AKINAMAMA DAKAWA WAFUGA NYUKI KUPAMBANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA

Ofisa Nyuki wa Wilaya ya Mvomero, Oscar Kunambi (aliyechuchumaa kushoto) akisaidiana na mwanakikundi cha Dakawa Green Voices, Neema O...



Ofisa Nyuki wa Wilaya ya Mvomero, Oscar Kunambi (aliyechuchumaa kushoto) akisaidiana na mwanakikundi cha Dakawa Green Voices, Neema Obeid, kuweka vizuri mzinga.
Mwanahabari Judica Losai (wa pili kushoto) akimuuliza maswali Ofisa Nyuki wa Wilaya ya Mvomero, Oscar Kunambi, wakati wakiwa kwenye eneo la ufugaji wa nyuki.

Baadhi ya mizinga ya akinamama wa Dakawa Green Voices ikionekana kuning’inia kwenye miti. Mizinga hii tayari ina nyuki.

Akinamama wa Dakawa Green Voices wakisikiliza maelezo kutoka kwa mtaalam wa ufugaji nyuki, Oscar Kunambi, ambaye hayupo pichani.

Ofisa nyuki wa Wilaya ya Mvomero,, Oscar Kunambi, akiwaelekeza akinamama wa Dakawa Green Voices namna ya ufugaji bora wa nyuki.


TAKRIBAN kilometa 10 kutoka Kijiji cha Dakawa kuna kitongoji cha Magogo kilichoko msituni kabisa ambako pia kuna mashamba ya mpunga.
Msitu huu ambao bado ungali na miti mingi ya asili ambayo imenusurika kucharangwa na wachoma mkaa na wanaotafuta ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo, ndiko akinamama wapatao 30 wameamua kutundika mizinga kwa ajili ya ufugaji wa nyuki katika shamba lenye ukubwa wa ekari nne.
Licha ya kujikwatua vilivyo, lakini wanapoingia katika msitu huu akinamama hawa hawana mchezo kabisa, baadhi yao wanavaa mavazi maalum ya kujikinga na nyuki na kuanza kukagua mizinga yao kama tayari nyuki wamekwishaingia.
“Kujipamba ni jambo la kawaida, lakini tunapokuja huku tuko kikazi zaidi,” anasema Neema Obeid huku akipenya kwenye vichaka kuiendea mizinga ambayo iko juu ya miti mikubwa.
Akina mama hao wa kikundi cha Dakawa Green Voices Women Group wameamua kuingia kwenye ujasiriamali wa ufugaji wa nyuki kwa malengo makubwa mawili – kupata fedha kutokana na mazao ya nyuki pamoja na kupambana na mabadiliko ya tabinchi.
“Misitu inateketea, watu wanaendelea kuchoma mkaa na wengine wanafyeka miti ili wapate mashamba, lakini kwa kuanzisha ufugaji huu wa nyuki, kamwe hatutakubali kuona yeyote akikata hata fimbo, achilia mbali miti mikubwa,” anasema Bi. Mariam Bigambo, mshiriki kiongozi wa mradi huo.
Mariam Bigambo ni miongoni mwa akinamama 10 waliopatiwa mafunzo nchini Hispania mapema mwaka huu na wanatekeleza kwa vitendo mradi wa Green Voices, ambao unafadhiliwa na taasisi inayojihusisha na maendeleo ya wanawake wa Afrika, ijulikanayo kama Women for  Africa Foundation  inayoongozwa na Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania, María Teresa Fernández de la Vega. Hapa nchini, mradi huo unasimamiwa na asasi ya Environment Media Agenda (EMA) chini ya uratibu wa Bi. Secelela Balisidya
Akinamama wengine wanatekeleza miradi mbalimbali ya ujasiriamali unaoendana na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabianchi katika mikoa ya Dar es Salaam, Morogoro, Kigoma, Kilimanjaro, Pwani na Mwanza.
Mama Bigambo anasema kwamba, ufugaji huo unahitaji kutunza mazingira ili kuwawezesha nyuki kupata chakula chao hasa nekta na maji, hivyo ni vizuri kuhakikisha mazingira yanakuwa salama.
Aidha, anasema kwamba, kwa kuwa Tanzania, kama zilivyo nchi nyingine duniani, inakabiliwa na mabadiliko ya tabianchi, ni vizuri kufanya shughuli za uchumi zinazohakikisha kwamba mazingira yanatunzwa na wakati huo huo shughuli hizo zikichangia kupambana na mabadiliko ya tabiachi, huku ufugaji wa nyuki ukiwa miongoni mwa shughuli hizo.
“Bila kutunza mazingira hata hao wanaokata mkaa na wanaotafuta mashamba watalia baadaye kwa kuwa miti itakwisha, tutabaki na jangwa ambao halitatoa mazao tena. Tutakufa,” anasisitiza.
Kuhusu ufugaji huo wa nyuki, Mama Bigambo anasema kwamba, ingawa zamani ilionekana kama shughuli za akina baba, lakini kama wanawake watafundishwa wanaweza kuendesha ujasiriamali huo bila shida.
“Gharama kubwa ya ufugaji wa nyuki iko mwanzoni tu – kutafuta mizinga pamoja na eneo bora linalofaa kwa ufugaji ambalo maua na maji yanapatikana kwa urahisi, baada ya hapo kazi yako ni kutembelea na kuangalia maendeleo.
“Nyuki hawachungwi kama ng’ombe, mbuzi au nguruwe wala hawaangaliwi kama kuku, hawahitaji chanjo ya ugonjwa wowote, hivyo ni rahisi kutundika mizinga yako katika eneo husika na kuendelea na shughuli zako nyingine,” anafafanua.
Akizungumzia umuhimu na faida za nyuki, Mama Bigambo anasema kuwa licha ya kusaidia kutunza mazingira, lakini nyuki ni muhimu kwa maisha ya binadamu na viumbe hai vyote, kwani ndio wanaofanya uchavushaji wa mimea.
Anazitaja faida za ufugaji nyuki kuwa ni asali na nta, mazao ambayo yana faida kubwa hata katika soko la kimataifa.
Katibu wa kikundi hicho, Amina Buteta, ana matumaini makubwa kwenye mradi huo na anasema kwamba unaweza kuwakomboa wanawake wa Dakawa na vijiji vya jirani kwa kujipatia kipato kikubwa.
“Tunakuja huku shamba kila baada ya wiki, wakati mwingine tunakuja kwa zamu kuangalia maendeleo, hivyo hatubanwi na ufugaji wa nyuki na tunaendelea na shughuli zetu nyingine,” anasema.
Amina anasema kwamba, wameanza na mizinga 30, lakini malengo yao ni kuwa na mizinga 4,000, lakini changamoto wanayokabiliana nayo ni mtaji wa kununulia mizinga hiyo.
Inaelezwa kwamba, mzinga mmoja unauzwa Shs. 70,000, lakini kutokana na uchumi kuwa mdogo, wengi wanashindwa kupata fedha za kununulia.
“Lakini ipo siku tutafanikiwa tu, hakuna shida, kwa sababu tumedhamiria,” anasema.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Dakawa, Andrea Muhando, anasema ufugaji wa nyuki siyo tu utawakomboa kiuchumi wanawake hao na jamii nzima kwa ujumla, lakini utasaidia kutunza mazingira katika eneo hilo ambalo limeshindwa kuzalisha mazao vya kutosha kutokana na mafuriko ya mara kwa mara pamoja na mvua zisizo za uhakika.
Anasema, kukosekana kwa mvua katika misimu tarajiwa kama ilivyokuwa zamani pamoja na mafuriko makubwa yanayosababisha maafa ni matokeo ya mabadiliko ya tabianchi, hivyo ni vyema wananchi wakaangalia miradi mingine endelevu yenye kipato lakini inayoweza kutunza mazingira.
“Kila mwaka mvua zinashindwa kunyesha kwa wakati na kwa kiwango kinachotakiwa, na zinaponyesha zinakuja kwa nguvu na kuleta madhara hata kwa mimea kama tunavyoshuhudia katika eneo hili kila mwaka.
“Mwaka huu mafuriko yameharibu hekta 240 za mazao mbalimbali, ukiwemo mpunga ambao umekuwa mkombozi wa mkulima, na sasa tunategemea tu katika maeneo ya kondeni pekee,” anasema.
Kwa upande mwingine, Ofisa Nyuki wa Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, Oscar Kunambi, anasema kwamba kuanzishwa kwa mradi wa akinamama hao kutachochea jamii kuingia kwenye ufugaji wa nyuki wilayani humo badala ya kutegemea kilimo na mifugo pekee.
Anasema kwamba, soko la asali ni kubwa nchini Tanzania, ambapo tayari kuna kiwanda kikubwa wilayani Kibaha kinachohitaji malighafi lakini asali inayozalishwa haitoshelezi mahitaji.
Aidha, anasema kwamba, wilaya hiyo ina maeneo mengi yenye misitu ambayo ikitumiwa kwa ufugaji wa nyuki inaweza kuleta faida kubwa kwa jamii na taifa kwa ujumla.
“Unapofuga nyuki, mbali ya kupata faida kutokana na mazao yake, lakini unasaidia kuyalinda maeneo hayo kwa sababu hakuna mtu mwenye akili timamu anayeweza kwenda kukata miti sehemu ambayo kuna nyuki, kwanza usalama wake utakuwa mdogo,” anasema.
Vyanzo vya habari vinaeleza kwamba, asali ina soko zuri kwani kilo moja inauzwa kwa Shs. 15,000 ikiwa shambani.
Kwa mujibu wa Kunambi, mzinga mkubwa wa kisasa una uwezo wa kutoa kati ya kilo 10 hadi 20 za asali baada ya miezi sita tangu nyuki kuingia kwenye mzinga.
Amewataka wananchi katika wilaya hiyo kujitokeza na kuanzisha miradi ya ufugaji nyuki, huku akiahidi kwamba yuko tayari kufanya kazi usiku na mchana kuwasaidia utaalamu na ushauri.
Mkurugenzi wa Wilaya ya Mvomero, George Mkindo, amewapongeza akinamama hao kwa jitihada zao na akasema halmashauri yake itawaunga mkono kwa kila hali.
“Nimeambiwa kwamba wanahitaji shamba, nadhani itakuwa vyema kama tukiongea na vijiji ili kutenga mashamba kwa ajili ya ufugaji wa nyuki kwa sababu inatupunguzia hata sisi kazi kubwa ya kupambana na waharibifu wa mazingira, kwa kuwa wananchi wenyewe watakuwa walinzi,” anasema.

<Mwisho>.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,301,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,23,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: AKINAMAMA DAKAWA WAFUGA NYUKI KUPAMBANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA
AKINAMAMA DAKAWA WAFUGA NYUKI KUPAMBANA NA UHARIBIFU WA MAZINGIRA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifWgm1kDSOmRqVNyLwmdP85tM-Db91uelN1uyt1FMPccvO_RCi9n1zvEeewCk38WVX3nXiwqqazDWhnfvKHYwOHR0BA3RXM8wQmg0w9_IEIwG5EFaNwNggxE1vxEkt-Gq4nR_4d1GztDjb/s640/Dakawa1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEifWgm1kDSOmRqVNyLwmdP85tM-Db91uelN1uyt1FMPccvO_RCi9n1zvEeewCk38WVX3nXiwqqazDWhnfvKHYwOHR0BA3RXM8wQmg0w9_IEIwG5EFaNwNggxE1vxEkt-Gq4nR_4d1GztDjb/s72-c/Dakawa1.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/akinamama-dakawa-wafuga-nyuki-kupambana.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/akinamama-dakawa-wafuga-nyuki-kupambana.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy