DC UKEREWE ASHAURI WANANCHI KULIMA VIAZI LISHE KWA WINGI

 Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania, Maria Tereza Fernandez akisalimiana na viongozi wa serikali wilayani Ukerewe mara baada ya kuwas...



 Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania, Maria Tereza Fernandez akisalimiana na viongozi wa serikali wilayani Ukerewe mara baada ya kuwasili katika bandari ya Nansio tayari kwa kuzindua mradi wa wanawake.

 Mama Maria Tereza akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya mkuu wa wilaya Ukerewe.
 Mama Maria Tereza akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa wilaya. Kushoto kwake ni Balozi Getrude Mongella.
Wananchi wakiwa katika mkutano wa hadhara mjini Nansio.

MKUU wa Wilaya ya Ukerewe mkoani Mwanza, Estomih Chang’a, ameshauri wananchi wa wilaya hiyo kulima kwa wingi viazi lishe (viazi vitamu vya njano) ili kuongeza uhakika wa chakula.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi wa kilimo cha viazi lishe wa kikundi cha wanawake wa Green Voices Bukongo Jumanne Julai 12, 2016, DC Chang’a alisema kwamba kutokana na mabadiliko ya tabianchi yanayosababishwa na uharibifu wa mazingira, ni vizuri wananchi kugeukia kilimo cha viazi lishe ambavyo vinastahimili ukame, lakini pia vina tija kubwa kwa kuongeza pato la familia.
“Ninashauri wananchi wote wa Ukerewe kulima viazi lishe kwa sababu mbali ya kuongeza akiba ya chakula, lakini vinaongeza pato la familia na taifa hasa vikichakatwa ili kutoa bidhaa mbalimbali,” alisema.
Kikundi cha wanawake 25 cha Green Voices Bukongo katika mji wa Nansio, kinachoongozwa na Leokadia Vedastus kinatekeleza mradi wa kilimo cha viazi lishe pamoja na uchakataji wa bidhaa mbalimbali za zao hilo ikiwa ni jitihada za kuwawezesha wanawake kushiriki miradi inayolenga kutunza mazingira pamoja na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo, Makamu wa Rais mstaafu wa Hispania, Maria Tereza Fernandez de la Vega, alivutiwa na mradi huo na kusema ni vizuri jamii ikahamasishwa kulima zao hilo ili kujikomboa kiuchumi pamoja na kujihakikishia usalama wa chakula.
Mama Tereza, ambaye ni Rais wa taasisi ya Women for Africa Foundation inayofadhili miradi ya Green Voices Tanzania, aliwataka wanawake wa kikundi hicho waongeze juhudi pamoja na kuwa waalimu wa wenzao kuhakikisha kilimo hicho kinasonga mbele.
“Dunia inapambana na mabadiliko ya tabianchi, sasa mradi huu unapaswa kuwakomboa akinamama kwa sababu unawahakikishia upatikanaji wa chakula kwa familia na wanaweza kuongeza mnyororo wa thamani kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali,” alisema.
Naye balozi wa Mfuko huo wa Wanawake Afrika, Getrude Mongella, akizungumza katika uzinduzi huo kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Bukongo mjini Nansio, aliwaomba watendaji wa serikali kusimamia kidete mradi huo ili kuondoa njaa katika visiwa vyote vya wilaya ya Ukerewe.
Alisema kwamba, kuanzishwa kwa mradi huo wilayani humo siyo tu kutawakwamua wanawake na wananchi wote, lakini pia kunaifanya Ukerewe kuwa kiini cha usambazaji wa zao hilo katika maeneo mengine ya Mkoa wa Mwanza.
“Ninawaomba watendaji wa serikali ya wilaya hamasisheni zao hili lilimwe katika visiwa vyote na kama ilivyokuwa zamani ambao mbegu zote za pamba zilitoka Ukerewe, basi tengenezeni na zalisheni mbegu za kutosha msambaze katika wilaya nyingine za Mkoa wa Mwanza.
“Naamini mkoa wote ukilima zao hili njaa haitakuwepo na wanawake wanaweza kutengeneza bidhaa mbalimbali ambazo wakiziuza zitawakwamua kiuchumi,” alisema.
Awali, kabla ya uzinduzi huo, Mama Maria Tereza na ujumbe mkubwa kutoka Dar es Salaam walitembelea mradi husika na kujionea kilimo hicho pamoja na uoteshaji wa mbegu, ambapo mshiriki kiongozi wa mradi huo, Leokadia Vedastus, alisema kwamba ekari moja iliyostawi vizuri inaweza kutoka jumla ya tani 7 (kilogramu 7,000) za viazi.
Mbali ya kiasi hicho, Leokadia alisema kwamba, viazi hivyo licha ya kuliwa kwa mapishi ya kawaida, lakini bado vinaweza kuchakatwa na kutoa bidhaa zaidi ya hamsini zikiwemo pilau la viazi, maandazi, kaukau (chips), chapatti, tambi na sambusa.
Leokadia ni mmoja wa wanawake 15 ambao walipatiwa mafunzo nchini Hispania mapema mwaka huu kuhusu uanzishaji wa miradi inayoendana na utunzaji wa mazingira na baada ya kurejea alifanikiwa kuwaunganisha wanawake 25 kutekeleza mradi huo.
Hata hivyo, alisema kwamba mpaka sasa wanawake wengi wamekuwa wakijitokeza kutaka kujifunza, ambapo alibainisha kwamba wameamua kuendesha mafunzo kila Jumamosi ili kuwapa fursa wanawake wengi kushiriki katika kilimo hicho.
Kwa upande mwingine, Leokadia amehamasisha mradi huo hadi kwa wanafunzi wa sekondari ambao wamepatiwa elimu ya uelewa na mabadiliko ya tabianchi pamoja na namna ya kupambana na uharibifu wa mazingira na mpaka sasa jumla ya wanafunzi 50 ambao ni mabalozi wa vita dhidi ya uharibifu wa mazingira wamekwishapatikana.
Mradi wa Green Voices unatekelezwa nchini Tanzania katika mikoa ya Mwanza, Kigoma, Dar es Salaam, Morogoro, Pwani na Kilimanjaro ambapo wanawake 10 wanatekeleza miradi mbalimbali ikiwemo kilimo cha viazi vitamu, kilimo hca matunda, kilimo cha uyoga, mboga mboga, ufugaji wa nyuki, usindikaji wa mazao ya muhogo, ukaushaji wa mboga mboga na kadhalika.
Nchini Tanzania, mradi huo unaratibiwa na Secelela Balisidya.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4810,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: DC UKEREWE ASHAURI WANANCHI KULIMA VIAZI LISHE KWA WINGI
DC UKEREWE ASHAURI WANANCHI KULIMA VIAZI LISHE KWA WINGI
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidxUrMJaYyaPqrZJKeOH8sA2VMgNJ5X2aC3cGjM8dDrVzAhHYtb2iYYatCGqsDAXtGqpM3nJuem_J47am3FfO8KDA-9fPJVfax70iVwo2fGiltuKruKgOrTJAzdNRsxnqyUDjPenU_GU0c/s640/UK1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEidxUrMJaYyaPqrZJKeOH8sA2VMgNJ5X2aC3cGjM8dDrVzAhHYtb2iYYatCGqsDAXtGqpM3nJuem_J47am3FfO8KDA-9fPJVfax70iVwo2fGiltuKruKgOrTJAzdNRsxnqyUDjPenU_GU0c/s72-c/UK1.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/dc-ukerewe-ashauri-wananchi-kulima.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/dc-ukerewe-ashauri-wananchi-kulima.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy