ZULMIRA ATAKA KAZI KWA PAMOJA KUHAMI MAENEO YA URITHI WA DUNIA

Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigu...

Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues amewakumbusha wadau wa urithi wa dunia na maeneo ya hifadhi kufanyakazi kwa pamoja kwa lengo la kuhifadhi na kuyaendeleza maeneo hayo bila kuondoa ushiriki wa wananchi wanayozunguka.

Kauli hiyo ameitoa katika mafunzo yaliyoandaliwa na Shirika lake kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia mjini Marangu Moshi, kufuatia makubaliano na serikali ya Tanzania.

Alisema akizungumza na washiriki kwamba UNESCO inachofanya ni kuanzisha safari ambayo inaweza kuwa ngumu na ndefu lakini washiriki wake ni lazima kutambua namna ya kuendelea kufanya menejimenti ya maeneo ya hifadhi na urithi wa dunia kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho.

Akifungua mafunzo hayo ambayo wataalamu ni washiriki wenyewe wakitumia njia ya kuelewa ya methodolojia ya uchambuzi wa vikwazo (Bottleneck Analysis Methodology) alisema safari ya kufanikisha menejimenti ya maeneo hayo duniani na hasa hapa nchini ni yenye changamoto nyingi na kwamba wadau wote wanatakiwa kuwa pamoja kuvishinda vikwazo hivyo na kuifanikisha safari.

Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akizungumza katika warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na shirika lake kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia iliyomalizika mwishoni mwa wiki mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.(Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)

Akizungumza katika warsha hiyo ambayo imechukua wadau mbalimbali wa masuala ya urithi na menejimenti zake kutoka serikalini, taasisi zisizo za kiserikali na wananchi wengine, alisema kwamba maeneo hayo yamezungukwa na wananchi na pamoja na kuwawekea sheria za kutoharibu na kuyachakaza ipo haja ya kushirikiana nao namna ya kupanga kuyaendeleza maeneo hayo huku yakiwa yamebaki katika hali inayotakiwa.

Mafunzo hayo yamelenga kuwajengea uwezo wa kupanga maendeleo katika maeneo ambayo ni ya urithi wa dunia, binadamu na maeneo ambayo uhai unaweza kuwepo.

Aidha akifafanua zaidi mtawala huyo wa UNESCO nchini Tanzania amesema mafunzo hayo yamelenga kuwapa wahusika nadharia zinazofaa katika safari ndefu ambayo UNESCO nayo itashiriki na isingelipenda kumwacha hata mtu mmoja nyuma.

Mafunzo hayo yanatolewa kufuatia mpango wa UNESCO wa kutaka kuwa na uhakika na kuhami maeneo hayo ya urithi; huku mamlaka zikitoa ushirikiano ili kuwezesha malengo ya maendeleo endelevu, ambayo ndiyo ajenda ya dunia kuelekea 2030, yanafikiwa bila kuathiri maeneo tajwa.
Ofisa anayeshughulikia watu na maeneo yenye uhakika wa uhai: Biashara zinazozingatia mazingira na uchumi unaombatana nao kutoka Sekta ya Sayansi Ofisi ya Unesco, Dar es salaam, Myoung Su Ko akiwasilisha mada kwa washiriki wa warsha hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Kilimanjaro Resort mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.

Alisema kwa kuwa kitaifa, serikali imeshatoa matamko ya kisera na kuweka mikakati ya utekelezaji wa taratibu za kuhami maeneo ya kiutamaduni na ya asili ipo haja ya wadau wengine kuona namna ya kufanyakazi kama timu katika safari ambayo kila mmoja anastahili kuwaijibika kwa namna yake hata kama kunatokea changamoto.

Alisema wadau wanatakiwa kuangalia namna ya safari zao zinavyostahili kufanywa na kuwa, kwa lengo la kutumia raslimali zilizopo kutekeleza mipango ya maendeleo na ya kuhami maeneo hayo bila kutegemea msaada wa wafadhili au wahisani.

Awali katika ujengaji wa wazo la mafunzo ilielezwa kuwa pamoja na kuwapo na juhudi kubwa za kuhami maeneo ya urithi wa dunia na kuyasajili maeneo ambayo uhai unaweza kuwapo na wanadamu, kumekuwepo na changamoto kubwa za maendeleo ambazo zinatishia kuvuruga mfumo tete wa ikolojia uliopo.

Katika kufanikisha hifadhi ya maeneo hayo kumeonekana changamoto za upungufu wa rasilimali watu wenye uwezo na vifaa vya kushughulikia uharibifu, ukosefu wa uwezo wa kuhifadhi maeneo hayo kwa kuoanisha na uwapo wa watu.
Mtaalamu wa programu na utamaduni kutoka Ofisi za Unesco Afrika Mashariki Bi. Karalyn Monteil akiwasilisha mada kuhusu makubaliano ya ulinzi katika maeneo ya urithi na utamaduni wa dunia katika warsha hiyo iliyomalizika mwishoni mwa juma mjini Marangu, Moshi.

Mathalani eneo la Urithi la Kilimanjaro lina changamoto kubwa ya uwezo kiasi ya kwamba mazingira yanaharibiwa huku wakazi wa maeneo hayo wakiwa hawashirikishwi katika maamuzi ya kulinda eneo hilo na hivyo kutojitambua kwamba wao ni kiungo muhimu katika maendeleo na utalii ambao ungewaingizia mapato.

Kutokana na kutoshirikishwa baadhi ya mambo wanayofanya wananchi yanakwenda kinyume na nadharia nzima ya uhifadhi wa maeneo hayo.

Inatarajiwa baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo washiriki watakuwa wamepata uelewa wa mbinu zinazostahili kutumika katika kuwashirikisha na kuhifadhi maeneo hayo huku ajenda za kidunia za maendeleo endelevu zikiendelea kufanywa.
Aidha watakuwa wameelewa mbinu mbalimbali zinazoweza kutumika kuhifadhi na kuendeleza maeneo ya urithi na yale ambayo yamehifadhiwa kwa kuwa uhai unaonekana kuwapo. Aidha mameneja watakuwa na uwezo wa kutambua haja ya ushiriki na ushirikishi katika mipango ya maendeleo na hifadhi pale walipo.Warsha hiyo imemalizika Juni 25.
Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues akiendelea kuwapiga msasa wadau na mameneja wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia katika warsha ya siku tatu iliyofanyika mkoani KIlimanjaro.
Pichani juu na chini ni washiriki wakitoa maoni katika warsha ya siku tatu kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia iliyomalizika mwishoni mwa juma mjini Marangu, Moshi.

Ofisa Utamaduni wa Shirika la UNESCO, Dar es Salaam, Michaela Konopikova (kulia) akiteta jambo na Mtaalamu wa programu na utamaduni kutoka Ofisi za Unesco Afrika Mashariki Bi. Karalyn Monteil wakati warsha ya siku tatu kwa wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia iliyoandaliwa na UNESCO, mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.
Sehemu ya wadau wa mazingira ya hifadhi na urithi wa dunia waliohudhuria warsha ya siku tatu iliyoandaliwa na UNESCO, mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.

Mtaalamu wa programu na utamaduni kutoka Ofisi za Unesco Afrika Mashariki Bi. Karalyn Monteil akifafanua jambo kwa washiriki wa warsha hiyo. Kulia ni Mkuu wa ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Tanzania, Zulmira Rodrigues
Ofisa Maliasili wa Mkoa waKilimanjaro, Emanuel Kiyengi akipitia moja ya makabrasha yanayoonesha maeneo ya urithi wa dunia katika washa hiyo ya siku tatu iliyomalizika mwishoni mwa juma mjini Marangu, mkoani Kilimanjaro.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: ZULMIRA ATAKA KAZI KWA PAMOJA KUHAMI MAENEO YA URITHI WA DUNIA
ZULMIRA ATAKA KAZI KWA PAMOJA KUHAMI MAENEO YA URITHI WA DUNIA
https://blogger.googleusercontent.com/img/proxy/AVvXsEjxYy92vogYRzNueyOqqYXpvpWskNuuk7DGwkiTXItxt0fav083EBW4CmlrnHxLW284y50tvvJksYakA_baQBxuK6D2exnit2xR4xaUeeFddlYJDxgvwCoiqnRbfHEQlBSHLDQZF6xn9zeNJwLZn6qWZulUMlxqgV-lsFYClnG0rlvP_Q3jhtY0RX3n1eba1RCoGnylIxutYXSNoM676GSx0jhXF2WbSraGAHUUmRu43fmv2pXR3Br3b6wsLz5ML-umhyphenhyphentR2CoHHxdZfZXRZFfgLjaRnrwcOMjs83OhzGnWDDhMvwA9WUH52e7nVHmBMwmGUSTNvsWdQbR3u2-3Hws=
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/06/76-of-many-zulmira-ataka-kazi-kwa.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/06/76-of-many-zulmira-ataka-kazi-kwa.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy