadiriwa kuwa sh milioni 183.
Machinjio yalikadiriwa kukusanya sh milioni 25 na kufanya upotevu kuwa sh milioni 56. Kwa siku wanachinjwa ng’ombe 45 na ushuru ni sh 5,000 kwa mwaka 25.
Mwenyekiti wa halmashauri, Leonard Mlowe alisema kuwa katika kuhakikisha makusanyo hayo yanafikia asilimia 100, atakuwa akikutana na watendaji wa serikali za mitaa na kata kujadili namna ya kukusanya mapato hayo.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha ,Leah Lwanji alisema suala hilo watalifanyia kazi kwa kulirudisha kamati ya fedha kwa ajili ya namna ya kudhibiti upotevu wa fedha hizo ili kuweza kufikia malengo yaliyowekwa.
Na Fadhili Abdallah, Kigoma
BAADHI ya wananchi wanaojishughulisha na uzalishaji wa asali kupitia mradi kuendeleza sekta ya nyuki, wameeleza kunufaika nao na kushuhudia mabadiliko ya kiuchumi waliyo nayo.
Wakizungumza na gazeti hili wakati wa mkutano wa wadau uliotumika kutoa
taarifa na tathmini ya utekelezaji wa mradi huo wa miaka minne,
baadhi ya wananchi walisema wana mafanikio makubwa kiuchumi.
Mkazi wa Nguruka kati wilaya ya Uvinza mkoani Kigoma, Seifa Kabobo alisema
baada ya kupata elimu na mbinu za uzalishaji wenye tija
ameweza kuongeza uzalishaji na mauzo.
Alisema amewaondoa watoto wake kwenye kazi za uzalishaji wajikite kwenye masomo kitendo ambacho kimewezesha watoto wake wawili kufaulu vizuri kwenye mtihani wa kidato cha nne.
Kwa upande wake Sawia Damas mkazi wa kijiji cha Itumbiko wilaya ya Kakonko
mkoani Kigoma alisema mradi huo umemwezesha kuongeza thamani ya mazao
hayo kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali ikiwemo mafuta ya kujipaka,mvinyo,
sabuni za kuogea,mishumaa na dawa za ngozi.
Alisema ametanua wigo wa biashara na kuifanya sekta ya nyuki kuwa na manufaa kiuchumi kwa
wazalishaji.
Sawia alisema amekarabati nyumba yake imekuwa bora na anaendelea kufanya shughuli nyingine za ujasiliamali kutokana na kipato kinachotokana na mazao ya nyuki .
Mradi huo uliokuwa ukifadhiliwa na Serikali ya Ujerumani kupitia shirika
lake la maendeleo (BTC) umefikia mwisho. Mratibu wa mradi huo kwa mkoa
Kigoma, Nicodemus Mpemba alisema wanayo mafanikio makubwa katika miaka
minne ya utekelezaji wa mradi huo.
Mpemba alisema elimu iliyotolewa kwa wafugaji
nyuki imesaidia wazalishaji wa asali kuboresha njia za uzalishaji,uchakati
kuongeza thamani,mbinu za kutafuta masoko na kupanua miradi yao jambo
ambalo limewezesha kusaidia kuongeza uzalishaji nyuki maradufu mkoani
Kigoma.
Mratibu wa mradi huo kwa wilaya za Kibondo na Kakonko, Seif Salum alisema miaka minne ya utekelezaji wa mradi huo wazalishaji wa asali wameongeza kutoka 2500 na kufikia zaidi ya 6000 ambapo uzalishaji umeongezeka kutoka tani 100 hadi kufikia tani 400 kwa mwaka jambo ambalo pia linasaidia kuongeza kipato cha mzalishaji wa
asali.
Na Veronica Mheta, Arusha
UCHELEWESHWAJI wa fedha za miradi pamoja na mchakato wa upitishaji wa fedha
za manunuzi vimetajwa kuwa miongoni mwa mambo yanayokwamisha utekelezaji wa miradi ya
maendeleo kwenye halmashauri mbalimbali nchini.
Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(Tamisemi), Mussa Iyombe alisema hayo wakati akifungua kikao cha kujadili mapitio ya Mradi wa Uboreshaji Miji Tanzania (ULGSP) inayotekelezwa katika halmashauri zaidi ya 18 inayofadhiliwa na Benki ya Dunia .
Iyombe alisema awali ucheleweshwaji huo ulikwamisha
miradi mbalimbali katika halmashauri zinazofadhiliwa na benki ya dunia.
Alisema awali mchakato wa manunuzi ulikuwa na hatua mbalimbali lakini kwa maboresho hayo ya serikali, itakuwa rahisi kwa halmashauri kuendesha miradi yao kwa kupitisha fedha kwa ridhaa ya madiwani zenye thamani ya kuanzia sh milioni 50 hadi sh milioni 900.
"Awali wakurugenzi walipata tabu kusimamia miradi mbalimbali katika halmashauri zao sababu ya mchakato wa sheria za manunuzi lakini hivi sasa
miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia itatekelezwa kwa wakati kutokana na serikali kurahisisha mchakato huu wa manunuzi, " alisema.
Aliwataka wakurugenzi wa halmashauri kuhakikisha wanatumia fursa hiyo kuleta maendeleo kwa wananchi pamoja na kuainisha vipaumbele vya miradi ya maendeleoi kutatua changamoto zilizokuwa zikiwasumbua wananchi kwenye halmashauri zao.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita, Marx Kamaoni aliishukuru serikali kwa kuwezesha kuiboresha sheria hiyo ya manunuzi.
Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Songea, Jenifa Omolo alisema ULGSP umeleta maendeleo kwa manispaa hiyo kwani umewezesha ujenzi wa stendi ya
mabasi ya kisasa inayotarajia kuzinduliwa mwezi huu.
Mhandisi wa mradi huo wa ULGSP, Gilbert Mfinanga alisema ulianza mwaka 2013 na unatarajia kuisha 2018 na utqgharimu dola za kimarekani milioni 255.
Washiriki wa mkutano huo ni wakurugenzi, wahandisi, wachumi, maofisa mazingira, maofisa maendeleo ya jamii na watunza hazina wa halmashauri 18. Pia unahudhuriwa na ujumbe kutoka Uganda ukiongozwa na Waziri wa Nchi, Maendeleo ya Miji, Rosemary Najemba.
Na Mwandishi Wetu
BENKI ya FNB imepanua wigo kitaifa kwa kufungua tawi jipya jijini Mwanza.
Akizungumza jana wakati wa ufunguzi wa tawi hilo katika eneo la Rock City Mall, Mkuu wa Biashara wa benki hiyo, Francois Botha alisema uzinduzi umelenga kukidhi ongezeko kubwa la mahitaji ya huduma za kibenki na za kifedha katika mkoa huo.
“Uzinduzi wa tawi la Mwanza ni sehemu ya uwekezaji endelevu na mkakati wa kuhakikisha maeneo mengi ya nchi yanapata huduma bora za kifedha. Pia tumezingatia ukuaji wa haraka wa mkoa wa Mwanzaambao una mchango mkubwa katika kukuza uchumi wa Tanzania.”
Botha alisema tawi la Mwanza ni la tisa miongoni mwa mtandao wa matawi ya FNB Tanzania ikiwa ni sehemu ya mpango mkakati wa kupanua mtandao wa matawi ili kuyafikia maeneo yote nchini.
“ First National Bank (FNB) daima tunafikiri njia mbalimbali za ambazo tunaweza kutoa huduma za kibenki kwa urahisi kwa wateja wetu. Tawi letu la Mwanza litatoa ufumbuzi wa kina kwa wateja wanao ishi Mwanza na maeneo jirani yenye biashara inayokua kwa kasi,” alisema Botha.
Aliongeza kusema; “Mara kwa mara tunafikiria mbinu mpya za kutuwezesha kutoa huduma inayowapa unafuu wateja wetu kwa kupeleka huduma hiyo karibu na makazi pamoja na biashara zao. Tawi hili litarahisisha huduma kwa wateja wetu wanaoishi jijini Mwanza na maeneo ya jirani ambayo yana biashara nyingi zinazokua kwa kasi.”
Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella alisema mkoa wake una uwezo mkubwa wa kiuchumi na ukuaji mkubwa wa sekta mbalimbali za kiuchumii karibuni ni ishara kuwa Mwanza inakua kwa kasi.
"Tunakaribisha uwepo wa FNB na tunatazamia kuwasaidia kuimarisha huduma zenu hapa na mikoa mengine," alisema Mongela.
Alisema mbali na mkoa wa Mwanza kuwa na mchango mkubwa katika maendeleo ya uchumi wa nchi bali pia inazalisha mali nyingi na ina utajiri mkubwa wa rasilimali.
Tawi hilo lililofunguliwa kwenye jengo jipya la Rock City Mall litatoa huduma za kawaida za kibenki pamoja na huduma za dijitali kwa masaa 24 ili mahususi kukidhi mahitaji ya watumiaji huduma pamoja na wafanyabiashara katika eneo hilo.
Ends
Huziangyang Jacko, Meneja wa Huawei nchini Tanzania.
TAARIFA
KWA VYOMBO VYA HABARI
29 Aprili 2016
Dar es Salaam
Mkakati
wa Huawei katika kubadili namna uonavyo dunia iliyokuzunguka
Mwezi Aprili, Huawei wamezindua simu
iliyokua ikisubiriwa kwa muda mrefu katika mlolongo wao wa simu zao za P
Series; Huawei P9. Uzinduzi wa Huawei P9 umezingatia kipaumbele cha teknolojia
ya hali ya juu. Toleo hili la tisa la P Series limewezeshwa na Kampuni ya Huawei
pamoja na kampuni mashuhuri kwa utengenezaji wa camera duniani Leica. Simu hii
ina kamera ya kipekee yenye lenzi mbili, ambayo imeweka rekodi katika
teknolojia ya kamera za simu za kisasa, ikiwa na mwanga Zaidi na ubora Zaidi,
kupata picha zenye rangi nzuri Zaidi katika staili ya Leica ya kipekee.
Watanzania wanategemea kupata simu
hii yenye teknolojia ya hali ya juu na ya kipekee katika kamera hivi karibuni.
Hii inafuatia uzinduzi wa simu hiyo uliofanyika mji wa Dubai wiki hii. Uzinduzi
huo wa kipekee ambao ulihudhuriwa na viongozi wa Huawei Tanzania na Waandishi
wa Habari umeashiria upatikanaji wa simu hii katika soko la Tanzania hivi
karibuni.
Tokea uzinduzi wake mji wa London,
simu hiyo imepata mapokezi makubwa kama simu “inayobadili namna uonavyo dunia”.
Simu mpya ya kipekee Huawei P9 ina malengo kubadili ubora wa picha unaopatikana
katika timu za kisasa maarufu kama “smartphone”. Teknolojia katika simu hiyo
inabadili namna tunavyopiga na kufurahia picha, hii imetokana na shauku ya
Huawei kuendelea kuvuka mipaka ya uvumbuzi, ikilinganishwa na uzoefu na kipaji
katika utengenezaji wa kamera na lenzi wa Leica pamoja na ushirikiano mzuri
katika kutengeneza P9.
Waliokuwepo katika uzinduzi huo ni
pamoja na viongozi wakuu wa Huawei Tanzania akiwemo Bwana Huziangyang Jacko,
Meneja wa Huawei nchini Tanzania, Lydia Wangari Meneja Masoko kampuni ya Huawei
Tanzania, waandishi wa Habari na wadau mbalimbali kutoka Tanzania.
Akionglea ujio wa simu hiyo katika
soko la Tanzania Bwana Huziangyang Jacko, Meneja wa Huawei nchini Tanzania
alisema ”Tunategemea kuleta simu mpya ya Huawei P9 kwa wateja wetu wa Tanzania
hivi karibuni; Tunaamini teknolojia hii ya hali ya juu na ya kipekee
iliyotokana na utafiti wa hali ya juu na shauku ya kubadili namna watumiaji
wetu waonavyo dunia inayo wazunguka, P9 ikifanya kazi na Leica, tumeweza
kufanya maajabu katika teknolojia ya lenzi ya kamera”.
Akiongea katika uzinduzi huo, Lydia
Wangari Meneja Masoko Huawei Tanzania alisema, ”Tunaendelea kuzindua simu mpya ,
tukitilia mkazo katika teknolojia ya kipekee. Kwa kushirikiana na wadau
wengine, tumeweza kujumuisha utamaduni, mtindo ya maisha ya wateja wetu na teknolojia
ili kuwapatia wateja watu simu bora zaidi”.
Kuongezeka kwa aina mbalimbali za
simu za mkononi za smartphone nchini Tanzania inaashiria ukuaji na umuhimu wa
Tanzania katika soko duniani huku wa Tanzania Zaidi wakigundua umuhimu wa
teknolojia maishani mwao. Mahitaji katika maendeleo na simu za kiteknolojia yanaongezeka kila kukicha nchini
Tanzania na kampuni ya Huawei imeendelea kutatua hitaji hilo nchini Tanzania.
Kufuatia mafanikio ya simu aina ya P
zijulikanalo kama “P Series”, kwa ujumla mapokezi ya simu ya Huawei P9 ni
mazuri duniani kote. Huawei Tanzania wana matarajio makubwa juu ya ufanyaji
kazi wake katika soko la Tanzania. Wakiahidi watumiaji simu yenye nguvu na
ubora wa kipekee usio linganishwa, simu mpya ya P9 itapatikana katika rangi
nne: Dhahabu, kijivu, Dhahabu iliyoiva Zaidi na Siliva huku P9 Deluxe Version
ikipatikana katika rangi ya dhahabu na Nyeupe.
Familia ya simu za Huawei P9 imetumia njia za kipekee na ubora wa hali ya
juu kubadili namna tunavyoona dunia iliyotuzunguka. Inaendeleza heshima ya
Huawei ya simu zenye ubora wa juu ambazo zimeacha alama katika soko kwa ubora
na ufanisi.
Huawei itaendelea kukamata fursa mbalimbali
ili kubadili soko na kuinuka duniani katika biashara za watumiaji wa simu za
mkononi. Huku simu za kampuni hiyo zikizidi kua na teknolojia ya hali ya juu,
Huawei itaendelea kutengeneza vifaa vinavyoweza tumika na mteja wakati wowote
na mahali popote. Na Wataendelea kuungana na wadau wengine katika soko la
vifaa, programu. Kupitia uvumbuzi wa teknolojia pamoja na kushirikiana na wadau
mbalimbali, kampuni ya Huawei ina ahidi kuleta vifaa Zaidi kwa wateja wake wote
duniani.
Kuhusu Huawei
Huawei
ni vinara wa teknolojia na mawasiliano hususani katika kutimiza matakwa ya
wateja wao, katika kuhakikisha wanawapa wateja wao kile kilicho bora katika
viwango vya juu, umuhimu wa mawasiliano na vifaa vya mawasiliano vinatumika
katika nnchi Zaidi ya 170 na mikoa yake, Huawei ilishika nafasi ya 228
ulimwenguni kwa mwaka kutokana na mapato yake mwaka 2014 kati ya makampuni 500.
Mapato ya kampuni yamefikia kiasi cha dolla za kimarekani bilioni 46.5. Huawei
imeshika nafasi ya 3 kwenye usambazaji wa simu kwa mwaka 2015 kwa kusambaza zaidi
ya simu milioni 100 duniani kote, Kampuni ya Huawei ipo katika kuhakikisha
inatoa ushirikiano katika kukuza na kuboresha vifaa vya mawasiliano duniani kote.
Kampuni
ya Huawei inajihusisha na utengenezaji wa simu za mkononi, huduma za intaneti
kwa njia ya modemu na vifaa vya matumizi ya nyumbani.
Huawei
imeimarisha mahusiania ya biashara na makampuni kama Tigo, Vodacom, Tigo,
Vodacom, Airtel, Zantel, Sasatel, TTCL, SmileCom, Safaricom, MTN, CellC,
Telefónica, China Mobile, Vodafone, T-Mobile, BT, China Telecom, NTT Docomo, France
Telecom, na China Unicom.
Kupata
habari Zaidi tembelea www.huaweidevice.com
COMMENTS