KULAANI MATUKIO YA UVUNJAJI WA HAKI ZA BINADAMU ZANZIBAR NA HASA PEMBA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vitendo vya u...



TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI


Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya vitendo vya uhalifu na uvunjaji wa haki za binadamu vinavyoendelea kufanyika Zanzibar, hususan kisiwani Pemba.

Kwa muda mrefu sasa hivi tokea kufutwa kwa Uchaguzi Mkuu wa tarehe 25 Oktoba, 2015 na hasa baada ya kufanyika Uchaguzi Mkuu wa Marejeo Zanzibar tarehe 20 Machi, 2016 kumekuwapo vitendo vya uhalifu na uharibifu wa mali, ikiwemo kukata vipando mbalimbali yakiwemo mazao ya muda mrefu na mfupi. Vilevile kumefanyika vitendo vya hujuma ikiwemo kuchoma moto nyumba katika baadhi ya makazi ya watu Kisiwani Pemba.

Aidha kumekuwepo na taarifa za matukio kama vile migomo takriban maeneo mengi ya Mikoa ya Pemba na baadhi ya maeneo katika kisiwa cha Unguja, yenye kuashiria vitendo vya kubaguana, kwa maana ya kutoshirikiana katika shughuli za kijamii na huduma za kijamii. Kwa mfano baadhi ya watu wananyimwa usafiri katika magari, kususiwa harusi, maziko na nyumba za ibada. 

Vitendo vya kukata na kuharibu mali, ikiwemo kuchoma nyumba moto ni kinyume na haki za binadamu kwani kila mtu ana haki ya kumiliki mali kama ilivyoelezwa katika Ibara ya 24(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, na Kifungu cha 17 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984.

Kuwanyima watu huduma ya aina yoyote katika jamii ni kinyume na misingi ya haki za binadamu, hasa haki ya kutobaguliwa kama ilivyoelezwa katika ibara ya 12 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, na Kifungu cha 11 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984. Vitendo vyote hivyo vinaathiri shughuli za kijamii na kiuchumi pia ni kinyume na haki za binadamu kwa mujibu wa Katiba na Sheria.

Tume pia imepata taarifa kuwa tofauti za itikadi za kisiasa zinasababisha ndoa kuvunjika kutokana na wanawake kuadhibiwa kwa kupewa talaka kutokana na kutotii amri za waume zao za kuwazuia kushiriki uchaguzi wa marejeo.

Kifungu cha 21(1) cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kama ilivyorekebishwa mwaka 2010 kinaeleza kuwa, “kila Mzanzibari anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kupitia wawakilishi waliochaguliwa kwa hiari”. Haki hii haitakiwi kuingiliwa na mtu yeyote, kwani ni haki inayotambua uhuru na utu wa kila mwanadamu kuamua yeye mwenyewe kushiriki au kutoshiriki katika shughuli za kisiasa, awe mwanamume au mwanamke.

Aidha Kifungu cha 21(2) cha Katiba ya Zanzibar kinatamka kuwa ”kila Mzanzibari anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu wa mambo yanayomuhusu yeye maisha yake au yanayolihusu Taifa”.

Wakati Tume ikiyasema haya, inapenda kutamka kwamba imeshangazwa na kusikitishwa  na tamko la Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Zanzibar kuhusu kuwakataza Mawakili kuwawakilisha watuhumiwa katika kesi zinazotakana na uvunjifu wa amani Zanzibar, au makosa yanayoashiria kufanyika kwa msukumo wa kisiasa. Zuio hilo la mawakili ni batili,  kwani ni kinyume na misingi ya haki za binadamu, na misingi ya haki sawa, yaani (fair trial principles,) ambayo inatamka kwamba kila mtu hatotiwa hatiani mpaka ikithibitika hivyo,(presumption of  innocence until proven guilty), au kila mtu ana haki ya kuwakilishwa mahakamani (right of legal representation).

Tume inatamka kwamba matamko hayo hayaendani na dhana ya utawala wa sheria na utawala bora, ambapo kila taasisi, na kila mtu anatakiwa kutenda kazi zake kwa kuzingatia Katiba, yaani Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na Sheria ya mwenendo wa Makosa ya Jinai ya Zanzibar, Namba 7 ya mwaka 2004, pamoja na Mikataba ya Kimataifa hasa Mkataba wa haki za kisiasa na kiraia wa mwaka 1966 ambao Tanzania imeridhia.

Ibara ya 13(6) Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 na kifungu cha 12(6), ya Katiba ya Zanzibar 1984 zinaweka miongozo ya usimamizi wa haki, ambayo ni pamoja na mtu kupewa haki ya kusikilizwa kwa ukamilifu, wakati wa upelelezi na uendeshaji wa kesi za jinai, na wakati mtu anapokuwa chini ya ulinzi, utu wake utaheshimiwa, zinapiga marufuku mateso au adhabu za kinyama au zinazomtweza au kumdhalilisha mtu.

Kifungu cha 41 cha Sheria ya Mwenendo wa Jinai 2004, kinampa haki Wakili aliyesajiliwa na Mahakama Kuu chini ya Sheria ya Legal Practitioners Decree Cap. 28 kumuwakilisha au kumshauri mtu yeyote anayetuhumiwa au kushtakiwa kwa kosa lolote.

 Tume inasisitiza kuwa mamlaka zote zenye kusimamia upelelezi na kuendesha mashtaka zitekeleze kazi zake kwa weledi na kuheshimu matakwa hayo ya Katiba na sheria.

Tume inapendekeza kwamba ili hali ya maelewano irudi kama ilivyokuwa hapo awali kisiwani Pemba na Zanzibar kwa ujumla, panahitajika hatua za makusudi zitakazo leta maelewano  katika jamii. Tume inashauri yafuatayo:-

(i)            Hatua za makusudi na haraka zifanyike kwa Viongozi wa Kitaifa na wa vyama vyote vya siasa vikiwemo  CUF na CCM wakae pamoja kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa suluhisho la kudumu litakalozuia matatizo ya uvunjifu wa amani  kujirejea.

(ii)          Taasisi zinazosimamia ulinzi na usalama, hususan Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya dola, ziwe makini katika kufanya kazi zake kwa kufuata misingi ya utawala bora, haki za binadamu na utawala wa sheria ili kuepukana na madhara yasiyotarajiwa katika jamii.

(iii)         Wananchi wote wanatakiwa kutii sheria za nchi, na kutojiingiza katika vitendo vya uvunjifu wa amani na usalama.


SIGNED
Bahame Tom Nyanduga
Mwenyekiti
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA.

COMMENTS

Name

Anga,11,Arusha,27,Burudani,302,burundani,1,come rain,1,come sun,1,Crazy in Love kama wimbo kama wao wenyewe,1,dahh sijui kweli mbona shida,1,Dar utakuja je tumejiandaa,1,daraja sahau nini,1,demokrasia ya upanga,1,Dodoma,77,Dole tupu vijana wa zamani,1,Duhh bibie endeleza libeneke,1,Duhh kaisikie Walibana,1,duhh kwa mbagala mama lazima awe supa,1,Fedha za maiti haziliwi bure,1,Fedha za watu kwa maendeleo ya watu,1,Fikira,14,filamu,238,Filamu ndio kielelezo cha ukuzi wa taifa,1,flamu,7,Gandamiza Kibara baba ake,1,Habari,4816,habari. dodoma,24,hadithi,19,hakika tumeweka historia,1,hakuna noma jongwe,1,hapa kwetu inakuwaje vile,1,hasira hasara,1,hata maji,1,hataki masikhara na maisha yake,1,hatubonyezi kizenji,1,haya ndiyo mambo ya Ulaya,1,haya si yangu ni ya mdau mwenye hasira,1,haya wabongo na mambo kutoka nje,1,He he he wananikumbusha upishi wa shaba,1,Headline,1,Hii hurejesha uhai,1,Hii iko sawa kweli?,1,Hii imekaa vizuri,1,Hii inakaaje vile,1,Hii kweli noma,1,Hii maana yake Moro kuna uhaba wa chakula,1,Hii mexico,1,Hii mihasira mingine bwana,1,Hii ndio moro sio mpaka dar,1,hii ni hatari,1,Hii ni kiboko anayetaka kubisha ajibishie tu,1,Hii ni moja ya staili za kunyoa nywele,1,Hii si lukwangule,1,hii staili mpya,1,hili ni jengo pacha la malaysia ghorofa 88,1,Hivi ni ngoma tu,1,hivi nini siri za serikali,1,hivi sisi tunajua kama kuna vitu vya aina hii,1,hivi vitu bwana,1,Hiyo ndiyo gharama ya demokrasia,1,Hizi imani nyingine ni hatari,1,Hizi takwimu hizi mhh,1,Hongera bibie,1,Hongera dada etu kwa kutuletea kaka etu (shemeji) kwani mwenye dada hakosi shemeji,1,Hongera sana,1,huhitaji mifedha kuwa msafi,1,Huko Ulaya,1,Huu ndio ustaarabu,1,huu ujiko utakuwa mkubwa,1,imetosha,1,Inahitaji nidhamu fulani,1,inakuuma au...,1,Inakuwaje kama filamu yenyewe itahitaji busu la nguvu,1,Inaonekana watanzania hatukuwepo,1,Ipo kazi Maximo,1,Iringa,22,Isiwe mijineno tu manake mihela hubadili watu kweli,1,Itakuwa laki moja ya halali,1,jamani huu kama si ushamba kumbe nini,1,Jamani mbona Mungu anatupigania,1,Jamani watoto wanatakiwa kupendwa,1,jamani.. jamani ukiikosa Diamond usijutie,1,Je nyumbani hakuna vitu vya aina hii?Tuambie,1,je walikuwepo watu wa huduma ya kwanza,1,Je watanzania wanalipa kodi,1,jela kwa raha,1,Jolie,1,juhudi za lazima kuinua filamu,1,kama si kiwanda cha chumvi nani atawajua hawa,1,Kama kweli ndio kweli basi kila heri,1,Kama Mkristo naamini hilo hiyo si sahihi,1,kama unajua kuyarudi nenda Malta,1,kama wao wanaweza sisi je,1,Kamua baba waache wakanyagane,1,karibu nyumbani dada yote maisha tu,1,karibu Tatiii,1,KARIBUNI,1,Katavi,5,kaza buti hakuna kukata tamaa inalipa,1,kazi kwako mheshimiwa waziri wa madini,1,kazi na burudani,1,keep it up bloggers,1,kero ya usafiri sasa kwisha,1,Kila chenye roho na mwili kitaonja umauti,1,kila kitu kina vitu,1,Kila la Heri jamila,1,kila la heri kwani ni changamoto,1,Kipya,51,Kiuno bila mfupa,1,Kolelo mzimu ambao bado hai,1,KUBWA,1,Kudumisha urafiki wa dunia,1,Kuna dalili za wasomi kukubali Uafrika,1,kuna makala humu humu ndani ya blogu sijui mnasemaje,1,Kuu,113,kwa mara nyingine tena Tigo imewezesha,1,Kwa mchanganyiko huu muungano lazima udumu,1,Kwa mihasira hajambo,1,kweli,1,Kweli ina mkono mrefu tuone,1,Kweli duniani tunatofautiana,1,la maana ni kuwa na jiko au vipi,1,labda halitabadilika tena,1,lakini mwafaka lazima,1,lengo ni kutafakari,1,leteni vitu tuvione,1,lets us,1,Lucy wanakuelewa hawa...,1,Lukwangule nyumbani kwetu,2,M ungu bariki mikono ya madaktari wafanikiwe,1,MAARUFU,1,maendeleo ya soka siku zote yanahitaji fedha ili yapatikane,1,maisha ni vyema kuyaangalia,1,MAJIBU,1,makala,51,mama ni mama tu anapendeza,1,mambo mengine we angalia tu,1,mambo msimamo,1,mambo sasa mchanganyiko,1,Mara nyingine huona tunakotoka kwa kuona wenzetu,1,Mashabiki wa rhumba mpooooooooo,1,Masitaa,12,Maskani,1,MASOKO,3,Masupa staa mnaoinukia mpoo,1,Matamasha,6,mavazi ya kuogelea yanaposhindaniwa,1,Mbeya,11,Mchakamchaka anti Asmah,1,Mchanganyiko,81,MCHANYATO,1,mchezo,5,mengi wanayoyaita siri ni public information,1,mfumuko wa bei mpaka noma,1,Mhh sijui watu wa Sua ambao wako huko wanasemaje,1,Mhh ugua pole dada watu wanataka burudani,1,Michezo,501,Michezo maalum inatakiwa kupigiwa debe,1,miguu,1,miguu babu,1,Mikataba mingine ama hakika tuiangalie hata wakopeshaji nao wanatugeuza sakala,1,MIMI NI KISURA NAJITAMBUA,1,Mimi sijajua hasa kumetokea nini kwani ninavyojua hawa huwa na ungalizi wa hali ya juu,1,Mimi simo,1,mimi sisemi,1,mkiwa chumvi basi mkoze,1,Mkiwa taa mulikeni,1,Mnaonaje je hii imekaa vyema,1,Mnaweza wakwetu hapa,1,Morogoro,51,mrithi wa mwanadada Whitney Houston,1,Mtwara,4,Mungu aiweke mahali pema roho yake,4,Mungu amrehemu,1,Mungu amweke pema peponi,1,Mungu awabariki sana,1,Mungu awe nao,1,Mungu ibariki Tanzania,1,Mungu tuepushe na imani hizi za kishirikina,1,mungu tufanye tuwe na upendo,1,Mungu twaomba utuhurumie,1,Muziki,350,muziki na fasheni,5,Mwanahabari,33,Mwanza,6,Mwendo mdundo dada,1,Mwenge huo utakimbizwa duniani kwa siku 130,1,Mwenge wa olimpiki ni ishara ya urafiki,1,Mzee wa Farasi nakupa saluti,1,Mzimbabwe huyu kutoka kwa mama mkali,1,N i dar mpaka Moro au bao tatu bila,1,Na sisi je,1,Naam kama haiwezekani hapa,1,Nairobi waanzisha tena utalii,1,namna bora ya kusaidia jamii,1,nani abebe hukumu na lawama,1,nani asiyejua utamu wa pipi,1,Nani kama baba,1,naona inafaa kuchangia mimi sitoi hoja,1,ndoa za mastaa huwa na mgogoro,1,nenda mwaya nenda,1,New Zanzibar Modern Taarab na wapenzi big up,1,news,5,Ni bikini kwa kwenda mbele,1,Ni Dar mpaka Moro au.. tatu bila,1,ni furaha za muungano,1,Ni kazi ngumu yenye kuhifadhi utamaduni,1,Ni kuchakarika kuonyesha urafiki na biashara pia,1,ni mfumuko wa bei au mfumuko wa nchi,1,Ni muhimu kutazama afya yako,1,ni muziki kwa kwenda mbele,1,Ni muziki mpaka China,1,Ni raha tupu,1,Ni Serengeti Premium Lager,1,Ni Tigo na mawasiliano ya kisasa,1,Ni wakati wa kuujadili utamaduni,1,Ni zaidi ya jazz,1,Nitasubiri and welcome home,1,nje je?,1,NUKUU YA LEO,1,nyie mnasemaje kuhusu hili,1,Ona Kolelo na sindikizwa na Wazee wa Gwasuma,1,ona vya dunia,1,One step ahead,1,patna mwingine mjamzito,1,Pengine anamuogopa Jada Pinkett manake kwa wivu..,1,picha,494,Pole Jamila hayo ndiyo mashindano,1,poleni sana,1,poleni sana wanyalukolo,1,Powa sana,1,Profesa jamaa wanakumaindi,1,Roho za marehemu zipate pumziko la milele,1,Ruvuma,9,sakata dansi mpaka kwenye kilele cha dunia,1,sasa kumebakia ugonjwa mmoja polisi kuendesha mashtaka,1,sasa mifedha kila mahali hongereni,1,Sasa ni mavuno,1,Sasa ni wakati wa kutafuta upenyo ndani ya IDOLS,1,SAYANSI,1,SAYANSI ANGA,1,See Uluguru Montains,1,serikali inataka kujihami kwanini,1,Show of support Big Up Madame,1,Si kitu kidogo hata kidogo,1,si unajua tena namie naimwaga hivyo hivyo,1,Siasa,346,siasa habari,2,Sijui kama City wanajua Mbagala noma,1,Sijui tunaishi karne gani yailahi,1,Sinema,9,sio advencha....kaaa ...niko kibaruani,1,Sisi ndio tunaanza vitongoji,1,Sisi yetu macho na masikio,1,Slow slow jamani,1,sto,1,tabasamu kali la mwenge wa olimpiki,1,Tabora,1,Tazama Waziri Mkuu Pinda wasije wakapindisha maamuzi yako,1,TEKNOLOJIA,1,Thats big man game,1,This is crazy Africa,1,This is Mgeta,1,Tibet wamegeuza Olimpiki jukwaa la siasa,1,Titbits collection,1,Tubadili tamaduni,1,Tuchangie mambo yaive,1,tuendeleze sanaa,1,tuienzi na sisi mbona wizara haituambii,1,Tuipeleke kaskazini,1,Tuisaidie serikali shida ya Mererani,1,tujue namna ya kupumzika,1,Tulienda kustarehe au kufanya fujo,1,Tumsaidie mtototo huyu kurejea katika hali ya kawaida,1,tunahitaji haya,1,Tunajifunza kweli kutoka kwao,1,Tunapandisha chati tu,1,Tunasubiri,1,tunazidi kuhesabu siku,1,TUNAZISUBIRI ZA VINARA ADAR,1,Tuombe nafuu kwa wagonjwa,1,Tuombe rehema kwa mungu,1,Tuone yatufae,1,Tusingoje wengine watusemee,1,tutampa tafu kubwa Prof,1,tuuenzi utamaduni au vipi,1,Tuukuze na kuulinda,1,tuvipende,1,tuwalinde maalbino,1,Tuwe kweli wakweli,1,ubunifu siku zote hulipa,1,uchumi huzunguka kwa kuwawezesha wasukaji,1,udumu muungano,1,Ugonjwa huu wa sasa ni kitendawili,1,Ukiiona kolelo utaipenda,1,Ukirejea salama kila mtu anafurahi,1,Umelenga Mkuchika utamaduni unakufa,1,unaposaka uwakilishi wa dunia,1,urafiki,1,Usisahau wazee wa Ngwasuma,1,UTAMADUNI,1,Video,2,Vionjo vipya ndani ya Gwasuma,1,Vita dhidi ya ufisadi,1,vitongoji Miss Tanzania navyo vimeanza,1,Vitu vikali vyazidi kuingia Dar,1,Vituko,77,Vituo vya polisi Tanga vyatelekezwa,1,VIVALO,1,Wacha tujifue,2,Wadau ilitolewa kiingereza,1,wakali wa ubunifu,1,wala usibabaike mwakwetu hii noma,1,wanadamu wanapotaka kujua zaidi,1,wanasema mpaka kieleweke,1,Wanataka kujua mali za JK na wengine,1,Wanawake wenye mvuto: Monroe,1,Wapo mabinti wa matawi ya juu,1,watu wanapofanya weli kwenye sanaa,1,waweza kurejea enzi ya Moro jazz na Cuban malimba,1,Wazee tupo kusindikiza,1,waziri,1,welcome dar baby,1,Wenzetu wameona sisi tunangoja nini kuangalia,1,wewe unasemaje,1,wigo mpana wa utamaduni,1,wilaya ya 'Mbagala' mlie tu,1,Yaaani sijui itawezekana,1,Yaani wakati mwingine hata huelewi prioty over priority,1,yeye mbele sisi nyuma,1,Yote maisha dada,1,ZA MOTOMOTO,1,Zanzibar,79,zawadi zinatakiwa ziende shule,1,ZILIZOTIA FORA,1,zitachangia kupunguza makali ya bei za umeme,1,
ltr
item
Lukwangule Entertainment: KULAANI MATUKIO YA UVUNJAJI WA HAKI ZA BINADAMU ZANZIBAR NA HASA PEMBA
KULAANI MATUKIO YA UVUNJAJI WA HAKI ZA BINADAMU ZANZIBAR NA HASA PEMBA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjw5IJe9JJzbZXhCQCUp5L3kEydbY9Fx-BjZsrtbnYlAlFOWt473bnM2EOxx-ZlVmWhAYELB5syZJhXUv5NpSDrvF51we5m6SwY9GhVV30S1yoWeH9cTSK4ifl1V58JrUyOy3-AXFgxj8w/s320/karafuu+pemba.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjw5IJe9JJzbZXhCQCUp5L3kEydbY9Fx-BjZsrtbnYlAlFOWt473bnM2EOxx-ZlVmWhAYELB5syZJhXUv5NpSDrvF51we5m6SwY9GhVV30S1yoWeH9cTSK4ifl1V58JrUyOy3-AXFgxj8w/s72-c/karafuu+pemba.jpg
Lukwangule Entertainment
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/kulaani-matukio-ya-uvunjaji-wa-haki-za.html
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/
http://lukwangule.blogspot.com/2016/07/kulaani-matukio-ya-uvunjaji-wa-haki-za.html
true
934549962738256429
UTF-8
Loaded All Posts Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All RECOMMENDED FOR YOU LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy